Tuesday, October 17

TAARIFA KWA UMMA:OFISI ZA BAKWATA ZAHAMIA KWA MUDA JENGO LA TIGER TOWER-MTAA WA TOGO

Ndugu zangu Wanahabari,

Assalaamu Alaykum (Amani ya Mwenye ezi Mungu iwe kwenu)

Napenda kuufahamisha umma wa kiislamu kuwa kufuatia kuanza mradi wa ujenzi wa msikiti wa Mohammed VI unaojengwa katika eneo la Bakwata makao Makuu Kinondoni Road.

Hivyo basi napenda kuchukua nafasi hii kuufahamisha umma kuwa ili kupisha mradi huo Bakwata Makao Makuu imehamisha ofisi zake na kuzipeleka katika mtaa wa Togo jengo linalotambulika kama TIGER TOWER na shughuli zote zinaendelea kama kawaida.

Mwisho kabisa tunaomba radhi kwa usmbufu wowote uliojitokeza katika kipindi hiki cha ujenzi.

Wabillahi TTaufiiq

USTAADH TABU KAWAMBWA

MKURUGENZI HABARI NA MAHUSIANO.




Waziri Mkuu Kassim Majaliwa  wakishuhudia wakati Mufti Mkuu wa Tanzania, Sheikh Abubakary Zubeir (kulia)  akitia saini Makubaliano ya ujenzi wa Msikiti kwenye eneo la BAKWATA, Kinondoni jijini Dar es salaam Oktoba 25,2016. PICHA NA MAKTABA

No comments:

Post a Comment