Sunday, July 9

WAZIRI DKT. MPANGO AHIMIZA UCHUMI WA VIWANDA KATIKA MAONESHO YA SABASABA


 Afisa Mwandamizi wa Idara ya Bajeti wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Adam Msumule akitoa elimu ya Bajeti kwa wananchi waliotembelea katika banda la Wizara hiyo katika maonesho ya Sabasaba Jijini Dar es salaam.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kulia) akipeana mkono na Balozi wa China nchini Tanzania Dkt. LU Youqing, walipokutana katika viwanja vya Maonesho ya 41 ya Kimataifa ya Biashara (sabasaba), Jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango (Mb) (kulia) akitoa maelekezo kwa wafanyakazi wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) kuhusu namna ya kuongeza kasi ya utoaji elimu kwa umma kuhusu umuhimu wa kukata bima ili kujikinga na majanga, alipotembelea Banda la Wizara ya Fedha na Mipango lilipo katika viwanja vya maonesho ya 41 ya Kimataifa ya Biashara (sabasaba), Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika hilo Bw. Sam Kamanga.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kulia) akisikiliza maelezo ya Mkurugenzi wa uendeshaji wa Wakala wa Huduma ya Ununuzi Serikalini (GPSA), Naftal Sigwejo baada ya kuulizwa kuhusu ubora wa baadhi ya bidhaa zinazotolewa Serikalini baada ya kutembelea Banda la Wizara ya Fedha na Mipango katika Maonesho ya 41 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) Jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kulia) akimpongeza Mzazi wa kijana Msuya Mageta (katikati) aliyejiunga na Mfuko wa Pensheni wa PPF kupitia mpango wa Wote Scheme katika Banda la Wizara ya Fedha na Mipango kwenye Maonesho ya 41 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba), Jijini Dar es salaam.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (wa saba kulia) akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Mfuko wa Pensheni wa PPF baada ya kutembela Banda la Wizara hiyo katika Maonesho ya Sabasaba Jijini Dar es salaam.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (wa pili kulia) akiwa tayari kupokea fomu ya kujiunga kupitia mfumo wa uchangiaji wa hiari kupitia Mfuko wa Pensheni wa PSPF kutoka kwa Msanii Mrisho Mpoto baada ya kutembelea Banda la Wizara hiyo katika Maonesho ya 41 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba), Jijini Dar es salaam.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kulia) akipata maelezo kutoka Mfuko wa Pensheni wa GEPF kuhusu huduma na mchango wa mfuko huo katika maendeleo ya viwanda, alipotembelea Banda la Wizara hiyo katika Maonesho ya Sabasaba Jijini Dar es salaam.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kulia) akipata maelezo kutoka  Banda la Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kuhusu njia ya kisasa ya ufugaji Samaki alipotembelea Banda hilo katika Maonesho ya Sabasaba jijini Dar es salaam.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kulia) akimpongeza mtumishi wa Suma JKT baada ya kutoa maelezo ya mtambo wa kuvuta maji katika viwanja vya maonesho ya Sabasaba Jijini Dar es salaam.

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-WFM)

NDOTO YA MWALIMU YATIMIA, LUGHA YA KISWAHILI LULU YA AFRIKA


Na Judith Mhina - MAELEZO

Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Rais wa Kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni muasisi aliyeenzi lugha adhimu na tamu ya Kiswahili na anastahili tuzo maalum kwa kutambua umuhimu wa lugha  hiyo katika kuleta umoja, mshikamano, na maendeleo barani Afrika.

Mwalimu kwa kutambua umuhimu wa lugha ya Kiswahili, alianza kuweka mfumo wa matumizi ya lugha hiyo katika utendaji wa serikali, jamii nzima ya Tanzania na Umoja wa Afrika. Aidha, sera za Tanzania za kushiriki katika kupigania Uhuru wa nchi kadhaa za Afrika na uwepo wa wakimbizi nchini kwa idadi kubwa imewezesha lugha hii kuvuka mipaka na kuenea kote kusini mwa Afrika.

Mwalimu amepata wapiganaji mahiri wa lugha ya Kiswahili ambao wapo wengi, lakini kwa uchache makala yangu itaangazia viongozi yaani, Rais mstaafu wa Awamu ya Pili, Mzee Ali Hassan Mwinyi, na Rais mstaafu wa Msumbiji Joachim Chissano, Marais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni, Rwanda, Paul Kagame, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Joseph Kabila na Jemedari wa kuenzi lugha ya Kiswahili anayeifanya lugha hii kuwa Lulu, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli. 

Mtakubaliana nami mchango wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi katika kutumia lugha ya Kiswahili fasaha, katika shughuli zote za Serikali na za kijamii zilisukuma mwamko wa gurudumu la kiswahili kusonga mbele haswa kwa wale wanaodhani lugha za kigeni ni bora kuliko lugha yao.

Mwinyi, alipata ushirikiano wa matumizi ya lugha ya Kiswahili kutoka kwa Marais walio wengi wa Afrika Mashariki ambao kwa njia moja au nyingine walikaa Tanzania wakati wa kupigania uhuru wa nchi zao au kama wakimbizi wakati wa machafuko katika nchi husika.

Rais Mstaafu wa Msumbiji, Mhesimiwa Joachim Arbeto Chisano ni kati ya wapigania uhuru ambao waliishi nchini Tanzania kwa miaka kadhaa na kufanikiwa kufahamu Kiswahili, alithibitisha hili alipohutubia Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Umoja wa Afrika kwa Kiswahili kwa mara ya kwanza alipokuwa akifunga mkutano huo na kumaliza muda wake wa kuwa mwenyekiti wa Umoja huo Julai 2004 jijini Addis Ababa, Ethiopia.

Amini usiamini huu ukawa ni mwanzo wa lugha za kiafrika kutumika katika mkutano mkubwa wa viongozi wa Umoja wa Afrika yaani Kiswahili ambapo Mwalimu Nyerere alilitamani siku zote kwa kusema: “Sio kama lugha za kigeni ni nzuri kuliko za kwetu bali ukoloni mamboleo ndio umetufikisha hapa”

Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni ambaye ameishi na kusoma Tanzania, anafahamu lugha ya Kiswahili na mara zote anapokuwa Tanzania mara nyingi hutumia lugha adhimu na pendwa ya Kiswahili kuonyesha ubora na umuhimu wa lugha hiyo katika masuala ya serikali, siasa, kijamii, udugu na katika ujirani mwema.

Rais Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, pia ni miongni mwa wasomi na walioishi Tanzania kwa miaka mingi, ambapo Kiswahili chake hakina tofauti na Mtanzania yeyote kwa ufupi kama humjui utasema huyu Mtanzania ametoka wapi huku Kongo – DRC.

Rais Kabila amekuwa akipendelea kutumia lugha hiyo adhimu yenye utajiri wa maneno, nyepesi kujifunza na kueleweka kutokana na matamshi yanaelekeza jinsi ya kutamka silabi moja kwa moja tofauti na baadhi ya lugha ambazo matamshi huwa yanapishana na maandiko ya lugha husika.

Rais wa Rwanda, Paul Kagame ni mtaalamu mzuri wa lugha ya Kiswahili ambaye ameipamba lugha hiyo kwa kuona umuhimu wa elimu itolewayo nchini kwake, ijumuishe lugha ya Kiswahili kama somo, ili kuwaunganisha Wanyarwanda na wanajumuia ya Afrika Mashariki kwa ukaribu zaidi.

Kagame anastahili pongezi kwa kuweka mitaala ya Kiswahili na kutoa fursa kwa walimu kutoka Tanzania,  kufundisha lugha hiyo tangu shule za msingi, sekondari hadi Chuo Kikuu. Rais huyo ametambua njia rahisi ya kuwaunganisha wana Jumuia ya Afrika Mashariki, aghalabu atumie filosofia ya Baba wa Taifa,Mwalimu Julius Nyerere kwa kuleta mshikamano, umoja wa wananchi katika kunufaika na soko la pamoja la Jumuia na kuleta maendeleo kwa ujumla. 

Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Joseph Kabila ni mdau mkubwa wa lugha ya Kiswahili ambapo amewezesha wafanyabiashara na wanamuziki wengi kutoka nchini kwake wanaongea lugha ya Kiswahili na kuiimba kwa ufasaha. Kama tujuavyo muziki ni tasnia muhimu sana katika upelekaji wa ujumbe aidha, wa kuunganisha au kubomoa, hivyo lugha ya Kiswahili ikitumika vizuri katika mataifa ya kiafrika kama ilivyo sasa tunafanya biashara na kuendeleza tasnia ya muziki kwa faida ya nchi zetu.

Kwa kuwa nimeitaja tasnia ya muziki japo sio kiongozi wa nchi, ni vema nikaeleza umuhimu wake katika matumizi ya lugha yetu ambaye ni mwana Diplomasia wetu kupitia muziki Naseeb Abdul au kwa jina maarufu Diamond Platnum. Mwanamuziki huyu ni miongoni mwa wasanii wanaopenyeza lugha ya Kiswahili katika nchi zote ambazo muziki wake unapigwa. Mfano nitapenda kuwa shuhuda kwa kuonyesha wanamuziki kutoka nchini Nigeria anaoshirikiana nao katika kuimba nyimbo zake au zao na kufanya Kiswahili kitumike sana katika muziki wa Afrika Magharibi.

Binafsi nimekutana na Wacameroon waliofika nchini kwa masuala ya utalii nikashangaa wanapenda sana nyimbo za Naseeb Abdul na kupata wasaa wa kuchambua maneno anayoimba kwa Kiswahili na wanaelewa maana yake, hivyo ni vema balozi huyu akatambua mchango wake  wa lugha kwa ufasaha na usahihi katika uimbaji na kufika ujumbe utakaochangia kuleta umoja, mshikamano na maendeleo barani Afrika. Hii ina maana Naseeb Abdul atakuwa ni mwalimu mzuri wa lugha ya Kiswahili.

Msumari wa mwisho katika wapiganaji na viongozi wa lugha ya Kiswahili katika makala yangu ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Joseph Magufuli anavyoithamini na kuijali kwa hali ya juu lugha ya Kiswahili. Rais ameleta msisimko wa pekee na kuwafanya hata viongozi wengine barani  Afrika ambao walikuwa wanaona lugha ya Kiswahili “si mali kitu iwe mali kitu”.

Pengine viongozi hao wametambua filosofia ya Mwalimu Nyerere ya kuleta umoja na kuunganisha wananchi kwa kutumia lugha, kuwa na uelewa wa pamoja na masikilizano katika nchi, pia katika kunufaika na soko la pamoja la Jumuia na kuleta maendeleo kwa wananchi, ambapo Rais Magufuli amelitambua hilo mapema.

 Magufuli amekuwa akitumia muda wake wote katka kuwatumikia wananchi wa Tanzania, kila mara  afanyapo chochote kile, huwaita wanahabari na kuhakikisha tukio hilo analiwasilisha kwa lugha ya Kiswahili ili kueleweka kwa Watanzania wote. Hii inafanya Serikali ya Awamu ya Tano kuwa ya uwazi    zaidi pia, kueleweka kwa wananchi wote nini anafanya, hili ni suala muhimu sana katika uongozi bora.

Hakika mwenye macho haambiwi tazama, utakubaliana nani Rais amepaisha lugha ya Kiswahili kitaifa na kimataifa kwa uamuzi wake wa kutumia lugha ya Kiswahili, kila anapokwenda iwe kwenye mikutano ya taifa au ya kimataifa, hivi karibuni pale Addis Ababa Ethiopia alihutubia kwa Kiswahili.

Aidha, kutokana na utendaji wa Rais na  Serikali ya Awamu ya Tano uliotukuka, kazi zote anazofanya husambaa dunia nzima na kila kiongozi anayeifikiria Tanzania kwa sasa anaona umuhimu wa kujua lugha ya Kiswahili kwa kuwa Rais ameishikia bango na ndiyo anayoitumia kuwafafanulia jambo wananchi.

Matokeo ya bango la Rais Magufuli kutumia lugha ya Kiswahili imezaa ajira lukuki za kufundisha lugha hiyo nchini Ethiopia, Rwanda, Afrika ya Kusini, Sudan Kusini na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, ambazo ni rasmi. Pia kuna ajira za kufundisha lugha ya Kiswahili sehemu mbalimbali duniani kwenye vyuo vya kimataifa ambapo Watanzania wako huko hizi ni zile ambazo sio rasmi.

Huu ni uthibitisho tosha kuwa Mwalimu Nyerere alilitambua hili na hakika amepata wapiganaji sahihi wakiongozwa na Dkt Magufuli, hakika wanastahili pongezi na daima wanakuenzi,   “Pumzika kwa Amani Mwalimu”.
Lugha ya Kiswahili kwa sasa inatumika katika nchi zote za Afrika Mashariki, Kati na Pembe ya Afrika, yaani Kenya, Uganda, Tanzania, Rwanda, Malawi, Burundi, Somalia, Msumbiji, Zambia, visiwa vya Comoro na Mashariki mwa Kongo. Hivyo zaidi ya  watu milioni 150 kwa sasa wanaongea Kiswahili hii ni neema kwa Tanzania.

Azimio la kuteuliwa kwa Lugha ya Kiswahili kuwa lugha rasmi na ya kazi ya Umoja wa Afrika lilifanyika huko Durban, Afrika Kusini tarehe 9 – 11 mwezi Julai mwaka 2002 wakati wa kikao hicho chini ya Uenyekiti wa Rais Levy Mwanawasa (aliyekuwa Rais wa Zambia)

KIJANA MJASILIAMALI AIOMBA SERIKALI IZITAMBUE BIDHAA ZA MBAO ILI APATE KIWANDA


Na Karama Kenyunko-Globu ya Jamii

, Mjasiliamali anayejihusisha na utengenezaji wa extension za Umeme kwa kutumia mbao, anaiomba Serikali izitambue bidhaa za mbao ili apate kiwanda kikubwa ambacho kitamuwezesha kutoa ajira kwa vijana na bidhaa hizo kufika hadi nje ya nchi.

Charles Antoni Sanga, ambaye ni mwafrica wa kwaza kugundua ujuzi wa kupitisha umeme kwenye mbao, ameongea hayo katika maonyesho ya 41 ya biashara (Sabasaba) yanayoendelea jijini Dar es Salaam.

Amesema, upitishaji wa Umeme kwenye mbao ni bora na siyo rahisi kusababisha shoti ya Umeme, pia ujuzi huo unatoa fursa kwa kuwainua wajasiliamali wanaochaji simu vibandani.

"Ninahamasidha kauli mbiu ya Mh.Rais kuwa Tanzania ya viwanda inawezekana sababu kuna vitu tunavyobuni watanzania ambayo ni imara kuliko vile vya kutoka nje ya nchi".

Aidha ameiomba Serikali na wadau mbali mbali wanaopenda bidhaa hizo za mbao kujitokeza na kumuinua kwani anafanya kazi katika mazingira magumu kwani hata TBS walimuagiza kuwa awe na karakana na machine Au hata jengo lakini hana chochote kwani hana fedha za kumuwezesha kuwa na vifaa hivyo.

Akielezea safari yake ya iliyomfikisha hapo anasema, alikuwa akiishi bila ya kipato chochote ndipo akaamua kubuni kitu ambacho hajawahi kukiona mahali popote ndipo akaja na wazo la extension ya mbao.

Anasema, alipokamilisha moja, watu wengi walivutiwa nayo ndipo akaamua kutengeneza kwa oda hiyo ilikuwa mwaka 2012 ambapo baadae alishiri maonyesho ya SIDO nyanda za juu kusini, huko alikutana na viongozi kutoka nchi mbali mbali wakiwemo TBS ambao walishangaa ubunifu huo ambao hawakuwa wameuona mahali popote duniani.

Sanga anaongeza, TBS walimshauri kwenda Tume ya Sayansi yabTeknolojia ili wachunguze kama bidhaa hiyo ipo mahali popote duniani lakibi haikuonekana mahala popote na kumfanya awe Mwafrica wa kwanza kupitisha umeme kwenye mbao.

Anasema, baada ya uchunguzi alifanikiwa kupata cheti cha ugunduzi (Patent) kwenda kwa mwanasheria Mkuu wa ugunduzi ambaye alisubiri pingamizi kwa muda wa miaka miwili lakini hakukuwa na pingamizi.

Sanga anawaomba wadau wajitokeze na kumuunga mkono ili aweze kutoa ajira kwa vijana hali kadhalik serikali imsaidie kuwezesha jambo hilo.
 Mgunduzi wa Soketi ya Mbao Charles Sanga akieleza Kwa Makini jinsi alivoweza kutengeneza Soketi hizo
 Charles Sanga akionesha moja ya Soketi aliyoitengeneza

STAMICO SASA KUMEKUCHA NA MAKAA YA MAWE


· Yaanza kuuza makaa hayo kwa kasi
· Yakiri kuwa na akiba ya makaa ya mawe ardhini ya kuchimba kwa zaidi ya miaka mia moja. 

Na Koleta Njelekela-STAMICO

Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) limeanza rasmi kuuza makaa ya mawe yanayozalishwa katika Mgodi wake wa Kabulo ili kukidhi mahitaji ya watumiaji wakiwemo viwanda vya saruji na nguo na hivyo kukuza Pato la Taifa.

STAMICO ilianza uzalishaji wa majaribio wa makaa ya mawe katika mgodi wa Kabulo uliopo Kijiji cha Kapeta, Wilaya ya Ileje Mkoa wa Songwe mnamo tarehe 30 Aprili 2017 na mpaka sasa imeweza kuzalisha tani 6,197.

Akihojiwa na Mwandishi wa Habari hii, mara baada ya zoezi la uuzaji makaa ya mawe kuanza rasmi huko Kabulo jana (6 Julai 2017), Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa STAMICO Bwana Hamis Komba, amesema Shirika kupitia mradi wake wa makaa ya mawe wa Kabulo, sasa linaweza kukidhi mahitaji ya watumiaji wote wa makaa ya mawe nchini, katika kipindi cha miaka mia mfululizo kutokana na kuwepo kwa mashapo ya kutosha (mineral resources) na nyenye ubora wa juu katika mgodi huo.

Bwana Komba amesema matarajio ya Shirika ni kuongeza kiwango cha uchimbaji makaa ya mawe kutoka tani 600 hadi tani 1000 kwa siku, hatua ambayo itaiwezesha STAMICO kuzalisha zaidi ya tani 300,000 kwa mwaka. 

“Nchi yetu ina rasilimali nyingi za madini yakiwemo makaa ya mawe, hivyo tunapenda kuwahikishia wenye viwanda vinavyotumia makaa hayo hususani viwanda vya Saruji (Cement), kwamba nchi ina makaa ya kutosha hivyo Serikali haitoshindwa kutosheleza mahitaji na makaa yam awe huku ikitekeleza kwa vitendo azma yake kujenga Tanzania yenye viwanda, ili kukuza uchumi wa Taifa" Alifafanua Bwana Komba.

Amewataka wenye viwanda nchini, kuwasilisha maombi ya kununua malighafi ya makaa ya mawe, ili STAMICO iweze kuwauzia makaa hayo, ambayo yana viwango vya ubora vinavyofaa katika uzalishaji wa nishati ya umeme viwandani. 

Aidha Kiongozi Mtendaji Mkuu wa STAMICO amesema hivi sasa Shirika linaendelea kuimarisha mradi huo wa Kabulo, kwa kuboresha miundombinu, maabara ya kudhibiti ubora wa makaa na kununua mashine mpya (Crusher) kwa ajili ya kuponda makaa, kulingana na mahitaji mahususi ya vipimo vinavyhitajiwa na wateja katika soko.

“changamoto zilizopo katika utekelezaji wa mradi huu ni pamoja na mtaji mdogo, mabadiliko ya hali ya hewa hasa nyakati za mvua na ubovu wa kipande cha barabara yenye urefu wa zaidi ya kilomita 15 kutoka katika eneo la mgodi, mpaka eneo la mauzo, ambapo barabara hiyo haiwezi kumudu malori ya zaidi ya uzito wa tani 15 kupita”. alibainisha Bwana Komba.

Awali Mratibu wa Mradi wa Makaa ya Mawe wa Kabulo-Kiwira Bwana Alex Rutagwelela, amesema amefurahishwa na matokeo chanya ya mradi huo ya kufikia hatua ya uuzaji makaa ya mawe, kwani ni fursa nzuri kwa Shirika, baada ya Serikali kuweka zuio la kuagiza makaa ya mawe kutoka nchi za nje; wakati nchi ikiwa na makaa mengi ya mawe ardhini.

Amesema STAMICO kupitia mradi huo, itaendelea kuimarisha viwango vya uzalishaji wa makaa ya mawe ili kuwafikia wateja wote kulingana na mahitaji yao

“Uwezo wetu na utaalam katika uchimbaji makaa ya mawe ni wa kimkakati ili kuweza kukidhi soko la ndani na nje ya nchi. Lengo kuu la mradi huu ni kutosheleza mahitaji ya kuzalisha umeme wa viwango mbalimbali katika Mradi wa Umeme wa Kiwira na pia kutosheleza mahitaji ya Viwanda nchini vikiwemo vya saruji.”

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Rasilimali watu na Utawala wa STAMICO, Bwana Deusdedith Magala amewasihi watumishi na wataalam wa Shirika hilo, kuendelea kujifunga mkanda na kufanya kazi kwa bidii ili kuivusha salama STAMICO katika kipindi hiki cha mpito, ambapo Shirika linafufua miradi yake ya uchimbaji madini; itakayoleta mafanikio makubwa na yenye maslahi mapana kwa Taifa.

Bwana Magala amesema STAMICO imeweza kuanza uzalishaji wa makaa ya mawe katika Mgodi wa Kabulo kwa kutumia mtaji mdogo na kubana matumizi; hatua ambayo imedhihirisha kwamba STAMICO tumethubutu na tunaweza kutekeleza miradi yetu kwa wakati, pamoja na hali ngumu ya kifedha inayolikabili Shirika kwa sasa.

“ni matumaini kuwa katika kipindi cha muda mfupi ujao, watumishi wote STAMICO tutafurahi, kwani tutaweza kupanua uzalishaji wa makaa ya mawe huku tukileta matokeo makubwa ya uzalishaji yenye maslahi makubwa kwa Shirika” Alifafanua Bwana Magala.

Awamu ya kwanza ya Mradi wa uchimbaji makaa ya mawe wa Kabulo inatekelezwa kupitia leseni zake mbili za uchimbaji mdogo wa madini Primary Mining Licences (PMLs) zilizopo ndani ya leseni ya utafiti ya Kabulo zenye ukubwa wa Hecta 16.52. 

Leseni hizo mbili za Uchimbaji wa Awali wa Madini katika eneo hilo la Kabulo, zina zaidi ya tani milioni 35 zilizothibitishwa za mashapo ya makaa ya mawe, yaliyoko karibu na uso wa ardhi, katika mgodi huo wa Kabulo. 

Kamishna wa Madini Tanzania Mhandisi Benjamin Mchwampaka akiwa katika picha ya pamoja na timu wa wataalam wa STAMICO (wanaotekeleza Mradi wa Uchimbaji Makaa ya Mawe-Kabulo) alipotembelea Mgodi huo hivi karibuni kukagua maendeleo ya mradi huo ambao ulianza rasmi uzalishaji makaa yam awe tarehe 30 Aprili, 2017 na kufanikiwa kuzalisha tani 6197 mpaka sasa. Soko la ndani la makaa hayo linawalenga wazalishaji viwandani hususani wale wa viwanda vya Saruji (Cement) na watengenezaji wa nguo, pamoja na magereza na watumiaji wengine wa majumbani.

Shughuli za Uchimbaji Makaa ya Mawe zikiendelea katika mgodi wa Kabulo Kiwira, uliopo katika Kijiji cha Kapeta, wilaya ya Ileje, Mkoa wa Songwe. Leseni za Uchimbaji wa Awali wa Madini katika eneo hilo la Kabulo, zina zaidi ya tani milioni 35 zilizothibitishwa za mashapo ya makaa ya mawe, yaliyoko karibu na uso wa ardhi, katika mgodi huo wa Kabulo. Mashapo hayo yanaweza kuchimbwa kwa mfululizo kwa miaka mia moja ijayo.

Mratibu wa Mradi wa Uzalishaji Mkaa ya Mawe wa Kabulo-Kiwira Bwana Alex Rutagwelela ambaye pia ni Kaimu Mkurugenzi wa Utafiti na Uchorongaji wa STAMICO akielekeza kuhusu zoezi zima la upakiaji makaa ya mawe katika Malori tayari kwa ajili ya kupeleka katika eneo la mauzo lililopo katika kijiji cha Kasumulu, Wilaya ya Kyela, mkoa wa Mbeya. Mgodi huo wa Kabulo-Kiwira uliopo katika kijiji cha Kapeta, Wilaya ya Ileje mkoa wa Songwe unamilikiwa na kuendeshwa na STAMICO kwa niaba ya Serikali.
Malori ya Kampuni ya Lake Cement yakipakia Makaa ya Mawe katika eneo la mauzo ya makaa hayo, lililopo umbali wa kilometa mbili kutoka katika barabara kuu ya Mbeya, iendayo nchini Malawi. Eneo hilo la mauzo lipo katika kijiji cha Kasumulu, Wilaya ya Kyela, mkoa wa Mbeya. Makaa hayo ya Mawe yanazalishwa na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), katika mgodi wake wa Makaa ya Mawe wa Kabulo, ulipo katika kijiji cha Kapeta, Wilaya ya Ileje mkoa wa Songwe.

WAZIRI DKT. MWAKYEMBE AWA MGENI RASMI FAINALI ZA SHINDANO LA BONGO STYLE,AKARIBISHA SHINDANO HILO KUFANYIKA BUNGENI DODOMA 2018.


Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mh.  Dkt. Harrison Mwakyembe akitoa hotuba yake wakati wa fainali za shindano la Bongo Style, lililofanyika makumbusho ya Taifa Jijini Dar ,linalohusisha fani za ubunifu wa mavazi,upigaji picha na uandishi wa miswada ya filamu ambapo aliipongeza Taasisi isiyo ya kiserikali ya Faru Arts and Development Organization(FASDO) kwa kuandaa mashindano hayo, alisema kuwa Serikali inalojukumu la kusaidia Asasi kama FASDO ambazo zinaingia katika maswala ambayo Serikali hawakuyawekea msingi mkubwa. "Naomba niagize na kuwa kuna watendaji wetu wa wizara katika sherehe hii mkae chini na watu wa FASDO ili mwaka kesho zoezi hili lifanyikie Bungeni Dodoma" Alisema Dkt. Mwakyembe.
 Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mh.  Dkt. Harrison Mwakyembe (wa tatu kutoka kulia) akimkabidhi Agnes Nyahonga  tuzo na zawadi ya mfano wa Hundi yenye thamani ya Tsh 1,000,000 aliyeshinda   shindano la Bongo Style katika kipengele cha ubunifu wa mavazi.
 Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mh.  Dkt. Harrison Mwakyembe(wa pili kutoka kulia) akimkabidhi Goodhope Elieskia maarufu kwa jina la Zagamba  tuzo na zawadi ya mfano wa Hundi yenye thamani ya Tsh 1,000,000 aliyeshinda   shindano la Bongo Style katika kipengele cha uandishi wa miswada ya Filamu
 Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na MichezoMh.  Dkt. Harrison Mwakyembe(wa kutoka kulia) akimkabidhi Masoud Masoud  tuzo na zawadi ya mfano wa Hundi yenye thamani ya Tsh 1,000,000 aliyeshinda   shindano la Bongo Style katika kipengele cha ubunifu wa mavazi.

 Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na MichezoMh.  Dkt. Harrison Mwakyembe(wa pili kutoka kulia) akimkabidhi Philip Florian  tuzo ya Best Personality aliyopokea kwa niaba ya Kelvin Mwanasoko ambaye hakuweza fika katika Mashindano hayo.
 Msanii Dullah Aka DY akitumbuiza wakati wa Fainali hizo
 Katibu Mkuu wa Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) Godfrey Mngereza akizungumza wakati wa fainali za Shindano la Bongo Style na kuipongeza Asasi ya Kiraia ya FASDO kwa ubunifu mkubwa.
 Mratibu wa FASDO Nchini Tanzania Bi. Joyce Msigwa akizungumza wakati mambo mbalimbali yanayohusu Asasi hiyo ikiwa ni pamoja na mafanikio waliyoyapata kama kuendesha shindano la Na mimi nipo pamoja na FASDO CUP na mengine mengi yahusuyo asasi hiyo.
Ilikuwa ni 'Surprise' Kati kati ya Sherehe za Shindano la Bongo Style ambapo Mratibu Mkuu wa FASDO na Muasisi wa Asasi hiyo isiyo ya kiserikali Bi. Lilian Nabora(Aliyevaa Gauni Jekundu) alipofanyiwa Hafra fupi ya siku yake ya Kuzaliwa ambapo alitimiza miaka 50. Waliomsindikiza ni 'Team' ya FASDO pamoja na washiriki wa shindano hilo kwa mwaka 2017.
Mratibu Mkuu na Muasisi wa FASDO Lilian Nabora akiongea wakati wa fainali za Bongo Style, alisema kuwa wamewekeza sana katika mitandao ya kijamii na hasa tovuti ya www.fasdo.org ili kuwafikia vijana wengi zaidi Tanzania nzima ambao wanauwezo na wanajiamini kuwa wanavipaji katika mambo mbalimbali wapate kujiunga katika taasisi hiyo,aliongeza kuwa mchakato wa kuwapata washindi ulipitia mchujo mpaka kuwapata washiriki bora 30,kisha 15, mpaka kufikia washindi watatu(3) "Mpaka sasa tumeweza kuwafikia vijana wanaokadiliwa kuwa 1,500 na mpaka sasa bado tunawahimiza wapate kujiunga nasi" alisema Bi. Lilian.
 Waliokaa katika Meza ni Majaji Upande wa ubunifu wa mavazi, na walio mstari wa mbele ni Majaji upande wa Miswada ya Filamu na upigaji picha.
Baadhi ya washiriki upande wa Ubunifu wa Mavazi wakiwa wanaonesha Mavazi yao waliyo yabuni wao wenyewe
 Wageni waalikwa  wakifuatilia sherehe za Fainali za shindano la Bongo Style
 Mwenyekiti wa FASDO Bw. Stanley Kamana akitoa neno la Shukurani wakati wa Fainali za Bongo Style
 Washiriki wa Shindano la Bongo Style kwa Mwaka 2017 wakiwa wanafuatilia mambo mbali mbali wakati wa Shindano hilo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Asasi ya Kiraia ya FASDO Bw. Tedvan Nabora akitoa neno la Shukurani kwa wote waliohudhuria katika Fainali za shindano la Bongo Style
Picha ya pamoja ya  Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mh.  Dkt. Harrison Mwakyembe,Uongozi na Team ya FASDO,Majaji na washindi wa Bongo Style Competition kwa mwaka 2017.
Picha zote na Laden Tedvan Nabora.

RAIS MSTAAFU BENJAMIN MKAPA AWASILI CHATO KWA AJILI YA KUKABIDHI NYUMBA 50 ZA WATUMISHI WA AFYA KATIKA MIKOA YA SIMIYU, KAGERA NA GEITA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkaribisha Rais mstaafu wa awamu ya Tatu Benjamin William Mkapa Chato mkoani Geita. Rais Mstaafu Mkapa katika siku ya kesho anatarajiwa kukabidhi nyumba 50 za watumishi wa sekta ya Afya zilizojengwa na Taasisi ya (Mkapa Foundation) katika mikoa ya Simiyu, Kagera na Geita.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkaribisha Rais mstaafu wa awamu ya Tatu Benjamin William Mkapa Chato mkoani Geita. Rais Mstaafu Mkapa katika siku ya kesho anatarajiwa kukabidhi nyumba 50 za watumishi wa sekta ya Afya zilizojengwa na Taasisi ya (Mkapa Foundation) katika mikoa ya Simiyu, Kagera na Geita. Kushoto ni Mke wa Rais, Mama Jannet Magufuli.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Balozi wa Japan hapa nchini Masaharu Yoshida mara baada ya kuwasili Chato mkoani Geita. Balozi huyo wa Japan katika siku ya kesho anatarajiwa kukabidhi mtambo wa kukamua Mafuta ya Alizeti (Double Refine) uliojengwa Chato mkoani Geita kwa Msaada wa Serikali ya Japan.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkaribisha Rais mstaafu wa awamu ya Tatu Benjamin William Mkapa Chato mkoani Geita.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Rais mstaafu wa awamu ya Tatu Benjamin William Mkapa pamoja na wageni mbalimbali waliofika Chato kwa ajili ya shughuli mbalimbali za kimaendeleo zinazotarajiwa kufanyika kesho.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoani Geita Josheph Kasheku Msukuma aliyefika Chato pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Geita. PICHA NA IKULU.

WAZIRI MKUU AWAHAKIKISHIA WAWEKEZAJI MAFANIKIO


Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa akizungumza na wananchi waiyo hudhuria katika maadhimisho ya miaka 60 tangu Mtukufu Agakhan alipo chaguliwa kuwa Imamu mkuu wa madhehebu ya Shia Ismailia duniani, akiwa amemuwakilisha Rais Dkt. John Magufuli, Julai 9, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa akizungumza na wananchi waiyo hudhuria katika maadhimisho ya miaka 60 tangu Mtukufu Agakhan alipo chaguliwa kuwa Imamu mkuu wa madhehebu ya Shia Ismailia duniani, akiwa amemuwakilisha Rais Dkt. John Magufuli, Julai 9, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa akisalimiana na mama Zakia Megji wakati wa maadhimisho ya miaka 60 tangu Mtukufu Agakhan alipo chaguliwa kuwa Imamu mkuu wa madhehebu ya Shia Ismailia duniani, akiwa amemuwakilisha Rais Dkt. John Magufuli, (kushoto) ni Rais wa Jumuiya ya Shia Ismailia Amin Lakhani Julai 9, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa akisalimiana na Rais wa Jumuiya ya Shia Ismailia Amin Lakhani wakati wa maadhimisho ya miaka 60 tangu Mtukufu Agakhan alipo chaguliwa kuwa Imamu mkuu wa madhehebu ya Shia Ismailia duniani, akiwa amemuwakilisha Rais Dkt. John Magufuli, (katikati) ni Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sofia Mjema Julai 9, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa akipokea shada la maua wakati akikaribishwa kwenye maadhimisho ya miaka 60 tangu Mtukufu Agakhan alipo chaguliwa kuwa Imamu mkuu wa madhehebu ya Shia Ismailia duniani, akiwa amemuwakilisha Rais Dkt. John Magufuli, (katikati) ni Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sofia Mjema Julai 9, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa akisaini kitabu cha wageni kwenye maadhimisho ya miaka 60 tangu Mtukufu Agakhan alipo chaguliwa kuwa Imamu mkuu wa madhehebu ya Shia Ismailia duniani, (kushoto) ni Rais wa Jumuiya ya Shia Ismailia Amin Lakhani na (kulia) ni muwakilishi wa AKDN Resident Amin Kurji, wakati alipomwakilisha Rais Dkt. John Magufuli, (katikati) ni Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sofia Mjema Julai 9, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa akizungumza na Muwakilishi wa AKD resident Amin Kurji katika maadhimisho ya miaka 60 tangu Mtukufu Agakhan alipo chaguliwa kuwa Imamu mkuu wa madhehebu ya Shia Ismailia duniani, yaliyofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee, akiwa amemuwakilisha Rais Dkt. John Magufuli,(katikati) ni Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Aga Khan Suleiman Shabbudin Julai 9, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa akiteta jambo na Rais wa Jumuiya ya Shia Ismailia Amin Lakhani, katika maadhimisho ya miaka 60 tangu Mtukufu Agakhan alipo chaguliwa kuwa Imamu mkuu wa madhehebu ya Shia Ismailia duniani, akiwa amemuwakilisha Rais Dkt. John Magufuli, Julai 9, 2017. 
Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa akipokea maandano ya maadhimisho ya miaka 60 tangu Mtukufu Agakhan alipo chaguliwa kuwa Imamu mkuu wa madhehebu ya Shia Ismailia duniani yaliyofanyika katika viwanja vya Diamond Jubilee, Waziri Mkuu amemuwakilisha Rais Dkt. John Magufuli katika sherehe hiyo, Julai 9, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

……………………………………………………………..

*Asema nchi ina utulivu wa kisiasa na uchumi unaokuwa kwa kasi

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewahakikishia uwekezaji wenye tija wawekezaji watakaokuja nchini kwa kuwa Tanzania ni nchi yenye amani, utulivu wa kisiasa na uchumi wenye kukua kwa kasi.

Ameyasema hayo leo (Jumapili, Julai 09, 2017) alipomuwakilisha Rais Dkt. John Magufuli katika maadhimisho ya miaka 60 tangu Mtukufu Aga Khan alipochaguliwa kuwa Imamu Mkuu wa madhehebu ya Shia Ismailia duniani.

Waziri Mkuu amesema Serikali inatambua na kuthamini shughuli mbalimbali zinazofanywa na mtandao wa taasisi za Aga Khan zilizopo hapa nchini, hivyo Serikali itaendelea kushirikiana nao.

Ameupongeza mtandao wa taasisi za Aga Khan kwa kumuunga mkono Rais Dkt. Magufuli katika kutoa kipaumbele cha kuwapa fursa watu wenye kipato cha chini kushiriki katika uzalishaji ili waweze kujikwamua kiuchumi.

“Nawahakikishia kwamba uwekezaji wenu hapa nchini utakuwa na baraka kwa sababu nchi imetulia kisiasa na uchumi wake unakua kwa kasi. Nawaomba muendelee kuwaalika wanajumuia wa madhehebu ya Shia Ismailia popote walipo duniani waje kuwekeza nchini fursa bado zipo.”

Kwa upande wake Rais wa Jumuiya ya Madhehebu ya Shia Ismailia Tanzania, Bw. Amin Lakhani ameishukuru Serikali kwa ushirikiano inaowapa na kwamba ameahidi kuendelea kushirikiana nayo katika kuboresha sekta mbalimbali nchini.

Amesema mtandao wa maendeleo wa Aga Khan unatoa huduma mbalimbali zikiwemo za afya, elimu, kilimo na kunaendesha miradi katika mabara ya Afrika na Asia kwa kuwapa fursa watu wenye kipato cha chini kushiriki katika uzalishaji ili kujikwamua kiuchumi.

Awali, Mkuu wa wilaya ya Ilala, Bi. Sophia Mjema aliipongeza taasisi hiyo kwa mpango wake wa upanuzi wa hospitali na kuongeza vituo 35 vya afya kutoka 15 walivyonavyo.