Tuesday, October 17

Janet Museveni: Mabinti zangu waliolewa wakiwa mabikira


Kampala, Uganda. Mke wa Rais Yoweri Museveni, Janet Museveni amesema kuwa aliwatunza mabinti zake vizuri hadi wanaolewa wakiwa bikira kwa kutumia njia asilia za Kiafrika za kumlea mtoto wa kike.
“Niliwataka mabinti zangu wote kusaini kadi za ‘kusubiri upendo wa kweli’ na walijizuia kufanya ngono hadi usiku wa harusi ambao walionyesha kadi zao kwa wenza wao,” alisema mama Janet na kuongeza kuwa “jambo hili linaweza kufanikishwa hata leo.”
Janet alikuwa akizungumza katika wilaya ya Kyenjojo wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Kike Alhamisi iliyopita.
Aliongeza: “Hivyo ndivyo sisi, hapo zamani, tulilelewa na wazazi wetu, hakukuwa una ukosefu wa maadili kama ilivyo sasa.”
Siku hiyo ilifuatiwa na mjadala uliofanywa na wadau waliokuwa na utayari wa kulinda haki za vijana wa kike.
Mabinti wa mama Janet ni pamoja na Diana aliyeolewa na Geoffrey Kamuntu, Natasha aliyeolewa na Edwin Karugire, na Uvumilivu aliyeolewa na Odrek Rwabwogo.
“Mwanamume awe mkubwa au mdogo, sema hapana na kimbia, mwanamume anaweza kutumia lugha tamu kukushawishi, usimruhusu mwanamume yeyote kukuchezea wakati wewe ni binti mdogo, mwanamume asikuingize kwenye ngono hadi pale utakapoolewa, penzi la kweli husubiri,” Janet alitoa ujumbe huo kuwalenga wasichana

No comments:

Post a Comment