Tuesday, October 17

TAARIFA KWA UMMA:OFISI ZA BAKWATA ZAHAMIA KWA MUDA JENGO LA TIGER TOWER-MTAA WA TOGO

Ndugu zangu Wanahabari,

Assalaamu Alaykum (Amani ya Mwenye ezi Mungu iwe kwenu)

Napenda kuufahamisha umma wa kiislamu kuwa kufuatia kuanza mradi wa ujenzi wa msikiti wa Mohammed VI unaojengwa katika eneo la Bakwata makao Makuu Kinondoni Road.

Hivyo basi napenda kuchukua nafasi hii kuufahamisha umma kuwa ili kupisha mradi huo Bakwata Makao Makuu imehamisha ofisi zake na kuzipeleka katika mtaa wa Togo jengo linalotambulika kama TIGER TOWER na shughuli zote zinaendelea kama kawaida.

Mwisho kabisa tunaomba radhi kwa usmbufu wowote uliojitokeza katika kipindi hiki cha ujenzi.

Wabillahi TTaufiiq

USTAADH TABU KAWAMBWA

MKURUGENZI HABARI NA MAHUSIANO.




Waziri Mkuu Kassim Majaliwa  wakishuhudia wakati Mufti Mkuu wa Tanzania, Sheikh Abubakary Zubeir (kulia)  akitia saini Makubaliano ya ujenzi wa Msikiti kwenye eneo la BAKWATA, Kinondoni jijini Dar es salaam Oktoba 25,2016. PICHA NA MAKTABA

Kenya yasaidia majeruhi wa Somalia

Baadhi ya watu waliojeruhiwa Mogadishu wakisubiri kusafirishwa Uturuki. Wengine wamepelekwa Kenya.
Ubalozi wa Somalia nchini Kenya pamona na shirika la Red Cross, na serikali ya Kenya,mapema Jumanne walizindua mpango wa kusaidia wahanga wa shambulio la kigaidi lililowaua watu zaidi ya 300 mjini Mogadishu,Somalia.
Mpango huo ni pamoja na uzinduzi wa namba maalum ya kuchangisha pesa kutoka kwa wahisani, na dawa za kuwatibu manusura.
Waziri wa masuala ya nje wa Kenya Amina Mohamed ametangaza kuwa Kenya imetuma ndege mbili Mogadishu zikiwa na tani 31 za dawa.
Mlipuko wa bomu kwenye lori ulitokea Jumamosi
Mlipuko wa bomu kwenye lori ulitokea Jumamosi
Ndege hizo zinatazamiwa kuwasafirisha hadi Nairobi majeruhi takriban 20, watakaopokelewa na hospitali za Kenya.
Utoaji wa damu kwa hiari ili kuwasaidia wahanga hao wa shambulio la bomu, umekuwa ukiendelea Jumanne hii katika eneo la Estleigh,Nairobi lenye watu wengi wa asili ya Kisomali.
Majeshi maalum ya Kikosi cha AMISOM nchini Somalia pia yalizindua zoezi kama hilo la kutoa damu kwa hiari, katika mji wa Mogadishu.
Misaada zaidi ya matibabu na upkoaji imetolewa na mataifa ya Djibouti, Turkey na Marekani.
Shambulio la bomu Jumamosi lililowaua watu zaidi ya 300 na kujeruhi wengine wengi, limetajwa kama mbaya zaidi nchini Somalia katika miongo miwili iliyopita.

WASIRA: KUIKOSOA SERIKALI SI JINAI


ALIYEKUWA waziri katika Serikali za awamu nne za kwanza, Stephen Wasira, amesema si jinai kuikosoa Serikali bali kuitukana ndiyo kosa kisheria.
Mwanasiasa huyo mkongwe nchini aliyewahi kuwa Mbunge wa Bunda kabla ya kushindwa na Esther Bulaya (Chadema) katika uchaguzi mkuu uliopita, ni miongoni mwa wanachama wa CCM waliojitokeza kuwania urais ndani ya chama hicho katika Uchaguzi Mkuu uliopita.
Akizungumza na MTANZANIA kwa simu jana akiwa nchini Marekani, Wasira ambaye  alikuwa waziri katika kipindi chote cha miaka 10 ya uongozi wa Rais Mstaafu, Jakaya Kikwete, alisema watu waikosoe Serikali kwa hoja na si kutukana.
“Ipo tofauti kati ya kutukana na kukosoa. Mimi naweza nikasema na bado nisitukane, mfano Zitto Kabwe (Mbunge wa Kigoma Mjini), huwa nasoma maandiko yake anaonekana ana hoja kabisa ambayo inahitaji kujibiwa na sijawahi kusikia akikamatwa.
“Lakini wapo wanasiasa; akisimama asipotukana hajisikii vizuri hao naona ndiyo wanaoshughulikiwa. Unaweza ukaikosoa Serikali bila kutukana, kukosoa Serikali si jinai lakini kutukana ndiyo jinai,”alisema Wasira.
Kuhusu viongozi wa vyama vya siasa wanaokamatwa na vyombo vya dola pale wanapoikosoa Serikali, alisema hata kama wakikamatwa watakwenda mahakamani na baadaye Mahakama itasema kama kuna kesi au laa.
“Akikamatwa si anakwenda mahakamani na kama hana kesi anaachiwa, hivyo pale mahakama inapotoa uamuzi kuwa hakuna kesi watapunguza ukamataji wa aina hiyo watawakamata wale wenye makosa tu,”alisema.
Katika kushughulikia suala hilo, Wasira alilitaka Jeshi la Polisi kufanya kazi kwa uangalifu na kusisitiza kuwa watu wasiokuwa na hatia wasikamatwe.
“Jeshi la Polisi liwe na uangalifu, waendelee kufanyakazi lakini wasikamate watu wasio na hatia,”alisema Wasira.
Aidha mwanasiasa huyo mkongwe ambaye ameshiriki na kuongoza kamati maalum iliyoandaa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015-2020, alizungumzia pia uongozi wa awamu ya tano kulinganisha na awamu zilizopita, akisema haiwezekani watu wote wawe na mtazamo sawa.
“Kuna siku niliulizwa swali kama hilo kuwa nimefanya kazi karibu na viongozi wote, nikaulizwa nani kafanana na nani na mimi nikasema hakuna anayefanana na mwingine.
“Nikimaanisha kwamba kila kiongozi ana style yake ya kuongoza. JK (Jakaya Kikwete) alikuwa anapenda kushirikisha watu wote anaopingana nao, alikuwa akiwakaribisha wapinzani wake lakini pamoja na yote hayo alitukanwa, aliitwa dhaifu.
“Amekuja JPM (Rais John Magufuli) wanasema ni mkali mara dikteta, lakini aliyekuwa mpole, msikilizaji wa maoni yao ni dhaifu. JPM anayesimamia misingi anayoiamini yeye wanasema ni dikteta…Kikwete aliwapa uhuru mwingi sana,”alisema.
Akifafanua hoja hiyo, Wasira alisema Rais anayo haki ya kuongoza watu wake na pale wananchi wanapolalamika anao wajibu wa kuwasikiliza.
“Rais kama kiongozi wetu ana wajibu wa kuwasikiliza wananchi wake na pale malalamiko yanapozidi lazima awasikilize na si lazima akakubaliana na kila kinachosemwa lakini ni wajibu wake kusikiliza.
“Kwa kusikiliza wanachokisema anaweza kupata ukweli na uongo…atatofautisha pumba na mchele na katika kuwasikiliza anaweza akaujua ukweli ambao alikuwa haufahamu,”alisema Wasira.
TUKIO LA LISSU
Katika mazungumzo hayo, Wasira alizungumzia kwa masikitiko tukio la kushambuliwa kwa risasi Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, ambapo alisema tukio hilo ni la kulaaniwa na wapenda amani wote.
Wasira ambaye amewahi kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, (Mahusiano na Uratibu) katika Serikali ya awamu ya nne, alisema siasa za chuki na visasi hazifai na kwamba hoja zijibiwe kwa hoja na si kutoa roho za watu.
Alisema matukio ya aina hiyo alikuwa akiyasikia nchi nyingine lakini ameshtushwa kutokea kwa nchi kama Tanzania ambayo kwa muda mrefu imekuwa ikisifiwa kwa kuwa na amani.
“Tukio la Lissu ni baya sana…watu wote wapenda amani tunasikitishwa, tunalipinga na kulilaani. Tunataka siasa ziendeshwe kwa hoja na hoja zijibiwe kwa hoja…tupingane kwa hoja.
“Kutoa roho za watu na kukatisha maisha ya mtu hiyo si siasa, siasa za chuki na visasi hazipendezi, mauaji ni hatua ya juu kabisa ya visasi…haifai.
“…Mambo haya tulikuwa tunayasikia nchi zingine na tusiige mambo hayo, hatuyakubali kabisa,’alisema Wasira.
Alisema Jeshi la Polisi, lina wajibu wa kujua watu hao waliofanya kitendo hicho kibaya ili kuwaondolea wananchi hofu.
Aidha mwanasiasa huyo alisema katika mazingira kama hayo, watu wabaya wanaweza wakaingia katikati kwa lengo la kuichonganisha Serikali na wananchi.
“Polisi wana wajibu wa kujua haya yanayoendelea…watu wabaya wanaweza wakaingia katikati yetu, wakaichonganisha Serikali na wananchi.
“Watu wabaya wapo hapa duniani; yaani kama Polisi haiwachukulii hatua wahalifu watu hao wabaya wanaweza wakampiga Lissu na baadaye wakasema Serikali imefanya hivyo,”alisema Wasira.
Lissu ambaye pia ni Mwanasheria Mkuu wa Chadema na Rais wa Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS), alishambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana Septemba 7, mwaka huu mjini Dodoma, yupo Nairobi nchini Kenya akiendelea na matibabu zaidi.
MIILI ILIYOOPOLEWA BAHARINI
Akizungumzia kuhusu miili ya watu walioopolewa baharini, Wasira alisema Jeshi la Polisi linapaswa kufanya uchunguzi na kutoa taarifa ili kuwaondolea wananchi hofu.
“Jeshi la Polisi lina wajibu wa kulinda amani na utulivu pamoja na mali za watu, hivyo lina wajibu wa kutoa taarifa na kuwahakikishia amani Watanzania,”alisema Lissu.
KATIBA MPYA  
Akizungumzia kuhusu Katiba mpya ambapo alikuwa mjumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, Wasira alisema yapo mambo yanaenda kwa mahitaji ya wakati na kipaumbele cha Serikali.
“Rais Magufuli wakati analihutubia Bunge alisema amerithi kiporo cha Katiba mpya, hivyo atashughulikia kwa wakati.
“Hivyo ni suala la wakati ambao Serikali imeona itafaa, lakini huwezi kusema haina mpango nao wakati tulikaa siku 120 kuandika Katiba inayopendekezwa hivyo ghafla tu huwezi ukaibuka ukasema haihitajiki isipokuwa ni siku ya kuliendeleza.
“Tunahitaji Katiba mpya, maji, chakula, zote zinatokana na rasilimali, hivyo kupanga ni kuchagua,”alisema.
AMVAA NKAMIA
Wasira alieleza kushangazwa na hatua ya Mbunge wa Chemba, Juma Nkamia kutaka kupeleka hoja binafsi bungeni ya kuongezwa miaka saba ya uchaguzi.
Wasira ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, alihoji mbunge huyo alipotoa hoja ambayo haina manufaa kwa wananchi.
“Hivi ameitoa wapi, anaitaka miaka saba ya nini? Tuzungumze katiba kwa ujumla…sijui miaka saba…mimi hata simwelewi huyu Nkamia, sijui anataka ya nini na nimeshaongea naye tayari.
“Katiba huwa inaamsha hisia za watu, atueleze miaka saba ya nini na hiyo mitano amefanya nini? Watanzania waulizwe…hamuwezi kubadili katikati ya mchezo haiwezekani kabisa,”alisema.
HANA MPANGO WA KUGOMBEA
Kuhusu matarajio yake ya kisiasa baada ya kushindwa ubunge katika uchaguzi uliopita, Wasira alisema hana mpango wa kugombea na kwamba ameacha hiyo kazi, bali kwa sasa anagombea vyeo ndani ya chama chake.
“Mwaka 2020 sigombei, nimeacha hiyo kazi. Kwa sasa nagombea vyeo vya CCM nagombea mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC), wakinipitisha sawa,”alisema.
Akitoa maoni yake kuhusiana na kauli ya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole kwamba hivi sasa chama hicho kitawapitisha wagombea ubunge ambao ni wakaazi wa eneo husika, Wasira alisema: “Hilo ni jambo la kikatiba, kisheria.
“Kama Polepole amelisema litakuja katika vikao vya chama tutalizungumza kwa sasa nimeliona kwenye mitandao tu, hivyo kwa sasa sina maoni kuhusiana na hilo kwa sababu lazima lije kwenye vikao,”alisema.

Leo ni siku ya kupambana na umaskini duniani

Leo ni siku ya kupambana na umaskini duniani, huku kaulimbiu ya mwaka huu ikiwa inasema ''Njia ya kuelekea jamii zenye amani na umoja''.

Bangladesch Kinderarbeit in Dhaka (picture-alliance/NurPhoto/M. Hasan)
Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa, siku ya kupambana na umaskini inaadhimishwa kwa kuzingatia wito uliotolewa miaka 25 iliyopita ya kutambua ujuzi na ujasiri wa familia zinazoishi katika umaskini duniani kote, umuhimu wa kuwafikia zaidi maskini na kuanzisha ushirikiano na wananchi wanaotoka katika mazingira yaliyokuwa na umaskini na wenye nia ya kuutokomeza umaskini.
Wito huo ulichukuliwa na kufanyiwa kazi katika nchi nyingi duniani na umewawezesha watu wanaoishi katika umaskini uliokithiri kuvunja ukimya na kuzungumza kuhusu umaskini pamoja na kuchukua hatua katika kushirikiana na wale wanaotamani kuwa washirika wao. Kaulimbiu ya mwaka huu inakumbushia umuhimu wa maadili ya heshima, mshikamano na kuwa na sauti moja katika kuitikia wito wa kuutokomeza umaskini kila mahali.
Maadili hayo pia yanaonekana katika ajenda ya Umoja wa Mataifa ya Malengo ya Maendeleo Endelevu ya mwaka 2030, ambayo yameliweka suala la kupambana na umaskini kama lengo kuu na kuzilazimisha nchi zote kuutokomeza umaskini katika mifumo yote, kupitia mikakati inayohakikisha kwamba inatimiza haki zote za binadamu na kuhakikisha hakuna mtu anayeachwa nyuma.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres anasema aina nyingi za umaskini zinasababishwa na kuongezeka kwa idadi ya watu wasio na ajira, kukosekana kwa usalama na usawa, mizozo na mabadiliko ya tabia nchi.
Watu milioni 800 duniani wanaishi na umaskini
''Leo tunaungana na watu milioni 800 duniani wanaoishi katika umaskini uliokithiri. Lakini tumepiga hatua katika kuondoa umaskini tangu 1990 na nchi zote zimejizatiti katika kuutokomeza umaskini. Ajenda ya 2030 ya Malengo ya Maendeleo Endelevu inaahidi kuhakikisha dunia yenye afya, salama na kujenga jamii iliyo na amani na umoja unaoheshimikwa kwa wote,'' alisema Guterres.
Russland St. Petersburg International Economic Forum Antonio Guterres (Reuters/S. Karpukhin)
Katibu Mkuu wa UN, Antonio Guterres
Umuhimu wa uelewa wa umma, sauti ya pamoja na kuwashirikisha ipasavyo watu wanaoishi katika umaskini uliokithiri, unatambuliwa katika ajenda yenyewe na kwenye mchakato wa mashauriano yanayoongozwa na Umoja wa Mataifa kuhakikisha kwamba uwajibikaji na vipaumbele vya mamilioni ya watu, hasa wale wanaoishi katika umaskini uliokithiri, wanajumuishwa na kusikilizwa. Kushirikishwa ipasavyo kwa watu wanaoishi katika umaskini uliokithiri, kutasaidia kwa kiasi kikubwa kufanikisha Malengo ya Maendeleo Endelevu.
Kampeni ya kimataifa pia inawakaribisha watu binafsi, jumuiya, mashirika na nchi mbalimbali kuiadhimisha siku hii katika njia tofauti, ikiwemo kugundua au kuelezana jinsi umaskini unaweza ukatokomezwa, wakati watu wanapoungana pamoja katika juhudi za kuimarisha haki kwa wote.
Mwaka huu pia ni kumbukumbu ya miaka 30 ya Siku ya Kuushinda Umaskini Uliokithiri Duniani. Siku hii ilitambuliwa na Umoja wa Mataifa baada ya wito uliotolewa na Padre Joseph Wresinski. Oktoba 17, 1987, watetezi wa haki za binaadamu na haki za kiraia kutoka duniani kote walikutana mjini Paris, Ufaransa kwa lengo la kuahidi kuonyesha mshikamano na watu wote ulimwenguni na kujitahidi kuondoa umaskini uliokithiri.
Kwa mujibu wa mkutano huo uliohudhuriwa na zaidi ya watu 100,000, ''Pindi wanaume na wanawake wakiishi katika umaskini uliokithiri, haki za binaadamu zinakiukwa.'' Wanaharakati hao wanasema waliungana pamoja kuhakikisha haki hizo zinaheshimiwa, kwani huo ni wajibu wao. Mafanikio ya ulimwengu usio na umaskini, yanatoa mwelekeo wa kuzifikia jamii zenye amani na umoja kama ilivyoandikwa kwenye Lengo la 16 la Malengo ya Maendeleo Endelevu.

Mahakama: Mwenyekiti wa IEBC hana uwezo wa kurekebisha matokeo Kenya

Jaji mkuu David Maraga
Image captionJaji mkuu David Maraga
Mahakama ya upeo nchini Kenya imeunga mkono uamuzi wa mahakama ya rufaa unaomnyima uwezo mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati kurekebisha matokeo ya uchaguzi kutoka maeneo bunge.
Mahakama hiyo ya juu iliamua kwamba matokeo ya uchaguzi yaliotangazwa katika maeneo bunge ni ya mwisho.
FOMU 34
Katika uamuzi wa mwisho , majaji watano wa mahakama hiyo walisema kuwa kulikuwa na hitilafu kati ya matokeo ya fomu 34A na 34B, mwenyekiti anafaa kutangaza matokeo ya uchaguzi na kuwaachia mahakama swala hilo kuamua.
Majaji hao walisema kuwa bwana Chebukati ana wajibu wa kukagua matokeo hayo kama yalivyopeperushwa kwa njia ya kielektroniki.
Hatahivyo kila anapokumbana na hitilafu , anapaswa kuelezea vyama vilivyopo, wachunguzi wa uchaguzi na raia na kuwachia swala hilo mahakama ya uchaguzi.
Katika uamuzi uliosomwa na naibu jaji mkuu Philomena Mwilu ,mahakama ilisema kuwa uwezo wa mwenyekiti kuchunguza matokeo sio agizo lililotolewa na mahakama bali ni sheria iliopo katika katiba na sheria za uchaguzi.
Walisema kuwa ukaguzi huo ulilenga kuhakikisha kuna usahihi na kuzuia wizi wa kura.
Mahakama: Mwenyekiti wa IEBC hana uwezo wa kurekebisha matokeo Kenya
Image captionMahakama: Mwenyekiti wa IEBC hana uwezo wa kurekebisha matokeo Kenya
Jaji Jacton Ojwang alikuwa na uamuzi tofauti huku jaji David Maraga, Philomena Mwilu, Smokin Wanjala na Isaac Lenaola wakitoa uamuzi wa wingi.
Kesi ya Kiai:
Katika kesi yake, tume ya uchaguzi nchini Kenya IEBC ilisema kuwa ombi hilo lilikuwa haliangazii uamuzi wa mahakama ya juu wa tarehe mosi mwezi Septemba.
Tume hiyo iliongezea kwamba ombi hilo sio rufaa dhidi ya uamuzi wa mahakama ya rufaa inayojulikana kama Kesi ya Maina Kiai, ilioamuru kwamba matokeo yatakayotangazwa katika vituo vya kupigia kura ndio matokeo ya mwisho.

Mbowe: Tundu Lissu kutoka hospitali wiki ijayo

Mwenyekiti wa chama cha upinzani Tanzania, Chadema Freeman Mbowe
Image captionMwenyekiti wa chama cha upinzani Tanzania, Chadema Freeman Mbowe
Mbowe amewaambia wanahabari kwamba kwa mujibu wa madaktari, hali ya Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu imeimarika hivyo wakati wowote kuanzia wiki ijayo anaweza kutolewa hospitali.
"Bw Lissu ametolewa katika chumba cha wagonjwa mahututi na kuwekwa katika wodi ya kawaida huku akiwa na uwezo kamili wa kuongea na kutembea kwa kutumia kiti cha magurudumu," alifafanua Mbowe. Hata hivyo, Chadema imesema kuwa, kwa kuhofia usalama wa Lissu, kwa sasa hawatamrudisha nchini Tanzania.
"'Kwa sababu za kiusalama hatutaweza kusema atakwenda wapi lakini itoshe tu kuwaambia kuwa ataanza awamu ya tatu ya matibabu nchi nyingine, sio Tanzania wala sio jirani''
Tundu Lissu alipigwa risasi zaidi ya thelathini na watu ambao mpaka sasa hawafahamiki mwanzoni mwa mwezi jana huko mjini Dodoma alipokuwa akihudhuria vikao vya bunge. Hivi karibuni, ndugu zake Bw Lissu wameitaka serikali kuvishirikisha vyombo vya upelelezi vya kimataifa kama vinavyoshirikishwa katika mambo mengine ili kuongeza ufanisi katika upelelezi huo.
Jeshi la polisi nalo limeomba lipewe nafasi wa kufanya upelelezi.Tundu Lissu yuko nchini Kenya kwa takribani wiki nne sasa kwa ajili ya matibabu.

Takukuru yamtaka Nassari kuacha kuingiza siasa katika taarifa zake


Dar es Salaam. Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Valentino Mlowola amemtahadharisha Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari kuacha kugeuza taarifa anazoziwasilisha kwenye taasisi hiyo kuwa ni za kisiasa.
Mlowola ametoa tahadhari hiyo kwa Nassari leo Jumanne, Oktoba 17, 2017 alipozungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
Amesema endapo Nassari ataendelea kuingiza siasa kwenye suala hilo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.
Mlowola amesema kitendo cha mwanasiasa huyo kuweka hadharani taarifa za uchunguzi ni kinyume cha sheria kwa kuwa kazi hiyo inatakiwa kufanyika kwa siri na Mahakama ndiyo yenye jukumu la kuchukua hatua.
Amesema Takukuru ina wajibu wa kumlinda mtoa taarifa lakini jukumu hilo linakuwa tofauti kwa Nassari ambaye ameamua kujitokeza hadharani.
"Alicholeta Nassari kwetu ni taarifa si ushahidi. Ameleta tumezipokea na tunazifanyia kazi, inashangaza anapozungumza na vyombo vya habari na kutuelekeza namna ya kufanya kazi," amesema.
Mlowola amesema, "Tulishampa angalizo kuwa mambo tunayoongea ni siri lakini mwenzetu inaonekana anafanya siasa kama anavyosema mwenyewe kuwa ataendelea kuleta ushahidi kama series ya Isidingo."
Mkurugenzi mkuu huyo amemtaka Nassari kuacha kukiingiza chombo hicho kwenye siasa ili kifanye kazi kwa uhuru kama sheria inavyoelekeza.
"Nitoe rai kwa Nassari na wengine wote, ukishaleta taarifa kwenye chombo husika kama hiki kiache kifanye kazi. Hakuna sababu ya kukishinikiza au kukiingiza kwenye malumbano ya kisiasa. Ukweli wa mambo utajulikana mahakamani," amesema.

Mbowe atoa maelezo ya kiasi hicho cha matibabu ya Lissu



Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe 
By Ibrahim Yamola, Mwananchi iyamola@mwananchi.co.tz
Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amesema gharama za matibabu ya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu aliyelazwa katika Hospitali ya Nairobi nchini Kenya zimefikia Sh412.7 milioni.
Lissu ambaye ni mwanasheria wa chama hicho, amelazwa hospitalini hapo tangu Septemba 7 aliposhambuliwa na kujeruhiwa kwa risasi akiwa maeneo ya nyumbani kwake Area D mjini Dodoma.
Mbowe akizungumza na waandishi wa habari leo Jumanne, Oktoba 17, 2017 jijini Dar es Salaam, Tanzania amesema gharama ni kubwa, ila anawaomba Watanzania wasichoke kuchangia kwa kuwa Lissu atarudi barabarani.
“Tunaishukuru sana familia ya Lissu, imekuwa na msimamo kama Lissu mwenyewe. Tumefanya kazi na familia na tutaendelea kufanya kazi na familia. Tutakapokwenda katika matibabu ya tatu, tutaiacha kwa familia iwe msemaji wa kwanza, mgonjwa anaweza kuongea na kujitambua,” amesema.
Kuhusu mchanganuo wa michango, Mbowe amesema wabunge wa Chadema wamechanga Sh48.4 milioni.
Amesema wananchi wamechangia Sh24.2 milioni kupitia simu ya Mbunge wa Tarime Mjini (Chadema), Esther Matiko.
“Watu mbalimbali wakiwemo wanachama wa Chadema wamechanga Sh90 milioni kupitia akaunti iliyofunguliwa katika Benki ya CRDB,” amesema.
Mbowe amesema wabunge wote wakiwemo wa Chadema wamechanga Sh43 milioni na kwamba, Watanzania walio nje ya nchi wamechanga kupitia Go fund me Dola 29,000 za Marekani.
Kiongozi huyo wa Chadema amemshukuru Mange Kimambi kwa kufanya kazi kubwa ya kuhamasisha michango.
Mbowe amesema wafanyabiashara wakihamasishwa na Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema wamechanga Dola 18,000.
Amesema wana orodha nzima ya wote waliochangia na amewaomba Watanzania waendelee kuwapigania.

Naibu waziri wa zamani asema amefika kituoni


Dodoma. Aliyekuwa Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Anastazia Wambura ameufananisha utumishi wa umma na chombo cha usafiri ambacho abiria hushuka kituoni baada ya kufika na dereva kuendelea na safari.
“Mheshimiwa waziri, viongozi wenzangu na ndugu zangu watumishi wa wizara, mimi nimefika kituoni, naibu waziri nakukabidhi kijiti endelea na safari, endelea kuwatumikia Watanzania kama ambavyo ilani ya chama tawala inavyoeleza,” amesema Wambura.
Amesema hayo leo Jumanne, Oktoba 17,2017 baada ya mrithi wake Juliana Shonza kuwasili katika ofisi za wizara mjini Dodoma na kupokewa na Waziri wa wizara hiyo, Dk Harrison Mwakyembe, viongozi wa wizara na watumishi wengine.
Wambura amempongeza Shonza kwa kuteuliwa kushika wadhifa huo. Pia, amemshukuru Rais John Magufuli kwa kumuamini na kumpa nafasi ya kuwatumikia Watanzania.
Kwa upande wake, Shonza ameahidi kushirikiana na watendaji wa wizara, wadau na wananchi kwa jumla kusimamia maadili ya Mtanzania.
“Wizara hii ni muhimu kwa kuwa inajenga taswira ya Taifa kupitia sekta zake za habari, utamaduni, sanaa na michezo hivyo nitahakikisha tunashirikiana kwa karibu katika kuwatumikia wananchi,” amesema Shonza.
Amesema atahakikisha maadili bora kwa jamii yanazingatiwa ili kuendelea kujenga Taifa imara kwa kuzingatia mavazi yenye heshima na nyimbo zenye kujenga.
Shonza katika taarifa iliyotolewa na Idara ya Habari (Maelezo) amesema ni wajibu wao wakiwa watumishi wa umma kuhakikisha wanatekeleza ilani ya chama tawala kilichoahidi kuwatumikia Watanzania ili kuhakikisha malengo ya Serikali yanafikiwa kwa wakati.
Waziri Mwakyembe amemuahidi ushirikiano wa hali na mali Shonza katika kuwahudumia wananchi kupitia sekta za habari, utamaduni, sanaa na michezo.

Nassari asema hawezi kukaa kimya kama hatua hazitachukuliwa


Dar es Salaam. Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari amesema kuwa hatokaa kimya endapo haoni hatua zinazochukuliwa.
Nassari amesema hayo leo Jumanne muda mchache baada ya Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Valentino Mlowola kumtaadharisha Nassari kuacha kugeuza taarifa anazoziwasilisha kwenye taasisi hiyo kuwa ni za kisiasa.
Hata hivyo Nassari amesema, “Mlowola inabidi asome sheria ya ‘Whistle blower’ ili nikae kimya lazima nione jitihada zinazofanyika kama hakuna nitaendelea kuongea. Sitokubali kutishwa ili nisiendelee kupeleka ushahidi ninachotaka kuona ni wahusika wanachukuliwa hatua sio madiwani, wahusika wakuu ni mkuu wa wilaya na mkurugenzi,”
Awali akizungumza leo Jumanne asubuhi, Mlowola ametoa tahadhari hiyo kwa Nassari leo Jumanne, Oktoba 17, 2017 alipozungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
Amesema endapo Nassari ataendelea kuingiza siasa kwenye suala hilo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.
Mlowola amesema kitendo cha mwanasiasa huyo kuweka hadharani taarifa za uchunguzi ni kinyume cha sheria kwa kuwa kazi hiyo inatakiwa kufanyika kwa siri na Mahakama ndiyo yenye jukumu la kuchukua hatua.
Amesema Takukuru ina wajibu wa kumlinda mtoa taarifa lakini jukumu hilo linakuwa tofauti kwa Nassari ambaye ameamua kujitokeza hadharani.
"Alicholeta Nassari kwetu ni taarifa si ushahidi. Ameleta tumezipokea na tunazifanyia kazi, inashangaza anapozungumza na vyombo vya habari na kutuelekeza namna ya kufanya kazi," amesema.
Mlowola amesema, "Tulishampa angalizo kuwa mambo tunayoongea ni siri lakini mwenzetu inaonekana anafanya siasa kama anavyosema mwenyewe kuwa ataendelea kuleta ushahidi kama series ya Isidingo."
Mkurugenzi mkuu huyo amemtaka Nassari kuacha kukiingiza chombo hicho kwenye siasa ili kifanye kazi kwa uhuru kama sheria inavyoelekeza.
"Nitoe rai kwa Nassari na wengine wote, ukishaleta taarifa kwenye chombo husika kama hiki kiache kifanye kazi. Hakuna sababu ya kukishinikiza au kukiingiza kwenye malumbano ya kisiasa. Ukweli wa mambo utajulikana mahakamani," amesema.

Takukuru yawahoji madiwani waliojiuzulu Arusha

Diwani wa kata ya Mbuguni wilayani Arumeru
Diwani wa kata ya Mbuguni wilayani Arumeru mkoani Arusha, Ahimidiwe Rico aliyerekodi sauti akishawishiwa ajiuzulu nafasi yake kulia akitoka nje ya ofisi za Takukuru mkoani Arusha mara baada ya kuhojiwa leo pembeni yake ni diwani aliyemsindikiza wa kata ya Nkoanenkoli, Wilson Nanyaro,picha na Moses Mashalla 
Arusha. Maofisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kutoka makao makuu jijini Dar es Salaam, wamewahoji kwa zaidi ya saa sita, madiwani waliojiuzulu Chadema wanaotuhumiwa na Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari kuwa walipewa rushwa.
Waliofika Takukuru ni Catherine Mtui, aliyekuwa diwani wa viti maalumu, Japhet Jackson (aliyekuwa diwani wa Ambuleni) na Bryson Isangya (aliyekuwa diwani wa Maroroni). Baada ya kuhojiwa hawakutaka kuzungumza chochote wakisema wanaacha uchunguzi uendelee.
Pamoja nao, diwani wa Mbuguni, Ahimidiwe Rico anayedaiwa kuwa ndiye alirekodi sauti na picha wakati akishawishiwa na viongozi wa Serikali na wa Halmashauri ya Meru amehojiwa kwa zaidi ya saa tatu leo Jumanne Oktoba 17, 2017.
Rico amesema amewaeleza Takukuru kila kitu ambacho anakifahamu katika sakata hilo, ikiwemo kuwarekodi viongozi ambao walimshawishi kujiuzuru udiwani.
"Msimamo wangu ni kwamba, nachukia rushwa. Nimewaeleza kila kitu na wao waliniuliza kuhusu vifaa nilivyotumia kuwarekodi nikawaambia ni mali ya mbunge, alivitoa nchini Uingereza," amesema.
Rico aliyesindikizwa na diwani wa  Nkwanankore, Wilson Nanyaro amesema  ana imani na Takukuru kwamba watafanya uchunguzi wa kina na kuchukua hatua.

"Nimewaeleza wazi kuwa hata shauri hili likienda mahakamani nipo tayari kwenda kutoa ushahidi na kuthibitisha sauti za watu ambao niliwarekodi," amesema.
Amesema baada ya mahojiano yaliyoanza saa tatu hadi saa sita mchana, maofisa wa Takukuru wamemwambia aondoke na watamuita watakapomuhitaji.
Hakuna ofisa wa Takukuru aliyekuwa tayari kuzungumzia mahojiano hao wakisema wasemaji ni makao makuu ya ofisi hiyo Dar yaliyoko jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na Mwananchi leo Jumanne, mbunge Nassa

Janet Museveni: Mabinti zangu waliolewa wakiwa mabikira


Kampala, Uganda. Mke wa Rais Yoweri Museveni, Janet Museveni amesema kuwa aliwatunza mabinti zake vizuri hadi wanaolewa wakiwa bikira kwa kutumia njia asilia za Kiafrika za kumlea mtoto wa kike.
“Niliwataka mabinti zangu wote kusaini kadi za ‘kusubiri upendo wa kweli’ na walijizuia kufanya ngono hadi usiku wa harusi ambao walionyesha kadi zao kwa wenza wao,” alisema mama Janet na kuongeza kuwa “jambo hili linaweza kufanikishwa hata leo.”
Janet alikuwa akizungumza katika wilaya ya Kyenjojo wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Kike Alhamisi iliyopita.
Aliongeza: “Hivyo ndivyo sisi, hapo zamani, tulilelewa na wazazi wetu, hakukuwa una ukosefu wa maadili kama ilivyo sasa.”
Siku hiyo ilifuatiwa na mjadala uliofanywa na wadau waliokuwa na utayari wa kulinda haki za vijana wa kike.
Mabinti wa mama Janet ni pamoja na Diana aliyeolewa na Geoffrey Kamuntu, Natasha aliyeolewa na Edwin Karugire, na Uvumilivu aliyeolewa na Odrek Rwabwogo.
“Mwanamume awe mkubwa au mdogo, sema hapana na kimbia, mwanamume anaweza kutumia lugha tamu kukushawishi, usimruhusu mwanamume yeyote kukuchezea wakati wewe ni binti mdogo, mwanamume asikuingize kwenye ngono hadi pale utakapoolewa, penzi la kweli husubiri,” Janet alitoa ujumbe huo kuwalenga wasichana

Marekani yataka utulivu baada ya wanajeshi wa Iraq kuingia Kirkuk

Iraqi forces flash a victory sign while driving past an oil production plant near Kirkuk. Photo: 16 October 2017Haki miliki ya pichaAFP/GETTY IMAGES
Image captionWanajeshi wa Iraq wakisherehekea ushindi
Marekani imeomba kuwepo utulivu baada ya wanajeshi wa serikali ya Iraq kuingia mji wa Kirkuk kaskazini mwa nchi hiyo na kutwaa udhibiti wa maeneo muhimu kutoka kwa Wakurdi.
Msemaji wa wizara ya mambo ya ndani Heather Nauert amezitaka pande zote kuzuia makabiliano zaidi.
Wanajeshi wa Iraq walielekea Kirkuk wiki tatu zilizopita, baada ya jimbo la Kurdistan kuandaa kura ya maoni ya uhuru iliyokumbwa na utata.
Lengo lao limekuwa ni kuteka sehemu zilizo chini ya udhibiti wa Wakurdi waliochukua usukani baada ya Islamic State kuondoka eneo hilo.
Wenyeji wa maeneo yaliyo chini ya udhibiti wa Wakurdi ukiwemo mji wa Kirkuk, kwa wingi waliunga mkono kujitenga kutoka kwa Iraq wakati wa kura ya tarehe 25 mwezi Septemba.
Map showing Iraqi Kurdistan and areas controlled by Kurdish forces
Image captionRamani ya maeneo yanayodhibitiwa na vikosi vya kurdi
Licha ya mji wa Kirkuk kuwa nje ya eneo la Kursistan, wapigaji kura wa Kurdistan walio mjini humo waliruhusiwa kushiriki kura hiyo ya uhuru.
Waziri mkuu wa Iraq Haider al-Abadi aliitupilia mbali kura hiyo na kuitaja kuwa iliyo kinyume na katiba.
Huku hayo yakijiri, wapiganaji wanaoungwa mkono na serikali wamechukua udhibiti wa mji wa Sinjaar Kaskazini magharibi mwa mkoa wa Nineveh.
Hatua hiyo katika mji unaodaiwa na wakurdi na pia mamlaka za Iraq, ilifanyika bila ya kuwepo mapigano baada ya wanajeshi wa Wakurdi wa Peshmerga kuondoka eneo hilo.
Iraqi forces near an oil facility in Kirkuk, Iraq (16 October 2017)Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionJeshi la Iraq limedhibiti vituo vya mafuta
Katika taarifa Bi Nauert alisema kuwa Marekani ina wasiwasi kutokana na ripoti za kuendelea mapigano katika mji wa Kirkuk.
Bi Nauert alisema kuwa Marekani ilikuwa ikishirikiana na maafisa kutoka pande zote, kushiriki mazungumzo ikionya kuwa bado kuna kazi kubwa ya kulishinda kundi la Islamic State nchini Iraq.
Mapema Rais Donald Trump alikuwa amesema kuwa maafisa wa Marekani hawapendelei upande wowote.