Thursday, May 23

Bajeti Nishati kupoza kiu ya Wanamtwara?

Profesa Sospeter Muhongo 

Dodoma/Mtwara. Wakati mjadala mkali ukitarajiwa kuibuka bungeni leo wakati Serikali itakapokuwa ikiwasilisha bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini, joto limezidi kupanda mkoani Mtwara ikielezwa kuwa wananchi wamehamasishana kwa mara nyingine kuacha shughuli zote ili kusikiliza kama hotuba hiyo italinda masilahi yao.
Hotuba hiyo ambayo itasomwa leo mara baada ya kipindi cha maswali na majibu bungeni na Waziri wa wizara hiyo, Profesa Sospeter Muhongo, inatarajiwa kuibua mengi yakiwamo yanayohusu suala la gesi ya Mtwara.
Mjini Mtwara vipeperushi vinavyopingana vilisambazwa kuhamasishana ‘kuacha shughuli zao zote na kubaki nyumbani ili kufuatilia matangazo ya televisheni wakati Profesa Muhongo atakapotangaza bajeti hiyo, huku vingine vikipinga.
Ahadi za matumaini
Licha ya kampeni hizo za watu wa Mtwara, Serikali nayo imeweka matangazo katika vyombo vya habari likiwemo gazeti hili ikieleza namna mikoa ya Mtwara na Lindi itakavyonufaika na utafutaji na uendelezaji wa Gesi Asilia.
Tangazo lililotolewa na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania limeainisha faida za gesi hiyo kwa Mkoa wa Mtwara ukiwamo umeme utakaotokana na gesi asilia. Pia imeelezwa jinsi mafunzo kwa vijana juu ya matatizo ya gesi asilia yaliyodhaminiwa na Wizara ya Nishati na Madini na kampuni mbalimbali kuanzia mwaka 2010.
Vilevile imeelezwa jinsi uboreshaji wa huduma za jamii kama ujenzi wa shule, hospitali na ujenzi wa viwanda kama kile cha saruji cha Dangote na mitambo ya kusafishia gesi utakavyowanufaisha wakazi wa mkoa huo.
Gesi hiyo ambayo pia inachimbwa katika Kisiwa cha Songosongo inatajwa kwamba itawanufaisha wakazi wa Mkoa wa Lindi kwa kupata umeme, kunufaika na kodi ya wawekezaji wa gesi na udhamini wa mafunzo kutoka kampuni mbalimbali na wizara.
Wiki iliyopita Profesa Muhongo alijigamba kuwa bajeti ya wizara yake atakayosoma leo itakuwa ya karne ya 22 itakayomaliza tatizo la umeme nchini kwa kuwa imetoa vipaumbele kwa sekta binafsi kusaidia upatikanaji wa umeme wa uhakika.
Wabunge wapania
Dalili za kuibuka mjadala mkali katika bajeti ya leo zilianza kujitokeza mwishoni mwa wiki wakati wa semina ya wabunge kuhusu masuala ya gesi ambapo wizara hiyo ilibanwa juu ya mambo ya mikataba.
Hata hivyo, semina hiyo ilitafsiriwa kuwa ililenga kuwapoza wabunge na kupunguza hasira zao huku wizara ikijipanga namna ya kuwashawishi waikubali bajeti baada ya kuona mwelekeo wao.
Wasiwasi Mtwara
Hali ya wasiwasi imeanza tena kutanda mkoani hapa hasa kutokana na vipeperushi vinavyokinzana na ujumbe tofauti kwa njia ya simu unaosambazwa.
Hali hiyo imejirudia tena huku ikionekana dhahiri kuwa na kauli kutoka makundi tofauti zinapishana katika vipeperushi hivyo huku wengine wakitaka mwendelezo wa kusitisha huduma ufanyike na wengine wakipinga.
Mojawapo ya kipeperushi kilisisitiza huduma zote zisitishwe kuanzia bajaji, bodaboda, masoko na magari yote yaendayo mikoani na wilayani yasiingie wala kutoka.
Huku vipeperushi vingine vikipinga: “Tunafahamu gesi ni mali yetu wote Wanakusini na tunafahamu kunyanyasika kwetu na Serikali ya nchi yetu na Mei 17 tuliunga mkono kufunga maduka na biashara zote, lakini hatukunufaika na chochote.
“Sasa Jumatano tena tusifanye biashara. Tuache ujinga Wanakusini wenzetu wengine hawana kazi wala gesi. Kampeni zitafanya tuwe maskini zaidi. Tarehe 22.05.2013 hatufungui duka wala hoteli, hata soko,” kilisomeka kimoja kati ya vipeperushi hivyo.
Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Linus Sinzumwa aliwataka wananchi waendelee na shughuli zao za kila siku bila kujali vitisho hivyo kwa kile alichokidai kuwa ulinzi umeimarishwa.
ya za Tandahimba, Masasi, Newala na Nanyumbu waliendelea na shughuli za uzalishaji bila bughudha


Wednesday, May 22

BUNGE lisitishwa jioni hii kutokana na hali tete ya mtwara



Spika ameahirishwa bunge hadi kesho kutokana na hali ya Mtwara. Spika kasema amepokea hali ya vurugu mtwara, hivyo bunge limeahirishwa ili kutoa fursa kwa kamati ya bunge kujadili suala hilo na serikali imetakiwa kutoa majibu katika kikao cha kesho.
Spika kasema kuwa wabunge wangependa kujadili hali ya Mtwara leo  lakini watajadili nini wakati hata wao wabunge wamepata taarifa hizo  kwenye vyombo vya habari? Hivyo, akaiagiza serikali kuleta majibu sahihi kesho bungeni na kuwaomba wabunge kuwa na subira hadi kesho na kisha akaahirisha bunge.
Akahitimisha kwa kusema kamati ya bunge inakwenda kujadili suala hilo sasa hivi.

Breaking News: Vurugu za Mtwara


Askari wanne na Wananchi Kadhaa Wameuawa. Hadi kufikia saa hii (3:00 pm) kuna taarifa kwamba ofisiza CCM (maeneo ya Mdenganamadi na Majengo) zimechomwa moto; askari wanne wameuawa pamoja na wananchi kadhaa. Wananchi wanatumia baruti za kulipulia samaki kuwalipua majengo na askari.Hatari iliyopo ni kuchomwa kwa jengo la ofisi za mkuu wa mkoa. Yote haya ni kupinga bomba la gesi kujengwa kuelekea DSM.
Habari zilizofika muda huu zinaripoti kwamba hali sio nzuri huko Mtwara, kwa ufupi hali ni tete na hakuna amani, mabomu ya machozi yanarindima muda huu na huduma zote za kijamii zimefunngwa hakuna usafiri, masoko, maduka na bar zote zimefungwa, daladala, Taxi na Bodaboda hazifanyi kazi. Kwa ujumla kinachoendelea ni mapambano makali kati ya Jeshi la polisi na wananchi wenye hasira wanaopinga vikali kuendelea kwa mchakato wa gesi ilihali nchi ikiwa haina sera inayosimamia nishati hiyo.
Kufuatia Kambi ya Upinzani kuukataa mpango wa serikali wa ujenzi wa bomba la gesi kutoka Mtwara Mpaka Dar es salaam ilihali Waziri wa Nishati akisoma hotuba yake kwa hisia kali na mbwembwe na kusema bomba la gesi linajengwa kutoka Mtwara kwenda Dar es salaam Wananchi wa Mtwara wacharuka!
Daraja la Mikindani limevunjwa hakuna mawasiliano Mtwara na Dar es salaam.
Baadhi ya Wananchi wamepora Silaha na wanazitumia kujibu mashambulizi ya Jeshi la Polisi (habari haijathibitishwa rasmi)
Jengo la Ofisi ya CCM saba saba limechomwa moto.
Nyumba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, (Tamisemi), Hawa Ghasia yachomwa moto.
Lodge/Hotel (Shengena) inayoaminika kwamba ndiyo waliyofikia Askari wa Jeshi la Polisi (FFU) kutoka mikoa ya jirani kwaajili ya operation inayoendelea imechomwa moto.
Milio ya risasi na mabomu ndicho kinachosikika.
Nyumba kadhaa za watumishi wa Serikali zimechomwa maeneo ya Shangani. (habari haijathibitishwa rasmi)
Ni magari ya FFU ndio yaliyopo barabarani nayo yanapata wakati mgumu kupita kwasababu ya mawe na magogo makubwa yaliyowekwa na Wananchi.
Askari kadhaa wamekufa (habari hii haijathibitishwa rasmi)
Baadhi ya watu kadhaa wamechukuliwa na askari kwakuwa wamepita jirani na gari yao.
Yadaiwa askari wengi waliokuja si wa Mtwara, wengi wametoka Masasi na Lindi.
Ving'ora vinalia hovyo. Watoto wamefungiwa mashuleni walimu wamekimbia.
Vituo vya Redio vya Mtwara havizungumzii hali hii ya hatari bali vinapiga Muziki pengine vinakusanya matukio na habari ya majanga haya ili Wananchi wayapate.
Mabomu yanapigwa mfululizo maeneo ya Magomeni-Mtwara, mpaka sasa takriban mabomu 20 na ushee yameshapigwa.
Wakati waziri wa Nishati akisoma hotuba yake kwa hisia kali na mbwembwe na kusema bomba la gesi linajengwa kutoka Mtwara kwenda Dar Kauli mbiu ya Wananchi wa Mtwara ni "Gesi haitoki hata kwa bomba la peni"
Wananchi walalamikia kituo cha Television na Radio TBC kuzuia na kukata mawimbi yake kutoonekana wala kusikika katika Mkoa wa Mtwara kwa muda. Hatimaye hivi Punde matangazo yarejea.
Hili linaendelea wakati bajeti ya nishati na madini ikiendelea kujadiliwa muda huu Bungeni.

Bandari D’Salaam yapoteza Sh3 trilioni kwa mwaka


Dar es Salaam. Bandari ya Dar es Salaam imekuwa ikilikosesha taifa Dola 1.8 bilioni za Marekani (Sh2.8 trilioni) kwa mwaka, kutokana na kukosa ubora wa biashara.
Kutokana na hali hiyo, wataalamu wameeleza kuwa bandari hiyo inahitaji kufanyiwa maboresho muhimu ya hali ya juu, ili fedha hizo zisaidie nchi kuacha kutegemea misaada ya maendeleo.
Kwa mujibu wa ripoti iliyopo kwenye kitabu cha Opening the Gates: How the port of Dar es Salaam can transform Tanzania, licha ya Bandari ya Dar es Salaam kuwa sehemu nzuri, imekosa uwezo hivyo usimamiaji sera bora za kuiboresha zinatekelezwa taratibu. Ripoti hiyo inaeleza kuwa, mwaka 2012 pekee bandari hiyo ilikosesha taifa kiasi hicho cha fedha, huku ikizikosesha nchi jirani Sh1.3 trilioni.


“Fedha hizo ni sawa na asilimia saba ya pato la taifa, kitu ambacho kinawaathiri wanunuzi, wafanyabiashara na wakala mbalimbali wa Serikali,” inaeleza.
Mchumi Mkuu wa Benki ya Dunia (WB), Jacques Morisset ameihimiza Tanzania kuifanya bandari hiyo kuwa moja ya vipaumbele vyake vya juu kwa ajili ya kukua kwa uchumi.
“Watumiaji Bandari ya Dar es Salaam wanalipa fedha nyingi kwa wasimamizi wa bandari na wakala mbalimbali, kwa ajili ya huduma zao kuliko Mombasa,” alisema Morisset.
Akizungumzia ripoti hiyo, Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe alisema Serikali imekuwa ikijitahidi kuboresha bandari hiyo, lakini kazi ya ziada inahitajika kuifanya iweze kushindana na nyingine.


“Tunahitaji nchi jirani ziendelee kuitumia bandari yetu, bado tuna kazi kubwa ya kufanya ndiyo maana niko hapa, tunahitaji kuimarisha Kitengo cha Operesheni na maeneo mengine,” alisema Dk Mwakyembe.

Maalim Seif: Nitaomba kuwania tena urais mwaka 2015

Dar es Salaam. Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharrif Hamad amesema ataomba tena kugombea urais kupitia Chama cha Wananchi (CUF) katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.
Akizungumza katika kipindi cha Dakika 45 kinachorushwa na kituo cha runinga cha ITV, Maalim Seif alisema kuwa anachoomba tu Mwenyezi Mungu ampe afya njema.
“Ni uamuzi wa wananchi na wanachama wenyewe wa CUF lakini kama Mwenyezi Mungu akinipa afya na uzima bado nia ipo,” alisema Seif ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar.
Alisema hivi sasa chama hicho kimekuwa kikijiimarisha visiwani huko kwa kufanya mikutano Pemba na Unguja ili kuhakikisha kinaendelea kukubalika kwa wananchi.
Kauli hiyo ya Maalim Seif ambaye amekuwa akiwania nafasi hiyo tangu kuingia kwa mfumo wa vyama vingi, ilipokewa kwa hisia tofauti ambapo Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Bashiru Ali alisema vyama vya siasa ni lazima viwe vinatayarisha viongozi wa baadaye ambao watafahamu kwamba uongozi ni dhamana wanayopewa na wananchi.
Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Julius Mtatiro alisema Maalim Seif kama mwanachama wa chama hicho anaruhusiwa kwa mujibu wa Katiba kugombea nafasi yoyote ya uongozi wa dola.

UJIO WA RAIS OBAMA NCHINI TANZANIA

Rais wa Marekani Bw. Baraka Obama na Mkewe wanatarajia kufanya ziara ya nchi tatu barani Afrika itakayojumuisha nchi za Senegal, Afrika ya Kusini na Tanzania, Kuanzia tarehe 26 Juni hadi tarehe 3 Julai.

Katika ziara yake hiyo, Rais atawekea mkazo umuhimu ambao Marekani inauweka katika ushirikiano wetu wa kina na unaoendelea kuimarika na nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kupitia mipango mbalimbali ikiwemo ile ya kuimarisha ukuaji wa uchumi, uwekezaji na biashara, uimarishaji wa taasisi za kidemokrasia na uwekezaji katika kizazi kipya cha viongozi wa Kiafrika.

Rais atakutana na viongozi mbalimbali wa kiserikali, sekta binafsi na jumuiya huru ya kiraia ikiwemo vijana ili kujadili ubia wetu wa kimkakati katika ushirikano wetu rasmi na masuala mengine ya kimataifa.

Ziara hii itadhihirisha dhamira ya dhati ya Rais ya kupanua na kuimarisha ushirikiano kati ya Marekani na watu wa nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara katika kuimarisha amani na ustawi katika kanda hii na duniani kote kwa ujumla

Lissu abadili mbinu uzinduzi kampeni

Mbunge wa Same Mashariki (CCM), Anna Kilango akizozana na mnadhumu wa kambi ya upinzani, Tundu Lissu nje ya ukumbi wa Bunge jana baada ya Spika kuahirisha Bunge akiagiza hotuba ya kambi ya upinzani kuhusu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kufanyiwa marekebisho.Picha na Emmanuel Herman 

Ikungi. Mgeni rasmi katika uzinduzi wa kampeni ya uzinduzi wa nafasi ya udiwani Kata ya Iseke Tarafa ya Ihanja, Wilaya ya Ikungi, Tundu Lissu, juzi alishindwa kuuza sera za Chadema, na badala yake alitumia muda mwingi kuhimiza ‘sera ya kuwakataza’ wananchi kuchangia maendeleo yao .
Tundu ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki kupitia chama hicho, alipanda jukwaani huku akiwa amebeba makabrasha ya michanganuo ya Bajeti ya Serikali ya kuanzia mwaka wa fedha wa 2010/11 hadi 2013/14.

“Mimi leo sitaki kabisa kuzungumzia habari za Amosi Mghenyi ambaye ametusaliti kwa kuhama Chadema na kurejea CCM. Amosi kisiasa ni mfu, kwa hiyo siwezi kupoteza muda wangu kuzungumiza mambo ya mfu”,alisema na kushangiliwa kwa nguvu na wananchi waliohudhuria uzinduzi huo uliofanyika katika kijiji cha iseke.
Alisema ufunguzi wake utajikita zaidi katika kuwaelimisha wananchi wa Kata ya Iseke kwamba Serikali inazo fedha nyingi na za kutosha kugharamia maendeleo ya wananchi.
Akijenga hoja yake hiyo, alisema kwa mfano katika mwaka wa fedha wa mwaka 2010/11, Mkoa wa Singida, ulipewa zaidi ya Sh903 milioni za undeshaji wa shule, lakini zilizotumika ni Sh464 milioni na kubaki Sh438.2.
Alisema fedha hizo zaidi ya Sh438.2 milioni zilizobaki, hazijaainishwa zilipelekwa wapi. “Kwa vyo vyote zitakuwa zimeishia kwenye matumbo ya mgambo na watendaji wa Serikali ya CCM”.
Lissu ambaye pia ni mwanasheria kitaaluma, aliwataka wakazi wa Kata ya Iseke, kumchagua Emmnuel Jackson Jingu awe diwani wao.
ili waondokane na manyanyaso ya michango kama walivyojikomboa wakazi wa Jimbo la Singida Mashariki.
Wagombea wengine wa nafasi ya udiwani Kata ya Iseke, ni Amosi Munghenyi wa CCM na Abdallah Kinyenje maarufu kwa jina la Petro wa CUF.

JK: Lowasa jembe


Dodoma/Dar es Salaam. Rais Jakaya Kikwete amemwagia sifa Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa hatua ambayo inaweza kutafsiri mengi katika medani ya siasa nchini.
Akizungumza na wabunge wa CCM kwenye Ukumbi wa White House Dodoma juzi, Rais Kikwete ambaye pia mwenyekiti wa chama hicho, alisema nguvu za Lowassa pekee zinatosha kushinda uchaguzi mdogo wa kiti cha udiwani Kata ya Makuyuni kilichoko wilayani Monduli.
Kata ya Makuyuni iko wilayani Monduli, ambako Lowassa amekuwa mbunge wake tangu mwaka 1995.
Habari za kutoka ndani ya kikao hicho zinaeleza kuwa Rais Kikwete alitoa kauli hiyo kuhusu kampeni za uchaguzi huo wa Makuyuni, baada ya kuwa ametoa ruksa kwa makada wa chama hicho wanaotaka urais kuanza kujipitisha pitisha miongoni mwa wanachama wa chama hicho. Lowassa anatajwa kuwa miongoni mwa wanaCCM wanaotaka kumrithi Rais Kikwete kwenye Uchaguzi Mkuu mwaka 2010.
“Sina tatizo na pale Makuyuni, najua muscles (misuli) za Mzee Lowassa zinatosha kutupa ushindi; au vipi mzee?” alidokeza mmoja wa wabunge wa CCM akimnukuu Rais Kikwete.
Uchaguzi wa Udiwani Kata ya Makuyuni unaotarajiwa kufanyika Juni 16, mwaka huu, utakuwa wa ushindani mkali kati ya CCM na Chadema ambao historia yao kisiasa mkoani Arusha ni ya uhasama.
Katika uchaguzi huo, unaofanyika baada ya kifo cha Abdillah Warsama (CCM), chama hicho kitatetea nafasi yake kwa kumsimamisha Godluck Lerunya na Chadema ni Japhet Sironga.
Mbali na Kata ya Makuyuni, uchaguzi wa udiwani mkoani Arusha utafanyika pia katika Kata za Kaloleni, Themi, Kimandolu na Elerai, kutokana na waliokuwa madiwani wa kata hizo (Chadema), kufukuzwa na chama chao.
“Mnaweza kuchafuana leo, kesho mkapata mgombea mwenye nundu nyingi na mabandeji kila mahala, halafu mkapata shida kumnadi,” alisema.
Siyo mara ya kwanza kwa Kikwete kumsifia Lowassa kwani aliwahi kufanya hivyo mwaka jana huko Longido wakati akikabidhi ng’ombe.
Pia aliwahi kumsifia wakati wa kampeni za uchaguzi za mwaka 2010 wakati Kikwete alipomwelezea Lowassa kama Mbunge makini na kuwaomba watu wa Monduli kumchagua tena.
Hata hivyo, alipoulizwa kama baada ya kuruhusiwa kuanza kujipitisha kwa wanaCCM kama anataka kuwania urais, Lowassa alijibu kupitia watu wake wa karibuni kuwa asingependa kuzungumzia suala hilo hasa baada ya Rais kutoa kauli hiyo.
Kutangaza nia ruksa
Rais Kikwete aliwaeleza wabunge hao kuwa si kosa kwa watu kutangaza nia ya kugombea nafasi mbalimbali za uongozi ikiwamo urais mwaka 2015.
“Wabunge na mawaziri wenye nia ya kutangaza nia ya kugombea urais wawe huru, kwani hiyo ni haki yao, isipokuwa wafanye kwa wema bila kukivuruga chama na kuwagawa wanaCCM katika makundi. Sioni tatizo watu kujipitisha. Sisi sote hapa tulijipitisha. Lakini tufanye hivyo kistaarabu bila kuvurugana.”
Aliwaagiza wabunge wa chama hicho kwenda majimboni mwao kusikiliza kero za wananchi badala ya kusubiri wakati wa uchaguzi.
Membe
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe ambaye naye anatajwa kuwa miongoni mwa wagombea amewataka waandishi waache kuandika kila siku habari za urais na badala yake waandike mambo ya maendeleo.
Akizungumza na waandishi wa habari jana baada ya kukutana na mabalozi wa nchi zinazoendelea kuhusu Mkutano wa Smart Partnership, unaotarajiwa kufanyika nchini, Membe alisema ni vizuri yakaandikwa mambo ya maendeleo na si kila wakati kuandika mambo ya urais.
“Mkutano kama huu nchi kama Kenya watauripoti vizuri na kwa undani hivyo mfanye hivyo si kila kitu urais 2015,” alisema Membe. Mkutano huo utaanza Mei 28, hadi Juni Mosi na utajadili jinsi gani sayansi na teknolojia vinaweza kutumika kuzikwamua kiuchumi.
Imeandikwa na Kizitto Noya, Habel Chidawali na Boniface Meena.

Tuesday, May 21

hotuba ya SUGU bungeni


Hotuba ya upinzani yaahirisha Bunge


Dodoma. Mjadala wa Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo jana uliingia dosari na kulazimika kusitishwa kwa muda baada ya Bunge kukubaliana na hoja ya Mbunge wa Mbozi Magharibi (CCM), Godfrey Zambi kuwa Hotuba ya Kambi ya Upinzani, imejaa uchochezi.
Zambi alitoa hoja hiyo wakati Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi alipokuwa akiwasilisha hotuba ya Kambi ya Upinzani kuhusu makadirio hayo, baada ya kuomba mwongozo wa Spika.
“Kuhusu utaratibu,” alisema Zambi. Baada ya kurudia kauli hiyo mara kadhaa, Spika wa Bunge, Anne Makinda alimsitisha Mbilinyi kuendelea na hotuba yake na kumpa Zambi nafasi.
“Mheshimiwa Spika, hotuba hii ya upinzani ni ya uchochezi. Sisi kama Bunge hatuwezi kuruhusu ikaendelea kusomwa hapa na Watanzania wakasikiliza uongo. Kuanzia ukurasa wa kwanza hadi wa 14, imejaa uongo tu,” alisema Zambi na kuongeza:
“Kusema kwamba Tanzania inawatesa waandishi wa habari kwa kuwang’oa meno na kucha, siyo kweli. Huu ni uchochezi na ningependa kutoa hoja hotuba hiyo iondolewe bungeni, ni ya kichochezi.”
Baada ya kutoa hoja hiyo, karibu wabunge wote wa CCM walisimama kumuunga mkono na baadaye, Spika wa Bunge Anne Makinda alisimama na kusema: “Naomba wote mkae chini... kwanza kaeni,” kisha aliendelea: “Humu humu bungeni, sisi wenyewe, tulipitisha kanuni kwamba tusiingize neno uchochezi kwenye mijadala yetu. Haya, sasa naahirisha kikao mpaka jioni na naagiza Kamati ya Kanuni iende ikapitie hotuba hiyo kwanza kabla haijaletwa tena bungeni.”
Nje ya Bunge
Wakiwa wanatoka bungeni, mvutano ulioanzia ndani ya ukumbi, uliibuka nje ya lango kuu la Bunge ambako wabunge kadhaa wa CCM na Chadema waliendeleza mjadala huo na kuzozana hadharani.
Wabunge waliozozana kuhusu hotuba hiyo nje ya ukumbi ni Mnadhimu wa Kambi ya Upinzani bungeni, Tundu Lissu, Mbunge wa Same Mashariki (CCM), Anna Kilango, Mbunge wa Tabora Mjini (CCM), Ismail Aden Rage na Lucy Kihwelu (Viti Maalumu Chadema).
“Hamuwezi mkaharibu kanuni za Bunge letu kwa hotuba zenu za uchochezi,” alisema Kilango akimwambia Lissu.
“Hiyo kanuni ni ipi ambayo tumeiharibu? Huo ni ukorofi wenu tu, tunafahamu siku nyingi,” alijibu Lissu.
Baadaye akadakia Rage; “Hawa dawa yao ni .....” Kauli hiyo ya Rage ilijibiwa na Kihwelu aliyemwambia “Makofi yako ni Yanga tu. Umesahau umepigwa mabao 2-0.”
Mbilinyi atetea hotuba yake
Akizungumza na waandishi wa habari nje ya Ukumbi wa Bunge, Mbilinyi alitetea hotuba yake akisema kuwa haina tatizo lolote na imefuata kanuni zote za kusomwa bungeni.
“Hili kwetu (Chadema) ni changamoto, ila niseme tu kwamba hotuba yangu haikuwa na tatizo lolote na ilipitia hatua zote halali kabla ya kusomwa bungeni,” alisema.
Utaratibu uliowekwa na Bunge unataka hotuba za hoja za bajeti kuwasilishwa kwa Spika siku mbili kabla ya kusomwa.
Alisema hotuba hiyo haina chembe ya uongo, akisema ni ukweli kwamba waandishi nchini hawana uhuru wa kufanya kazi na baadhi wanateswa na kunyanyaswa.
Baadaye jioni
Katika kikao cha jioni, Spika Makinda alitoa mwongozo wake na kueleza sababu za kuahirisha hotuba ya Mbilinyi na kusema anakubaliana na hoja iliyokuwa imetolewa asubuhi na Zambi kwamba maneno yaliyopo katika hotuba ya Mbilinyi kuanzia ukurasa wa kwanza hadi wa 14 yaondolewe kwa kuwa yanaingilia Mahakama.
“Kwa kutumia Kanuni ya 72 ni mamlaka ya Spika kusimamia Bunge hivyo kwa kutumia Kanuni ya 64, naagiza maneno yote yanayozungumzia mauaji ya Daudi Mwangosi yaondolewe,” alisema Spika Makinda.
Alisema amefikia uamuzi huo baada ya Kamati ya Kanuni kupitia hotuba hiyo na kuona kwamba maneno yaliyopo katika kurasa hizo yanaingilia mhimili wa mahakama.
Baada ya Spika kueleza hayo, Mbilinyi aliruhusiwa kuendelea na hotuba yake na kuomba kuanzia jana jina la Sugu lisitumike tena bungeni.

SPIKA WA BUNGE AAMURU KUFUTWA KWA HOTUBA YA SUGU ILIYOSABABISHA BUNGE LISITISHWE ASUBUHI




Spika wa Bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Mh Anne Makinda, ameamuru kambi ya upinzani kuyaondoa maneno yote yaliyomo kuanzia ukurasa wa kwanza mpaka wa 14 katika hotuba rasmi ya Kambi ya upinzani iliyosmwa na mbunge wa Mbeya Mjini, Mh. Joseph Mbilinyi ‘Sugu,’ ambaye ni Waziri Kivuli wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.

Mh. Makinda ametoa amri hiyo baada ya Kamati ya Kanuni ya Bunge kujadili hotuba hiyo na kubaini kuwa ina kauli za uchochezi; na kusema kuwa kuwa Bunge sio sehemu kugombanisha wananchi, hivyo maneno yote ya uchochezi hayaruhusiwi.

Katika hotuba hiyo, Mh. Mbilinyi aliishutumu serikali kuhusika na kuteka nyara waandishi wa habari, kauli iliyopelekea Spika Makinda kuahirisha Bunge.

Monday, April 15

Mbowe, Slaa: Hatukubali Chadema kuhujumiwa

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe akizungumza kwenye kongamano la chama hicho lililofanyika jana jijini Dar es Salaam. Picha na Fidelis Felix.

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Willibrod Slaa wamesema “hawatakubali wala kuvumilia” hujuma dhidi ya chama chao.
Dar es Salaam. Viongozi hao kwa nyakati tofauti jana walisema hujuma hizo zimekuwa zikifanywa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) pamoja na Serikali ambayo imekuwa ikitumia vyombo vya dola na kwamba sasa wanapanga ugaidi wa kuwateka maofisa wa ngazi ya juu wa Chadema.
Suala la ugaidi liliibuka kwa nguvu katika wiki ya kwanza ya Bunge la Bajeti na sasa limehamia nje ya chombo hicho cha kutunga sheria kutokana na Chadema kuwatuhumu CCM na Serikali yake kwamba wanapanga njama za kuwateka maofisa wakuu wa chama hicho.
Jana Dk Slaa alipokuwa akimkaribisha Mbowe kufungua Mkutano wa Mafunzo na Mipango ya Vuguvugu la Mabadiliko ‘M4C’ na Kongamano la Katiba Mpya kwa Kanda ya Dar es Salaam na Pwani, alisema taarifa walizonazo zinaonyesha kuwa CCM ndiyo wanaofanya vitendo vya kigaidi wakishirikiana na Serikali.
“Tuna taarifa zote zinazoonyesha kwamba CCM ndiyo magaidi wakishirikiana na Serikali yake, lakini sisi tuko makini kuliko hata Serikali ya CCM na tuko makini kuliko hata Usalama wa Taifa na umakini huu ndiyo utakaotupeleka Ikulu mwaka 2015,”alisema Dk Slaa.
Hata hivyo Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alipotafutwa kujibu tuhuma hizo alisema hakuna jipya ambalo Chadema wamelisema.
“Kuna jipya katika hilo, ni yale yale ya kawaida na jana (juzi) Mwingulu alizungumza vizuri sana bungeni. Hiyo ni sawa na mchawi anapomwangia mtu na kufa anakuwa wa kwanza kwenda kulia msibani, nchi siku yoyotete haijengwi kwa ngonjera za maneno bali inajengwa kwa mipango,”alisema Nape.
Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Pereira Ame Silima alipotakiwa kutoa msimamo wa Serikali juu ya tuhuma hizo alisema, “Mimi siwezi kuzungumza ila mtafute Waziri (Dk Emmanuel Nchimbi),”alisema Silima.
Alipotafutwa Dk Nchimbi kupitia simu yake ya mkononi, ilikuwa ikiita bila kupokewa.
Kauli ya Mbowe
Kwa upande wake Mbowe alisema, CCM imekuwa ikitumia mbinu mbalimbali kuhakikisha inakisambaratisha chama hicho bila mafanikio.
“Watu wa Usalama wa Taifa wakishirikiana na CCM wamekuwa wakifanya mipango ya kutaka kuwateka maofisa wetu. Hawa watu ni wepesi sana na msiwaogope hata kidogo,”alisema Mbowe huku akishangiliwa na wanachama na makada waliofurika kwenye ukumbi wa Hoteli ya Blue Pearl.
Mbowe alisema: “Ukiona chama chochote tawala kinatumia jeshi la polisi kutengeneza ushahidi wowote wa kihalifu hiyo ni dalili ya hatari kwa mustakabali wa usalama wa nchi.”
Mbowe alisema mbinu za sasa za CCM zinatokana na kushindwa kukivuruga chama hicho kwa propaganda kuwa ni chama cha familia, ukabila, ukanda na baadaye udini.
Katiba na Elimu
Kuhusu mchakato wa Katiba Mpya, Mbowe alisema ikiwa itafika Aprili 30 mwaka huu bila hatua zozote kuchukuliwa, watamwamuru mjumbe wa tume hiyo kutoka Chadema, Profesa Mwesiga Baregu kujiondoa.
Chadema kinataka Serikali iwasilishe bungeni, muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Katiba ili yafanywe marekebisho mbalimbali kuhusu uwakilishi katika Bunge Maalumu la Katiba.
“Serikali inaona hili kama mchezo, sasa acha wakae kimya na baada ya Aprili 30 mwaka huu watachagua kusuka au kunyoa,”alisema Mbowe.
Kuhusu elimu, Mbowe alieleza kushangazwa na kile alichosema kuwa ni Serikali kutofahamu sababu za wanafunzi kufanya vibaya katika mitihani yao.
“Serikali eti haijui na kama haijui basi Waziri Mkuu (Mizengo Pinda) hatakiwi kuwa hapo alipo, kwani haiwezekani watoto wanafeli halafu anaunda tume,”alisema Mbowe na kuongeza:
“Mwaka 2011 waliunda tume ambayo ilitoa mapendekezo 27 lakini ripoti hiyo ilifichwa hadi mimi juzi (Jumatano) nilipoisoma bungeni wabunge wa CCM wakabaki vichwa chini.”
Alisema kuundwa kwa tume nyingine ambayo itatumia fedha za walipakodi ni kuwaumiza Watanzania ilhali tatizo na chanzo kinajulikana.
Ugaidi bungeni
Juzi wakati wa mjadala wa Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, wabunge wa CCM na Chadema kwa nyakati tofauti walituhumiana kwa ugaidi kiasi cha kusababisha vurugu na kutoelewana miongoni mwao.
Alhamisi akisoma maoni ya Kambi ya Upinzani, Mbowe alisema ugaidi ni ubunifu wa polisi na Serikali kwa ajili ya kuwabambikia kesi zisizo na dhamana kwenye mahakama maofisa wa vyama vya upinzani.
Kutokana na hotuba hiyo, Mbunge wa Iramba Magharibi (CCM), Mwigulu Nchemba aliishambulia hotuba ya Mbowe akieleza kuwa wanahusika kupanga kumdhuru mwandishi wa habari.

ADHANA YARUHUSIWA SWEDEN KWA MARA YA KWANZA

Msikiti mmoja katika kitongoji cha mji mkuu wa Sweden, Stockholm umeruhusiwa kuadhini kwa kutumia kipaza sauti kilicho kwenye mnara kwa ajili ya Sala ya Ijumaa.

Hii ni mara kwa kwanza kwa nchi hiyo ya Scandinavia kuruhusu adhana kwa sauti inayosikika nje ya msikiti.

Idara ya polisi mjini Stockholm imesema msikiti huo utaruhusiwa kuadhini kwa muda wa kati ya dakika tatu na tano katika kipindi cha baina ya saa sita na saa saba mchana kila Ijumaa.

Mkuu wa Jumuiya ya Utamaduni wa Kiislamu katika eneo la Botkyrka kusini mwa Stockholm Bw. Ismail Okur ameupongeza uamuzi huo. Ombi la kuadhini kwa sauti inayotoka nje ya msikiti liliwasilishwa miaka mitano iliyopita.

Kuna karibu Waislamu 7,000 katika eneo hilo na aghalabu wana asili ya Uturuki.

Chama chenye chuki dhidi ya Uislamu cha Sweden Democrats kimepinga uamuzi huo.

Katika miaka ya hivi karibuni, idadi ya Waislamu barani Ulaya imeongezeka kwa kasi na sambamba na hilo hitajio la misikiti pia limeongezeka. Waislamu raia wa nchi za Ulaya wamekuwa wakibaguliwa kwa muda mrefu na sasa wanapigania haki sawa na raia wengine wa Ulaya.

Saturday, April 13

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI Shilingi bilioni 620 za Deni la Taifa hazina maelezo by zittokabwe

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Shilingi bilioni 620 za Deni la Taifa hazina maelezo

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ametoa taarifa yake ya mwaka 2011/2012 na kuonyesha kuwa kuna skandali kubwa sana katika akaunti ya Deni la Taifa. Nanukuu

‘Uhakiki wa mchanganuo wa madeni ya Taifa kama ulivyokuwa tarehe 30 Juni, 2012 ulibaini kuwepo kwa marekebisho ya deni ya shilingi 619,803,554,183.91 ambayo uongozi haukuweza kutoa maelezo ya kuridhisha.’ (Taarifa ya CAG, Ripoti ya Serikali Kuu 2011/2012 uk 158). Mwisho wa Kunukuu

Katika Taarifa yake hiyo CAG anaendelea kuonyesha kuwa Deni la Taifa linazidi kukua na mwaka unaoishia mwezi Juni 2012 deni lilikuwa kwa asilimia 17 kutoka mwaka unaoishia mwezi Juni 2011.

Kukosekana kwa maelezo ya kuridhisha kuhusu zaidi ya nusu trilioni za Deni la Taifa ni jambo linalopaswa kutiliwa mashaka makubwa, kuchunguzwa na kupata majawabu stahiki. Tafiti mbalimbali duniani zinaonyesha kuwa kuna mahusiano makubwa sana kati ya Deni la Taifa la utoroshaji wa fedha kwenda kwenye mabenki ya ‘offshore’. Katika kitabu cha ‘Africa’s Odious Debts: How Foreign Loans and Capital flight bled a continent’ kilichoandikwa mabwana Leonce Ndikumana na James Boyce imeonekana kwamba Deni la Taifa huchochea utoroshwaji wa Fedha kwenda kuficha nje ya Tanzania.

Mabilioni haya kwenye akaunti ya Deni la Taifa yanashtusha sana. Kambi ya Upinzani Bungeni kwa miaka miwili mfululizo imekuwa ikitaka ukaguzi maalumu kwenye akaunti za Deni la Taifa lakini Serikali imeshindwa kufanya hivyo. Nikiwa Mwenyekiti wa Kamati ya PAC pia nimemtaka CAG afanye ukaguzi huu maalumu.

Kambi ya upinzani Bungeni ilisema hivi katika Bajeti yake kivuli 2012/13:

DENI LA TAIFA

Mheshimiwa Spika, Kambi ya Upinzani inasikitika kwa serikali kuendelea kutengeneza madeni kwa Taifa kwa kuendelea kukopa zaidi kwa matumizi ya kawaida ya serikali. Wakati Serikali inasisitiza kwamba Deni letu linastahmilika, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali anaonyesha mashaka makubwa sana kutokana na kasi ya kukua kwa Deni la Taifa. Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali inaonyesha kuwa Deni la Taifa linazidi kuongezeka kwa asilimia 38% kutoka shilingi trillion 10.5 mwaka 2009/2010 hadi shilingi trillion 14.4 mwaka 2010/2011. Kwa mujibu wa Waziri wa Fedha Deni la Taifa limefikia shilingi trillion 20.3 mpaka ilipofika mwezi Machi mwaka 2012. Ukisoma taarifa ya Mwezi wa Mei 2012 ya Benki Kuu ya Tanzania, Deni la Taifa sasa limefikia shilingi trillion 22.

Mheshimiwa Spika, Suala hapa sio ustahmilivu wa Deni kama inavyodai Serikali bali ni kwamba tunakopa kufanyia nini? Bajeti ya Mwaka 2012/13 inayopendekezwa inaonyesha kwamba Serikali itakusanya shilingi trilioni 8.7 kama makusanyo ya ndani na itatumia shilingi trilioni 10.6 kama matumizi ya kawaida. Ni dhahiri kwamba sehemu ya mikopo ambayo serikali inachukua sasa itakwenda kwenye matumizi ya kawaida. Hatutaki mikopo kwa ajili ya matumizi ya kawaida ya posho, kusafiri, magari nk. Tuchukue mikopo kuwekeza kwenye miradi itakayokuza uchumi na kuzalisha kodi zaidi. Bajeti inaonyesha kwamba Serikali itakopa shilingi takribani trillion 5 mwaka 2012/13. Serikali ikubalikutekeleza mapendekezoya Kambi ya Upinzani ya kuimarisha ukusanyaji wa kodi na kupanua wigo wa kodi katika maeneo muhimu kama sekta ya madini na mawasiliano, kuzuia misamaha ya kodi, kutokomeza ukwepaji kodi, na kuepuka matumizi mabaya ili kuepuka madeni yasiyo ya lazima.

Mheshimiwa Spika, Kambi ya Upinzani inapenda kusisitiza kwamba Bunge lifanye ukaguzi maalumu kuhusu akaunti ya Deni la Taifa ili kuweza kubaini ukweli kuhusu ustahmilivu wa Deni na mikopo ambayo Serikali inachukua kama inakwenda kwenye Maendeleo na miradi ipi na kama miradi hiyo ina tija. Vilevile tumependekeza kwamba Mikopo yote ambayo Serikali inachukua iwe inapata idhini ya Kamati ya Bunge ya Fedha na Uchumi au Bunge litunge sharia ili kiwango cha juu cha kukopa ambacho Serikali haipaswi kuvuka. Kuiacha Serikali inaendelea kukopa bila mpango ni kuliweka Taifa rehani na kupeleka mzigo wa kulipa madeni haya kwa kizazi kijacho. Hatuwezi kukubali Wazee wetu waishi maisha yao, waishi maisha yetu na pia wakope maisha ya watoto wetu. Mwisho wa kunukuu.

Kambi ya Upinzani inarejea kutaka ukaguzi maalumu kuhusu akaunti za Deni la Taifa na maelezo ya kina ya Serikali kuhusu shilingi 620 bilioni ambazo hazina maelezo kwenye Deni la Taifa. Hatuwezi kukaa kimya kuona Watanzania wanabebeshwa madeni ambayo kimsingi ni madeni bandia yanayotajirisha watu wachache wenye uwezo na ujasiri mkubwa wa kuiba, kupora nakufisidi hazina ya Taifa letu.

Kabwe Zuberi Zitto,Mb

Waziri Kivuli Fedha na Uchumi

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI Shilingi bilioni 620 za Deni la Taifa hazina maelezo by zittokabwe

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Shilingi bilioni 620 za Deni la Taifa hazina maelezo

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ametoa taarifa yake ya mwaka 2011/2012 na kuonyesha kuwa kuna skandali kubwa sana katika akaunti ya Deni la Taifa. Nanukuu

‘Uhakiki wa mchanganuo wa madeni ya Taifa kama ulivyokuwa tarehe 30 Juni, 2012 ulibaini kuwepo kwa marekebisho ya deni ya shilingi 619,803,554,183.91 ambayo uongozi haukuweza kutoa maelezo ya kuridhisha.’ (Taarifa ya CAG, Ripoti ya Serikali Kuu 2011/2012 uk 158). Mwisho wa Kunukuu

Katika Taarifa yake hiyo CAG anaendelea kuonyesha kuwa Deni la Taifa linazidi kukua na mwaka unaoishia mwezi Juni 2012 deni lilikuwa kwa asilimia 17 kutoka mwaka unaoishia mwezi Juni 2011.

Kukosekana kwa maelezo ya kuridhisha kuhusu zaidi ya nusu trilioni za Deni la Taifa ni jambo linalopaswa kutiliwa mashaka makubwa, kuchunguzwa na kupata majawabu stahiki. Tafiti mbalimbali duniani zinaonyesha kuwa kuna mahusiano makubwa sana kati ya Deni la Taifa la utoroshaji wa fedha kwenda kwenye mabenki ya ‘offshore’. Katika kitabu cha ‘Africa’s Odious Debts: How Foreign Loans and Capital flight bled a continent’ kilichoandikwa mabwana Leonce Ndikumana na James Boyce imeonekana kwamba Deni la Taifa huchochea utoroshwaji wa Fedha kwenda kuficha nje ya Tanzania.

Mabilioni haya kwenye akaunti ya Deni la Taifa yanashtusha sana. Kambi ya Upinzani Bungeni kwa miaka miwili mfululizo imekuwa ikitaka ukaguzi maalumu kwenye akaunti za Deni la Taifa lakini Serikali imeshindwa kufanya hivyo. Nikiwa Mwenyekiti wa Kamati ya PAC pia nimemtaka CAG afanye ukaguzi huu maalumu.

Kambi ya upinzani Bungeni ilisema hivi katika Bajeti yake kivuli 2012/13:

DENI LA TAIFA

Mheshimiwa Spika, Kambi ya Upinzani inasikitika kwa serikali kuendelea kutengeneza madeni kwa Taifa kwa kuendelea kukopa zaidi kwa matumizi ya kawaida ya serikali. Wakati Serikali inasisitiza kwamba Deni letu linastahmilika, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali anaonyesha mashaka makubwa sana kutokana na kasi ya kukua kwa Deni la Taifa. Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali inaonyesha kuwa Deni la Taifa linazidi kuongezeka kwa asilimia 38% kutoka shilingi trillion 10.5 mwaka 2009/2010 hadi shilingi trillion 14.4 mwaka 2010/2011. Kwa mujibu wa Waziri wa Fedha Deni la Taifa limefikia shilingi trillion 20.3 mpaka ilipofika mwezi Machi mwaka 2012. Ukisoma taarifa ya Mwezi wa Mei 2012 ya Benki Kuu ya Tanzania, Deni la Taifa sasa limefikia shilingi trillion 22.

Mheshimiwa Spika, Suala hapa sio ustahmilivu wa Deni kama inavyodai Serikali bali ni kwamba tunakopa kufanyia nini? Bajeti ya Mwaka 2012/13 inayopendekezwa inaonyesha kwamba Serikali itakusanya shilingi trilioni 8.7 kama makusanyo ya ndani na itatumia shilingi trilioni 10.6 kama matumizi ya kawaida. Ni dhahiri kwamba sehemu ya mikopo ambayo serikali inachukua sasa itakwenda kwenye matumizi ya kawaida. Hatutaki mikopo kwa ajili ya matumizi ya kawaida ya posho, kusafiri, magari nk. Tuchukue mikopo kuwekeza kwenye miradi itakayokuza uchumi na kuzalisha kodi zaidi. Bajeti inaonyesha kwamba Serikali itakopa shilingi takribani trillion 5 mwaka 2012/13. Serikali ikubalikutekeleza mapendekezoya Kambi ya Upinzani ya kuimarisha ukusanyaji wa kodi na kupanua wigo wa kodi katika maeneo muhimu kama sekta ya madini na mawasiliano, kuzuia misamaha ya kodi, kutokomeza ukwepaji kodi, na kuepuka matumizi mabaya ili kuepuka madeni yasiyo ya lazima.

Mheshimiwa Spika, Kambi ya Upinzani inapenda kusisitiza kwamba Bunge lifanye ukaguzi maalumu kuhusu akaunti ya Deni la Taifa ili kuweza kubaini ukweli kuhusu ustahmilivu wa Deni na mikopo ambayo Serikali inachukua kama inakwenda kwenye Maendeleo na miradi ipi na kama miradi hiyo ina tija. Vilevile tumependekeza kwamba Mikopo yote ambayo Serikali inachukua iwe inapata idhini ya Kamati ya Bunge ya Fedha na Uchumi au Bunge litunge sharia ili kiwango cha juu cha kukopa ambacho Serikali haipaswi kuvuka. Kuiacha Serikali inaendelea kukopa bila mpango ni kuliweka Taifa rehani na kupeleka mzigo wa kulipa madeni haya kwa kizazi kijacho. Hatuwezi kukubali Wazee wetu waishi maisha yao, waishi maisha yetu na pia wakope maisha ya watoto wetu. Mwisho wa kunukuu.

Kambi ya Upinzani inarejea kutaka ukaguzi maalumu kuhusu akaunti za Deni la Taifa na maelezo ya kina ya Serikali kuhusu shilingi 620 bilioni ambazo hazina maelezo kwenye Deni la Taifa. Hatuwezi kukaa kimya kuona Watanzania wanabebeshwa madeni ambayo kimsingi ni madeni bandia yanayotajirisha watu wachache wenye uwezo na ujasiri mkubwa wa kuiba, kupora nakufisidi hazina ya Taifa letu.

Kabwe Zuberi Zitto,Mb

Waziri Kivuli Fedha na Uchumi

Thursday, March 21

‘Tunahitaji dunia inayolinda maisha’

Vatican City. Mkuu wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis amesimikwa rasmi, huku akiitaka dunia kuungana kwa ajili ya kuwatetea wanyonge na kulinda mazingira.
Akizungumza wakati wa misa maalumu ya kumsimika katika wadhifa huo mpya iliyofanyika kwenye Kanisa Kuu la Mtakatifu Peter mjini Vatican, Papa Francis alisema hiyo ndiyo njia pekee ya kuijenga dunia iliyo njema na salama, isiyo na vifo visivyo vya lazima na maangamizi.
Francis akitoa hotuba yake alikuwa akishangiliwa na kufunikwa kila mara kwa sauti ya hadhira iliyokuwa ikimsikiliza, hasa alipozungumzia umuhimu wa kulinda mazingira, kusaidiana, kupendana na kutoruhusu namna yoyote ya maangamizi, chuki, wivu na majivuno yanayoweza ‘kuharibu maisha yetu’.
Alisema kwamba wajibu wake mkuu ni kunyoosha mikono yake na kulinda utu, hasa ‘wa maskini, wasiojiweza, wale wanaodharauliwa hasa ambao Mtakatifu Mathayo aliwataja alipokuwa akihitimisha falsafa ya upendo: wenye njaa, wenye kiu, wageni, wasio na mavazi, wagonjwa na wale waliofungwa magerezani’.
“Leo tunahitaji kuona mwanga wa matumaini katika giza lililopo mbele yetu na kuwa wanaume na wanawake wanaotoa tumaini jipya kwa wengine. Kulinda uumbaji, kulinda wanaume na wanawake, kuwaangalia kwa upendo na kujali, hii ikiwa njia pekee ya kutoa tumaini jipya, ili kutoa mwanga mpya na kuangaza kuliko na wingu nene,” alisema.
Kauli hiyo ilianza kutolewa na kiongozi huyo mkuu wa Kanisa lenye zaidi ya waumini 1.2 bilioni duniani tangu alipotangazwa rasmi kuchaguliwa na jopo la makadinali Jumatano wiki iliyopita, ambapo alianza kutangaza ujumbe wake wa amani wa kuwajali na kuwapenda maskini.
Katika misa hiyo maalumu iliyohudhuriwa na wageni maalumu 132 wakiwamo viongozi wa kidini na wa mataifa mbalimbali akiwamo Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe, ujumbe wake kwa wafuasi wa Kanisa hilo na watu wote duniani ulichukua muda mfupi usiofikia saa moja, hivyo kumfanya aonekane mtu mwenye staha na kujali muda.
“Ninawaomba wote wenye wajibu katika kusimamia uchumi, siasa, maisha ya watu kuwajibika.” pamoja na wanaume na wanawake wote wenye nia njema, tuwe walinzi wa uumbaji wa Mungu, tulinde mpango wa Mungu ulio wa asili, tulindane na kupendana na kuyalinda mazingira.”
Papa Francis alijumuika na waumini waliokusanyika katika uwanja huo ambapo alizunguka katika eneo hilo kwa kutumia gari maalumu, akisalimiana na waumini kuwabariki wasiojiweza na kuwabusu watoto wenye matatizo.

Lowassa afufua kashfa ya kigogo Ikulu

Dar es Salaam. Sakata la Mkuu wa Itifaki wa Ikulu, Anthony Itatiro, ambaye anahusishwa na njama za kutaka kuchota kiasi cha Sh3 bilioni kwa ajili ya safari hewa ya Rais, limechukua sura mpya baada ya Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje kutaka kujua hatima ya kigogo huyo jana.
Itatiro na maofisa wanne wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa walituhumiwa mwaka jana kuidhinisha kuchota kiasi hicho cha fedha bila ya kuwapo kwa ziara ya Rais kwenda nchi yoyote ya kigeni.
Mpango huo unadaiwa kusukwa Juni mwaka jana kwa maofisa haokuitaka Wizara ya Fedha kutoa kiasi hicho cha fedha kwa ajili ya safari hewa ya Rais.
Naibu Waziri wa wizara hiyo, Juma Mahadhi alitoa maelezo hayo baada ya kuulizwa swali na Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje ya Bunge, Edward Lowassa.
Lowassa, ambaye pia ni Mbunge wa Monduli aliuliza swali hilo ghafla kwa Mahadhi wakati akitoka nje, baada ya kumalizika kwa kikao cha kamati yake kilichofanyika kwenye ofisi za Bunge jijini Dar es Salaam.
Mahadhi, ambaye alilazimika kutoa ufafanuzi wa swali hilo baada ya kubanwa zaidi na waandishi wa habari, alisema Rais Kikwete ndiyo mwenye mamlaka ya kuchukua hatua dhidi ya Itatiro kutokana na ripoti ya uchunguzi ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na Mkaguzi wa Ndani wa Wizara hiyo.
Alisema pia kuwa walishauriwa kuwa maofisa walioshirikiana na Itatiro nao wachukuliwe hatua za kinidhamu kufuatia njama hizo.
Alipotafutwa kuzungumzia suala hilo, Katibu Mkuu Ombeni Sefue hakupokea simu. Pia hakujibu pindi alipotumiwa ujumbe mfupi kwa njia ya simu. Naye Katibu Mkuu katika Ofisi ya Rais anayeshughulikia Utumishi, George Yambesi alisema hakuwa tayari kuzungumzia suala hilo kwani alikuwa likizo.
Mahadhi alisema wakati tukio hilo linatokea viongozi wakuu wa wizara hiyo walikuwa kwenye majukumu mengine ya Serikali, jambo ambalo lilisababisha nafasi zao kukaimiwa na watendaji hao.
“Wale maofisa walitumia mwanya wao wa kukaimu nafasi ile ndiyo wakasuka mpango huo,” aliongeza Mahadhi.
Alisema kutokana na hali hiyo baadhi ya maofisa hao wamechukuliwa hatua za kinidhamu ikiwamo ya kuwashusha vyeo na kuwabadilisha vitengo.
Mahadhi alisema kwamba huwa ni utaratibu wa kawaida kwa Rais anaposafiri maofisa wa Itifaki na wale wa Wizara ya Mambo ya Nje kupewa fedha na hazina kwa ajili ya kufanikisha ziara zake.
“Ila maofisa hawa walitumia mwanya huo kuihadaa Wizara ya Fedha kwa kuandaa hoja ya safari feki ili kupata fedha hizo,” aliongeza Mahadhi.
Maofisa wengine ni pamoja na ofisa katika Idara ya Itifaki, Shamim Khalfa, Kaimu Mhasibu Mkuu, Kasim Laizer, Mhasibu, Deltha Mafie na karani wa fedha) aitwaye, Shabani Kesi.

OBAMA AFANANISHWA NA SHETANI...


Rais wa Marekani Barack Obama amefananishwa na shetani baada ya muigizaji Mohamen Mehdi Quazann kucheza sinema inayofanana na muonekano wa shetani huku akionekana kufafana na Obama

Kwa mujibu wa repoti ya CNN filamu hiyo ambayo imeonekana kuteka mashabiki wengi teyari imeshaanza kurushwa vipande vichache vinavyoonyesha jinsi Obama alivyofanana na Mohamen huku akionekana kama shetani kupitia channel ya 'The History'

Mpaka sasa inaonekana filamu hiyo kupata mashabiki wengi na kuteka vichwa vya habari vingi huku mashabiki wengi wakiwa wamemiminika katika mtandao wa twitter na kupata tweets zaidi ya 200 kwa muda mfupi

PRO-24

Saturday, February 23

Serikali ya Awamu ya Nne yaongoza kukopa


TAASISI isiyo ya kiserikali ina yojishughulisha na masuala ya Madeni ya Taifa na Maendeleo (TCDD), imesema Serikali ya Tanzania ndiyo inaongoza kwa kukopa zaidi, ikieleza kuwa kati ya mwaka 2008 hadi mwaka 2011, imekopa kiasi cha Sh15trilioni na kufanya deni la taifa kufikia Sh21trilioni.
Rais Kikwete aliingia madarakani mwaka 2005, baada ya rais aliye mtangulia, Benjamin Mkapa kumaliza kipindi chake cha uongozi wa miaka 10 kilichoanzia mwaka 1995 hadi mwaka 2005.
TCDD imebainisha kuwa Serikali inakopa fedha hizo kutoka Benki Kuu (BoT), Benki za Biashara, Kampuni za Bima na Mashirika ya Hifadhi za Jamii. Pia inakopa katika taasisi za kimataifa ikiwamo, Benki ya Dunia (WB), Benki ya Maendeleo Afrika (ADB) na Shirika la Fedha Duniani (IMF).
Katika maelezo yake, Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi hiyo Hebron Mwakagenda, alisema kuwa kite ndo cha Serikali kukopa fedha kwa ajili ya matumizi yasiyo muhimu pamoja na kuwalipa watumishi wake mishahara, ndiyo sababu ya kukua kwa deni hilo la taifa.
“Serikali ya awamu ya nne imekopa kwa kiwango kikubwa, kwani tangu iingie madarakani imeshakopa Sh15trilioni, sasa sijui mpaka inamaliza muda wake itakuwa imekopa kiasi gani?” alisema Mwakagenda akihoji na kuongeza;
“Hata kama kukopa ni kuzuri basi tukope na fedha tuzifanyie mambo ya maana hasa katika maendeleo, tukope tu pale inapokuwa lazima kufanya hivyo.”
TCDD imeeleza kwamba hali hiyo ni hatari, hasa ikizingatiwa kuwa miaka kadhaa iliyopita, Tanzania kupitia Mpango wa Nchi Maskini zenye Madeni Makubwa (HIPC), ilifutiwa kiasi kikubwa cha madeni, lakini sasa imeanza kukopa tena na deni kukua kwa kasi.
Taasisi hiyo pia imesema kitendo hicho kimechangia kuporomoka kwa uchumi wa taifa kunakosababishwa na riba kubwa za mikopo hiyo, ambapo kulingana na idadi ya Watanzania ukigawanya deni hilo kwa wote, inaonyesha kuwa kila Mtanzania anadaiwa wastani wa Sh450,000.
Mwakagenda, ambaye taasisi yake inafanya kazi ya kuishauri Serikali katika suala zima la deni la taifa na maendeleo, alisema hadi kufikia Oktoba mwaka jana, deni la nje lilikuwa Sh15.9 trilioni.
Kwa mujibu wa taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), aliyoitoa bungeni mjini Dodoma mwaka jana, taifa linapoteza Sh3 trilioni katika ukwepaji wa kodi na ubadhirifu, huku akishauri kuwa mambo mawili yakifanyiwa kazi deni hilo litapungua au kumalizika kabisa.
“Deni linakuwa kwa kiasi kikubwa na tunakopa katika mabenki ya biashara, ambayo riba yake ni kubwa, fedha nyingi zinazokopwa hutumika kulipa mishahara,” alisema Mwakagenda.
Alifafanua kwamba mwaka 2007 hadi 2008 deni la taifa lilikuwa Sh6.4 trilioni na kwamba, kuanzia mwaka 2007 hadi 2011 deni hilo limeongezeka hadi Sh21 trilioni.
Alisema deni ni utumwa na fedheha na kwamba nchi inatakiwa kukopa kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu, kwamba ifanye hivyo kama itashindwa kabisa kupata namna nyingine ya kugharimia maendeleo.
“Ukopaji katika benki za biashara zinazotoa riba kubwa kwa ajili ya kulipia matumizi ya kawaida ni hatari kwa taifa na kwa vizazi vya sasa na baadaye,” alifafanua.
Nini kifanyike
“Kama taifa, tukijipanga zaidi katika kuboresha usimamizi katika sekta mbalimbali sambamba na kusimamia mapato na ulipaji kodi, hatutakopa tena katika mabenki ya biashara,” alisema na kuongeza:
“Hata ukitazama ongezeko la deni hili la taifa, ni sawa na Sh3 trilioni kila mwaka, fedha ambazo kwa mujibu wa taarifa ya CAG zinapotea kila mwaka.”
Alifafanua kwamba hilo li nawezekana iwapo Serikali itaongeza wigo wa kudhibiti misamaha ya kodi, kuziba mianya ya ukwepaji kodi na kuangalia kwa makini sekta mpya kama za madini, gesi na utalii kuliko kukazana kukopa kama njia pekee ya kuendesha shughuli za maendeleo.
“Tunataka Serikali ifungue macho na kuona fursa mpya za kupata mapato ya ndani badala ya kugeuza mikopo kuwa ndiyo suluhisho la kudumu la mipa ngo yetu ya maendeleo,” alisema Mwakagenda.
Alisema jambo walilofanya kama TCDD ni kutoa mapendekezo kwamba Katiba ijayo iwe na kipengele kitakachoeleza kiwango cha ukomo wa kukopa (debt ceiling).
Januari 4 mwaka huu Mwakagenda aliliambia gazeti hili kwamba deni hilo ni kiwango cha juu kabisa kwa nchi kuweza kukopa kutoka kwenye masoko ya kimataifa. Deni limeongezeka kwa dola 456.1 milioni katika ki pindi cha mwaka mmoja tu tangu Oktoba 2011.
Alisema taarifa za Benki Kuu ya Tanzania zinaonyesha kuwa deni la ndani limefikia Sh5.1 trilioni hadi kufikia Oktoba mwaka jana na kwamba kiasi hicho ni sawa na ongezeko la Sh513 bilioni tangu mwaka 2011.
Alisema zipo fedha zinazotumika kujenga barabara, madaraja, majengo mbalimbali ya shule na vyuo, lakini kinachotakiwa ni Serikali kufikiri mara mbili kabla ya kuamua kukopa na kuzitumia fedha hizo za mkopo.
Katika mapendekezo yao, Mwakagenda alisema wameitaka Serikali kuwa na nidhamu katika kukopa kwa kuwa deni hilo limevuka kiwango cha kimataifa.
Katika ufafanuzi wake, Mwakagenda alisema baada ya kuwasilisha kwa Serikali kiwango hicho cha deni la taifa, Gavana wa Benki Kuu (BOT), Profesa Beno Ndulu alitoa takwimu kwamba hali ya deni siyo mbaya na kwamba imefikia asilimia 19, kiwango ambacho kinakubalika kimataifa kukopa tena.
“Waziri wa Fedha na Uchumi, Dk William Mgimwa yeye alitueleza kuwa bado tunakopesheka, lakini pamoja na hayo hatukubaliani na kauli ya Serikali kwa kuwa katika kipindi cha miaka mitano, deni limekuwa kwa kiwango kikubwa” alisema Mwakagenda.

Sunday, January 13

Zitto aingia matatani

 MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe ameingia matatani, baada ya kutakiwa kukanusha tuhuma alizozitoa bungeni katika Mkutano wa Tisa wa Bunge, kwamba mfanyabiashara wa kigeni, Moto Mabanga, alipewa vitalu vya mafuta kinyume na taratibu.

Mfanyabiashara huyo amesema kuwa iwapo Zitto atashindwa kukanusha tuhuma hizo, atafikishwa mahakamani.

Barua iliyoandikwa kwenda kwa mbunge huyo iliyosainiwa na Mwanasheria wa Mabanga, Lawley Shein wa Kampuni ya Uwakili ya Lawley Shein Attorneys, ambayo Mwananchi Jumapili limeiona, inaeleza kuwa hoja binafsi aliyoitoa Zitto, haikuwa na ukweli wowote.

Barua hiyo ya tarehe 28 Novemba, 2012 ilisema kuwa hoja hiyo ya Zitto ni ya uongo, imemkashifu mteja wao na kumshushia hadhi yake binafsi na biashara zake.

“Katika kuthibitisha kuwa tuhuma zako siyo za kweli katika hoja uliyotoa, umemtaja mteja wetu kama raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Mteja wetu ni raia wa Afrika Kusini, lakini, umeamua kumtaja kama raia wa Kongo bila kuangalia ukweli,” alisema Shein.

Katika barua hiyo, Shein pia amesema kuwa Zitto amemtuhumu mteja wake Mabanga kuwa aliwahonga baadhi ya vigogo serikalini na kuwapa rushwa wanasiasa katika mchakato wa kufanikisha upatikanaji wa vitalu hivyo.

“Tuhuma hizo siyo za kweli, mteja wetu alifuata taratibu zote kwa uwazi na mamlaka husika nchini na hakuwahi kutoa rushwa kwa mtu yeyote,” alisema mwanasheria huyo.

“Tuhuma hizi ni za uongo, zimemharibia jina mteja wetu na kumsababishia madhara. Kama hutazifuta kauli hizo, uongo huo utamsababishia mteja wetu madhara makubwa zaidi na tutalazimika kudai fidia,” Shein alionya kupitia barua hiyo.

Shein aliongeza kuwa pamoja na Zitto kuongea hoja hiyo akiwa bungeni hivyo kuwa na kinga ya kibunge, lakini kwa mazingira aliyotolea hoja hiyo alitumia vibaya kinga ya kibunge, anayopata mbunge yeyote anapotoa hoja akiwa bungeni.

Kupitia barua hiyo, Shein alimtaka Zitto kufuta kauli yake dhidi ya mteja wao na kwamba mteja wao ana haki zote za kushtaki dhidi ya hoja hiyo.

Zitto azungumza
Alipotakiwa kuzungumzia hoja hiyo na hatua atakazochukua, Zitto alisema kuwa amemwandikia barua Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah, kumjulisha hatua hiyo ya kutaka kushtakiwa.
“Nimemwandikia Katibu wa Bunge kumjulisha kwamba nimeletewa kusudio la kushtakiwa, maana hili ni suala la Kinga ya Bunge,” alisema Zitto na kuongeza:

“Mbunge ana kinga kwa masuala aliyozungumza ndani ya Bunge kwa mujibu wa Ibara ya 100 ya Katiba. Kwa hiyo Katibu (Dk Kashililah), atawajibu hao wanasheria.”

Ibara hiyo ya 100 (2) inaeleza kuwa; Bila ya kuathiri Katiba au masharti ya sheria nyingine yoyote inayohusika, mbunge yeyote hatashtakiwa au kufunguliwa shauri la madai mahakamani kutokana na jambo alilosema au kulifanya ndani ya Bunge, au alilolileta bungeni kwa njia ya maombi, muswada, hoja au vinginevyo.

Naibu Spika
Kwa upande wake Naibu Spika, Job Ndugai alisema kuwa hana taarifa za kusudio hilo la kutaka kushtakiwa kwa Zi tto, lakini akasema kwamba mbunge ana kinga ya Bunge pindi akitoa hoja au wazo lolote, akiwa ndani ya Bunge.

Ndugai alisema kuwa kutokana na mabadiliko madogo ya sheria yaliyofanyika, mwananchi anaweza kuandika barua kwa Spika wa Bunge kutokana na tuhuma alizotoa mbunge dhidi yake bungeni.
“Mtu anaweza kuandika barua kwa Spika na Spika ataona hatua zaidi za kuchukua za kibunge,” alisema Ndugai.

Uswisi imeiumbua serikali, sasa fedha zirejeshwe

   
NILIMSIKILIZA kwa makini Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Frederick Werema, alipokuwa akijibu bungeni hoja ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe aliyoiwasilisha bungeni Novemba mwaka jana kuhusu mabilioni ya fedha yaliyotoroshewa katika mabenki mbalimbali nchini Uswisi.

Werema alisema kuwa Serikali imeanza kuzifanyia uchunguzi tuhuma hizo na kwamba Serikali haijalala bali inaendelea na uchunguzi.

Alisema vyombo vya usalama ikiwamo Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (Takukuru), wanalifanyia kazi suala hilo. Akatoa wito kwa Zitto na wananchi wengine kama wana ushahidi zaidi wauwasilishe katika vyombo hivyo ili fedha hizo ziweze kurejeshwa.

Wakati akiwasilisha hoja hizo Zitto alikwenda mbali zaidi ya kuwaelezea watu walioficha fedha hizo nje ya nchi na miaka ambayo walifanya hivyo.

Bila ya kuwataja kwa majina, Zitto aliwataja watu hao kwa nyadhifa kuwa ni watu wote walioshika nyadhifa za uwaziri mkuu katika kipindi cha 2003 hadi 2010, walioshika nyadhifa za uwaziri wa nishati na madini katika kipindi hicho na waliokuwa makatibu wakuu Wizara ya Nishati na Madini.

Wengine ni mawaziri na makatibu wakuu wa Wizara ya Ulinzi, wakuu wa majeshi, wanasheria wa Serikali, makamishna wa nishati, walioshika wadhifa wa Ukurugenzi Mkuu wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Uenyekiti na Ujumbe wa Bodi wa TPDC katika kipindi cha mwaka 2003 hadi 2010.

Pia Zitto alitaka Serikali kuwasiliana na Benki ya Dunia kupitia kitengo cha ‘Assets Recovery Unit’ ili mabilioni ya fedha na mali ambazo zimetoroshwa nje ya nchi kwenda Uswisi, Dubai, Mauritus na maeneo mengine ziweze kurejeshwa.

Hoja hiyo ya Zitto iliungwa mkono na Wabunge mbalimbali wakiwamo wa CCM ambao walitaka serikali kuchukua hatua za haraka kurejesha fedha hizo na wahusika wachukuliwe hatua.
Wapo wabunge ambao walikwenda mbali zaidi ya kutaka watu hao waliotorosha fedha hizo wakipatikana wanyongwe kwa sababu hao ni wasaliti wan chi yetu.

Mwisho wa mjadala bunge likaazimio kuipa serikali muda hadi bunge lijalo kutoa taarifa ya utekelezaji wa azimio hilo la kurejesha fedha hizo nyumbani.

Baada ya hapo kila mmoja tukajua kweli sasa serikali huenda ikalifanyia kazi azimio la bunge la kuzirejesha fedha hizo, kwa sababu siku zote serikali imeonyesha kuwa nzito katika kuzirejesha fedha hizo.

Kauli ya serikali ya Uswisi kuwa Serikali Tanzania haijaonyesha nia ya dhati kutaka kuchunguza na kupata mabilioni ya fedha yaliyofichwa na Watanzania katika benki mbalimbali nchini humo, inashtua sana.

Balozi wa Uswisi nchini, Olivier Chave alisema Ijumaa ya wiki hii kuwa mpaka sasa hakuna jitihada zozote zilizofanywa na Serikali ya Tanzania kutaka ufumbuzi wa tuhuma hizo.

Chave alisema Uswisi iko tayari kushirikiana na Tanzania kujua uhalali wa fedha hizo na endapo zikigundulika ni fedha chafu basi tutazirejesha nchini.

Alisema Serikali yao haina tatizo, kwani wameshafanya hivyo kwa nchi za Ufilipino na Nigeria hivyo watafurahi na Tanzania kama watamaliza suala hilo.

Alisema habari zinazoandikwa kuhusu mabilioni hayo kuhifadhiwa katika Benki za Uswisi, yanaharibu picha ya nchi hiyo mbele ya mataifa mengine, hivyo angependa suala hilo kumalizwa na kwamba wao wako tayari.

Kwa hakika, kauli ya balozi huyu imeimbua serikali ambayo imekuwa ikitoa visingizio vya vingi kwamba inashindwa kuzirejesha fedha hizo kutokana na kukosa ushirikiano.

Naamini kama alivyosema Zitto na watu wengine nchini kwamba fedha hizo zinamilikiwa na vigogo ndani ya serikali au waliowahi kushika nyadhifa za juu serikalini ndiyo maana inakuwa vigumu kuchukua hatua.

Kama serikali ya Uswisi inasema iko tayari kutoa ushirikiano wa kurejeshwa kwa fedha hizo nyumbani, serikali inataka msaada gani tena zaidi ya huo?

Ni kitu cha kushangaza tunapomuona Werema na mawaziri wengine wa serikali Rais Jakaya Kikwete wakisimama kuwapaka mafuta Watanzania kwa maneno matamu kwamba wameanza uchunguzi kuhusu suala hilo, wakati hata hawajawasiliana na serikali ya Uswisi.

Kuonyesha kuwa hawana nia ya dhati hata Zitto mwenyewe hadi sasa anasema Serikali haijamfuata kutaka kutoa ushirikiano wa aina yeyote kuhusu tuhuma hizo.

Zitto alikaririwa Ijumaa ya wiki hii akisema kuwa ingawa Serikali ilitaka iachiwe tuhuma hizo ili iweze kuzifanyia kazi, lakini hadi sasa ukimya umetawala.

Sasa tunaitaka serikali kuacha kutumia visingizio ili kuwazunga Watanzania, tunahitaji fedha hizo zirejeshwe na wahusika wachukuliwe hatua.
0754 304336
juliusmagodi@yahoo.com

Palestinian Leader Yasser Arafat To Be Exhumed For Toxicology Tests


The body of the former Palestinian leader, Yasser Arafat, is to be exhumed next week amidst suspicions he may have been poisoned.

Arafat, who led the Palestine Liberation Organisation for 35 years, died eight years ago after becoming the first president of the Palestinian Authority in 1996.

He fell ill in October 2004 and in spite of treatment in a French military hospital in Paris died on 11 November 2004, aged 75.

Medical records for Arafat said he died after suffering a stroke because of blood disorders. However, a French court opened a murder inquiry after high levels of radioactive polonium were found by a Swiss Institute on his clothing, which had been provided by his widow, Suha.

Arafat is buried in Ramallah on the West Bank in a tomb that was sealed off earlier this month. Once the former PLO leader's body is removed, scientists from France, Switzerland and Russia will each take samples, former Palestinian intelligence chief Tawfik Tirawi told the BBC.

No autopsy was carried out on Arafat when he died at the request of his widow, but she has since agreed to this exhumation to enable the Palestine Authority to find the truth about her husband's death, according to reports. Many Palestinians have long suspected that he was murdered by Israel, which has rejected such claims.

The exhumation is scheduled to take place on Tuesday.

Saturday, January 12

UTATA KUHUSU MUONEKANO WA DARAJA LA MANZESE


Picha hii imekua ikisambaa kwenye mitandao ya kijamii wakidai kuwa huu ndiyo utakua muonekano wa daraja la Manzese. ....

Mdau wa tulonge amejaribu kufanya uchunguzi kugundua kuwa hii ni project ambayo ilipangwa kufanywa na wachina huko Thailand mwaka 2010.....

Mimi binafsi pia sijawahi sikia serikali ikisema kuwa huu ndiyo utakua muonekano wa daraja la Manzese na Morogoro road kwa ujumla.....

Kama kuna mdau anafahamu mengi kuhusu hili atujuze ili tusije tukawa tunadanganyana na kufarijiana.....





POLISI WATANO WATIWA MBARONI KWA UPOTEVU WA MILIONI 150 KATIKA TUKIO LA WIZI LILILOTOKEA KARIAKOO HIVI KARIBUI




Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam linashikilia askari Polisi watano kwa tuhuma za kuhusika na upotevu wa Sh milioni 150 zilizoporwa na watu wanaosadikiwa kuwa majambazi eneo la Kariakoo.

Sambamba na askari hao pia wamekamatwa watu wawili wanaodaiwa kuhusika na tukio hilo ambao ni Deogratias Kimaro (30), mkazi wa Kalakata na Kulwa Mwakabala (30) mkazi wa Kijiwesamli Ilala.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Dar es Salaam, Kamanda wa Kanda hiyo, Suleiman Kova alisema askari hao wanashikiliwa kutokana na uchunguzi wa kina uliofanywa na jopo la upelelezi likiongozwa na Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai wa Kanda hiyo, Ahmed Msangi.

Alisema baada ya tukio hilo zilipatikana taarifa kwamba fedha hizo zilipotea baada ya mtuhumiwa Augustino Kayula au Frank Mwangiba, kukamatwa akiwa na bastola aina ya Browning bila fedha zilizoporwa wakati inasemekana ndiye aliyepora fedha hizo akiwa na wenzake.

“Askari hawa tunawashikilia na tayari mashitaka ya kijeshi yameanza huku uchunguzi ukiendelea na utakapokamilika, tutapeleka jalada kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa hatua za kisheria ili kuleta uwazi na uwajibikaji ndani ya jamii yetu”.

Alisema Jeshi hilo limekuwa likionesha uwajibikaji ambapo mwaka jana pekee askari 20 walichukuliwa hatua mbalimbali za kinidhamu.

Aidha, alisema majina ya askari hao yanahifadhiwa kwa sasa, kwa ajili ya usalama na wakati ukifika yatawekwa wazi huku polisi wakiendelea na upelelezi na gwaride la utambulisho.

Alisema baada ya tukio hilo kulikuwa na taarifa zenye kutuhumu askari hao juu ya upotevu wa fedha hizo na ndipo uchunguzi ulipoendelea ili kubaini ukweli.

“Baada ya uchunguzi wa kina na ushahidi uliokusanywa, umefanya askari hao washikiliwe na kuhojiwa … pamoja na uchunguzi askari kwanza watajibu mashitaka ya kijeshi,” alisema.

Katika tukio hilo la uporaji Desemba mwaka jana, inadaiwa Kayula na wenzake wakiwa wamepanda pikipiki mtindo wa ‘mshikaki’, walivamia duka la Kampuni ya Artan Limited na kupora Sh milioni 150, zilizokuwa zikitolewa dukani Kariakoo kwenda benki, ambapo watu watatu walipoteza maisha.

Waliopoteza maisha ni pamoja na mtuhumiwa Kayula, Sadiki Juma (38) na Ahmed Issa (55) waliopigwa risasi na majambazi katika eneo la tukio.

Katika hatua nyingine, Kova alikanusha taarifa kwamba alisema ameunda tume ya kuchunguza tukio la kiongozi wa Jumuiya ya Madaktari, Dk Stephen Ulimboka badala yake akasema ameunda Jopo la Upelelezi.

MCHAKATO WA KATIBA:Mtikila aibua mapya



MAKUNDI maalumu jana yaliendelea kutoa maoni yao kwenye mchakato wa Katiba Mpya, huku DP kikipendekeza Rais aapishwe baada ya siku 90 tangu kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu.
Mbali na maoni hayo yaliyowasilishwa na Mwenyekiti wa chama hicho, Mchungaji Christopher Mtikila, makundi mengine; wakulima, wafugaji, wanahabari na Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) nayo yalijitokeza kutoa moyoni.
Mtikila alisema kipindi hicho cha siku 90 kitatoa fursa kwa watu wanaotaka kuwasilisha pingamizi dhidi ya ushindi wa Rais mteule kufanya hivyo, kabla ya kuapishwa.
Alisema pingamizi linaweza kufanyiwa kazi kwa kipindi hicho cha miezi mitatu ili kuhakikisha kuwa taifa linapata kiongozi halali mwenye ridhaa ya wananchi.
“Pia tunataka kinga ya Rais ikome pale anapomaliza muda wake wa uongozi, kama alifanya makosa yoyote ya jinai aweze kushtakiwa ili kujenga nidhamu ya uongozi katika ofisi ya umma. Utaratibu wa kumwondoa madarakani uimarishwe asisubiriwe hadi amalize muda wake wa uongozi.”
Alisema kuwa Katiba ya nchi inapaswa kuwa mali ya wananchi wenyewe ili watawala wasijihusishe katika kuwaundia wananchi Katiba kama ilivyo kwa mchakato unaoendelea sasa wa kupata Katiba Mpya.
“Kumekuwa na hoja ya kuwapo kwa Serikali ya Tanganyika, hilo ni jambo muhimu na watu kutoka Tanganyika ni lazima wawe na Serikali yao ndani ya mipaka ya ardhi yao kupitia Katiba Mpya,” alisisitiza Mchungaji Mtikila.
Aliongeza kuwa nafasi za wabunge wa viti maalumu bungeni ziondolewe ili viti hivyo vishindaniwe kidemokrasia. Alisema wanawake wanatakiwa waelimishwe na kupikwa ili wahimili ushindani katika medani za kisiasa. Alisema kuwa taifa linahitaji viongozi bora na siyo kustarehesha jinsia.
Jukwaa la Wahariri
Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) limependekeza Katiba ijayo kutambua uhuru wa vyombo vya habari, haki ya kupata habari na uhuru wa kutoa mawazo.
“Kwa Katiba hii na sheria nyingine yoyote isiyoendana na Katiba hii, milele haitaruhusiwa kudhibiti habari nchini Tanzania,” ilieleza taarifa hiyo.
TEF ilisema kuwa haitakiwi kuwe na vikwazo katika kuanzisha magazeti au vyombo vya habari binafsi, kwamba wahariri na wachapishaji wa magazeti na vyombo vingine vya habari hawatakiwi kudhibitiwa au kuingiliwa na Serikali.
“Chombo chochote cha habari chenye wajibu wa kusambaza taarifa kwa jamii ambacho kinachapisha taarifa kuhusu, au dhidi ya mtu yeyote kinawajibika kutoa fursa ya kuchapisha mawazo ya upande wa pili, ikiwa yapo, kutoka kwa mtu ambaye taarifa au chapisho linamhusu,” ilieleza taarifa hiyo.
Vilevile, wamependekeza kuwe na sheria ya Bunge ya kuanzisha Baraza la Habari la Taifa, ndani ya miezi sita tangu siku ya kuanza kutumika kwa Katiba Mpya, baraza ambalo litakuwa na wajumbe 15 kutoka katika taaluma mbalimbali.
“Wajibu wa Baraza la Habari la Taifa itakuwa ni kusimamia vyombo vya habari, kuweka viwango vya kitaaluma kwa vyombo vya habari, kufuatilia utekelezaji wa viwango vilivyowekwa, kukuza taaluma na weledi katika vyombo vya habari,” ilisema taarifa hiyo na kuongeza;
“Kusikiliza mashauri au malalamiko dhidi ya vyombo vya habari, gharama za uendeshaji wa baraza. Kwa mujibu wa Katiba hii, Baraza la Habari la Taifa ndicho kitakuwa chombo cha mwisho katika kusimamia tasnia ya habari nchini.”
Katika suala la haki ya kupata habari, TEF imesema kila mwananchi ana haki ya kupata taarifa zozote hata zile zilizopo mikononi mwa Serikali.
Katika suala la uhuru wa kutoa mawazo Jukwaa hilo limeeleza kwamba kila mtu ana uhuru wa mawazo unaohusisha uhuru wa kutafuta, kupokea au kutoa taarifa au mawazo.
Baraza hilo limesema kuwa uhuru huo hautahusisha propaganda kwa ajili ya vita, uchochezi wa kuanzisha vurugu, hotuba za chuki, utetezi wa chuki, ukabila, ubaguzi kwa watu wengine au kuchochea mapambano.
Mtandao wa Jinsia
Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) umetaka Katiba Mpya iwe na dira ya kitaifa inayosisitiza ustawi wa wananchi katika kujenga mazingira ya kuwezesha mihimili mitatu kufanya kazi zake.
Mwenyekiti wa TGNP, Mary Rusimbi alisema kuwa moja ya mambo muhimu ambayo Katiba kwa kupitia itikadi hiyo inapaswa kuyasimamia na kuyastawisha ni haki za wanawake.
“Mchango wa mwanamke ni lazima utambulike kikatiba. Wanawake wana mchango mkubwa katika suala zima la malezi na uzalishaji mali wa aina mbalimbali, hivyo rasilimali za nchi pamoja na bajeti ya nchi zinapaswa kuwanufaisha wanawake kama ilivyo kwa wanaume,” alisema Rusimbi.
Profesa Ruth Meena alisema ni wajibu wa Serikali kuhakikisha mwanamke hafi kwa matatizo ya uzazi kwa kuboresha huduma ya uzazi katika hospitali zote nchini.
“Pia tunataka kuwapo na uwajibikaji wa viongozi. Viongozi ambao hawatimizi wajibu wao wanapaswa kujiuzulu badala ya kusubiri hadi wamalize muda wao wa uongozi, uwe wa miaka mitano au zaidi. Katiba ya sasa haiwapi wananchi mamlaka ya kuwawajibisha viongozi wazembe,” alisema Prof Meena.
Kuhusu Viti Maalumu, Profesa Meena alisema vinapaswa kuboreshwa ili hata wanawake ambao hawana chama cha siasa waweze kuwa na fursa ya kuteuliwa au kuchaguliwa kushika nafasi za uongozi.
Alisema kuwa kwa mfumo wa sasa ni wanawake walio kwenye vyama tu ndiyo wenye haki ya kupata nafasi za viti maalumu.
Wakulima
Wakulima nchini wametaka Katiba Mpya iweke uwiano sawa katika ugawaji wa ardhi kati ya wakulima na wafugaji ili kuondoa migogoro ya mara kwa mara.
Mwenyekiti wa Chama cha Wakulima Taifa (Taso), Engelbert Moyo alisema hatua hiyo itasaidia kuondoa migogoro ya wakulima na wafugaji na kuimarisha uchumi wa nchi.
“Tunapozungumzia wakulima hata ufugaji unaingia hapo ndiyo maana tukaona kuna haja ya kupendekeza kuwe na maeneo maalumu ya kufanyia shughuli hizo. Katiba iwe chanzo cha kuondoa migogoro hiyo kwa kuweka uwiano sawa katika ugawaji ardhi,” alisema na kuongeza;
“Kama Katiba Mpya itasema hivyo kwamba kutakuwa na ugawaji sawa wa ardhi kwa wakulima na wafugaji itasaidia kuondoa migogoro ambayo inaibuka mara kwa mara kati ya wakulima na wafugaji kitu ambacho hakileti picha nzuri kwa taifa letu.”
Alisema zaidi ya asilimia 80 ya uchumi wa taifa unategemea kilimo, lakini bado maisha ya wakulima yapo chini kitu ambacho ni vyema Katiba Mpya ikaliona.
Wafugaji
Umoja wa Wafugaji, umependekeza Katiba Mpya ijayo ianzishe sheria mpya ya ardhi kwa jamii pamoja na kutambua na kulinda mila na tamaduni za jamii mbalimbali nchini.
“Katiba itambue miliki ya pamoja ya ardhi kwa wafugaji inayoratibiwa na taasisi za jadi kwa mujibu wa sheria za mila za jamii mbalimbali,” alisema William Olenasha.
Alisema kitendo cha hakimiliki ya ardhi kuwa mikononi mwa Rais ni kuwanyima haki wananchi hususan wafugaji.
Rehema Mkalata, mfugaji kutoka Morogoro alisema kwa muda mrefu jamii ya wafugaji imeonekana kuwa ni jamii ya watu duni ndiyo maana hata matatizo yao hayapewi kipaumbele.
Alisema kuwa ni matarajio yake kwamba Katiba Mpya itawatambua jamii ya wafugaji kuwa na thamani sawa na watu wengine.
Pia alisema kuwa Katiba Mpya inatakiwa kuzitambua dawa asilia kuwa zinafaa kwa ajili ya matumizi ya binadamu.

Imeandikwa na Fidelis Butahe, Aidan Mhando, Ibrahim Yamola na Matern Kayela.

Thursday, January 10

Tucta yataka haki ya migomo,maandamano katika katiba

SHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (Tucta), limependekeza kwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, migomo na maandamano viwe haki ya msingi ya raia.
Wakati Tucta likitoa pendekezo hilo, Chama cha UPDP kimeungana na CCM kutaka mgombea binafsi aruhusiwe, huku NCCR Mageuzi kikiungana na Chadema kutaka umri wa urais ushushwe na apunguziwe madaraka.
Tucta, mbali na kutaka maandamano na migomo viruhusiwe, limependekeza hayo yafanyike kisheria baada ya kufutwa sheria kandamizi zinazowabana wafanyakazi wanaodai haki na masilahi yao.
Katibu Mkuu wa Tucta, Nicholas Mgaya alisema jana baada ya kuwasilisha maoni ya shirikisho hilo kuwa Katiba Mpya lazima iwe mkombozi wa wafanyakazi.
Alisema wanataka Katiba itamke kwamba kila mfanyakazi atakuwa na haki ya kugoma na kufanya maandamano wakati wanapoona haki zao hazizingatiwi.
“Sheria zilizopo zinazoruhusu maandamano na migomo ni kandamizi. Tunataka Katiba Mpya izifute na ziwepo sheria ambazo si kandamaizi ili kuwapa nafasi wafanyakazi kudai haki zao kwa maandamano bila vikwazo.”
Mgaya alisema Katiba Mpya iwe na kifungu kitakachoeleza uhusiano kazini ili kuhakikisha wafanyakazi wananufaika na kazi wanazofanya.
“Tunataka Katiba Mpya itamke kila mfanyakazi atakuwa na haki ya kushiriki na kushirikishwa kupitia vyombo mbalimbali vya mashauriano na vinavyohusika katika uamuzi wa kazi. Hiyo itakuwa njia sahihi ya kutoa nafasi kwa wafanyakazi kueleza mambo ambayo wanaona hawanufaiki nayo katika sehemu zao za kazi,” alisema.
Pia alisema: “Tunataka Katiba Mpya itamke kwamba ndani ya Bunge kutakuwa na uwakilishi wa wafanyakazi ili kutatua matatizo ya wafanyakazi.”
UPDP na mgombea binafsi
Mkurungezi wa Sheria na Katiba wa UPDP, Juma Nassoro alisema pamoja na mambo mengine, wamependekeza mgombea binafsi aruhusiwe katika nafasi zote za uongozi isipokuwa urais.
Alisema mfumo wa sasa unaolazimisha mgombea kutokana na chama cha siasa ni kuwanyima wananchi wasio na vyama kushiriki katika uongozi wa nchi kwa kutumia haki yao ya kuchagua na kuchaguliwa.
Alisema mantiki ya kutaka mgombea wa urais atokane na vyama vya siasa ni kutoa nafasi kwa wananchi kufanya tathmini za sera za vyama husika... “Yawezekana mtu akajitokeza kuwa mgombea urais na akawa na sera inayopingana na Katiba na maadili ya nchi. Ili kuepuka hilo Katiba Mpya isiruhusu mgombea binafsi kwa nafasi ya urais.”
Pia alisema wamependekeza muundo wa Serikali uwe wa Serikali tatu; Tanganyika, Zanzibar na Muungano... “Katika uongozi kwenye Serikali hizo kutakuwa na marais watatu kutoka kila Serikali huku Serikali za Tanganyika na Zanzibar zikiwa na mawaziri viongozi na ya Muungano ikiwa na waziri mkuu atakayeteuliwa na Rais wa Muungano na kuthibitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano.”
NCCR na umri wa Rais
Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, James Mbatia kwa upande wake alisema wametaka Rais asirundikiwe madaraka makubwa na asiruhusiwe kuteua viongozi wa mihimili mingine ya dola.
“Umri wa mtu kupiga kura uwe miaka 18, ila tunataka mtu mwenye miaka 21 ndiye awe na uwezo wa Kikatiba kugombea ubunge na udiwani pamoja na uwakilishi Zanzibar,” alisema Mbatia na kuongeza: “Katika urais tumependekeza kuwa umri wa kugombea nafasi hiyo uwe miaka 35 badala ya 41 ya sasa.”
Pia NCCR-Mageuzi kimependekeza muundo wa Serikali tatu; Tanganyika, Zanzibar na Serikali Kuu Shirikisho yenye mamlaka ya kidola, ambayo itakuwa chini ya mkataba unaoeleweka kimataifa.
Chama hicho pia kimependekeza Katiba kukitambua Kiswahili kuwa lugha ya taifa na itumike kufundishia katika ngazi zote za elimu.
Kuhusu mgombea binafsi alisema chama hicho kimependekeza Katiba iruhusu kwa kuwa kila mwananchi anayo haki ya kuchagua na kuchaguliwa hata kama si mfuasi wa chama chochote cha siasa.
“Haki ya kuchagua na kuchaguliwa ni ya kila mtu na inalenga mtu mmojammoja na si chama cha siasa, taasisi au kikundi cha watu,” alisema Mbatia.
Kuhusu muundo wa Serikali alisema wamependekeza kwamba Baraza la Mawaziri lisiwe kubwa kama ilivyo sasa na Katiba iweke idadi ya wizara na majina yake na zisizidi 15.
Jukwaa la Katiba na jinsia
Jukwaa la Katiba Tanzania limetaka Katiba Mpya iguse maeneo yote muhimu ikiwa ni pamoja na wanawake, wazee na watu wenye ulemavu ili kuhakikisha haki zao zinatambulika kikatiba.
Pia linataka itamke raia wa nchi hii ni nani na haki anazopaswa kupewa ili kumtofautisha na wageni wanaoingia.Mwenyekiti wa Jukwaa hilo, Deus Kibamba alisema Katiba ya sasa haimtofautishi raia wa Tanzania na wa kigeni kwani haielezi ni nani na haionyeshi haki anazopaswa kupewa.
Kuhusu elimu, Kibamba alisema Katiba Mpya itamke kwamba elimu ya ngazi ya msingi iwe hadi kidato cha nne ili kuongeza uelewa wa wanafunzi na itamke pia kwamba elimu hiyo itakuwa ni haki ya msingi kwa kila raia.
Imeandikwa na Fidelis Butahe, Aidan Mhando na Daniel Mwingira

TAWALA ZA MAJIMBO NA SERIKALI ZA MITAA

1. Nchi ya Tanganyika itagawanywa katika maeneo kumi ya kikanda yatakayojulikana kama Majimbo kama ifuatavyo:

(a) Jimbo la Nyanza Magharibi ambalo litaundwa na mikoa ya sasa ya Kagera, Geita na Shinyanga;

(b) Jimbo la Nyanza Mashariki litakaloundwa na mikoa ya sasa ya Mara, Mwanza na Simiyu;

(c) Jimbo la Ziwa Tanganyika litakalojumuisha mikoa ya sasa ya Kigoma, Katavi na Rukwa;

(d) Jimbo la Kati litakaloundwa na mikoa ya sasa ya Tabora, Singida, Dodoma na Iringa;

(e) Jimbo la Kaskazini litakaloundwa na mikoa ya sasa ya Arusha, Kilimanjaro na Manyara;

(f) Jimbo la Pwani ya Kaskazini litakaloundwa na mikoa ya sasa ya Tanga, Wilaya za Bagamoyo, Chalinze, Kibaha, Kisarawe na Mkuranga katika Mkoa wa sasa wa Pwani na Wilaya za Gairo, Kilosa, Mvomero, Morogoro na Kilombero katika Mkoa wa sasa wa Morogoro;

(g) Jimbo la Mji Mkuu wa Dar es Salaam;

(h) Jimbo la Pwani ya Kusini litakaloundwa na mikoa ya sasa Lindi, Mtwara na Wilaya za Rufiji na Mafia katika Mkoa wa sasa wa Pwani, na Wilaya ya Ulanga katika Mkoa wa sasa wa Morogoro;

(i) Jimbo la Nyanda za Juu Kusini litakaloundwa na mikoa ya sasa ya Mbeya, Njombe na Ruvuma;

2. Majimbo yataongozwa na Gavana atakayechaguliwa moja kwa moja na wananchi katika Jimbo husika.

3. Miji, manispaa na jiji ndani ya majimbo itaongozwa na Meya atakayechaguliwa moja kwa moja na Wananchi katika Mji husika;

Tuesday, December 25

"MZIKI WA BONGO FLEVA NI WA KIJINGA"....TID


Inaonekana bado mambo hayamwendei poa Top In Dar licha ya kuwa na hit ya ‘Kiuno’ hewani ambayo imeendelea kufanya poa.Hiyo ni baada ya nyota huyo ambaye jina lake halisi ni Khalid, kuamua kutumia Facebook kutoa maoni yake jinsi muziki huo unavyoenda.
“This Bongo Fleva Music is so stupid yaani kiasi kwamba we don’t even sell it only adios get sponsorship to play it lakini sisi tuko majalala,” aliandika TID.
Ujumbe huo ulivuta hisia za Chidi Benz ambaye aliamua kuchangia kwa kuandika: "Uoga. Unazaa vijana wanataka ustaa so wanakubali chochote. Wakongwe wanataka maisha so wanahitaji kuongezwa chochote. Vitu vinagongana vitu havieleweki."
Chidi aliongeza,”Watangazaji na wadau wamekua mameneja. Haikatazwi. Ila kama wewe si line yake atakupa vipi na asimpe msanii wake. We utapita vipi? Ujinga unajizaa kwa style ya mapacha."
TID naye aliongeza, “now watangazaji sasa hivi wanatutukana and they can do anything to anyone wanaweza wakasema TiD amecopy wimbo bila ya research yoyote yaani anaweza kufanya kila kitu hana limit.”

Mume wa ofisa wa Takukuru ampa jukumu Dk Hoseah

MUME wa aliyekuwa Ofisa Uchunguzi wa Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru), marehemu Bhoke Ryoba ambaye aliuawa juzi kwa kupigwa risasi amesema kifo cha mkewe kimegubikwa na utata mwingi.
Akizungumza na jana, mumewe huyo, Charles Gibore, pamoja na mambo mengine alimtaka Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Dk Edward Hoseah na Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi wa kina kuhusu tukio hilo kubaini ukweli.
“Mke wangu aliuawa na mfanyakazi mwenzake na tukio hilo limegubikwa na utata ambao Takukuru na Polisi ndiyo pekee wanaoweza kutupa ukweli,” alisema Gibore nje ya chumba cha kuhifadhi maiti katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Dar es Salaam.
Gibore alieleza kuwa mkewe huyo aliuawa usiku wa kuamkia Jumapili katika tafrija ya kuagana na kupongezana na baadhi ya wafanyakazi wenzake wa Takukuru waliokuwa wamepandishwa vyeo, tafrija ambayo Bhoke alipewa zabuni ya kupika chakula.
Alisema pia mkewe aliombwa pia awapatie wenye sherehe hiyo, vijana wawili wa kuwachomea nyama... “Vijana hao walikwenda asubuhi ukumbini ili kuandaa eneo la kuchomea nyama, huku Bhoke akiwa bado nyumbani akiandaa chakula,” alisema Gibore na kuongeza:
“Wale vijana walinieleza kwamba baadaye saa 8:30 mchana, Bhoke na wenzake walifika ukumbini na kuwakuta vijana wawili wanaofanya nao kazi wakinywa pombe, huku wakichezea silaha aina ya bastola kujaribu shabaha.”
“Vijana hao walifyatua risasi juu na ndipo muuaji alipompiga kichwani marehemu katika jicho na mauti yalimfika muda mfupi,” alisema.
Alisema baada ya hapo muuaji huyo alitoweka kisha kujisalimisha mwenyewe katika Kituo Kikuu cha Polisi Mkoa wa Temeke, Chang’ombe.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Temeke, Engelbert Kiondo alithibitisha mtuhumiwa huyo kujisalimisha na kisha kushikiliwa kituoni hapo na kueleza kuwa amekuwapo hapo Jumamosi iliyopita.Kamanda Kiondo alisema pamoja na mtuhumiwa huyo kujitambulisha kuwa ni mfanyakazi wa Takukuru, polisi wanaendelea kuchunguza ili kubaini ukweli wa taarifa hizo.
“Tunaendelea kumshikilia hapa na uchunguzi utakapokamilika tutamfikisha mahakamani kwa taratibu nyingine za kisheria,” alisema Kiondo.
Marehemu Bhoke Ryoba alizaliwa Juni 18, 1978 katika Kijiji cha Kiterere, Wilaya ya Tarime mkoani Mara na anatarajiwa kuzikwa kesho kijijini kwao.
Ameacha watoto watatu; Doloresy (10), Dolrisy (4) na Dolrick Gibore ambaye ana mwaka mmoja.

Mwekezaji atiwa mbaroni kwa ujangili

MENEJA wa Hoteli ya Kitalii ya Tree Top, iliyoko katika Hifadhi ya Taifa ya Tarangire, wilayani Monduli ametiwa mbaroni kwa tuhuma za kukutwa na ngozi za chui nyumbani kwake, akiwa katika harakati za kuisafirisha kinyemela kwenda nje ya nchi.
Habari zilizothibitishwa na Meneja Uhusiano wa Shirika la Hifadhi za Taifa (Tanapa), Paschal Shelutete, zilisema mtuhumiwa huyo anayeaminika kuwa ni raia wa Afrika Kusini alikotarajia kupeleka ngozi hiyo, alikamatwa saa 11 jioni ya Desemba 21, mwaka huu.
Kwa mujibu wa habari hizo, kabla ya kutiwa mbaroni, Kikosikazi kinachoundwa na askari kutoka Tanapa, Jeshi la Polisi na Mamlaka ya Hifadhi ya Bonde la Ngorongoro (NCAA), kilifanya upekuzi nyumbani kwa meneja huyo baada ya kupokea taarifa za siri kuwa anajihusisha na ujangili na kuuza isivyo halali, nyara za Serikali.
“Ni kweli mtuhumiwa huyo alikamatwa baada ya kikosikazi chetu kupata taarifa kuwa anamiliki nyara za Serikali kinyume cha sheria na kweli baada ya upekuzi alikutwa na ngozi ya chui,” alisema Shelutete kwa njia ya simu jana.
Alisema suala hilo tayari limefikishwa polisi katika Kituo cha Mto wa Mbu, wilayani Monduli kwa ajili ya uchunguzi na hatua zaidi za kisheria kabla ya mtuhumiwa kufikishwa mahakamani.
Habari zaidi zilidai kuwa mtuhumiwa aliyepelekwa katika Kituo cha Polisi cha Karatu ambako ndiko yalipo makao makuu ya Kikosikazi cha kupambana na ujangili katika Hifadhi za NCAA, Manyara na Tarangire.
Inasemekana hata hivyo aliachiwa kwa dhamana baada ya kudhaminiwa na mfanyakazi mmoja wa Hoteli za Sopa Lodges inayomiliki msururu wa hoteli kwenye mbuga za wanyama katika Mikoa ya Arusha na Mara.
Katika nyumba ilimokutwa nyara hizo za Serikali, inasemekana nyara zilikutwa zikiwa zimefungwa kwenye mfuko maalum tayari kusafirishwa huku jina na anwani ya mpokeaji ikiwa pia imeandikwa.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Lebaratus Sabas aliyezungumza kwa njia ya simu akiwa njiani akitokea Moshi kwenda Arusha, aliahidi kulifualia suala hilo na kulitoa ufafanuzi suala hilo baada ya kufika ofisini.
Katika siku za hivi karibuni kumekuwa na ongezeko la matukio yanayohusishwa na vitendo vya ujangili hatua ambayo inahatarisha usalama wa baadhi ya nyara za Serikali. Wiki iliyopita Serikali ilitangaza kutia mbaroni mtandao wa ujangali uliokuwa ukijihusisha na biashara haramu ikiwemo wa pembe za ndovu

JWTZ: Tunamsaka askari aliyepiga picha na Lema

WAKATI Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), likihaha kumtafuta aliyepiga picha na Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema akiwa amevaa sare za jeshi hilo, mtu huyo ameibuka na kusema yuko tayari kufukuzwa kazi kuliko kuacha kuishabikia Chadema.
Kauli hiyo ya JWTZ imekuja baada ya jana, gazeti la mwananchi kuchapisha picha ya mtu huyo aliyejitambulisha kuwa ni askari wa JWTZ akiwa amepiga picha na Lema pamoja na Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari, huku akiwa amenyoosha vidole viwili alama inayotumiwa na Chadema.
Baada ya taarifa hiyo, JWTZ lilitoa taarifa likieleza kushtushwa na tukio hilo na kusema kwamba linamtafuta mtu huyo kwa udi na uvumba ili kujiridhisha kama kweli ni askari wake.
‘‘Kimsingi Jeshi linafanya uchunguzi wa kumtambua mtu huyo kama kweli ni askari,’’ ilisema sehemu ya taarifa ya Kurugenzi ya Habari na Uhusiano ya jeshi hilo ambayo iliyatilia shaka mavazi aliyokuwa amevaa mtu huyo kama ndiyo yanayotumiwa na jeshi hilo sasa.
Taarifa hiyo ya JWTZ, ilisema ingekuwa rahisi kumtambua mtu huyo kwa kuangalia paji la uso lakini alilifunika ili asitambulike.
‘‘Pamoja na hayo, jeshi linamtafuta ili kumchukulia hatua za kinidhamu kutokana Kanuni za Majeshi ya Ulinzi likisema Sheria namba Nne ya Mabadiliko ya Nane katika Katiba ya Nchi ya mwaka 1992, Ibara ya 147(3), mwanajeshi yeyote hatakiwi kujihusisha na masuala ya kisiasa,’’ ilisema taarifa hiyo.
Mbali ya taarifa hiyo, Msemaji wa JWTZ, Kanali Kapambala Mgawe alisema endapo itabainika kuwa aliyevaa sare hizo ni mwanajeshi, moja ya hatua dhidi yake ni kufukuzwa kazi mara moja.
Mbali na hatua hiyo, Kanali Mgawe alisema kuanzia sasa, Jeshi limepiga marufuku mtu yeyote kuvaa sare zake katika mikutano yote ya siasa na atakayebainika atachukuliwa hatua kali za kinidhamu.
Kuhusu kitendo cha askari huyo kupiga picha na Lema, Kanali Mgawe alisema moja ya masharti muhimu ya askari anapiojiunga na jeshi ni kutambua na kutii sheria inayomzuia kujihusisha na masuala ya siasa na kwamba kitendo cha mtu huyo kimemshangaza na kumfanya amtilie shaka kama kweli ni askari aliyekamilika.
Msimamo wa mtuhumiwa
Kwa upande wake, mtu huyo aliyejitambulisha kuwa ni askari wa Kikosi cha Chuo cha Mafunzo Monduli (TMA), mkoani Arusha, alisema ni bora afukuzwe kazi kuliko kunyimwa kujiunga na Chadema.
Akizungumza jana kwa sharti la kutotajwa jina akiwa Mirerani, Simanjiro mtu huyo alisema Chadema ni chama makini chenye uwezo wa kuongoza nchi kwani kinatetea wanyonge na kujali masilahi ya jamii.
Alisema kwa kuwa Katiba ya nchi hairuhusu wanajeshi kujihusisha na vyama vya siasa, yuko tayari kufukuzwa kazi ili aendelee kukishabikia chama hicho.
Alisema ruhusa ya kikatiba kwa wanajeshi ya kupiga kura kuchagua madiwani, wabunge na Rais haitoshi na kwamba ameamua kujiunga kabisa na chama. Askari huyo alipiga picha na Lema baada ya mbunge huyo kuhutubia mkutano uliofanyika huko Mirerani. Katika mkutano huo wa hadhara, Lema alisema: “Ninapoongoza maandamano ya makamanda ninakuwa natetea masilahi yenu mkiwamo polisi ambao mnanipiga mabomu.
Sisi hatuangalii wake zetu wamevaa hereni za dhahabu ila tunaandamana kudai haki, mishahara mizuri kwa madaktari, walimu, askari na maisha bora kwa Watanzania.”
Raymond Kaminyoge, Patricia Kimelemeta, Dar na Joseph Lyimo, Simanjiro.