Tuesday, April 10

Serikali yamjibu Nape

Dodoma. Serikali imemjibu Mbunge wa Mtama (CCM) Nape Nnauye na kumueleza kuwa si kweli kuwa imetelekeza miradi ya uzalishaji wa umeme kwa njia ya gesi.
Hayo yameelezwa leo Aprili 10, bungeni na Waziri wa Nishati, Medard Kalemani wakati akichangia bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu katika mwaka wa fedha 2018/19.
 Dk Kalemani amesema si kweli kwamba ilani ya uchaguzi haijataja kabisa mradi wa uzalishaji wa umeme.
“Katika kifungu cha 43 (a) ilani hiyo imeeleza juu ya uzalishaji wa umeme kwa gharama nafuu ikiwa ni pamoja na kutumia gesi na maji lakini haikutaja aina ya mradi,”amesema.
Nape aliibua hoja hiyo jana wakati akichangia hotuba ya ofisi ya Waziri Mkuu na alihoji kuwa ilani ya uchaguzi ya CCM haijazungumzia kuhusu mradi wa Stieglers Gauge na kwamba miradi ya gesi haien

No comments:

Post a Comment