Saturday, September 23

Seneta wa Republican ampinga Trump kuhusu Obamacare

Bima ya wagonjwa iliyoanzishwa na Rais Barack Obama ijulikanayo kama ObamaCare inawahudumia Wamerakani wa kipato cha chini.Haki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionBima ya wagonjwa iliyoanzishwa na Rais Barack Obama ijulikanayo kama ObamaCare inawahudumia Wamerakani wa kipato cha chini.
Seneta wa chama cha Republican aliyekuwa wakati mmoja mgombeaji wa Urais, John McCain, amesema kuwa atapiga kura kupinga mpango wa chama chake wa kufutilia mbali bima ya wagonjwa iliyoanzishwa na Rais Barack Obama ijulikanayo kama ObamaCare.
Alisema kuwa moyo wake haumruhusu kuunga mkoto upigaji marufuku wa bima hiyo inayowasaidia watu wa mapato ya chini bila kuwa na takwimu za kuonyesha watakaonufaika na watakaoathirika.
Mbali na Bwana McCain, seneta mwingine mmoja wa Republican amesema kuwa anapinga ufutiliaji mbali wa bima hiyo.
Tayari wengine wawili wametangaza kuwa wanapinga mswada huo wa chama cha Republican.
Seneta John McCain wa Republican
Image captionSeneta John McCain wa Republican
Kwa kuwa vyama vikuu viwili katika bunge la Seneti linashindiana wanachama wachache sana ni dhahiri kuwa mswada huo hautapita.
Rais Trump ametumia mtandao wa Twitter kumkosoa yeyote anayepinga kuangamizwa kwa bima ya ObamaCare.
Hata hivyo wafadhili wa mswada huo wanasema wataendelea kuusukuma siku zijazo hadi wafaulu.

No comments:

Post a Comment