Saturday, March 10

WATOTO WASIORIPOTI MASHULENI WAZAZI WAO KUCHUKULIWA HATUA -SANGA


Halmashauri ya wilaya ya Mkuranga imesema mpaka ifikapo machi 31 mwaka huu, itawachukulia hatua Kali za kisheria wazazi na walezi wote ambao watoto wao wamefaulu na hawajaripoti shuleni mpaka sasa kwa Sababu zisizo na msingi. 

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu Wa wilaya ya Mkuranga wakati akifungua kikao cha bajeti ya mwaka 2018/2019 cha baraza la madiwani kilicho fanyika wilayani humo,na kusema kuwa wanafunzi walioripoti ni 3,439 sawa na asilimia 46 na wanafunzi 217 hawajaripoti mpaka sasa ambao ni sawa na asilimia 5.46.

Aidha amesema mpaka ifikapo march 31 mwaka huu,wazazi na walezi ambao watakuwa hawajatoa taarifa zozote kuhusu sababu za watoto wao kutoripoti shuleni watachukuliwa hatua Kali za kisheria.

Aidha Sanga amewataka madiwani wote  wa wilaya hiyo kushirikiana nae kufuatilia kwa undani suala hilo ili kuhakikisha kuwa wanabaini changamoto zilizopelekea wanafunzi hao kutofika shuleni mpaka sasa."tunachotaka watoto wetu wasome,hatutaki kusukia mtu ameacha shule kwasababu ya kuolewa,wazazi watoe taarifa vinginevyo hatua zitachukuliwa dhidi yao".alisema Sanga.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mkuranga Juma Abeid amesema wamepitisha bajeti ya wilaya ya zaidi ya bilion 47 ya 2018/2019 ambayo imekidhi katika katika sekta zote na kipaumbele chao ni kwa mwaka huu ni elimu,afya na maji.

Abeid amesema elimu imepewa kipaumbele kwa sababu wananchi wengi wameitikia wito wa Rais Dkt John Pombe Magufuli kwa kupeleka watoto wao shule hivyo kusababisha utitiri aa wanafunzi hali inayopelekea uhaba Wa vyumba vya madarasa.

Naye Kaimu Mkurugenzi mtendaji Wa wilaya ya Mkuranga Peter Nambunga amesema wao wamelenga sana kwenye elimu na afya kwa sababu na jiografia ya wilaya hiyo pamoja na miundo kutokuwa rafiki hali inayosababisha Mwananchi kutembea umbali mrefu kufuata elimu na huduma ya afya.

Aidha Nambunga ameongeza kuwa katika harakati za kupunguza changamoto za huduma ya wanampango Wa kutafuta mobile clinic ili kuweza kuvifikia vijiji vya pembezoni kama koma na kwale.
Mwenyekiti Wa Halmashauri ya Mkuranga,Juma Abeid akizungumza na Madiwani wa Wilaya ya Mkuranga katika mkutano wa bajeti ya mwaka 2018/2019.Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii.
Diwani wa kata ya Mwanandege,Adroph Kowero akifafanua jambo katika mkutano huo.
Madiwani wakimsikiliza Mwenyekiti Wa Halmashauri ya Mkuranga,Juma Abeid.

MNEC SALIM ASAS BADO ANAUMIZWA NA USHINDI WA MBUNGE MSIGWA WA MWAKA 2015

MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) MNEC Salim Asas bado anaumizwa na matokeo ya ubunge wa jimbo la Iringa mjini baada ya wapinzani kushinda kwa kishindo mwaka 2015 kwa ni jambo ambalo hakulitegemea.
Akizungumza wakati wa baraza la UWT manispaa  ya Iringa Asas alisema kuwa usaliti uliofanywa katika uchaguzi wa mwaka 2015 umekuwa ukimuumiza hadi sasa na kitendo anafikiri kitadumu moyoni mwake hata kwa miaka kumi kwakuwa bado anakumbuka mara kwa mara.

“Naombeni niongee ukweli kitendo kilichofanywa na wanaCCM wa manispaa ya Iringa katika uchaguzi wa mwaka 2015 kilikuwa kitendo ambacho ni usaliti mkubwa ambao unaumiza sana kichwa changu” alisema Asas

Asas alisema kuwa uchaguzi huo kulikuwa na wanaCCM wengi ambao mchana walikuwa CCM  na usikuwa walikuwa kwa wapinzani hivyo lazima tuondoe usaliti kwenye chama bila hivyo tutaendelea kushindwa kila siku.

“Unakuta rasilimali zilizokuwa zinatolewa na  CCM zote zinatumika kwa wapinzani kuhakikisha wanaiangusha,sasa hicho kitu ndio ambacho kinaniumiza sana kichwa hadi hii leo” alisema Asas.

Asas aliutaka umoja wa wanawake (UWT) manispaa ya Iringa kufanya kazi kwa umoja unatakiwa na kuhakikisha kuwa ccm inakuwa ila na isiyo na makundi ili kufika mwaka wa uchaguzi wanashinda kwa kishindo kwa kutumia umoja wao.
“Nawaombe muutunze umoja huu ambao sasa mnao hadi kipindi cha uchaguzi wowote ule ambao upo mbele yetu na kuhakikisha kuwa tunashinda kila chaguzi kwa kishindo kwa kuwa nyie akina mama ndio huwa mnakula ambazo haziamishiki” alisema Asas
Kwa upande wake mwenyekiti wa UWT manispaa ya Iringa Ashura jongo alimuhakikishia MNEC Salim Asas kuwa kosa lilofanyika mwaka 2015 halitajirudia tena katika chaguzi yoyote ambayo itakuwa inafanyika katika manispaa ya Iringa.
“Ndugu MNEC kwa kweli tumejifunza na tunajutia kitu kilichofanyika mwaka 2015 hivyo tunakuhadi kuwa kwenye umoja wetu wa wanawake Manispaa ya Iringa hakitaa tokea kama kilivyotokea,na tutashinda chaguzi zetu kwa kuwa kila mtu anaumia na kilichotokea mwaka 2015” alisema Jongoo.
“Mheshimiwa MNEC umoja ambao tunao hivi sasa tunatakiwa kuulinda na kuudumisha hadi kipindi cha chaguzi zote na kuhakikisha kuwa ccm inashinda kwa kushinda na kuendelea kuwa ngoja ya chama hicho kama ilivyokuwa hapo awali” alisema Jongoo
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) MNEC Salim Asas  akiwahutubia wajumbe wa baraza kuu la umoja wa wanawake manispaa ya Iringa na kusema kuwabado anaumizwa na matokeo ya ubunge wa jimbo la Iringa mjini baada ya wapinzani kushinda kwa kishindo mwaka 2015 kwa ni kitendo ambacho hakukitegemea.
Mwenyekiti wa umoja wa wanawake UWT manispaa ya Iringa Ashura jongo akimtoa hofu MNEC Salim Asas juu ya kukomba jimbo baada ya kulipoteza kwa kusalitia mwaka 2015 
 Baadhi ya wageni waliokuwa wamealikwa kwenye baraza hilo kwa ajili ya kujifunza na kutoa mapendekezo pale wanapopata nafasi
 Baadhi ya viongozi wa chama cha mapinduzi mkoani Iringa walipokuwa wakimsikiliza kwa umakinimjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) MNEC Salim Asas alipokuwa anatoa ya moyo kuhusu kushindwa katika uchaguzi wa mwaka 2015

TANZANIA YASHIRIKI MAONESHO YA KIMATAIFA YA UTALII ITB BERLIN 2018 NCHINI UJERUMANI

Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Maj. Gen. Gaudence S. Milanzi ameongoza msafara wa Tanzania unaoshiriki katika Maonesho ya Kimataifa ya Utalii ya ITB 2018 yanayoendelea Jijini Berlin nchini Ujerumani.
Lengo la Maonesho hayo ni kutangaza fursa za utalii zilizopo nchini Tanzania katika masoko mbalimbali ya utalii barani Ulaya na duniani kote.Sekta ya utalii inachangia wastani wa asilimia 25 ya fedha zote za kigeni zinazoingia nchini Tanzania na asilimia 17.5 ya pato la Taifa .
Maonesho hayo yalianza tarehe 7 mwezi huu na yanatarajiwa kufikia tamati keshokutwa tarehe 11 Machi, 2018. Ushiriki wa Tanzania katika maonesho hayo umehusisha Sekta ya Umma na Sekta Binafsi.

Washiriki kutoka sekta ya umma ni pamoja na Idara ya Utalii – Wizara ya Maliasili na Utalii, Bodi ya Utalii Tanzania, Shirika la Hifadhi za Taifa, Mamlaka ya Hifadhi Ngorongoro na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania.

Kwa upande wa Sekta Binafsi jumla ya kampuni 60 zimeshiriki maonyesho hayo ikiwemo Kampuni moja inayoshughulika na uratibu wa matukio (Events and Exhibitions management), Kampuni tatu zinazoshughulika na usafiri wa anga, Kampuni ishirini na saba zinazoshughulika na huduma za malazi (hoteli, loji na kambi za utalii), na Kampuni ishirini na tisa za Wakala wa biashara ya kusafirisha watalii.

Pamoja na shughuli za maonyesho hayo, Katibu Mkuu Milanzi amefanya pia mikutano kadhaa na wadau wa utalii na washirika wa maendeleo waliopo nchini Ujerumani.
Picha ya pamoja ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Maj. Gen. Gaudence S. Milanzi (wa tano kushoto) na baadhi ya washiriki wa maonesho ya Kimataifa ya Utalii ya ITB 2018 yanayoendelea Jijini Berlin nchini Ujerumani.
 Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Maj. Gen. Gaudence Milanzi (wa pili kulia) akijadili jambo na wadau walioshiriki maonesho hayo kutoka Tanzania. Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Utalii TANAPA, Ibrahim Mussa.


WANAOTAKA KUUZA FIGO ILI WAPATE FEDHA SASA WAPIGWA MARUFUKU



*Rais Chama cha Madaktari bingwa wa figo atoa sababu, atoa ushauri kwa Watanzania

Na Said Mwishehe, Globu ya Jamii

CHAMA cha Madaktari Bingwa wa magonjwa ya figo Tanzania kimepiga marufuku biashara  ya uuzaji figo nchini na kueleza kuwa huo si utaratibu mzuri kwa madhara yake ni makubwa.

Pia kimeelezea hali ya ugonjwa wa figo nchini na kwamba kwa mwaka huu wanatarajia kupandikiza figo kwa wagonjwa 50 huku kikielezea jitihada za Serikali katika kuhamasisha wananchi kuzuia ugonjwa figo.

Hayo yamesemwa jijini Dar es Salaam na Rais wa Chama cha Madaktari bingwa ya figo Tanzania Dk.Onesmo Kisanga wakati anazungumza na Michuzi Blogu,ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Siku ya Figo Duniani ambayo huadhimishwa kila Alhamis ya pili ya kila Machi.Siku hiyo hutumika kutoa elimu kuhusu ugonjwa wa figo na hatua ambazo wanataalamu wanachukua ili kukabiliana nao.

Akizungumzia kuhusu tabia ya watu kuuza figo ili kupata fedha,Dk.Kisanga ambaye pia ni Daktari bingwa wa magonjwa ya figo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili amesema kuwa kwa sasa wamepiga marufuku biashara ya watu kuuza figo kwani ina madhara makubwa.

“Nikiri tunapokea maombi mengi pale Muhimbili kutoka kwa watu ambao wanataka kuuza figo ili wapate fedha.Nieleze tu hii biashara ya kuuza figo haitakiwi kabisa nchini Tanzania.Hata Chama cha madaktari bingwa duniani nacho kimepiga marufuku biashara ya figo,"amesema Dk.Kisanga.

Amesema kikubwa ambacho wanakifanya ni kuendelea kutoa elimu kwa wale ambao wanataka kuuza figo kuwa hairuhusiwi na kubwa zaidi ikifanywa ni biashara maana yake wale wasiokuwa na uwezo watashindwa kununua matokeo yake watokosa matibabu.


WATU 50 KUPANDAKIZWA FIGO MWAKA HUU

Wakati huo huo Dk.Kisanga amesema mwaka huu wanatarajia kupandikiza figo kwa wagonjwa 50 na huo ndio mkakati wao na kufafanua kuwa mwezi huu wanatarajia kupandikiza figo kwa wagonjwa watano na mwezi unaokuna watapandikiza kwa wagonjwa saba.Serikali ya Awamu ya Tano imeamua kutoa kipaumbele kwenye sekta ya afya na hivyo kufanya idadi ya madaktari bingwa katika kutibu magonjwa ya figo kuongezeka.

"Kwa mara ya kwanza Tanzania tulipandikiza figo mwaka 2017 na tumefanikiwa kwa kiasi kikubwa.Aliyepandikizwa figo yupo salama na aliyetoa figo naye yupo salama,"amesema Dk.Kisanga.


DALILI KWA MGONJWA WA FIGO

Dk.Kisanga amesema ni ngumu kubaini dalili za mgonjwa wa figo kwa haraka na wakati mwingine hadi unapoanza kuona dalili maana yake figo itakuwa imeharibika kwa asilimia 70 hadi 90.Ndio maana wanashauri Watanzania kujenga utamaduni wa kupima afya zao mara kwa mara.Hiyo itasaidia madaktari bingwa wa magonjwa ya figo kubaini mapema na kuzuia ugonjwa.
Ametaja baadhi ya dalili za ugonjwa huo ni mwili kuchoka sana, kuvimba miguu, mikono, sura na tumbo na wakati mwingine kupata shida wakati wa kujisaidia haja ndogo.

AZUNGUMZIA ULAJI VYAKULA

Dk.Kisanga amesema kuna baadhi ya vyakula ambavyo mlaji anatakiwa kuwa makini navyo na kufafanua kuwa vyakula vyenye mafuta mengi vinaweza kusababisha matatizo ya figo.Hivyo chakula lazima kiwe bora na mlaji ale kwa kiasia.Kula kupita kiasi kuna madhara yake yakiwamo ya kuongezeka uzito, kupata shinikizo la damu na sukari na ugonjwa wa figo.

Pia amesema chakula kisiwe na chumvi nyingi kwani nayo huchangia ugonjwa figo na kufafanua wanapopima ili kubaini kama kuna ugonjwa wa figo pia wanapima na mkojo kwani hautakiwi kuwa na protini ambayo nayo ni hatari na si dalili nzuri kwani inaashiria ugonjwa wa figo.Amehimiza watu kufanya mazoezi ili kuweka miili yao katika afya njema.
Pia ameomba watu kutokuwa na tabia ya kupenda kula dawa aina ya Dicropa mara kwa mara kwani moja ya madhara yake ni kusababisha ugonjwa figo.

JAJI MKUU: KIINGEREZA KINAZUIA WANANCHI KUPATA HAKI MAHAKAMANI




JAJI Mkuu, Profesa Ibrahimu Juma, amesema lugha ya Kiingereza inayotumika mahakamani ni moja ya kikwazo kinachowazuia wananchi kupata haki kwa kuwa wengi wanatumia Kiswahili.
Kauli hiyo aliitoa mjini hapa jana katika kikao cha kazi kinachojumuisha watendaji na wataalamu wa mahakama wanaotathmini utekelezaji wa mpango mkakati wa miaka mitano (2015-2020) pamoja na utekelezaji wa mradi wa maboresho ya utoaji huduma za mahakama na changamoto ambazo WB ilizibaini na kuzitaja kuwa ndizo zilizosababisha ikubali kushirikiana na Serikali katika mradi wa kuifadhili Mahakama ya Tanzania.
“Andiko la WB lilirejea utafiti uliogundua asilimia 60 ya watumiaji wa mahakama, walisema tovuti za mahakama hazitoi taarifa za kutosha kuhusu mashauri yao.
“Tovuti zetu bado hazitumii lugha ya Kiswahili, jana nilitembelea tovuti ya mahakama nikakuta nyaraka tano kuhusu suala muhimu la mirathi.
“Nyaraka hizo zimewekwa katika lugha ya Kiingereza, lugha ambayo inawatenga watumiaji wengi wa mahakama lakini pia imelenga matumizi ya wanasheria zaidi ya wananchi. Tovuti zetu ziongee lugha ya wananchi na ziwe zenye msaada kwa mwananchi wa kawaida,” alisema Profesa Juma.
Pia aliwataka watendaji wa mahakama kuacha kuficha upungufu na makosa waliyonayo kwa sababu WB huangalia wananchi wa kawaida, wafanyabiashara na wanyonge katika jamii.
Aliwataka watendaji hao kuhakikisha wanafanya tathmini ya wazi kuhusu makosa na upungufu waliofanya kwa miaka miwili na nusu ya uhai wa mpango mkakati wa mwaka 2015/2016 na 2019/2020.
“Tusipokubali makosa hatutapata nafasi ya kujirekebisha na tutarudia makosa hayo hayo wakati wabia wetu Benki ya Dunia na Serikali wanatutathmini pia,” alisema Profesa Juma na kuongeza:
“Hapa ni lazima tutambue WB itafanya tathmini yake kama mbia. Hapana shaka, itarejea itatathmini kwa kiasi gani zile changamoto zilizozitaja katika andiko lake la mradi zinatekelezwa.
“Baadhi yake zinagusa upatikanaji taarifa kwa wananchi, zinaweza kuchukuliwa kuwa suala dogo. Lakini kwa mwananchi wa kawaida upatikanaji wa taarifa ni nyenzo muhimu katika kumuwezesha kupata haki yake mahakamani.”
Aliyataja maandiko yaliyo katika mradi kuwa WB iligusia wananchi na wafanyabiashara ambao hukosa taarifa za kimahakama kuwaongoza kufungua mashauri, ada stahiki na kutopata taarifa namna ya kupata rekodi za mashauri.
Pia alisema hawajui sekta mbalimbali za kisheria zinahusikaje katika uendeshaji mashauri na utoaji wa haki kwa sababu andiko lilitarajia kila mahakama kuwa na miongozo kwa watumiaji kuwaongoza wanapotafuta huduma za mahakama.
Alisema WB ilionyesha kutambua upungufu wa stadi na utaalamu umepunguza uwezo wa mahakama kutoka haki kwa weledi na wakati, ambapo andiko lilibaini mfumo wa upimaji na utendaji unahusu watumishi wasio mahakimu au majaji na hakuna upimaji kwa majaji, wasajili na mahakimu.
“Kutokuwapo kwa mfumo wa kupima utendaji wa majaji, mahakimu na wasajili kutaulizwa na WB katika tathmini yake,” alisema Jaji Mkuu Prof. Juma.
Aliyataja maeneo mengine yaliyoonyesha wasiwasi wa WB na kuhitajika kufanyiwa kazi ni pamoja na matumizi madogo ya suluhu nje ya mahakama na upatanishi, gharama za huduma za mawakili hazidhibitiwi kikamilifu.
Pia kuwapo kwa ukubwa wa gharama za madalali kunakofikia hadi asilimia 22 ya thamani ya mali inayobishaniwa mahakamani.
Awali, Mtendaji Mkuu wa Mahakama, Hussein Katanga, alisema zipo changamoto zinazoikabili mahakama ikiwamo upangaji na uendeshaji wa kesi hususani mahakama za chini hatua inayohitaji kutiliwa mkazo.

Jeshi la Syria laigawa Ghouta Mashariki

Vikosi vya serikali ya Syria vimeugawa mji wa Douma, ambao ni mkubwa katika ngome inayoshikiliwa na waasi Ghouta Mashariki kutoka kwenye eneo jengine lililobakia la mji huo.

Syrien Angriffe auf Ost-Ghuta (Reuters/B. Khabieh)
Jeshi la Syria leo limedhibiti zaidi ya nusu ya Ghouta Mashariki kutokana na mashambulizi ya wiki tatu, ikiwemo barabara inayoiunganisha miji ya Douma na Harasta miji miwili mikubwa Ghouta Mashariki na kuligawa eneo hilo katika sehemu tatu, huku Douma ikiwekwa na maeneo yanayouzingira, Harasta ukiwa upande wa magharibi na maeneo yaliyobaki yakielekezwa upande wa kusini.
Shirika linalofuatilia haki za binaadamu nchini Syria lenye makao yake nchini Uingereza limesema kuwa jeshi la Syria pia limeudhibiti mji wa Misraba wakati likisonga mbele, huku barabara kati ya Douma na Harasta zikiwa ndani ya eneo ambalo mashambulizi yanaweza kufanywa.
Shirika la habari la Ufaransa, AFP limeripoti kuwa mashambulizi ya anga pamoja na makombora yamekuwa yakiendelea leo Jumamosi.
Syrien Krieg - Ostghuta bei Damaskus | Kinder (Reuters/B. Khabieh)
Watoto wakiwa Ghouta Mashariki
Makundi mawili makuu ya waasi wenye itikadi kali za Kiislamu ya Jaish al-Islam na Failaq al-Rahman bado yamebakia Ghouta Mashariki, pamoja na idadi ndogo ya wapiganaji kutoka kundi la Nusra Front ambalo lilikuwa tawi la mtandao wa kigaidi wa Al-Qaeda nchini Syria.
Februari 18, majeshi ya serikali yalianzisha mashambulizi Ghouta Mashariki, eneo la mwisho linalodhibitiwa na waasi karibu na mji mkuu wa Syria, Damascus na sasa yanaudhibiti zaidi ya nusu ya mji huo. Kwa mujibu wa shirika hilo, mashambulizi hayo yamesababisha raia wapatao 1,000 kuuawa, zaidi ya robo ya idadi hiyo wakiwa watoto. Mamia ya watu wamejeruhiwa.
Zaidi ya watu 400,000 wamezingirwa
Umoja wa Mataifa unakadiria kuwa kiasi ya watu 400,000 wamezingirwa katika eneo hilo ambalo limekuwa chini ya udhibiti wa waasi tangu 2013. Licha ya Umoja wa Mataifa kutoa wito wa kusitishwa kwa muda mapigano nchini Syria, serikali ya Rais Bashar al-Assad imeendelea na operesheni yake kwa lengo la kuwaondoa wapiganaji wenye itikadi kali kwenye eneo hilo.
Wakati huo huo, Rais wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan leo ameahidi kuongeza mashambulizi ya Uturuki nchini Syria dhidi ya wanamgambo wa Kikurdi hadi kwenye miji muhimu ya mpakani inayodhibitiwa na wanamgambo hao hadi kwenye eneo la mpaka na Iraq.
Kwa mujibu wa shirika linalofuatilia haki za binaadamu nchini Syria, vikosi vya Uturuki vimesonga mbele na kufika kwenye viunga vya mji wa Afrin baada ya operesheni ya wiki kadhaa dhidi ya kundi la wanamgambo wa Kikurdi nchini Syria, YPG. Uturuki na makundi washirika ya waasi yanasonga mbele kwenye mji huo kutoka mashariki huku vikifanya mashambulizi ya mabomu.
Syrien CIRC-Hilfskonvoi in der belagerten Stadt Douma (Reuters/B. Khabieh)
Msafara wa ICRC katika mji wa Douma
Januari 20, mwaka huu Uturuki ilianzisha operesheni yake ya kuwaondoa wapiganaji wa YPG, kutoka mji wa Afrin ulioko kaskazini mwa Syria.
Jana usiku idadi ndogo ya wapiganaji wa Nusra Front waliruhusiwa kuondoka Ghouta Mashariki na familia zao chini ya mkataba maalum. Aidha, Kamati ya Kimataifa ya Shirika la Msalaba Mwekundu duniani, ICRC iliripoti kuwa malori 13 yaliyojaa msaada wa kuwafikia kiasi ya watu 12,000 Ghouta Mashariki, kabla ya kulazimika kuondoka baada ya kuanza tena kwa mashambulizi.

Waandishi wa habari, demokrasia hatarini - Ripoti

Mwandishi wa habari na bloga Daphne Caruana Galizia alipokuwa akiwasili mahakamani nchini Malta April 27, 2017.
Maelfu ya waandamanaji mara nyingine tena wamejitokeza Ijumaa katika mitaa ya miji ya nchi ya Slovakia kufuatia mauaji ya mwandishi wa habari za uchunguzi na mchumba wake wiki mbili zilizopita.
Waandamanaji hao wanataka kuwepo uchaguzi mpya na wanaelekeza hasira zao dhidi ya serikali.
“Ni lazima serikali iaachie madaraka. Ni kwamba watawala hao wameshikana pamoja, wote hao wanataka kuendelea kutawala katika nafasi zao,” mmoja wa waandamanaji Miroslav Sputsova aliuambia umati uliokusanyika siku ya Ijumaa jioni huko mji wa Bratislava.
Mauaji hayo ya mwandishi Jan Kuciak na mchumba wake, Martina Kusnirova yaliofanyika Februari 25, 2018 yameitikisa nchi ya Slovakia na nchi za Ulaya, ambako wasiwasi umeongezeka juu ya kuminywa uhuru wa habari na ukosefu wa usalama baada ya matukio kadhaa ya vitendo vya kuwadhuru wanahabari kutokea miezi ya hivi karibuni.
Washukiwa watatu wametuhumiwa kuhusika na mauaji ya Galizia. Lakini mara nyingi, haki imekuwa ikipindishwa, imesema ripoti..
Sheria zimeendelea kuwa kandamizi ulimwenguni na hali ya siasa kuwa tata baada ya vikundi vyenye pesa kuvidhibiti vyombo vya habari, wakizuia ujumbe na wakati mwengine kulazimisha ujumbe potofu kuwafikia wananchi, wanasema wachambuzi wa siasa huko Ulaya.
Na pengine juu ya yote hayo, wanadhani upo usaliti wa fikra nzima ya wananchi kulindwa na sheria na uhuru wa mahakama, Waandishi wa Habari wasio na mipaka wametahadharisha hilo katika ripoti yao.
Wameongeza kuwa katika baadhi ya maeneo ya Ulaya, na nchi nyingine ulimwenguni vyombo vya habari huru - na hivyo demokrasia yenyewe - iko hatarini
Wiki hii ujumbe wa wabunge wa Umoja wa Ulaya walitembelea nchi ya Slovakia katika shughuli maalum ya kutafuta ukweli juu ya hali ya demokrasia.
Umoja wa Ulaya umeeleza kuongezeka kwa wasiwasi juu ya suala zima la uhuru wa habari. Watu wanaohamasisha uhuru wa habari wanasema uminyaji wa demokrasia na vitisho vinaongezeka.
Serikali kandamizi zinaibuka kuanzia Uturuki na Urusi, na hivi sasa wimbi hilo linaelekea Slovakia, Jamhuri ya Czech ambako hivi sasa rais ameiita hadharani silaha feki ya Kalashnikov na kusema ‘hii ni kwa ajili ya waandishi wa habari.’
Pia ukandamizaji huo uko Bulgaria, na iliyokuwa Yugoslavia ya zamani,” amesema makamu rais wa Jumuiya ya Waandishi wa Habari Ulaya, William Horsley.
“Katika nchi zote hizo kandamizi, uvunjifu wa amani, kukosekana ulinzi wa raia, na ukandamizaji unaofanywa na vyombo vya serikali vinaendelea kila siku,” Horsley ameiambia VOA.
Mwezi Octoba 2017, Mwandishi wa habari wa nchi ya Maltese Daphne Caruana Galizia aliuwawa kwa kutegewa bomu katika gari lake. Mwanamke huyu alikuwa akichunguza ufisadi na alikuwa anakabiliwa na kesi kadhaa za kuwakashifu watu, moja wapo iliokuwa imefunguliwa na Waziri Mkuu Joseph Muscat.

Rais Kenyatta na kiongozi wa upinzani Odinga, waahidi kuwaunganisha Wakenya

Raila Odinga (kulia) amekuwa akikataa kumtambua Uhuru Kenyatta kama rais halali wa KenyaHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionRaila Odinga (kulia) amekuwa akikataa kumtambua Uhuru Kenyatta kama rais halali wa Kenya
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta amekutana na kiongozi wa muungano wa upinzani nchini humo Raila Odinga katika afisi yake Jumba la Harambee, Nairobi.
Wawili hao wamekubaliana kuundwe mpango wa pamoja wa kuangazia utekelezaji wa malengo ya pamoja ya viongozi hao wawili, ambao utazinduliwa rasmi karibuni
Balozi Martin Kimani ataongoza kuundwa kwa mpango huo upande wa Rais Kenyatta naye mshauri wa Bw Odinga Paul Mwangi atawakilisha Bw Odinga, kwa mujibu wa taarifa ya pamoja iliyotiwa saini na Bw Kenyatta na Bw Odinga baada ya mkutano huo.
Mkutano huo ulifanyika muda mfupi kabla ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Rex Tillerson kuwasili nchini humo kwa ziara ya siku nne.
Bw Tillerson, akihutubu baadaye amewasifu wawili hao kwa kukutana.
Hata hivyo, alieleza wasiwasi wake kuhusu kukandamizwa kwa kidemokrasia nchini Kenya, akitaja wka mfano kufungiwa kwa baadhi ya vituo vya runinga nchini humo hivi majuzi.
Marekani imekuwa ikihimiza kufanyika kwa mazungumzo na mashauriano kutatua mzozo wa kisiasa uliokumba taifa hilo baada ya uchaguzi uliojaa utata mwaka jana.
Naibu Rais William Ruto ameonekana kufurahishwa na mkutano huo.
Bw Mungai Kihanya naye amelinganisha mkutano wao wa leo na tangazo kwamba Rais wa Marekani Donald Trump atakutana na kiongozi wa Korea Kaskazini hivi karibuni.
Bw Odinga alitangulia kuhutubia taifa moja kwa moja na baadaye Bw Kenyatta akatoa hotuba yake.
Bw Kenyatta amesema wamekubaliana na Bw Odinga kwamba taifa la Kenya ni muhimu kuliko mtu binafsi na kwamba lazima viongozi washirikiane.
Rais huyo amesema siku za usoni za Kenya haziwezi kuongozwa na uchaguzi ujao bali "uthabiti wa taifa."
"Demokrasia si mwisho wa kila kitu. Ni shughuli na nia ya wananchi lazima iongoze."
"Tumekubaliana tutaleta pamoja wananchi na kujadiliana kuhusu matatizo yanayoathiri taifa letu na wananchi, na kuunda taifa lenye umoja na lililo imara ambapo hakuna araia anayehisi ametengwa."
"Huu ni mwanzo mpya kwa taifa letu."
"Tunaweza kutofautiana lakini kusalia tukiwa tumeungana kama Wakenya."
Raila na Uhuru
Bw Odinga amesema kwa muda mrefu Kenya imeangazia kubadilisha taasisi na miaka saba iliyopita katiba mpya ilianza kutekelezwa.
"Sasa lazima tuwe na ujasiri wa kukubali kwamba hilo halijafanikiwa. Bado hatujabadilisha mengine," amesema Bw Odinga.
"Ndugu yangu na mimi tumekutana pamoja leo na kusema yamefikia kikomo. Tumekataa kuwa watu ambao chini yake Kenya imekuwa taifa lililofeli."
Bw Tillerson atawasili nchini Kenya baadaye leoHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionBw Tillerson atawasili nchini Kenya baadaye leo
Bw Odinga amesema wamekubaliana kufanikisha mabadiliko yatakayofanikiwa mageuzi nchini humo, na pia kukomesha kulaumiana.
Amewataka Wakenya waunge mkono mpango wa viongozi hao wawili.
"Tumesafiri mbali sana kiasi kwamba hatuwezi kurudi tena bandarini. Isitoshe, hatuwezi kufika tunakoenda bila kufanya mabadiliko la sivyo tutazama baharini," amesema Bw Odinga.
"Tumekuja pamoja na ndugu yangu Kenyatta, tumeongea kwa kirefu na kukubaliana kwamba tunataka kuunganisha Kenya iwe taifa moja. Mgawanyiko ambao umekuwepo tangu uhuru utakwisha hapa na sisi. Tutembee pamoja," amesema Bw Odinga.

Matukio makuu mzozo wa kisiasa Kenya

  • 8 Agosti, uchaguzi mkuu wafanyika ambapo Bw Uhuru Kenyatta alitangazwa mshindi
  • 1 Septemba, Mahakama ya Juu yabatilisha ushindi wa Bw Kenyatta katika kesi iliyowasilishwa na Bw Raila Odinga, na kuagiza uchaguzi urudiwe
  • 26 Oktoba, uchaguzi wa marudio wafanyika, huku upinzani ukisusia. Bw Kenyatta atangazwa mshindi.
  • 30 Januari, Bw Odinga ala kiapo kuwa 'Rais wa Wananchi' na kusisitiza kwamba hatambui Bw Kenyatta kama rais halali wa Kenya
  • 9 Machi, Bw Kenyatta akutana na Bw Odinga katika afisi ya rais Jumba la Harambee, wawili hao waahidi kushirikiana kuwaunganisha Wakenya.

Kushinikiza mageuzi

Bw Odinga alisusia kushiriki uchaguzi wa marudio uliofanyika 26 Oktoba mwaka jana akishinikiza mageuzi yafanywe kwanza katika Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
Uchaguzi huo ulitokana na hatua ya Mahakama ya Juu kufuta matokeo ya uchaguzi wa tarehe 8 Agosti ikisema ulikuwa na kasoro nyingi.
Mahakama hiyo ilikuwa inatoa uamuzi katika kesi iliyokuwa imewasilishwa na Bw Odinga kupinga matokeo hayo.
Bw Kenyatta alishinda uchaguzi huo wa marudio kwa kura 7.5 milioni ambazo ni sawa na asilimia 98 ya kura zilizopigwa.
Idadi ya waliojitokeza ilikuwa ni asilimia 38.84 ya waliokuwa wamejiandikisha kushiriki uchaguzi huo.
Uchaguzi ulitatizika sana katika maeneo yenye wafuasi wengi wa upinzani. Katika majimbo manne magharibi mwa Kenya ambayo ni ngome ya Bw Odinga, uchaguzi uliahirishwa kwa siku kadha na baadaye haukufanyika.