Friday, September 8

Macron ataka kujadiliwa kwa mustakabali wa Ulaya

Macron anasema hii ndio njia pekee ya kulikomboa bara hilo
Image captionMacron anasema hii ndio njia pekee ya kulikomboa bara hilo
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron ametaka kufanyika kwa mkutano wa haraka kujadili mustakabali wa bara la Ulaya.
Akizungumza mjini Athens, Macron ameonya kwamba Ulaya itakufa iwapo haitabadilika.
Amesema viongozi wa Ulaya wanapaswa kuwasilisha mapendekezo yao ifikapo mwishoni mwa mwaka, yatayofungua mjadala kwa wananchi kuamua ni aina gani ya muungano wanaouhitaji.
Mependekezo hayo yanatarajiwa kutoa picha mpya ya namna ya kuboresha umoja wa Ulaya
Image captionMependekezo hayo yanatarajiwa kutoa picha mpya ya namna ya kuboresha umoja wa Ulaya
Macron ameahidi kuwasilisha mapendelezo yake ndani ya wiki chache zijazo, huku akisema itahusisha njia za kidemokrasia zaidi ikiwemo bunge la nchi yake.

No comments:

Post a Comment