Friday, September 8

Ndege za Israel zashambulia kiwanda cha silaha za kemikali nchini Syria

Ndege za Israel zashambulia kiwanda cha silaha nchini SyriaHaki miliki ya pichaIVAN SIDORENKO
Image captionNdege za Israel zashambulia kiwanda cha silaha nchini Syria
Syria inasema kuwa ndege za jeshi la Israeli zimeshambulia kituo cha kijeshi magharibi mwa nchi huku ripoti zikiseka kuwa kiwanda cha silaha za kemikali zilishambuliwa.
Taarifa za jeshi zilisema kuwa makombora yaliyofyatuliwa kutoka anga ya Lebanon yalilenga kiwanda hicho kilicho karibu na Masyaf na kuwaua wanajeshi wawili.
Ripoti ambazo hazijathibitishwa zinasema kuwa kiwanda ya kutengeneza silaha za kemikali kilishambuliwa
Israeli ambayo imefanya mashambulizi kadha kwenye viwanda vya silaha nchini Syria awalia haijasema lolote.
Kisa hicho kinatokea siku moja baada wachunguzi wa Umoja wa Mataifa kusema kuwa serikali ya Syria ilihusika na shambulizi la silaha za kemikali katika mji unaoshilkiliwa na waasi mwezi Aprili.
Image captio
Takriban watu 83 waliuawa katika mji wa Khan Sheikhoun na Styria imekana kutumia silaha za kemikali.
Ujasusi wa nchi za magharibi unasema kuwa Syria inandelea kuunda silaha za kemikali.
Isarel inaripotiwa kuendesha mashambulizi ya ndega maeneo yanayotajwa kutumika kuunda silaha za kemikali miaka ya hivi karibuni.
Hivi karibuni Isreal iliishitumu Syria kwa kuruhusu hasimu wake Iran kujenga viwanda vya makombora nchini humo na inasema inalenga kuzuia kupelekwa kwa silaha kutoka Syria hadi kwa wanamgambo wa Lebanon, Hezbolllah.

No comments:

Post a Comment