Tuesday, September 26

VIJANA NA WATEJA WA VODACOM TANZANIA WALETEWA MKOMBOZI WA MAWASILIANO

Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania Ian Ferrao (katikati) na wafanyakazi wa kampuni hiyo wakionyesha mabango yanayoelekeza jinsi yakupata vifurushi vya bando la”Pinduapindua” kwa ajili ya wateja wao hususani vijana wakati wa uzinduzi wa bando hilo ambapo mteja anatakiwa kupiga namba *149*01# kisha kuchagua kifurushi cha siku, cha wiki au cha mwezi,Kutoka kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano, Jaquiline Materu, Mkuu wa Kitengo cha Masoko, Nandi Mwiyombela ,Mkurugenzi wa Masoko, Hisham Hendi na Mkuu wa Kitengo cha Bidhaa na Huduma kwa Wateja, Linda Riwa.

Vijana wakitanzania na wateja wote kwa ujumla wa Vodacom Tanzania PLC,wameletewa Uhuru na wepesi zaidi wa kutumia bando jipya la”Pinduapindua” lililozinduliwa jana na kampuni hiyo likiwa mahususi kwaajili ya wateja wa mtandao huo.

Akiongea wakati wa Uzinduzi wa huduma hiyo,Mkurugenzi wa biashara na Masoko wa Vodacom Tanzania PLC, Bw. Hisham Hendi alisema huduma ya bando hili jipya la “Pinduapindua” ni ya kwanza na yakihistoria katika kampuni zote za mawasiliano nchini,Hii ni moja ya mikakati ya kampuni yetu kutaka kuleta mabadiliko kwenye jamii hususani vijana kwa kuwarahisishia maisha yao ikiwemo kuongeza vipato na dhamira kubwa yakuwapeleka watanzania katika ulimwengu wa sayansi na teknolojia.

“Utafiti wetu unaonyesha kwamba vijana ni moja ya kiungo kikubwa sana kwa mapinduzi yakiuchumi nchini pia ni tabaka linalokuwa kwa kasi ya kuridhisha na wana mahitaji maalum yakipekee yakiteknolojia tunapenda vijana watambue kwamba Vodacom Tanzania PLC imesikia kilio chao ndiyo maana leo hii tumewaletea Pinduapindua ”, alisema Hendi.

Pinduapindua ni kifurushi huru na chakipekee zaidi kuliko vifurushi vingine vinavyowapangia wateja wa kampuni zingine za mawasiliano nchini,Bando hili litawapatia vijana na wateja uhuru wao wa kuchagua kiasi cha kupangia kwenye data, kupiga simu (voice) au ujumbe mfupi (SMS) kulingana na mahitaji ya wakati huo. “Pinduapindua” pia itamwezesha mteja kutumia Facebook (ikiwa pamoja na picha), Whatsapp (maandishi na picha) na SMS hadi 200 bure.

Mkurugenzi huyo alifafanua zaidi kwamba kampuni inaelewa kwamba mahitaji ya wateja wao ya utumiaji hubadilika siku hadi siku kuna siku unaweza kuhitaji matumizi ya mtandao (data) zaidi ya muda wa maongezi, kwa hiyo unakuwa huru kupangilia matumizi ya kifurushi chako kuendana na mahitaji yako na jinsi yakupata vifurushi vya bando

hili ni rahisi mteja atahitaji kupiga namba *149*01# kisha kuchagua kifurushi cha siku, cha wiki au cha mwezi. Vifurushi hivi vinaweza kulipiwa kupitia muda wa maongezi au Mpesa na mara baada ya kununua, mteja atapatiwa kifurushi chake, Facebook BURE, Whatsapp BURE na SMS, vyote ambavyo vitatumika kwa muda wote wa kifurushi alichochagua” alisema Hendi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania Ian Ferrao (katikati) akicheza na wafanyakazi wa kampuni hiyo wakati wa uzinduzi wa bando jipya la Pinduapindua kwa ajili ya wateja haswa vijana,Jinsi yakupata vifurushi vya bando hili mteja anatakiwa kupiga namba *149*01# kisha kuchagua kifurushi cha siku, cha wiki au cha mwezi.
Wacheza shoo wa promosheni ya bando la Pinduapindua la Kampuni ya Vodacom Tanzania wakicheza wakati wa uzinduzi wa huduma hiyo, Dar es Salaam jana. Jinsi yakupata vifurushi vya bando hili mteja anatakiwa kupiga namba *149*01# kisha kuchagua kifurushi cha siku, cha wiki au cha mwezi.

No comments:

Post a Comment