Friday, September 8

Kimbunga Irma chasababisha uharibifu mkubwa Caribbean

Police patrol the area as Hurricane Irma slams across islands in the northern Caribbean on Wednesday, in San Juan, Puerto Rico, 6 SeptemberHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionKimbunga Irma kimesababisha uharibifu mkubwa huko Caribbean
Kimbunga kikali kwa jina Irma kimesababisha uharibifu mkubwa katika eneo la Caribbean ambapo takriban watu saba wameuawa.
Kisiwa kidogo cha Barbuda kilisemekana kukumbwa na uharibifu mkubwa hadi kutajwa kuwa kisichoweza kukalika huku maafisa wakionya kuwa maeneo ya kisiwa cha St Martin yanayomilikiwa na Uingereza yameharibiwa kabisa.
Jitihada za uokoaji zinatatizwa kutokana na kuwepo ugumu wa kuyafikia maeneo mengine.
Image captionKimbunga Irma kimesababisha uharibifu mkubwa huko Caribbean
Wakati huo huo upepo umetajwa kupata nguvu na kuwa vimbunga viwili.
Kimbunga Irma cha kiwango cha tano, ambacho ni kiwango cha juu zaidi kwa sasa kinapita kaskazini mwa Puerto Rico.
Zaidi ya nusu ya wakaazi wote milioni tatu wa Puerto Rico hawana umeme baaada ya kimbunga Irma kusababisha mvua kubwa na upepo mkali. Maafiasa wanasema huenda umeme ukakosa kwa siku kadhaa.
Image captionKimbunga Irma kimesababisha uharibifu mkubwa huko Caribbean
Kimbunga hicho chenye nguvu nyingi kuwai kushuhudiwa kwa miongo kadha kilikuwa na upepo wa kasi ya kilomita 295 kwa saa na kilitarajiwa kupita karibu na kwenye pwani cha Jamhuri wa Dominica leo Alhamisi
Kimbunga Irma kwanza kilikumba kisiwa cha Antigua na Barbuda. Takriban mtu mmoja aliripotiwa kuuliwa ambapo waziri mkuu Gaston Brown alisema kuwa karibu asilimia 95 ya majengo yaliharibiwa.
Image captionKimbunga Irma kimesababisha uharibifu mkubwa huko Caribbean
Hata hivyo alisema kuwa watu wote 80,000 nchini Antigua na Barbuda walinusurika maafa.
Maafisa wamethibisha vifo vya takriban watu 6 na uharibifu kwenye himaya za Ufaransa za St Martin na Saint Barthélemy.
Umeme umekatwa katika visiwa vyote na makundi ya kutoa huduma za dharura yanajaribu kufika maeneo yaliyoathirika zaidi.

No comments:

Post a Comment