Saturday, November 18

Mwanajeshi wa Korea Kaskazini aliyetorokea K Kusini apatikana na minyoo mingi

Minyoo yapatikana ndani ya mwili wa mwanbajeshi wa Korea Kaskazini aliyetorokea Korea KusiniHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionMinyoo yapatikana ndani ya mwili wa mwanbajeshi wa Korea Kaskazini aliyetorokea Korea Kusini
Mwanajeshi wa Korea Kusini aliyepigwa risasi alipokuwa akitorokea Korea Kusini katika mpaka wa mataifa hayo mawili amepatikana na vimelea vingi katika matumbo yake , kulingana na daktari wake.
Mtoro huyo alivuka eneo linalolindwa sana mpakani siku ya Jumatatu , lakini akapigwa risasi kadhaa na walinzi wa Korea Kaskazini.
Madaktari wanasema mwanajeshi huyo kwa sasa yuko katika hali nzuri , lakini idadi kubwa ya minyoo katika mwili wake unafanya hali yake kuwa mbaya.
Hali yake inaonyesha hali ya maisha yalivyo nchini Korea Kaskazini.
''Sijawahi kuona kitu kama hiki katika miaka yangu 20 kama daktari , daktari wa Korea Kusini Lee Cook-jong aliwaambia waandishi wa habari, akielezea kwamba kimelea mrefu katika tumbo lake alikuwa na urefu wa sentimita 27.
Mwanajeshi wa Korea Kaskazini akikimbizwa hospitalini Korea KusiniHaki miliki ya pichaEPA
Image captionMwanajeshi wa Korea Kaskazini akikimbizwa hospitalini Korea Kusini
Mwanadamu anaweza kupata vimelea kupitia kula chakula kichafu kwa kuumwa na wadudu ama vimela waliongia kupitia katika ngozi.
Kwa upande wa mwanajeshi huyo huenda vimelea hao waliingia kupitia chakula kichafu.
Korea Kaskazini inatumia kinyesi kama mbolea. Iwapo vinyesi hivyo havitibiwi na kutumiwa kama mbolea katika mboga ambayo haijapikwa ,vimelea hivyo vinaingia mdomoni hadi katika matumbo ya mwanadamu.

No comments:

Post a Comment