Wednesday, May 22

BUNGE lisitishwa jioni hii kutokana na hali tete ya mtwara



Spika ameahirishwa bunge hadi kesho kutokana na hali ya Mtwara. Spika kasema amepokea hali ya vurugu mtwara, hivyo bunge limeahirishwa ili kutoa fursa kwa kamati ya bunge kujadili suala hilo na serikali imetakiwa kutoa majibu katika kikao cha kesho.
Spika kasema kuwa wabunge wangependa kujadili hali ya Mtwara leo  lakini watajadili nini wakati hata wao wabunge wamepata taarifa hizo  kwenye vyombo vya habari? Hivyo, akaiagiza serikali kuleta majibu sahihi kesho bungeni na kuwaomba wabunge kuwa na subira hadi kesho na kisha akaahirisha bunge.
Akahitimisha kwa kusema kamati ya bunge inakwenda kujadili suala hilo sasa hivi.

No comments:

Post a Comment