Sunday, November 5

Vigogo 11 wakamatwa Saudi Arabia

Serikali ya Saudi Arabia imewakamata vigogo kadhaa wakiwemo wana wa kifalme, mawaziri na wafanyabiashara wakubwa katika kile inachosema ni vita dhidi ya ufisadi vinavyoongozwa na mrithi wa kiti cha ufalme.

König Salman Bin Abdul Aziz Al Saud und Kronprinz Mohammed Bin Salman Al Saud (picture-alliance/abaca/B. Press)
Bilionea mkubwa, Al-Waleed bin Talal, ni miongoni mwa wana wa kifalme 11 waliokamatwa usiku wa jana (Jumamosi, 4 Novemba 2017), mara tu baada ya kamisheni mpya ya kupambana na ufisadi inayoongozwa na Mwanamfalme Mohammed bin Salman kutangazwa kwa amri ya kifalme.
Katika tukio jengine, mkuu wa Kikosi cha Ulinzi cha Taifa, ambaye aliwahi kuwa mmoja wa waliotazamiwa kurithi kiti cha ufalme, na pia mkuu wa jeshi la pwani na waziri wa uchumi waliondolewa kwenye nafasi zao, ikiwa sehemu ya wimbi la ufutwaji kazi katika Ufalme wa Saudia.
Kituo cha televisheni cha Al Arabiya kinachomilikiwa na Saudi Arabia kiliripoti kwamba wana wa kifalme hao, mawaziri wanne wa sasa serikalini na mawaziri wengine kadhaa wa zamani walikamatwa, huku kamisheni hiyo ikianza uchunguzi juu ya visa vya zamani kama vile mafuriko yaliyoukumba mji wa Jeddah mwaka 2009.
Shirika la habari linalomilikiwa pia na serikali ya Saudia, SPA, lilisema lengo la kamisheni hiyo ni "kulinda fedha za umma, kuwaadhibu mafisadi na wale wanaoutumia vibaya nafasi zao."
Hisa zaporomoka
Billionär Al-Waleed Bin Talal bin Abdulaziz al Saud (Getty Images/AFP/I. S. Kodikara)
Bilionea Al-Waleed Bin Talal bin Abdulaziz al Saud
Hisa kwenye kampuni ya Kingdom Holding, ambazo zinamilikiwa kwa asilimia 95 na Mwanamfalme Al-Waleed, zilishuka kwa asilimia 9.9 wakati maduka ya hisa yalipofunguliwa asubuhi ya Jumapili, kukiwa tayari na taarifa za kukamatwa kwake.
Ofisi yake haikupatikana mara moja kuzungumzia suala hili.
"Kwa msako huu, ufalme unaanza enzi mpya na sera ya uwazi, usafi na uwajibikaji," alisema Waziri wa Fedha wa Saudi Arabia, Mohammed al-Jadaan, kwa mujibu wa shirika la habari la SPA.
"Maamuzi haya magumu yatalinda mazingira ya uwekezaji na kuinua imani kwenye utawala wa sheria."
Baraza kuu la maulamaa la nchi hiyo liliisifia pia hatua hiyo kuwa ni "muhimu", kauli ambayo inachukuliwa kama baraka za kidini kwa msako huo. 
Chanzo kimoja kutoka usafiri wa anga kililiambia shirika la habari la AFP kwamba vikosi vya usalama vimezizuwia ndege binafsi kuruka kutoka viwanja vyote vya ndege vya nchi hiyo, yumkini ikikusudiwa kuwazuwia vigogo kukimbia nchi.
Hatua hizi za kushitukiza zinakuja katika wakati ambapo taifa hilo lenye uhafidhina wa kiwango cha juu likianzisha mageuzi makubwa kwenye masuala ya kijamii na kiuchumi, kufuatia kutangazwa kwa Mwanamfalme Mohammed kuwa mrithi rasmi wa nafasi ya baba yake, Mfalme Salman, ambaye alimuondoa kwenye mstari wa urithi binami yake, Mwanamfalme Mohammed bin Nayyaf, aliyemuweka kwenye kizuizi cha ndani tangu mwezi Juni.

Wasaudia wafurahia kukamatwa wanawafalme kwa ajili ya rushwa

Mwanamfalme mrithi wa Saudi Arabia Mohammed bin Salman akihudhuria mkutano wa uwekezaji mjini Riyadh, Saudi Arabia, Oct. 24, 2017.
Wasaudia wamepokea kwa furaha tanagzo la Jumamosi la kukamatwa kwa wanawafalme 11 mawaziri wanne wa utawala wa hivi sasa na mawaziri kumi wa zamani katika kampeni mpya ya kupambana na ulaji rushwa na ufisadi katika taifa hilo la kifalme.
Tukio hilo ni la kwanza la aina yake kwa wanawafalme, matajiri na watu mashuhuri kukamatwa kwa kosa lolote na inachukuliwa ni sehemu ya mageuzi makubwa yanaoongozwa na mwanamfalme Mohammed bin Salman, na babake Mfalme Salman.
Akizungumza na Sauti ya Amerika mwandishi habari wa Redio ya Saudia Abdullah Muawiya anasema miongoni mwa walokamatwa ni tajiri mwenye ushawishi mkubwa mwana mfalme Miteb bin Abdullah bin Abdulaziz, ambae alikua waziri wa jeshi la ulinzi wa taifa na mtoto mkubwa wa mfalme aliyefariki miaka miwili ilyiopita.
FILE - Mwanamflame Miteb bin Abdul Aziz,kijana wa mfalme wa zamani Abdullah bin Abdul Aziz al-Saud.
FILE - Mwanamflame Miteb bin Abdul Aziz,kijana wa mfalme wa zamani Abdullah bin Abdul Aziz al-Saud.
Tajiri mwengine mashuhuri anaesemekana ndiye bilionea mkuu wa Mashariki ya Kati ni mwanamfalme Alwaleed bin Talal, mwenye makampuni makubwa katika nchi za Ulaya Magharibi na Asia na mwenye mradi wa kutaka kujenga jengo refu kabisa duniani huko Jeddah.
Vyombo vya habari vya serikali havijaeleza lolote kuhusu kukamatwa kwa maafisa hao. Hata hivyo kituo cha televisheni kinachomilikiwa na Saudi Arabia Al-Arabiya imetangaza kwamba watu hao wanashikiliwa ndani ya hoteli ya fahari ya Ritz Carlton mjini Riyadh.
Mwandishi Muawiya anasema tukio hili linazidisha mvutano wa ndani uliyopo katika familia ya kifalme huko Saudia lakini anasema inachukuliwa kama mbinu ya kuhakikisha mwanamfalme Mohammed bin Saman anachukua uwongozi bila ya matatizo yeyote lakini anasema pia ni hatua ya ujasiri mkubwa kuwakamata watu hao.

Marekani: Vikosi vya nchi kavu ndivyo vinaweza kuivamia Korea Kaskazini

Marekani: Vikosi vya nchi kavu ndivyo vinaweza kuivamia Korea KaskaziniHaki miliki ya pichaAFP
Image captionMarekani: Vikosi vya nchi kavu ndivyo vinaweza kuivamia Korea Kaskazini
Maafisa kutoka makao makuu ya ulinzi nchini Marekani, wanaamini kuwa uvamizi wa kutumia vikosi vya Marekani vya nchi kavu, itakua njia pekee ya kupata na kudhibiti maeneo ya nyuklia ya Korea Kaskazini.
Ripoti hiyo ilikuja kwenye barua iliyotolea na makao makuu ya ulinzi nchini Marekani, kujibu ombi la bunge la kutaka kufahamu kuhusu maafa yanayoweza kutokea ikiwa mzozo utalipuka na Korea Kaskazini.
Pia barua hiyo pia ilionya kuwa Korea Kaskazini anaweza kugeuka na kuwa eneo lenye silaha za kibaolojia na kemikali wakati wa vita.

Kamati Kuu ACT-Wazalendo kutuma wawakilishi polisi


Chama cha ACT-Wazalendo kimesema Kamati Kuu ya chama hicho haitakwenda kuripoti polisi kama ilivyoagizwa bali itawakilishwa na mwenyekiti na kiongozi wa chama hicho.
Novemba 2,2017 chama hicho kimesema kilipokea wito kutoka kwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) ukiwataka wajumbe wa Kamati Kuu ya ACT -Wazalendo kesho Novemba 6,2017 wafike Kituo cha Makosa ya Fedha kilichopo Kamata, Kariakoo wilayani Ilala.
Alipopigiwa simu, Msemaji wa Jeshi la Polisi, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Barnabas Mwakalukwa kueleza kama anafahamu kuhusu wito huo, alitaka apigiwe simu DCI, Robert Boaz ambaye hakupatikana.
Wito huo ulitolewa siku tatu baada ya Kiongozi wa chama hicho, Zitto Kabwe kuhojiwa Oktoba 31,2017 kuhusu masuala ya uchumi na takwimu.
Akizungumza leo Jumapili Novemba 5,2017 jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa chama hicho, Yeremia Maganja amesema kamati kuu ina wajumbe wengi walio kwenye mikoa tofauti.
"Ni vigumu kuwakusanya wajumbe wote na kuwapeleka polisi, hivyo tutawawakilisha mimi na Kiongozi wa chama (Zitto Kabwe)," amesema.
Maganja amehoji iweje kamati kuu iitwe kwenda kuhojiwa polisi. Amesema kamati kuu ni chombo cha kitaifa ambacho hakiwezi kwenda polisi kikiwa na wajumbe wote bali wawakilishi.
Amesema Kamati Kuu ni chombo cha kitaifa cha chama chenye mamlaka ya kufanya uamuzi kwa mujibu wa Katiba ya ACT-Wazalendo, hivyo polisi haina madaraka ya kushughulikia wala kuingilia uamuzi halali wa chombo hicho.
Akizungumzia hilo, Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mawasiliano kwa Umma wa chama hicho, Ado Shaibu amesema polisi watafute muda sahihi wa kuwahoji viongozi wa chama hicho lakini si kipindi hiki cha kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani utakaofanyika Novemba 26,2017 katika kata 43 nchini.
“Tulitakiwa kuelekeza nguvu zetu kwenye kampeni za uchaguzi mdogo badala ya mahojiano na polisi,” amesema.

Wananchi wa Lindi na Ruangwa watakiwa kujitokeza kwenye Maulid


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewataka wananchi wa Lindi na Ruangwa kutumia  fursa zilizopo ili kufanikisha maandalizi ya sherehe za Maulid na Baraza la Maulid Kitaifa mwaka huu.
Ametoa wito huo leo  Novemba 5 wakati akizungumza na viongozi wa dini ya Kiislamu wa Mkoa wa Lindi na wilaya ya Ruangwa mara baada ya kuwasili wilayani humo kwa ziara ya siku moja.
Waziri Mkuu amesema sherehe hizo zitafanyika Desemba mosi kwa mkesha wa Maulid na kufuatiwa na Baraza la Maulid litakalofanyika Desemba 2, saa 3 asubuhi kwenye viwanja vya shule ya msingi Likangale.
Amewataka  wananchi wa Ruangwa waharakishe kujenga nyumba za kulala wageni na sehemu za kula ili waweze kupokea ugeni huo mkubwa wa kitaifa. “Kila mmoja anayeona hapo kuna fursa, ni lazima aitumie vizuri,” amesisitiza.
“Kwa niaba ya wana-Ruangwa, tunamshukuru Mufti na Baraza la Maulamaa kwa kuridhia sherehe hizi zifanyike kitaifa hapa wilayani kwetu. Nitumie fursa hii kuwaomba Waislamu wote tuungane katika sherehe hizi licha ya tofauti za madhehebu yetu tuliyonayo,” amesema.
Amesema  uamuzi huo wa Bakwata  ulitangazwa kwenye Baraza la Maulid lililofanyika Singida, mwaka jana ya kwamba wameamua kuadhimisha sherehe hizo kwenye ngazi ya wilaya badala ya kuwa inafanyika makao makuu kila mwaka.
Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwaarifu viongozi hao kwamba maandalizi yanaendelea na kwamba vifaa mbalimbali kama mchele, vitoweo, unga wa ngano, sukari, maji, juisi, mahema, mikeka na mazulia vimekwishapatikana.
 “Ninaomba Kamati ya Uhamasishaji iifanye kazi hii kwa kutambua kuwa jambo hili si la kwenu peke yenu, bali linaungwa mkono na Serikali, na hii ni kwa sababu Serikali yenu inafanya kazi kwa karibu sana na viongozi wa dini,” amesema.
Amesema misingi ya amani katika nchi hii imejengwa na mahubiri ya viongozi wa dini.
Mwenyekiti wa Kamati ya Uhamasishaji, Sheikh Ali Mohammed Mtopa amesema Ruagwa iko tayari na imepokea wito huo wa kitaifa. “Tunakuhakikishia wewe Waziri Mkuu pamoja na wawakilishi wa Mufti waliopo hapa kwamba tumepokea hiyo heshima,” amesema.
Naye Mkurugenzi wa Itifaki kutoka Bakwata Makao Makuu na Msimamizi wa Malidi za Kitaifa, Sheikh Mohammad Nassir ambaye amesema wana Ruangwa  na  wana Lindi wanalo jukumu la kuhamasisha watu washiriki sherehe hizo.
 Waziri Mkuu anatembelea vijiji vya jimboni mwake ambako atahutubia wananchi.

UVCCM wadai Uchaguzi 2020 utakuwa mwepesi kwa Rais Magufuli


Tanga. Jumuiya ya vijana ya Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) imesema uchaguzi mkuu  wa mwaka 2020 utakuwa mwepesi kwa CCM kwa kuwa kazi iliyofanywa na Rais John Magufuli  inapendwa na wananchi wengi.
Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa ,Shaka Hamdu Shaka amesema hayo leo Novemba 5  jijini hapa wakati wa maadhimisho ya tathmini ya utendaji kazi wa Rais John Magufuli kwa kipindi cha miaka miwili tangu alipochaguliwa kushika wadhifa huo.
Amesema utendaji kazi uliofanywa na Rais John Magufuli katika kipindi cha miaka miwili haujawahi kufanywa na watangulizi wake wote jambo ambalo linaifanya CCM ijivunie kuwa itashinda kiti cha Urais, majimbo na kata nyingi zilizo chini ya upinzani hivi sasa vitarejeshwa.
“Ndani ya miaka miwili ya utendaji kazi wa Magufuli yametokea mabadiliko makubwa katika sekta ya kiuchumi, kijamii na kisiasa ambayo yamewezesha wananchi kujenga imani kubwa dhidi yake na huo ndiyo mtaji mkubwa kwa CCM” amesema Shaka.
Amesema  kutokana na utendaji kazi wa Rais Magufuli, viongozi ambao hawakuwa wasafi, wameanza kujiengua wenyewe ndani ya CCM na kwamba hata vyama wanavyokimbilia vina ugomvi wa ndani kwa ndani ambao unafukuta.
“Huko jirani kuna ugomvi mkubwa unafukuta ndani kwa ndani, hata kiongozi aliwahi kuwa Waziri Mkuu kwa miaka miwili anatamani kurejea CCM anashindwa kupata mlango wa kuingilia” amesema Shaka katika mkutano huo ulioandaliwa na UVCCM Wilaya ya Tanga.
Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Thobias Mwilapwa katika taarifa yake ya tathmini ya utendaji kazi wa Rais Magufuli kwa kipindi cha miaka miwili amesema amewezesha kujengwa kwa bomba la mafuta na kiwanda kikubwa kwa nchi za Afrika Mashariki  cha saruji  ambacho ujenzi wake unatarajiwa kuzinduliwa hivi karibuni.

“Agosti 5 mwaka huu Tanga iliandika historia ya viwanda kwa kupokea Marais John Magufuli na Yoweri Museveni waliozindua ujenzi wa bomba la mafuta, lakini Rais wetu atakuja tena hivi karibuni kuzindua ujenzi wa kiwanda kikubwa kwa nchi za Afrika Mashariki cha saruji”amesema  Mwilapwa.
Katibu wa CCM Mkoa wa Tanga, Allan Kingazi amesema uchaguzi wa chama hicho na jumuiya zake katika ngazi za kuanzia mashina hadi Wilaya tisa zilizopo umekamilika huku kukiwa na rufaa tatu za kuonyesha kutokubaliana.
Amesema rufaa hizo ni chache na zinaashiria kwamba chaguzi hizo ziliendeshwa kwa kufuatwa taratibu jambo linaloashiria kuwa hata uchaguzi wa ngazi ya mkoa utakufanyika kwa amani.

Bodi ya mikopo yatoa orodha mpya ya wanafunzi 7,901


Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HELSB) imetoa orodha ya awamu ya tatu ya wanafunzi 7,901 wa mwaka wa kwanza watakaopata mikopo.
Taarifa iliyowekwa kwenye tovuti ya bodi na kuthibitishwa na Meneja Mawasiliano wa HELSB, Omega Ngole imesema hadi sasa wanafunzi wa mwaka wa kwanza waliopata mikopo ni 29,578. Bodi ilisema jumla ya wanafunzi 30,000 watapata mikopo hiyo.
Katika awamu ya kwanza wanafunzi 10,196 wa mwaka wa kwanza walipata mikopo na awamu ya pili wanafunzi 11,481 walipata.
Ngole akizungumza na Mwananchi leo Jumapili Novemba 5,2017 amesema orodha ya wanafunzi waliopata mikopo inapatikana www.heslb.go.tz.
Amesema bado bodi inaendelea kuchambua majina ya wanafunzi wengine walioomba na taarifa zitatolewa baadaye.

Mali yenye thamani Sh 81.98 milion yakamatwa Namanga


 Mamlaka  ya Mapato Tanzania (TRA), kituo cha forodha Namanga mpakani mwa Kenya na Tanzania, kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama, wamekamata mali zenye thamani Sh 81.98  milioni, zilizokuwa zinaingizwa nchini kwa njia za magendo zikiwepo simu za mkononi 1155.
Kuanzia Januari hadi  Septemba bidhaa zilizokamatwa  zilikua na thamani ya sh 132.2 milioni, ambapo baada ya kutozwa  kodi zimepatikana kiasi cha Sh milioni 56.8 milioni
Iwato amesema ,  kodi ambazo Serikali itapata kwa simu hizo ni Sh  40.03 milioni, endapo mmiliki wake atazikomboa kabla ya siku 21 lakini zikikaa zaidi ya siku hizo gharama zitaongezeka pia na baada ya siku 90 zitapigwa mnada.
Meneja msaidizi wa  TRA Namanga, Edwin Iwato amesema  pamoja na simu hizo bidhaa nyingine walizokamata ni pamoja na katoni za vipodozi, dawa za binadamu na mifugo, maziwa ya paketi pamoja na mafuta ya kupikia.
Meneja huyo amesema,  katika operesheni iliyofanyika Octoba pekee pia wamekamata magari 10 yaliyohusika kusafirisha bidhaa hizo na kufanikiwa kuokoa kiasi Sh 43.3 milioni, ambazo wafanyabiashara hao walikua wakikwepa kuzilipa na kuamua kupitisha bidhaa zao kwa njia za magendo.
Akizungumzia operesheni hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Longido Daniel Chongolo ametoa onyo kwa wafanyabiashara kuacha kutumia njia za panya kukwepa kodi kwani kutokana na udhibiti uliopo hivi sasa wataendelea kupata hasara kwa mizigo yao kukamatwa.
‘’Natambua wafanyabiashara wengi wanakopa fedha ili kuboresha biashara zao lakini kama  wanataka kupiga hatua wasifanye biashara za magendo ambazo zitawafilisi na kuwafanya wateseke kulipa mikopo yao kwani hivi sasa udhibiti katika mpaka huo wa Namanga ni mkubwa’’ amesema 
Mkaguzi wa Mamlaka ya chakula na dawa(TFDA) katika mpaka wa Namanga, Elia Nyaura amesema miongoni mwa bidhaa zilizokamatwa hazijasajiliwa hapa nchini na nyingine hata hazifahamiki ni bidhaa za aina gani na zimetengenezwa wapi hivyo kushindwa hata kuthibitisha ubora wake.
Amesema kwa bidhaa hizo ambazo zimekiuka hata taratibu za awali za kuingiza hapa nchini hawawajibiki hata kuzipeleka kwa mkemia kuzipima na kutoa wito kwa wafanya biashara kuwa makini na kufuata taratibu pindi wanapotaka kuagiza bidhaa kutoka nje.
Mpaka wa Namanga ni miongoni mwa mipaka ambayo inatumiwa na wafanyabiashara wengi kuingiza nchini na kusafirisha nje ya nchi bidhaa mbalimbali.

Waliomshambulia mgombea udiwani kufikishwa mahakamani


Wafuasi 12 wa Chadema waliokamatwa juzi usiku Kwa kosa la kumshambulia mgombea wa udiwani wa kata ya Muriet, Francis Mbise wanatarajia kufikishwa mahakamani kesho.
Wafuasi hao akiwemo Kaimu Katibu wa Chadema wilayani Arusha, Innocent Kisanyage  walishikiliwa juzi na polisi eneo la FFU Kwa Morombo wakidaiwa kumshambulia mgombea huyo sehemu mbalimbali za mwili wake.
Mbali na polisi kuwashikilia wafuasi hao pia gari la matangazo linalotumika katika mikutano mbalimbali ya kampeni lilishikiliwa.
Akizungumza na waandishi wa habari Leo Novemba 5 Kamanda Polisi mkoani Arusha (RPC), Charles Mkumbo amesema kwamba wafuasi hao wote 12 watafikishwa mahakamani kesho.
Hata hivyo, Kamanda Mkumbo alipoulizwa kuhusu gari la matangazo lililoshikiliwa siku ya tukio hakuweza kukiri au kukataa endapo wameliachia gari hilo na kufafanua kwamba wao hawana shida na gari hilo.
"Sisi tumekamata watu na hatuna shida na gari la matangazo kwani tumekamata watu au gari" amesema Mkumbo

Serikali yajivunia mambo 10 miaka miwili ya Magufuli


Utawala wa Rais John Magufuli umebainisha mambo 10 yaliyofanyika katika kipindi cha miaka miwili tangu ulipoingia madarakani.
Rais Magufuli aliapishwa kuwa Rais wa Serikali ya Awamu ya Tano Novemba 5,2015 akichukua nafasi iliyoachwa na Rais Jakaya Kikwete aliyehudumu kwa miaka 10 kuanzia 2005-2015.
Akitoa tathimini ya utawala huo leo Jumapili Novemba 5,2017 jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo) ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali, Dk Hassan Abbasi amesema ndani ya miaka miwili mengi yamefanyika ambayo ameyagawa katika maeneo 10.
Mosi, Dk Abbasi amesema uwajibikaji wa watumishi wa umma na wananchi kwa jumla umekuwa mkubwa kwa kuwa kumekuwepo na ari ya kufanya kazi.
Pili, amesema ni msukumo ambao Serikali imeweka katika ukusanyaji wa kodi na kinachopatikana kinatumika ipasavyo.
"Zaidi ya Sh236 bilioni ziliokolewa kutoka kwa walipa kodi zilizokuwa zinawalipa watumishi hewa, tumeondoa watumishi wenye vyeti feki. Zaidi ya Sh142 bilioni nazo zimeokolewa kutoka kwa watumishi walioghushi vyeti na zote zimeelekezwa kutatua kero za wananchi," amesema Dk Abbasi.
Tatu, amesema vita ya ufisadi imekuwa kubwa na imesaidia kuleta mageuzi na fedha ambazo zimekuwa zikiokolewa kutokana na vita hiyo zinaelekezwa kwa wananchi kupitia miradi ya maendeleo.
"Kuna Mahakama ya mafisadi imeanzishwa, kesi zake zinaanzia ngazi ya chini na mpaka sasa kuna kesi tatu, mbili ziko Dar es Salaam na moja iko Mtwara na zingine 107 ziko ngazi za chini zinashughulikiwa," amesema.
Nne, amesema, "Serikali inavyopigania rasilimali za Taifa. Vita katika eneo la madini tumefanya kupitia upya mikataba na kubwa tumejitambua kama Taifa na sasa wawekezaji wanajua Tanzania ukienda lazima uheshimu sheria."
Tano, Dk Abbasi amesema uamuzi mgumu lakini makini uliofanywa na Serikali ingawa wapo waliopinga na kueleza haiwezekani, lakini imewezekana.
"Watumishi kutokwenda nje ya nchi, kati ya mwaka 2014/15, Sh216 bilioni zilitumika lakini kwa miaka miwili hii ni Sh25 bilioni pekee ndizo zimetumika. Mimi nimesafiri mara mbili tu," amesema akizungumzia moja ya uamuzi huo.
Amezungumzia azma ya Serikali kuhamia Dodoma akisema imefanikiwa kwa sehemu kubwa na tayari Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa yupo Dodoma. Amesema mwaka huu Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan atahamia na mwakani atakuwa ni Rais Magufuli.
Sita, ametaja ni azma ya nchi kujitegemea akisema wananchi wanafanya kazi ili kutekeleza hilo.Amesema ukusanyaji mapato umeongezeka kutoka Sh9.9 trilioni hadi Sh14 kwa mwaka.
Saba, amesema miradi mikubwa inatekelezwa kama vile ujenzi wa reli ya kisasa na uboreshaji wa shirika la ndege, akisema ununuzi wa ndege umefanyika na  hadi Julai,2018 zitakuwa zimewasili nchini.
Nane, amesema Serikali imeongeza bajeti katika maeneo muhimu ya sekta za afya, elimu bure na miundombinu ya barabara.
"Kumekuwepo na upatikanaji wa dawa katika hospitali zetu ukilinganisha na awali, hii inasaidiwa na mkakati wa Serikali wa kununua dawa moja kwa moja kwa wazalishaji na bajeti ya Wizara ya Afya imeongezeka kutoka Sh30 bilioni hadi Sh261 bilioni, yote haya ni mafanikio ya miaka miwili," amesema.
Tisa, Dk Abbasi amesema Rais Magufuli amekuwa akiahidi na kutekeleza.
Kumi, amesema suala la Tanzania ya viwanda licha ya kueleza ni gumu lakini ni lazima nchi ielekee huko.

Mvua kubwa kuendelea kunyesha nchini


Mamlaka ya hali ya hewa Tanzania imetoa tahadhari ya mvua kubwa katika baadhi ya mikoa kuanzia saa 3:00 usiku wa leo.
Kupitia utabiri wa hali ya hewa wa saa 24 zijazo baadhi ya mikoa inatarajia kuathirika na  vipindi vifupi vya mvua kubwa.
Baadhi ya maeneo katika mikoa ya Kagera, Geita, Mara, Mwanza, Shinyanga, Simiyu, Kigoma, Tabora, Katavi na Rukwa imeombwa kuchukua tahadhari ya mvua hizo.
Kupitia matazamio, mvua hizo zinaonekana kuendelea hadi Novemba 7 katika Ukanda wa ziwa victoria na Magharibi mwa nchi.

Aliyekuwa kiongozi wa Catalonia ajisalimisha kwa polisi

Catalonia's sacked former president Carles Puigdemont arrives to speak to journalists at the Press Club in Brussels, Belgium, on 31 OctoberHaki miliki ya pichaAFP
Image captionCarles Puigdemont
Aliyekuwa kiongozi wa Catalonia Carles Puigdemont na waliokuwa washauri wake wanne wamejisalimisha kwa polisi nchini Ubelgiji, kwa mujibu wa msemaji wa mkuu wa mshtaka.
Alisema kuwa jaji ataamua Jumatatu ikiwa atatekeleza waranti wa kukamatwa uliotolewa na jaji nchini Uhispania siku ya Ijumaa.
Bw Puigdemont alikimbia kwenda Ubelgiji baada ya ya Madrid kuchukua udhibiti kamili wa Catalonia kufuatia kura ya maoni ya uhuru.
Amesema kuwa atarudi nchini Uhispania ikiwa atahakikishiwa kupata hukumu iliyo ya haki.
Yeye pamoja na washirika wake wanne wanatafutwa kwa mashtaka ya uasi, uhaini na matumizi mabaya ya pesa za umma kufuatia kura ya maoni ambayo mahakama ya Uhispania iliitanga kuwa iliyo kinyume na sheria.
Wiki iliyopita waziri mkuu wa Uhispania Mariano Rajoy alitangaza udhibiti maalum kwa Catalonia, ambapo alivunja bunge la eneo hilo na kuitisha uchaguzi wa mapema.
Washirika wenegine wa Bw, Puigdemont walio kuzuizini ni pamoja na Meritxell Serret (waziri wa zamani wa kiliimo), Antoni Comín (Waziri wa zanai wa afya),Lluís Puig (waziri wa zmania wa utamaduni) na Clara Ponsatí (waziri wa zamnai wa elimu).
Catalan former officials Meritxell Serret (former agriculture minister), Antoni Comín (former health minister), Lluís Puig (former culture minister), and Clara Ponsatí (former education minister)Haki miliki ya pichaEPA
Image captionKutoka kulia: Meritxell Serret, Antoni Comín, Lluís Puig na Clara Ponsatí wamejisalimisha

Mtu aliyeundia ndege juu ya paa la nyumba yake India

Indian pilot Captain Amol Shivaji Yadav poses beside his self- constructed TAC-003 aircraft at The India Aviation 2016 airshow at Begumpet Airport in Hyderabad on March 16, 2016. Yadav, a pilot with Jet Airways, has manufactured the aircraft which has been certified by Hindustan Aeronautics Limited (HAL), at his home in the western Indian city of Mumbai. The fifth edition of India Aviation, a five day event scheduled to run from March 16-20, more than 200 exhibitors from 12 countries.Haki miliki ya pichaAFP
Image captionNdege ya Amol Yadav iliwekwa kwenye maonyesho mwezi mwaka uliopita
Miaka saba iliyopita Amol Yadav alitangaza kwa familia yake na marafiki kuwa angejenga ndege kwenye paa la nyumba yao katika mji wa Mumbai India.
Familia na marafiki waliokua wamepigwa na butwa walimuuliza rubani huyo ni vipi angeweza kuishukisha ndege ikikamilika
"Kwa uhakika sijui," aliwajibu.
Bw Yadav ni rubani wa ndege za kutumia injini mbili.
Walijikakamua kupandisha vifaa vya kuijengea ndege hiyo hadi paa la nyumba ya familia la ghorofa tano, ikiwemo injini iliyonunuliwa kutoka ng'ambo ya zaidi ya kilo 180.
Plane built on the roofHaki miliki ya pichaCOURTESY: AMOL YADAV
Image captionIlipokuwa ikijengwa juu ya paa la nyumba
Mwezi Februari mwaka uliopita, ndege hiyo ya injini moja yenye nafasi ya watu 6 ilikuwa imekamilika.
Kulingana na Bwa Yadavm, ndege hiyo ndiyo ya kwanza kujengewa nyumbani nchini India.
Anasema kuwa injini hiyo ina nguvu za kuiwezesha ndege hiyo kupaa umbali wa futi 13,000 na tanki lake linaweza kubeba mafuta ya kuiwezesha ndege hiyo kusafiri umbali wa kilomita 2000 kwa kasi ya kilomita 342 kwa saa.
Serikali ilikuwa imeandaa maonyesho ya vifaa vilivyotengenezwa chini India mji Mumbai.
Car with planeHaki miliki ya pichaCOURTESY: AMOL YADAV
Image captionIkipelekwa kufanyiwa majaribio
Wakati Yadav aliomba ruhusa kutoka kwa waandalizi kuonyesha ndege yake, walikataa wakisema kuwa hakukuwa na nafasi ya kutosha. Ilibidi ndugu wake wang'ang'a kutafuta nasafi.
"Kwa hivyo tuliamua kuobomoa ndege hiyo ili tuishukishe kwa sehemu tofauti na tuipeleke kwa maonyesho kwa lazima na kuionyeha kwa dunia, Bw Yadav alisema.
Waliibomoa ndege na kutenganisha injini, mkia na mabawa na kuishukisha kwa kutumia kreni.
Sehemu hizo ziliwekwa kwenye lori na kusafirishwa huku sehemu nyingine ikivurutwa na gari ndogo umbali wa kilomita 25.
Plane at Mumbai airportHaki miliki ya pichaANUSHREE FADNAVIS/INDUS IMAGES
Image captionNdege hiyo kwa sasa imeegeshwa katika uwanja wa ndege ya Mumbai
Waliruhusiwa kuingia kwa maonyesho ambapo yeye na mafundi wake waliiunganisha ndege hiyo kwa muda wa saa tatu.
Wakati maonyesho yalianza ndege hiyo iliwavutia watu wengi.
Gazeti moja liliandika taarifa hiyo hali iliyochangia wageni wengi kufika akiwemo waziri wa safari za ndege wa India na wafanyabiashara.
Bwana Yadav sasa anasema kuwa yuko tayari kujenga ndege ya kwanza kabisa kujengwa India.
Wawekezaji wameonyesha moyo wa kuwekeza na serikali ya BJP imeahidi kumpa ekari 157 za ardhi za kujenga kiwanda cha kuunda ndege za kubeba abiria 19.
Amol Yadav with his new plane prototypeHaki miliki ya pichaANSUHREE FADNAVIS/INDUS IMAGES
Image captionBw Yadav saa anajenga ndege yaabiria 19 juu ya paa la nyumba