Sunday, September 10

Wachimbaji dhahabu wahofiwa kufa mgodini




Wachimbaji wawili wa dhahabu katika mgodi wa Sekenke One kitalu namba moja wilayani Iramba wanahofiwa kufa baada ya kufukiwa na udongo.
Mgodi huo katika Kijiji cha Konkilangi kata ya Nwike tarafa Shelui mkoani  Singida.
Ajali hiyo imetokea jana Jumamosi saa 7:47 usiku mgodini humo na pia imesababisha majeruhi watano.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Isaya Mbughi amesema wachimbaji wanaohofiwa kufa ni Simon Odochi (26) maarufu kwa jina la Wamwanza mkazi wa Jiji la Mwanza.
Mwingine ni Kashinde Nkula (27), mkazi wa Kijiji cha Mangusu wilayani Kishapu mkoani Shinyanga.
Amesema juhudi za kuwaokoa zimeanza tangu usiku wa manane na kwamba hadi leo Jumapili saa 3:30 asubuhi wachimbaji hao walikuwa bado hawajapatikana.
Kaimu Kamanda Mbughi amesema ajali hiyo pia imesababisha majeruhi ambao ni Ayubu Msengi (34), mkazi wa Ntwike; Mwita Salumu (42) wa Gumanga; Lazaro Edward (28) wa Kiomboi Soweto; Jeremi Idd (41) wa Kijiji cha Gumanga na Jumanne Said (24) wa Kijiji cha Mgongo.
Majeruhi hao watano amesema waliokolewa na wenzao na chanzo cha ajali hiyo ni kutitia kwa udongo.

Rais Magufuli ateua Jaji Mkuu


Rais John Magufuli amemteua Profesa Ibrahim Juma kuwa Jaji Mkuu wa Tanzania.
Taarifa iliyotolewa na Ikulu imesema uteuzi huo unaanza leo Jumapili.
Kabla ya uteuzi huo, Profesa Juma alikuwa akikaimu nafasi hiyo tangu Januari alipostaafu Jaji Mkuu, Mohamed Chande Othman.
Ikulu imesema Jaji Mkuu ataapishwa kesho Jumatatu saa nne asubuhi, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais Magufuli Januari 17 alimteua Profesa Juma kuwa Kaimu Jaji Mkuu.
Kabla ya kuteuliwa katika nafasi hiyo, Profesa Juma alikuwa Jaji wa Mahakama ya Rufaa.
Jaji Mkuu mstaafu Chande hadi kufikia Januari Mosi alikuwa ameshafikisha miaka 65 ambayo ni ya kustaafu majaji wa Mahakama ya Rufani kama ilivyobainishwa katika Ibara ya 120 ya Katiba ya mwaka 1977.
Jaji Chande aliteuliwa katika nafasi hiyo na Rais mstaafu Jakaya Kikwete mwaka 2010 akichukua nafasi ya Jaji mstaafu Augustino Ramadhani.


Maswali tata shambulio la Lissu




Wakati hali ya mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu ikiwa bado haijatengemaa, yameibuka maswali kadhaa kuhusu shambulio dhidi yake lililotokea Alhamisi iliyopita mjini Dodoma.
Watu wasiojulikana walimshambulia rais huyo wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS) kwa risasi zipatazo 32 akiwa ndani ya gari lake baada ya kuwasili katika makazi yake eneo la Area D, na ni risasi tano zilizompata na kumjeruhi vibaya.
Lissu, ambaye ameibukia kuwa mwanasiasa aasiyeogopa kusema analoamini, amelazwa Hospitali ya Aga Khan jijini Nairobi ambako amewekwa chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi wa karibu.
Taarifa zilizopatikana jana zinasema mbunge huyo, bado anaangaliwa kwa karibu na madaktari.
Habari za shambulio dhidi yake zilitapakaa kwa kasi Ijumaa mchana, na juzi watu walikuwa wakitoa salamu za pole na kumuombea arudi katika hali yake, lakini jana kukaibuka maswali.
Gazeti hili limeyachambua maswali machache kati ya mengi ambayo yamejitokeza katika mijadala mbalimbali.
Miongoni mwa maswali hayo ni kwa nini Jeshi la Polisi halikuchukua hatua baada ya Lissu kutangaza kuwa kuna watu wanamfuatilia kwa muda mrefu.
Agosti 18, Lissu aliwaambia waandishi wa habari kuwa anafuatiliwa na watu anaowashuku kuwa ni maofisa usalama kwa takriban wiki tatu mfululizo.
Lissu alikwenda mbali zaidi kwa kumtaka Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Simon Sirro pamoja na mkurugenzi wa idara ya usalama wa Taifa (TISS) kuwaeleza wakubwa wao kuhusu watu hao kwamba wapambane na wahalifu badala ya kutumia rasilimali za nchi kufuatilia raia wasio na hatia.
Hata hivyo, juzi IGP Sirro aliwaambia waandishi wa habari mjini Dopdoma kuwa Lissu, ambaye amekuwa akikamatwa mara kwa mara na polisi kutokana na kauli anazotoa katika mikutano na waandishi wa habari, hakutoa taarifa hizo katika kituo chochote cha polisi.
“Hili ni swali ambalo lingefaa zaidi aulizwe yeye. Hivyo tunaomba apone halafu mumuulize kama alitoa taarifa kituo chochote cha polisi,” alisema Sirro.
Swali hapo ni, kama iliwezekana kumkamata kutokana na anachokisema kwenye vyombo vya habari, ilishindikana vipi kufuatilia madai anayoyatoa katika mikutano hiyo?
Hata hivyo, mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha), Patrobas Katambi amesema jana kuwa walishamuandikia IGP Sirro kuhusu tishio dhidi ya Lissu na hajawajibu.
Jibu hilo la IGP Sirro limeibua swali jingine; kwa nini Lissu hakutoa taarifa hizo polisi?
Swali jingine ni kitendo cha polisi kutochukua hatua za haraka kuhoji wahusika wa karibu na tukio. Jana, polisi ilitangaza kuwa inamsaka dereva wa Lissu ambaye tangu wakati wa tukio alikuwa akionekana na viongozi wa Chadema na alikuwepo Hospitali ya Mkoa wa Dodoma.
Ilikuwaje, polisi walishindwa kumchukulia kama ni mtu muhimu kumuhoji mara baada ya tukio badala ya kusubiri hadi siku tatu baadaye?
Swali jingine ni mazingira ya tukio hilo. Dereva wa Lissu alieleza kwamba kuna gari jeupe lilikuwa linawafuatilia kutoka bungeni mpaka nyumbani kwa Lissu, eneo ambalo wanakaa wabunge na mawaziri.
Kwa maelezo yake ni kwamba yeye ndiye aliyemzuia Lissu asishuke ndani ya gari na kumtaka alaze kiti wakati risasi zikipigwa kwenye gari lao.
Watu hao walikuwa wakimfuata kila siku hadi nyumbani? Na kama siku hiyo pekee walimfuata hadi anaanza kuelekea nyumbani, dereva hakuona hali ni tofauti na kuamua kupeleka gari sehemu salama au kutumia mbinu ambayo ingemthibitishia kuwepo kwa nia ovu?
Kingine kinachozua utata ni kufuatiliwa kwa gari la Lissu tangu bungeni. Hii ina maana kuwa watu hao wenye nia mbaya walikuwepo kwa muda mrefu kwenye viunga au eneo la jirani na Bunge wakimsubiri waliyemtaka.
Je, askari wanaolinda hapo na madereva wengine wa wabunge hawakuliona na kulitilia shaka gari hilo kwa siku zote kama Spika Job Ndugai alivyolieleza Bunge kuwa maeneo ya chombo hicho yako salama?
Swali jingine ni kuhusu hali ya usalama katika eneo la makazi ya wabunge na mawaziri. Je, viongozi hao wako salama? Kama washambuliaji walimudu kufyatua risasi takriban 32 na kufanikiwa kuondoka, bado wabunge na mawaziri wako salama?
Eneo wanalokaa vigogo hao lina ulinzi na wafanyakazi wa ndani. Wote hao hawakuona tukio hilo.
Kama kuna ulinzi au walinzi, walifanya juhudi gani kusaidia kudhibiti washambuliaji au kutoa taarifa ambazo zingewezesha polisi kuwabana mapema?
Hata hivyo, Jeshi la Polisi jana lilisema linawahoji baadhi ya majirani kuhusu tukio hilo.
Spika Ndugai alisema watu hao walifyatua risasi kati ya 28 na 32, kwa nini walitumia idadi hiyo kubwa kumshambulia mtu asiye na silaha?
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alisema shambulio hilo ni la kisiasa kwa kuwa Lissu hana adui nje ya siasa.
Hao maadui ndani ya siasa ni nani? Ni wanasiasa wa chama kingine au walio ndani ya Chadema? Ni maadui katika ngazi gani ya kisiasa ambayo inaweza kufikia kiwango cha kutaka kumuua mpinzani?
Katika hatua nyingine, taarifa zilizopatikana jana jioni kabla ya kwenda mitamboni zilisema Lissu alikuwa bado kwenye chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi wa karibu wa madaktari katika hospitali ya Aga Khan jijini Nairobi.
Hakuna kiongozi wa Chadema wala ndugu aliyekuwa tayari au kupatikana kuzungumzia maendeleo ya hali yake.
Lissu, mwanasheria wa kujitegemea na mwanaharakati wa haki za binadamu na mazingira, amejipatia umaarufu zaidi katika miaka ya karibuni, hasa kutokana na misimamo yake mikali na matukio ya kukamatwa kila mara na polisi na wakati mwingine kufunguiliwa mashtaka, hasa ya uchochezi.

Gwajima alaani Lissu kupigwa risasi




Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima amesema hatasita kukemea uhalifu nchini likiwemo tukio la kupigwa risasi Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu.
Gwajima amesema hayo leo Jumapili wakati wa ibada maalumu ya kumuombea Lissu aliyeshambuliwa kwa risasi Alhamisi wiki hii nyumbani kwake Area D mjini Dodoma na watu ambao hawajajulikana.
Lissu hivi sasa anaendelea na matibabu katika Hospitali ya Aga Khan iliyopo mjini Nairobi, Kenya.
"Naomba tusimame kidogo nizungumze jambo, nimesema leo nitakuwa na ibada maalumu ya kumuombea Lissu. Somo langu la leo linasema damu isiyo na hatia," amesema akizungumza na waumini.
Gwajima amesema kama kiongozi wa dini hatasita kukemea tukio lililomfika Lissu na kwamba, anashangaa viongozi wenzake wa dini kukaa kimya.
Amesema neno la Mungu linasema atakayemwaga damu ya mwanadamu mwenzake naye damu yake itamwagika vivyo hivyo.
“Damu inayomwagika chini ya ardhi ina sauti, inamlilia Mungu," amesema.
Awali, wanakwaya wa kanisa hilo waliimba wimbo maalumu wa kumuombea Lissu wakihamasisha Taifa lote kufanya hivyo.
"Amani ya Tanzania inapotea, wasione tuko kimya... kwa nini haya yanatokea na watu wasiyojulikana... Watanzania wote tumuombee Lissu," haya ni baadhi ya maneno katika wimbo huo.

Askofu mkuu KKKT atoa tamko Lissu kupigwa risasi




Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri nchini (KKKT), Askofu Dk Fredrick Shoo amewataka watu waovu watambue kumuondoa Tundu Lissu mmoja kutazalisha Lissu wengine maelfu.
Kauli ya Askofu Shoo inatokana na kuchukizwa na jaribio lililoshindwa la kumuua Lissu Alhamisi iliyopita mjini Dodoma, ambapo watu waliokuwa na silaha walishambulia gari lake kwa risasi 32.
Katika shambulizi hilo, kati ya risasi hizo 32 zilizofyatuliwa, risasi tano zilimpata Lissu maeneo mbalimbali ya mwili wake, na sasa anatibiwa katika hospitali ya Aghakhan ya Jijini Nairobi,Kenya.

Akizungumza  kutoka Bonn Ujerumani leo , Askofu Shoo ametoa  wito maalum kwa Serikali ya Rais John Magufuli, kuhakikisha wote waliohusika na unyama huo wanakamatwa.
“Nimeshtushwa na kusikitishwa sana na taarifa za kupigwa risasi Mheshimiwa Tundu Lisu. Watanzania tunapaswa kukataa na kulaani kwa nguvu zote vitendo kama hivi,”amesema na kuongeza;-
“Mimi ninaamini kuwa nguvu zile zile za uovu zilizokuwepo tangu awamu zilizotangulia ndizo zinazoendeleza unyama kama huu. Ninamwomba Mungu ampe (Lissu) uponyaji wa haraka”.
“Tundu Lissu amekuwa mstari wa mbele kufunua ufisadi unaoendeshwa na wababe wachache. Hawa wanaona sasa wameanza kutikiswa, na kwa kuwa kwao wingi wa mali na pesa ndio mungu wao”
“Hatushangai wakitumia kila njia kuzuia  ufisadi wao usianikwe hadharani. Watajaribu kila njia kuzuia ukweli  lakini wanasahau kuwa ukweli hauzuiliki milele kuna siku utajitokeza tu”.
“Kumwondoa Lissu mmoja kutazalisha Lissu maelfu. Wito wangu kwa serikali ya Dr Magufuli ni huu,  kwamba watu wote waliohusika wasakwe na wafikishwe mbele ya sheria,”.
Dk Shoo ambaye pia ni Askofu wa Dayosisi ya Kaskazini ya KKKT amesema Serikali yoyote makini inajua namna ya kuulinda upinzani kwani ukitumika vizuri unakuwa kioo cha serikali cha kujitazama.
Mara kadhaa, kiongozi huyo amekuwa akitoa hotuba zenye hisia kali akitaka Serikali na vyombo vyake vya usalama kuchukua hatua, kutokana na kuongezeka kwa matukio ya ajabu ya kihalifu.

UVCCM: Lissu si wa kwanza kupigwa risasi




Uongozi wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM), umesema mwanasheria wa Chadema, Tundu Lissu si kiongozi wa kwanza kupigwa risasi, hivyo vyombo vya dola viachwe vifanye upelelezi.
Lissu alishambuliwa na kujeruhiwa kwa risasi tano Alhamisi wiki hii nyumbani kwake Area D mjini Dodoma na sasa anaendelea na matibabu jijini Nairobi, Kenya.
Kaimu Katibu Mkuu wa umoja huo, Shaka Hamdu Shaka amesema hayo leo Jumapili, akilitaka Baraza la Vijana wa Chadema (Bavicha) lisione kwamba wao ndio wameguswa na tukio la Lissu kupigwa risasi kuliko Watanzania wengine.
“Ukweli ni kwamba sote tumeguswa na tukio hilo, jambo la msingi ni kuviachia vyombo vya Dola vifanye upelelezi,” amesema.
Shaka amesema kuna viongozi wengine walikufa kwa kupigwa risasi na uchunguzi ukafanyika kupitia vyombo vya ulinzi na usalama.
Kauli ya UVCCM imetolewa baada ya Bavicha kukaririwa ikiitaka Serikali kuunda tume huru itakayochunguza matukio ya uvunjifu wa amani likiwemo la kupigwa risasi Lissu.
Bavicha imesema tume hiyo inapaswa kuihusisha Chadema kwa kuwa viongozi wake wengi wamekumbwa na vitendo hivyo. Shaka amesema Bavicha iache kuingilia utaratibu wa upelelezi.
Amesema Rais wa Kwanza wa Zanzibar, Sheikh Abeid Amani Karume aliuawa kwa kupigwa risasi.
Kiongozi mwingine aliyeuawa kwa risasi amesema ni naibu waziri katika Serikali ya Awamu ya Pili, Nicas Mahinda.
Katika duru za kimataifa, Shaka alitoa mfano wa aliyekuwa Rais wa Marekani, John F. Kennedy na Rais wa Misri, Anuar Saadat  ambao waliuawa kwa kupigwa risasi.
“Matukio ya ujambazi yanayofanywa na watu wasiojulikana hutokea hata katika mataifa makubwa na mara nyingi upelelezi wake huchukua muda mrefu kwa wahusika kukamatwa,” amesema.
Amesema Bavicha waache kuyahusisha matukio makubwa yanayochukua uhai wa watu na masuala ya kisiasa.
Shaka amesema UVCCM inamuunga mkono Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe aliposema huu si wakati wa kunyoosheana vidole vya lawama bali viachiwe vyombo vya usalama vitimize wajibu wake.
“Mbowe ametamka matamshi yaliyopevuka kifikra, kiupeo na kisiasa,” amesema Shaka.
Amsema Bavicha wasitumie tukio la Lissu kupigwa risasi kama jukwaa lao la kufanya siasa.
Shaka amesema umoja huo unashauri wananchi wakaongozwa kwa busara kuliko ushabiki ambao unaweza kuliingiza Taifa katika machafuko.

Mdogo wake Lissu azungumza kanisani kwa Gwajima


Mdogo wake Tundu Lissu, Vicent Lissu akiwa na
Mdogo wake Tundu Lissu, Vicent Lissu akiwa na Mbunge wa Ubungo Saed Kubenea walipohudhuria Ibada katika kanisa la ufufuo na uzima. 
Vincent, mdogo wake Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu amesema kabla ya kaka yake kushambuliwa kwa kupigwa risasi aliwaeleza kwamba kuna mtu anafuatilia gari lake.
Akizungumza wakati wa ibada ya kumwombea Lissu iliyofanyika katika Kanisa la Ufufuo na Uzima leo Jumapili, amesema alimwona kaka yake akiwa amelala kitandani hospitalini mwili ukiwa na damu.
Amesema alipoamka leo asubuhi alielezwa na mtu kuwa kuna ibada maalumu ya kumwombea Lissu, hivyo akaamua kuhudhuria katika kanisa hilo la Mchungaji Josephat Gwajima.
Vincent amesema baada ya kaka yake kushambuliwa Alhamisi wiki hii, alienda Dodoma na kwamba anawashukuru madaktari waliofanya kila waliloweza kuokoa maisha ya ndugu yake.
Amesema kaka yake ni mpenda haki tangu akiwa mdogo na ameomba wananchi wazidi kumuombea.
Lissu hivi sasa anaendelea na matibabu katika Hospitali ya Aga Khan jijini Nairobi nchini Kenya.
Katika shambulio lililofanywa na watu wasiofahamika nyumbani kwa Lissu Area D mjini Dodoma, mbunge huyo alipigwa risasi tano.


Friday, September 8

Kimbunga Irma chasababisha uharibifu mkubwa Caribbean

Police patrol the area as Hurricane Irma slams across islands in the northern Caribbean on Wednesday, in San Juan, Puerto Rico, 6 SeptemberHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionKimbunga Irma kimesababisha uharibifu mkubwa huko Caribbean
Kimbunga kikali kwa jina Irma kimesababisha uharibifu mkubwa katika eneo la Caribbean ambapo takriban watu saba wameuawa.
Kisiwa kidogo cha Barbuda kilisemekana kukumbwa na uharibifu mkubwa hadi kutajwa kuwa kisichoweza kukalika huku maafisa wakionya kuwa maeneo ya kisiwa cha St Martin yanayomilikiwa na Uingereza yameharibiwa kabisa.
Jitihada za uokoaji zinatatizwa kutokana na kuwepo ugumu wa kuyafikia maeneo mengine.
Image captionKimbunga Irma kimesababisha uharibifu mkubwa huko Caribbean
Wakati huo huo upepo umetajwa kupata nguvu na kuwa vimbunga viwili.
Kimbunga Irma cha kiwango cha tano, ambacho ni kiwango cha juu zaidi kwa sasa kinapita kaskazini mwa Puerto Rico.
Zaidi ya nusu ya wakaazi wote milioni tatu wa Puerto Rico hawana umeme baaada ya kimbunga Irma kusababisha mvua kubwa na upepo mkali. Maafiasa wanasema huenda umeme ukakosa kwa siku kadhaa.
Image captionKimbunga Irma kimesababisha uharibifu mkubwa huko Caribbean
Kimbunga hicho chenye nguvu nyingi kuwai kushuhudiwa kwa miongo kadha kilikuwa na upepo wa kasi ya kilomita 295 kwa saa na kilitarajiwa kupita karibu na kwenye pwani cha Jamhuri wa Dominica leo Alhamisi
Kimbunga Irma kwanza kilikumba kisiwa cha Antigua na Barbuda. Takriban mtu mmoja aliripotiwa kuuliwa ambapo waziri mkuu Gaston Brown alisema kuwa karibu asilimia 95 ya majengo yaliharibiwa.
Image captionKimbunga Irma kimesababisha uharibifu mkubwa huko Caribbean
Hata hivyo alisema kuwa watu wote 80,000 nchini Antigua na Barbuda walinusurika maafa.
Maafisa wamethibisha vifo vya takriban watu 6 na uharibifu kwenye himaya za Ufaransa za St Martin na Saint Barthélemy.
Umeme umekatwa katika visiwa vyote na makundi ya kutoa huduma za dharura yanajaribu kufika maeneo yaliyoathirika zaidi.

Ndege za Israel zashambulia kiwanda cha silaha za kemikali nchini Syria

Ndege za Israel zashambulia kiwanda cha silaha nchini SyriaHaki miliki ya pichaIVAN SIDORENKO
Image captionNdege za Israel zashambulia kiwanda cha silaha nchini Syria
Syria inasema kuwa ndege za jeshi la Israeli zimeshambulia kituo cha kijeshi magharibi mwa nchi huku ripoti zikiseka kuwa kiwanda cha silaha za kemikali zilishambuliwa.
Taarifa za jeshi zilisema kuwa makombora yaliyofyatuliwa kutoka anga ya Lebanon yalilenga kiwanda hicho kilicho karibu na Masyaf na kuwaua wanajeshi wawili.
Ripoti ambazo hazijathibitishwa zinasema kuwa kiwanda ya kutengeneza silaha za kemikali kilishambuliwa
Israeli ambayo imefanya mashambulizi kadha kwenye viwanda vya silaha nchini Syria awalia haijasema lolote.
Kisa hicho kinatokea siku moja baada wachunguzi wa Umoja wa Mataifa kusema kuwa serikali ya Syria ilihusika na shambulizi la silaha za kemikali katika mji unaoshilkiliwa na waasi mwezi Aprili.
Image captio
Takriban watu 83 waliuawa katika mji wa Khan Sheikhoun na Styria imekana kutumia silaha za kemikali.
Ujasusi wa nchi za magharibi unasema kuwa Syria inandelea kuunda silaha za kemikali.
Isarel inaripotiwa kuendesha mashambulizi ya ndega maeneo yanayotajwa kutumika kuunda silaha za kemikali miaka ya hivi karibuni.
Hivi karibuni Isreal iliishitumu Syria kwa kuruhusu hasimu wake Iran kujenga viwanda vya makombora nchini humo na inasema inalenga kuzuia kupelekwa kwa silaha kutoka Syria hadi kwa wanamgambo wa Lebanon, Hezbolllah.

Macron ataka kujadiliwa kwa mustakabali wa Ulaya

Macron anasema hii ndio njia pekee ya kulikomboa bara hilo
Image captionMacron anasema hii ndio njia pekee ya kulikomboa bara hilo
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron ametaka kufanyika kwa mkutano wa haraka kujadili mustakabali wa bara la Ulaya.
Akizungumza mjini Athens, Macron ameonya kwamba Ulaya itakufa iwapo haitabadilika.
Amesema viongozi wa Ulaya wanapaswa kuwasilisha mapendekezo yao ifikapo mwishoni mwa mwaka, yatayofungua mjadala kwa wananchi kuamua ni aina gani ya muungano wanaouhitaji.
Mependekezo hayo yanatarajiwa kutoa picha mpya ya namna ya kuboresha umoja wa Ulaya
Image captionMependekezo hayo yanatarajiwa kutoa picha mpya ya namna ya kuboresha umoja wa Ulaya
Macron ameahidi kuwasilisha mapendelezo yake ndani ya wiki chache zijazo, huku akisema itahusisha njia za kidemokrasia zaidi ikiwemo bunge la nchi yake.

Mwanasiasa wa upinzani Tanzania Tundu Lissu apigwa risasi na watu wasiojulikana

Tundu Lissu,mwanasheria mkuu wa CHADEMAHaki miliki ya pichaBUNGE
Image captionTundu Lissu,mwanasheria mkuu wa CHADEMA
Mwanasiasa wa upinzani nchni Tanzania Tundu Lissu amepigwa risasi na watu wasiojulikana jijini Dodoma, katikati mwa Tanzania.
Mwanasiasa huyo amekimbizwa hospitali ya mkoa wa Dodoma na kupokea huduma ya kwanza na taarifa zinasema kuna mipango ya kumsafirisha hadi Nairobi kwa matibabu zaidi.
Rais wa Tanzania John Magufuli kupitia kwenye Twitter amesema amesikitishwa sana na kushambuliwa kwa mbunge huyo.
Ameandika: "Nimepokea kwa masikitiko tukio la kupigwa risasi Mh. Tundu Lissu, namuombea kwa Mwenyezi Mungu aweze kupona haraka. Aidha, vyombo vya dola viwasake wale wote waliohusika na tukio hili la kinyama na kuwafikisha ktk mikono ya sheria."
Kwa mujibu wa taarifa ya chama kikuu cha upinzani CHADEMA kwa vyombo vya habari, tukio hilo lilitokea wakati mbunge huyo wa Singida Mashariki akiwa nyumbani kwake.
Chama hicho kimelaani vikali tukio hilo.
Wakati huo huo, Chama tawala cha CCM, kupitia Katibu wao wa Itikadi na Uenezi,imesema kimepokea kwa mstuko mkubwa kushambuliwa kwa mbunge huyo wa upinzani.
"Chama cha Mapinduzi (CCM) kinalaani tukio hilo la kikatili na lisilo na utu tunalitaka Jeshi la Polisi kuwatafuta, kufanya uchunguzi wa tukio hili na kuchukua hatua kali za kisheria kwa wote waliohusika."
Kamanda wa polisi mkoani Dodoma, Kamishna Msaidizi, Jires Mroto ameiambia BBC kuwa wameanza uchunguzi wa tukio hilo.
"Tunaomba wananchi wenye taarifa ya uhalifu huu, waweze kujitokeza" amesema Kamanda Mroto.
Hivi karibuni, mbunge huyo kutoka chama cha upinzani cha CHADEMA, amekuwa akikamatwa mara kwa mara na polisi akishutumiwa kufanya uchochezi.
Kiongozi wa chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, akithibitisha tukio la leo alisema, amesema "yupo hospitali, bado anajaribu kupambana kuokoa maisha yake"
Gazeti la Mwananchi nchini Tanzania, limemnukuu Mganga mkuu wa hospitali ya Dodoma akisema wakili huyo ana majeraha ya risasi miguuni na tumboni.

Wednesday, September 6

Tom Thabane alaani mauaji ya mkuu wa jeshi Lesotho

Thabane amesema mauaji hayo yanarudisha nyuma juhudi za kutafuta amani nchini humo
Image captionThabane amesema mauaji hayo yanarudisha nyuma juhudi za kutafuta amani nchini humo
Waziri mkuu wa Lesotho ameelezea mauaji ya mkuu wa kikosi cha jeshi Khoantle Mots'omots'o yaliyofanywa na maafisa wa jeshi kama kitendo cha kurudisha nyuma juhudi za kutafuta amani nchini humo.
Tom Thabane amesema upelelezi unaendelea juu ya tukio hilo lililotokea katika mji mkuu Maseru siku ya Jumanne.
Mashuhuda wanasema, watu wawili waliovalia sare za jeshi waliingia katika ofisi ya Mots'omots'o na kisha kumfyatulia risasi kabla ya wao kuuawa na walinzi wa kiongozi huyo.
Lesotho ipo katika hali ya taharuki, ikiwa na hostoria ya mapinduzi ya kijeshi ya mara kwa mara.