Wednesday, June 7

Mghwira atemwa uenyekiti ACT Wazalendo







Kaimu Kiongozi wa ACT, Samson Mwingamba
Kaimu Kiongozi wa ACT, Samson Mwingamba akizungumza na wanahabari leo Jijini Dar es salaam Kuhusu maamuzi hayo 
Chama cha ACT Wazalendo kimmevua uongozi aliyekuwa mwenyekiti wake, Anna Mgwhira ambaye ameteuliwa na Rais John Magufuli kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro.
Chama hicho kimefikia hatua hiyo kwa kuzingatia ibara ya 17 ya katiba yake ambayo inatamka kuwa kiongozi wa chama atakoma kuendelea na madaraka yake iwapo atashindwa kutekeleza majukumu yake.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatano, Kaimu Kiongozi wa ACT, Samson Mwingamba alisema kamati ya uongozi wa ACT ulikutana leo lengo kuu ni kutafakari lililotokea kuona namna gani Mgwhira anaweza kutimiza majukumu yake kama Mwenyekiti na Mkuu wa Mkoa.
“Kama chama baada ya kutafakari kwa kina na baada ya mashauriano baina yake na viongozi kutumia katiba ya chama anakoma kuwa kiongozi kwa kuwa kutakuwa na mgongano wa majukumu, maslahi hivyo anakoma kuwa mwenyekiti,” alisema Mwigamba.
Mwigamba alisema kamati ya chama imemchagua Yeremia Maganja kuwa  Kaimu Mwenyekiti na kamati ilimpongeza Rais Magufuli kwa kumteua Mgwhira.
Hata hivyo, Mwigamba alisema Mghwira bado ataendelea kuwa mwanachama halali wa chama hicho.

WATOTO WENYE MATATIZO KUPATIWA MATIBABU NCHINI

WATOTO wenye matatizo ya usikivu watapata matibabu ya kupandikizwa vifaa vya usikivu hapa nchini katika Hospitali ya taifa ya Muhimbili badala ya kwenda nje ya nchi kwa matibabu kama ilivyokuwa awali.

Hayo yamesemwa na Waziri wa afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati alipozindua huduma hiyo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili leo jijini Dar es salaam.

“Serikali haitapeleka mgonjwa mwenye matatizo ya kusikia nje ya nchi kwa ajili ya kupandikizwa vifaa vya kusikia na badala yake atatibiwa nchini ili kupunguza rufaa za wagonjwa wan je ya nchi” alisema Mh. Ummy.

Aidha Waziri Ummy amesisitiza juu ya umuhimu wakujiunga na mfuko wa Afya wa Jamii wa NHIF ili kupata fursa ya kutibiwa kwa gharama ndogo zaidi, huku akisisitiza kuwa wananchi wote watakaokuwa na kadi ya NHIF wataweza kupata matibabu ya upandikizaji wa kifaa cha kusikia bure kupata huduma hii.

Mbali na hayo Mh. Ummy ameahidi kuwa Serikali kupitia Wizara yake ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kuunga mkono kwa kuisaidia hospitali ya Muhimbili ili kuendelea kufanikisha upasuaji wa Watoto hivyo kupunguza gharama inayopata Serikali kusafirisha Watoto hao nje ya nchi pindi wapatapo matatizo hayo.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Muhimbili Lawlence Mseru amsisitiza kuwa moja kati ya mipango ya Hospitali ya Muhimbili ni kuhakikisha kuwa wanapunguza idadi ya wagonjwa wanaokwenda kutibiwa nje ya nchi kila mara jambo linaloigharimu Serikali pesa nyingi. 

Aidha Dkt. Mseru aliongeza kuwa licha ya kufanikisha tukio hilo la Kihistoria wanaomba Serikali kupitia Wizara ya Afya kusaidia kuboresha Wodi za Wagonjwa mahututi, ununuzi wa Vifaa tiba, kuongeza vyumba vya upasuaji jambo litalopunguza msongamano wa shughuli za hospitali pia kuongeza Wataalamu waendao nje ya nchi kwaajili ya mafunzo ili kuendeleza huduma katika nchi yetu jambo litakalosaidia kuwa na Wataalamu wengi hivyo kuweza kufanikisha huduma kwa wagonjwa wengi zaidi.

Nae Prof. Sunil Narayan Dutt kutoka Hospitali ya Apollo nchini India ameipongeza Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa jitihada inayoonesha hasa katika kutetea haki za watoto.

Kwa upande Bi. Hilda Bohela ambae ni mzazi wa Apulie Bohela aliyepata huduma hiyo nchini amewasihi wazazi wenzie kuwapeleka watoto kufanyiwa uchunguzi pindi waonapo hali isiyokuwa yakawaida kwa watoto wao na kuachana na mila potofu jambo linalopelekea watoto wengi kupata ulemavu .



waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watot, ummy Mwalimu (katikati) akizungumza leo jijini Dar es Salaam kwenye uzinduzi wa Upasuaji wa Upandikizaji Kifaa cha Usikivu (Cochlear-Implant) kulishoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Profesa Lawrence Museru na kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini Hospitali ya Taifa ya Muhimbili(MNH), Profesa Charles Majinge.
waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, ummy Mwalimu akiwajulia hali wagonjwa waliolazwa katika hospitali ya Taifa Muhimbili leo jijini Dar es Salaam.
waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, ummy Mwalimu akiwasili katika hospitali ya Taifa Muhimbili leo jijini Dar es Salaam. 
waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, ummy Mwalimu akiwa katika picha ya pomoja na watendaji wa hospitali ya Taifa Muhimbili leo jijini Dar es Salaam.Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii.