Wednesday, August 28

TAARIFA YA RASMI YA KUREJESHWA URUSHAJI MATANGAZO RADIO IMAAN FM NA KWA NEEMA FM


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

KUREJESHWA KWA URUSHAJI MATANGAZO RADIO IMAAN FM NA KWA NEEMA FM RADIO

1.0 Utangulizi:

Mnamo tarehe 26/02/2013 Kamati ya Maudhui ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania ilitoa uamuzi wa kuvifungia vituo vya utangazaji vya Radio Imaan ya mjini Morogoro na Kwa Neema FM Radio ya jijini Mwanza baada ya kukiuka Sheria na Kanuni za Utangazaji.

Kamati ya Maudhui iliuita uongozi wa vituo hivyo tarehe 11/02/2013 na tarehe 14/02/2013 ili kujitetea na vyote vilikiri kosa. Baada ya kutafakari utetezi wa Radio Imaan na Radio ya Kwa Neema FM na kwa kuzingatia Sheria na Kanuni za Utangazaji, Kamati iliamua kutoa adhabu kwa vituo vyote viliwi kama ifuatavyo:-

a) Vituo vyote vilipewa onyo pamoja na kufungiwa kurusha matangazo kwa kipindi cha miezi sita kuanzia
tarehe 26/02/2013;

b) Vituo vyote vilitakiwa kuithibitishia Mamlaka ya Mawasiliano na Kamati ya Maudhui kwa maandishi kuwa hawatarejea kutenda kosa la aina hiyo au linalofanana na hilo. Ikiwa vitarudia Kamati ya Maudhui haitasita kuvifutia leseni zao za utangazaji.

2.0 Kutekeleza adhabu na hatua zilizochukuliwa na vituo hivyo na Mamlaka ya Mawasiliano:

Baada ya Uamuzi huo kusomwa, vituo vyote viwili vilianza kutekeleza adhabu mara moja kama ilivyotakiwa kwa mujibu wa Sheria na Kanuni za Utangazaji. Mamlaka ya Mawasiliano ilipokea barua ya udhibitisho wa kutofanya kosa tena yaani “Commitment letter” pamoja na sera ya uhariri (Editorial Policy) na ratiba ya vipindi kutoka kwa vituo vyote viwili.

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania ilifanya ukaguzi kwa vituo vyote viwili ili kujiridhisha na kuzipitia sera za uhariri pamoja na mwongozo wa vipindi kabla ya kuvifungulia.

3.0 Kurejeshwa kwa Matangazo

Kamati ya Maudhui iliandika barua tarehe 27/08/2013 kuhusu kuvifungulia vituo hivyo vya utangazaji vya Radio Imaan ya mjini Morogoro na Kwa Neema FM Radio ya jijini Mwanza baada ya kutumikia adhabu kwa mujibu wa Sheria na Kanuni za Utangazaji. Vituo hivi vimeanza kurusha matangazo yake kuanzia leo tarehe 28/08/2013 baada ya muda wa adhabu kuisha.

Kamati ya Maudhui inapenda kutumia fursa hii kuvionya vyombo vya habari vya utangazaji vya redio na televisheni kuwa makini katika kutekeleza masharti ya leseni pamoja na kufuata Sheria na Kanuni za Utangazaji. Kamati ya Maudhui haitasita kutoa adhabu kali au kuvifungia vituo vitakavyokiuka Masharti ya leseni, Sheria pamoja na Kanuni za Utangazaji au hata kuvifutia leseni zao.

Kamati ya Maudhui inatoa wito kwa vyombo vya habari vya utangazaji kuzingatia Sheria, Kanuni na Masharti ya leseni ilikuboresha Sekta ya Utangazaji na kudumisha amani nchini.

Eng. Margaret Munyagi
Mwenyekiti,
Kamati ya Maudhui Ya TCRA,
S.L.P. 474,
DAR ES SALAAM.
28/08/2013

----

KUHUSU KAMATI YA MAUDHUI:

1.1. Kamati ya Maudhui ni kamati iliyoundwa kwa mujibu wa sehemu ya IV kifungu cha 26 (1) cha Sheria Namba 12 ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania ya mwaka 2003, na marekebisho yake katika kifungu 173 cha Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta (EPOCA) Mwaka 2010

Kwa mujibu wa sheria, majukumu na kazi za Kamati ya Maudhui ni pamoja na:-

(a) Kumshauri Waziri wa Sekta kuhusiana na Sera ya Utangazaji nchini;
(b) Kushughulikia malalamiko kutoka kwa watangazaji na watumiaji wa huduma za utangazaji nchini;
(c) Kusimamia na kuhakikisha kuwa kanuni za utangazaji zinafuatwa.
(d) Kusimamia na kufuatilia maudhui ya vituo vya utangazaji.

1.2. Kamati hii ilianza kazi zake Oktoba 2012 baada ya kuzinduliwa rasmi na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk. Fenella Mukangara (MB) tarehe 4 Desemba, 2012.

1.3. Kamati ya Maudhui inaundwa na wajumbe watano. Wanne ni wateuliwa wa Waziri mwenye dhamana ya Sekta ya Utangazaji na Mwenyekiti ambaye huchaguliwa miongoni mwa wajumbe wa Bodi ya TCRA. Muundo huo umetolewa na sehemu ya 26 (2) ya Sheria ya TCRA ya Mwaka 2003.

Majina ya wajumbe ni kama ifuatavyo:-

i. Mhandisi Margareth Munyagi -Mwenyekiti
ii. Bwana Walter Bgoya -Makamu Mwenyekiti
iii. Bwana Abdul Ngarawa -Mjumbe
iv. Bwana Joseph Mapunda -Mjumbe
v. Bwana Yusuf Nzowa -Mjumbe

Sunday, June 30

LOWASSA AMTAKA OBAMA ASIZUNGUMIE MAMBO YA USHOGA NA NDOA ZA JINSIA MOJA AKIWA TANZANIA

Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo yaNje na Ushirikiano wa Kimataifa, Edward Lowassa, amemtahadhalisha kujiepusha na kauli za kuunga mkono ushoga.

Lowassa ambaye pia ni Mbunge wa Monduli, ameliambia NIPASHE Jumapili ofisini kwake jijini hapa jana kuwa ushoga na hai za ndoa kwa watu wa jinsia moja vinaweza `kuiharibu’ ziara yake hapa nchini.

Mapema wiki hii, Rais Obama alikaririwa akizungumzia masuala hayo yanayotajwa kuwa ni moja ya haki za msingi za binadamu, alipokuwa Senegal, lakini akapingwa.

“Watanzania hawatalikubali na wataendelea kushikilia uhuru na heshima walizojengewa tangu awali, kwamba ushoga na ndoa za jinsia moja havikubaliki,” alisema.

Akiwa Senegal, Rais Obama alitaka serikali za Afrika kutoa haki kwa mashoga kama inavyotoa kwa raia wengine.

"Ninachotegemea, I pray and hope (ninasali na kutegemea) kwamba kuhusu mashoga na ndoa za jinsia moja, Rais Obama hatarudia kauli aliyoitoa kule Senegal,” alisema.

Aliongeza, "ninasema hivi kwa sababu Tanzania hatuamini katika ushoga, na endapo utawalazimisha Watanzania, watakukatalia na kushikilia uhuru na heshima waliyojengewa toka awali."

AHIMIZA MAPOKEZI MAZURI
Hata hivyo, Lowassa aliwataka Watanzania kuiheshimu na kuitumiavema fursa ya kutembelewa na Rais Obama, hivyo wajitokeze kumlaki kwa wingi.

"Tutambue mataifa makubwa yanakimbilia maslahi ya karne inayofuata, kwa mfano Rais wa China, Xi Jiping siku moja baada ya kuapishwa kwake alikuja hapa nchini, " alisema.

Hivyo, alitoa wito kwa Watanzania kuhakikisha maslahi na fursa za kiuchumi zinakuwa za kwanza kulindwa, kwa kuwa ziara hiyo itafungua milango zaidi kwa wawekezaji kuja nchini.

Pia, Lowassa alisema ziara ya Rais Obama ni kielelezo cha amani na usalama uliopo, na kwamba itasaidia kuwavutia watalii na wadau wa sekta nyingine za maendeleo kuitembelea Tanzania.

KITUO CHA KIJESHI
Kuhusu hofu na tetesi kuwa ziara hiyo imelenga taifa hilo kuja hapa nchini kufungua kituo cha kujiimarisha kiulinzi, Lowassa alisema Watanzania wanapaswa kufahamu kuwa tayari nchi hiyo ina kituo cha kijeshi nchini Kenya.

"Tuangalie maslahi yetu tuachane na mitazamo hasi, kama ni kituo cha kijeshi tayari kipo Kenya, tujiulize kwa nini marais wa Marekani Bill Clinton na George Bush walivyofanyaziara zao hapa nchini hawakwenda Kenya," alisema.

WALINZI WA NDANI KUWEKWA KANDO
Kuhusu ziara hiyo kutumia ulinzi wa kimataifa huku majeshi ya Tanzania yakiwekwa kando kwa ushiriki wa moja kwa moja, Lowassa alisema Rais wa Marekani ana kiwango cha juu cha ulinzi unaosimamiwa na nchiyake pekee.

"Ni sahihi walinzi wetu kukaa pembeni, huyu ni kama Rais wa dunia, lakini hata majeshi yetu yanafanya kazi ya ulinzi lakini sio kwamba yatakaa nyuma tu," alisema.

SUMAYE: TUMKARIBISHE
Naye, Waziri Mkuu mstaafu, Fredrick Sumaye, alisema ziara ya Rais Obama haina ujumbe zaidi ya kuhimiza watu wajitokeze kumpokea.

Hata hivyo, Sumaye alikwepa kuzungumzia kwa undani hatua ya kuwafukuza wafanyabiashara kutoka kandoni mwa barabara, ili kupisha mapokezi ya Rais Obama.

“Ninachokielewa ni kuwa barabara ambazo wanapita viongozi kama Rais Obama zinatakiwa kuwa katikahali ya usalama na hivyo kutakiwa kuboreshwa,” alisema.

LIPUMBA: MAFANIKIO NI MADOGO KIUCHUMI
Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF) Profesa Ibrahim Lipumba, alisema mafanikio ya ziaraya Rais Obama yapo katika kujitangaza kimataifa kuliko kiuchumi.

Profesa Lipumba ambaye ni mchumi aliyebobea, alisema changamoto iliyopo ni kwamba bado biashara kati ya nchi mbili hizo siyo kubwa kama ilivyo kwa nchi kama China na Tanzania.

Alitolea mfano, mwaka 2012 bidhaa za hapa nchini zilizouzwa Marekani zilikuwa na thamani ya Dola milioni 66 ikilinganishwa na zile zilizouzwa China ambapo zilikuwa ni zaidi ya Dola milioni 500.

Alisema bidhaa zilizoagizwa kutoka Marekani zilikuwa na thamani ya Dola milioni 230 huku za kutoka China zikiwa na thamani ya zaidi ya Dola milioni 1,100.

"Utakubaliana nami kuwa mahusiano yetu na China ni makubwa kuliko Marekani licha ya nchi hii kutoa fursa kwetu ambazo hatujazitumia ipasavyo," alisema

Profesa Lipumba alisema Marekani kupitia mpango wake wa kusaidia Maendeleo ya Afrika (AGOA), ulitoa fursa kwa bidhaa za Afrika kuuzwa nchini humo bila ushuru, lakini Tanzania haikuitumia.

Pia alisema utawala wa George Bush, uliisaidia Tanzania kupitia Mfuko wa Changamoto za Milenia (Millenium Challenge Compact (MCC) kupewa Dola milioni 700 kwa ajili ya kusaidia miundombinu na ujenzi wa nyaya za umeme kutoka bandarini hadi Zanzibar.

"Pana uwezekano wa mpango wa pili wa MCC, Tanzania ikapata msaada wa kuimarisha miundombinu ya umeme, lakini pia kampuni za Marekani kuja kuwekeza hapa kwetu," alisema.

Alisema uwekezaji wa kampuni hizoutategemeana na wafanyabiashara wa hapa nchini pamoja na serikali kutumia fursa mbalimbali za nchi hiyo.

Katika hatua nyingine, Profesa Lipumba alisema ili nchi iweze kujikwamua na umasikini itatokana na jinsi itakavyotumia sera na juhudina siyo kutegemea msaada kutoka nje.

HOTELI ZIMEJAA
Wingi wa wageni wakiwamo watakaofika kwa ajili ya ziara ya Rais Obama, umesababisha hoteli nyingi za jijini Dar es Salaam `kujaa’.

Uchunguzi wa NIPASHE Jumapili ulibaini kwamba kwa zaidi ya wiki sasa, hoteli nyingi hazikupokea wageni kutokana na kile kilichoelezwa kuwa, nyingine zililipiwa ingawa vyumba havikutumika kwa wakati.

POLISI: WASIO NA KAZI WASIJE MJINI
Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohammed Mpinga, amewataka wananchi ambao hawatakuwa na mambo muhimu ya kufanya katikati ya jiji, wasifike huko kupunguza msongamano wa watu na magari baada ya kuwasili kwa Rais Obama.

Alisema, baadhi ya barabara zitafungwa kwa muda kwa ajili ya viongozi kuzitumia, hivyo kusababisha msongamano.

Hekaheka zimetanda jijini Dar es Salaam, ikiwa ni zaidi ya saa 24 kabla ya kuwasili kwa Rais Barack Obama.

Rais Obama, atawasili nchini kesho akitokea Afrika Kusini, ambapo pamoja na mambo mengine, alizungumza katika mkutano wa ‘viongozi vijana wa Afrika’ na kujibu maswali kutoka nchi tofauti.

Mkutano huo ulifanyika jana jioni huko Soweto nchini Afrika Kusini, ambapo alipokewaa na kujibu maswali kutoka Kenya, Uganda, Nigeria na Afrika Kusini kwenyewe.

Jijini Dar es Salaam, shughuli kadhaazikiwamo za ulinzi na usalama, zinafanyika kwa kasi na umakini kuhakikisha ziara ya Rais Obama inafanyika pasipo bughudha. kujibu maswali kutoka Kenya, Uganda, Nigeria na Afrika Kusini kwenyewe.

Jijini Dar es Salaam, shughuli kadhaazikiwamo za ulinzi na usalama, zinafanyika kwa kasi na umakini kuhakikisha ziara ya Rais Obama inafanyika pasipo bughudha.

Hata hivyo, sehemu kubwa inayohusu masuala ya itifaki, ulinzi na usalama yanafanywa na taasisi za Marekani, kwa kuzishirikisha taasisi za ndani kwa kiwango kidogo.

“Hawa jamaa (Wamarekani) wanapoingia nchi yeyote wakiwa naRais wao, shughuli nyingi na uamuzi wanafanya wao, sisi wa ndani inakuwa kushirikishwa kwa kiasi kidogo,” kilieleza chanzo cha NIPASHE Jumapili kutoka moja ya taasisi zinahusika katika ziara hiyo.

Maeneo kadhaa ya jijini humo, yaliendelea kudhibitiwa kwa ulinzi mkali na doria za mara kwa mara, huku kandoni mwa baadhi ya barabara wakionekana askari wa Jeshi la Wananchi (JWTZ).

Mathalani, kandoni mwa barabara ya Morogoro, eneo la Ubungo, walionekana askari wa JWTZ maarufu kama MP.

Shughuli nyingine zimehusisha pia operesheni zinazofanywa na polisi kwa kusaidiana na mgambo wa jiji, kuhakikisha watu na bidhaa zilizopokandoni mwa barabara zitakazotumika kwa ziara ya Rais Obama, vinaondolewa.

Magari yaliyowabeba polisi wenye silaha za moto na mabomu ya machozi, yalionekana katika mitaa kadhaa jijini humu, wakihakikisha operesheni hiyo inafanyika pasipo kikwazo kutoka kwa wahusika.

Kila palipofanyika operesheni hiyo, baadhi ya askari walifanya doria zamu kwa zamu, kuhakikisha kuwa bidhaa na watu walioondolewa, hawarejei.

Hata hivyo, waathirika katika operesheni hiyo walieleza kutofurahia, huku wakihoji ni kwa nini serikali haikuwaandalia mazingira mbadala kabla ya utekelezaji wake.

Walisema miongoni mwao, wamekopa mitaji kutoka kwenye taasisi za kifedha, hivyo kusimamisha biashara zao ili kupisha ujio wa Rais Obama, kutawaweka katika hali ngumu kiuchumi.

“Ikiwa ujio wa Rais Obama unatutesa wafanyabiashara kiasi hiki, ni vigumu kuhimili maisha yetu, kwa sababu hatujui hatma yetu baada ya yeye kuondoka,” alisema mfanyabiashara Zena Rashidi wa Kariakoo.

Hata hivyo, wamachinga walionekana jana katika kituo cha mabasi cha Mwenge walipofukuzwa, wakiwa wanaendelea na biashara zao.

Lakini walifanya hivyo kwa tahadhali ikiwamo kushika bidhaa chache mikononi, huku wakitumia 'janja' ya kupiga kelele za 'kumsifia' Rais Obama.

Walisikika miongoni mwao wakisema, 'praise to Obama' na wengine wakaitikia 'aaamen'. Walifanya hivyo zamu kwa zamu, lakini haikujulisha waliashiria nini.


BARABARA ZAPAMBWA
Aidha, barabara zote atakazopita Obama wakati wa ziara yake zimepambwa kwa bendera za Marekani na Tanzania; huku zikinakshiwa kwa picha yake ambayo imeandikwa 'President Barack Obama' karibu Tanzania.

Barabara hizo ni ile ya Nyerere kuanzia uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius K. Nyerere, Ali Hassan Mwinyi, Mwai Kibaki na Bagamoyo.

Imeshuhudia pichana bendera hizo zikiwa zimewekwa kwenye mabango yote yaliyo barabarani kuanzia Ikulu hadi kwenye barabara hizo huku usafi wa jiji ukionekana kuimarika zaidi.

Jana ilishuhudiwa karibu barabara zote, vijana wanaofanyakazi ya kuweka bendera na picha ya Obama wakifanyakazi hiyo.

Friday, June 21

"POLISI WATAENDELEA KUWAPIGA WALETA VURUGU HAPA NCHINI NA NINASEMA WAWAPIGE ZAIDA NA ZAIDA"... WAZIRI MKUU

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ameagiza vyombo vya dola kuwashughulikia kwa kuwapiga wale watakaokataa kutii amri wakati wakifanya vitendo vya uvunjifu wa amani.

Akizungumza katika Kipindi cha Maswali ya Papo kwa Hapo kwa Waziri Mkuu, bungeni Dodoma jana, Pinda alisema watu wanapokaidi wanajitakia matatizo na vyombo vya dola.

Alisema hayo alipokuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Kilwa Kaskazini (CCM), Murtaza Mangungu aliyeuliza: “Serikali ipo tayari kiasi gani kubainisha na kuchukua hatua stahiki, badala ya kusakama makundi fulani, tujue chanzo halisi cha vurugu hizi na matatizo haya na jinsi gani vyombo vya dola vinavyoshughulikia kwa sababu yapo malalamiko katika baadhi ya maeneo kama Mtwara kwamba wananchi wanapigwa na vyombo vya dola?”

Waziri Mkuu alijibu: “Ni lilelile nililosema... mwishowe unaona anasema vyombo vya dola vinapiga watu. Ukifanya fujo, umeambiwa usifanye hiki, ukaamua kukaidi, utapigwa tu... hamna namna nyingine, maana wote tukubaliane kwamba nchi hii tunaiendesha kwa misingi ya kisheria.

“Sasa kama wewe umekaidi, hutaki unaona kwamba ni imara zaidi... wewe ndiyo jeuri zaidi watakupiga tu.... Mimi nasema muwapige tu, kwa sababu hakuna namna nyingine... maana tumechoka.”

Pinda alisema Serikali imedhamiria kurejesha amani nchini ikiwamo mkoani Mtwara na kuwataka Watanzania waiache Serikali ifanye kazi hiyo. Alisema Serikali ina orodha ya watu wanaosemekana kuwa ni vyanzo vya vurugu na matatizo yaliyotokea Mtwara na kushangaa wale wanaopinga kukamatwa kwao.

“Lazima tuwakamate na kama katika kuwakamata watafanya jeuri, jeuri, watapigwa tu kabla ya kupelekwa tunapotakiwa kuwapeleka, kwa sababu hatuwezi kuendelea na hali hii, mkadhani kwamba tutafika tunapokwenda. Nami nasema vyombo vya dola vijipange imara vihakikishe vinadhibiti hali hii,” alisema.

Hata hivyo, jibu hilo lilipata upinzani wakati Mbunge wa Konde (CUF), Khatibu Said Haji alipomwuliza Waziri Mkuu: “Hapo awali umetoa kauli nzito ya kuliambia taifa hili kwamba wale raia wote, ambao watakaokuwa wakaidi wapigwe tu na watapigwa tu; naomba ninukuu Katika Ibara ya 13 na Kifungu cha 6B cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano.

“Ni marufuku kwa mtu yeyote aliyeshtakiwa kwa kosa la jinai kuteswa kama mtu mwenye kosa, mpaka itakapothibitika anayo hatia kwa kutenda kosa hilo.

“Pia ibara hiyohiyo Kifungu cha 6 E; kinasema ni marufuku kwa mtu yoyote, kuteswa, kuadhibiwa kinyama au kupewa adhabu zinazoweza kumdhalilisha. Kwa kauli yako uliyoitoa huoni kwamba umevunja Katiba?” Akijibu swali hilo, Pinda alisema ni lazima kutofautisha kati ya mtu aliyekwishakamatwa na kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria... “Mimi ninayemzungumza hapa ni mtu yule ambaye ameamua kufanya vitendo hajakamatwa na ndiyo maana nilikwambia usiandamane... hapa mahali hutakiwi kwenda wewe ukaamua kutumia mabavu kwa sababu mko wengi, ndiyo maana nikasema, hawa watu tutashughulika nao hivyohivyo.”

Mbunge huyo hakuridhishwa na majibu hayo na kumtaka Waziri Mkuu kuyafuta.

Hata hivyo, Spika wa Bunge, Anne Makinda aliingilia katika na kumweleza mbunge huyo kuwa kila mtu alikuwa amemwelewa Waziri Mkuu na hakukuwa na haja ya kuendelea na hoja hiyo.

Kabla ya swali lake la nyongeza, Mangungu aliuliza: “Ukisikiliza nyimbo nyingi za taifa katika Afrika zinasema hekima, umoja na amani ndiyo ngao zetu. Je, hali ambayo imejitokeza katika nchi yetu na matatizo yaliyojitokeza Arusha na maeneo mengine kama Mtwara. Nini tamko la Serikali?

Waziri Mkuu alijibu: “Swali lililoulizwa na Mheshimiwa Mangungu ni jambo linalotugusa sisi wote. Suala la amani, ulinzi, utulivu ndiyo hasa tunu ya kila nchi ingependa kuwa nayo. Ni kweli hivi karibuni kumejitokeza vurugu za hapa na pale kwa hiyo angependa tuwaeleze Watanzania kama Serikali tunafikiria tufanye nini.

Alisema ipo haja ya jukumu hilo kuachwa kwa viongozi wa kisiasa bila ya kujali itikadi zao... “Yako mambo ambayo lazima tukubali kwamba ni jukumu letu sisi wote na kila mmoja lazima azungumze lugha moja.

Ninyi wote ni mashahidi. Chadema waliposhinda hapa, wao walikuja waziwazi, wakasema tutahakikisha nchi hii haitawaliki. Sasa, inawezekana pengine ndiyo mwendelezo wa utekelezaji wa kauli hizo.

“La pili ni upande wa Serikali, lazima tuhakikishe kwamba wale wote ambao kwa kweli wanajaribu kuvunja amani kwa namna yoyote ile, kazi kubwa tuliyonayo ni kubanana, kupambana kwelikweli kwa njia zozote zile zinazoonekana zinastahili.

“Sasa mimi ninaomba sana Watanzania, maana kila juhudi zinapoonekana zinaelekea huko, unapata watu wengine wanajitokeza, unajua...unajua. Acheni Serikali itimize wajibu wake kwa sababu jambo hili ni la msingi, lazima tulilinde kwa nguvu zetu zote.

“Rai yangu kwa Watanzania kila mmoja ajue kwamba siku tukiingia katika vurugu, hakuna mshindi. Wote tutaumia, sasa wote tuhakikishe hili jambo tunalisimamia vizuri.”

Chadema waja juu

Akizungumzia kauli hiyo, Mkurugenzi Habari na Uenezi wa Chadema, John Mnyika alisema: “Kauli ya Pinda inakiuka Katiba ya nchi na imethibitisha kwamba matumizi mabaya ya vyombo vya dola na kusababisha mauaji ya raia yana baraka za Serikali.”

Alisema kauli ya Pinda kama ilivyokuwa ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi zinatoa mwelekeo kwamba mauaji ya Arusha yana baraka za Serikali.

Wanasheria wakerwa

Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dk Hellen Kijo-Bisimba alisema Waziri Mkuu hakustahili kutoa kauli kama hiyo.

Alisema Pinda hapaswi kuwa na jazba, bali anatakiwa kuwa na busara na kuzungumza kwa kuzingatia sheria za nchi badala ya kutoa matamshi ambayo siyo mwafaka kwa nchi inayoongozwa kwa kufuata sheria na taratibu.

Rais wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS), Francis Stola alisema kauli hiyo ya Waziri Mkuu, mbali ya kwenda kinyume cha Katiba na sheria ya nchi, inaweza kuhatarisha amani.

Stola alisema matumizi ya nguvu kupita kiasi kudhibiti hali yoyote korofi hayaruhusiwi.

Mbowe, Lema wahojiwa polisi,watoa msimamo

Arusha. Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema jana, walijisalimisha Makao Makuu ya Polisi ya Mkoa wa Arusha na kuhojiwa kwa zaidi ya saa nne kabla ya kuachiwa kwa kujidhamini wenyewe huku wakitakiwa kurejea kituoni hapo, Julai 22, mwaka huu.

Pia Mbowe na Lema wamemtaka Rais Jakaya Kikwete kuunda tume huru ya uchunguzi wa kimahakama ili kuchunguza vurugu za Arusha zilizoanza Jumamosi iliyopita baada ya bomu kurushwa kwenye mkutano wa Chadema na kusababisha vifo pamoja na zile zilizofuatia wakati polisi ilipowasambaratisha wafuasi wa chama hicho kwa mabomu walipokusanyika kwenye Viwanja vya Soweto kwa lengo la kutoa heshima za mwisho kwa marehemu.

Wakiongozwa na mawakili watatu, Mbowe na Lema waliwasili polisi saa 3.50 asubuhi na kuhojiwa hadi saa 9.10.

Viongozi hao walipokewa na Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Arusha, Diwani Nyanda kabla ya kutenganishwa kwenye vyumba viwili tofauti kwa mahojiano.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, Mbowe, Lema na wakili Albert Msando walitaja mambo mawili ambayo polisi waliwahoji kwanza ikiwa ni ushiriki wao katika mkusanyiko usio halali kwenye Viwanja vya Soweto, Jumanne iliyopita ambao ulisambaratishwa na polisi.

Jambo jingine ambalo polisi iliwahoji ni kauli yao ya kuwa na ushahidi unaohusisha polisi na tukio la bomu lililorushwa kwenye mkutano wa Chadema na kusababisha vifo vya watu wanne huku zaidi ya 60 wakijeruhiwa.

Mbowe alisema kwa pamoja wamewaeleza polisi kuwa hawaamini kama mkusanyiko wa Jumanne iliyopita haukuwa halali kwa sababu waliruhusiwa kuzungumza na wananchi waliokusanyika ili kuwashawishi watawanyike.

“Mkuu wa Polisi Wilaya (OCD) wa Arusha, Gilles Mroto ndiye aliyeturuhusu kuzungumza na wananchi wale kuwataka watawanyike na ndicho tulichofanya, lakini tukashangaa kuanza kupigwa mabomu mara baada ya kuwataka watu wanaotaka kutoa heshima za mwisho kwa marehemu kwenda Hospitali ya Mount Meru,” alisema Mbowe.

Alisema Mkuu wa Operesheni wa Polisi, Kamishna Paul Chagonja kuwa naye aliyewaomba viongozi wa Chadema kuwatawanya wafuasi wa chama hicho baada ya kuzuiwa kutoa heshima za mwisho katika viwanja hivyo vinavyomilikiwa na Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC).

Msimamo wa Mbowe

Kuhusu ushahidi anaodai unawahusisha polisi na tukio la bomu, Mbowe alisisitiza kuwa Chadema kina ushahidi wa kutosha kuthibitisha hilo lakini alisema hakitaukabidhi mikononi mwa polisi.

Alisema hakitafanya hivyo kwa kuwa jeshi hilo ni watuhumiwa wakuu hivyo hawawezi kuwa na dhamira na nia njema katika upelelezi wao. Alisema ndiyo maana badala polisi kuwaona ni msaada, kimeanza kutoa vitisho kwa wote wanaosema waliwashuhudia askari wakishambulia watu kwa risasi kabla ya kuondoka na aliyerusha bomu kwenye gari lao.

“Chadema tuko tayari kukabidhi ushahidi huu kwa tume huru ya uchunguzi ya Mahakama. Rais Kikwete atumie mamlaka yake ya kikatiba kuunda tume kuchunguza tukio la bomu Arusha ili ukweli ujulikane. Polisi ni watuhumiwa katika jambo hili, hivyo hawana dhamira safi na ushahidi wetu,” alisema Mbowe.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas alisema polisi inawasiliana na wanasheria kutafuta ushauri wa hatua za kuchukua... “Polisi ndiyo wenye jukumu la kuchunguza na kukusanya ushahidi wote kuhusiana na matukio ya uhalifu. Hili ni jukumu la kisheria la polisi. Chadema wakabidhi ushahidi wao badala ya kupiga danadana ya kutaka tume huru ya uchunguzi ya kimahakama.”

Alisema hata ikiundwa tume, bado jukumu la kuchunguza na kukusanya ushahidi litarejeshwa mikononi mwa polisi, hivyo Chadema wanapaswa kutimiza wajibu wa kusaidia uchunguzi kwa kuwasilisha ushahidi wao wa polisi kuhusika katika tukio la bomu.



Askofu alia na dola

Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Jimbo la Arusha Mashariki, Isaac Kisir ameitaka Serikali kuchukua hatua kali kulinda usalama huku akivitaka vyombo vya ulinzi na usalama kujitathmini kiutendaji.

Akizungumza katika ibada ya mazishi ya aliyekuwa kada wa Chadema, Judith Moshi iliyofanyika katika Usharika wa Sokoni One, Askofu Kisir alisema mlipuko wa bomu haukuwa mapenzi ya Mungu, bali ni ugaidi.

“Tunapomzika mwenzetu lazima tuseme ukweli, tusimung’unye maneno, ukweli utatuweka huru. Nchi yetu sasa haina usalama ule tuliokuwa nao. Kumekuwa na utekaji nyara watu wanaosema ukweli. Kumekuwa na matumizi ya nguvu kupita kiasi kwa vyombo vya usalama, uchomaji wa makanisa na milipuko ya mabomu.

“Tulitegemea Serikali itatoa adhabu kwa wanaohusika lakini tunasikia maneno ya kejeli… mara tuko mbioni, mara tuko imara, huku watu wanauawa na kupata vilema.”

Judith ni mmoja wa watu wanne waliouawa katika shambulio la bomu lililolipuka wakati wa kuhitimisha kampeni za udiwani za Chadema katika Viwanja wa Soweto Juni 15 mwaka huu, huku watu wengine zaidi ya 60 wakijeruhiwa.

"EDWARD LOWASSA ANAHUSIKA NA KUTEKWA KWANGU PAMOJA NI KIPIGO NILICHOPEWA"...NASSARI


Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari amemtuhumu Mbunge wa Monduli Edward Lowassa kwamba anahusika na kipigo alichokipata kutokana na chuki aliyonayo kwake.

Aidha amemtuhumu Spika wa Bunge, Anne Makinda kwamba naye ni miongoni mwa watu wanaomchukia pamoja na viongozi wengine wa Bunge, kwa kuwa hakuna kati yao aliyempigia simu au kumtumia ujumbe wa kumjulia hali kutokana na kipigo alichopata ambacho kimemsababishia maumivu makali.

Akizungumza jana akiwa kwenye chumba alicholazwa katika Taasisi ya Tiba ya Magonjwa ya Mifupa na Ufahamu Muhimbili (Moi), Nassari alidai Lowassa ambaye amewahi kuwa waziri mkuu kabla ya kujiuzulu, amemchukia tangu alipomshinda mkwewe Sioi Sumari, kwenye uchaguzi mdogo wa ubunge uliofanyika Aprili mwaka jana.


Nassari aliyekuwa amelazwa katika Hospitali ya Selian ya jijini Arusha kabla ya kuhamishiwa MOI, alidai kupigwa na kuchaniwa nguo na Green Guard wakati alipokuwa katika jitihada zake za kuhesabu kura kwenye uchaguzi wa udiwani wa Kata ya Makuyuni-Monduli.

“Kipigo nilichopata Lowassa anahusika ananichukia, anataka urais lakini hawezi kuupata kwa kuuumiza watu kama hivi, alifikiri kwamba nitakufa sitakufa hadi kwa mapenzi ya Mungu,” alisema.

Alisema kuna jambo ambalo wananchi wanapaswa kulifikiria ni jinsi ambavyo kumekuwa na matukio ya kutekwa na kuvamiwa, lakini hakuna yanayohusisha kiongozi wa CCM, badala yake ni raia wa kawaida na viongozi wa dini na siasa. Nassari alidai akiwa kama wakala mkuu wa Chadema katika kata hiyo, alikumbana na mambo kadhaa yaliyomshangaza, ikiwa ni pamoja na kufanyiwa jaribio la kutekwa mara mbili, kabla ya kushambuliwa kwa kipigo.

Alisema pia anashukuru kwamba askari wawili waliokuwepo katika eneo hilo walijitahidi kutaka kumnusuru, lakini walizidiwa nguvu na vijana hao, hasa kutokana na kutokuwa na bunduki, ambapo yeye alipofanikiwa kuchoropoka alikimbilia bastola yake na kuwanyoshea vijana hao bila kufyatua.

Akizungumzia kuhusu hali yake, Nassari alisema amepimwa kipimo cha X-ray ambapo imeonyesha kuwa pingili za mgongo wake zipo sawa, lakini daktari ameshauri afanyiwe kipimo kingine kiitwacho MRI ili kuangalia hali ya mishipa kutokana na maumivu makali anayoendelea kuyapata.

Aidha alitumia fursa hiyo kumshukuru Mbunge wa Kuteuliwa, Joseph Mbatia kuwa ndiye aliyemsaidia kufanya mipango kuwasiliana na uongozi wa Bunge na kumwezesha kuhamishiwa Moi, baada ya wabunge wote wa Chadema kwenda Arusha kushughulikia waliofariki kwa bomu.

Hata hivyo, Lowassa alipotafutwa kuhusiana na tuhuma hizo alikataa kuzungumzia suala hilo na kusema hilo aulizwe Msimamizi wa Uchaguzi, Paulo Kitaleki.

Mwananchi ilimtafuta Kitaleki ambaye pia ni katibu tarafa, alikanusha kuhusika kwa Lowassa akielezea kuwa siku ya tukio hilo alikuwa Geita.

“Huyu Nassari ni mwigizaji na anafaa kuwa msanii kwa kuwa anaigiza tu hata hakupigwa, bali yeye ndiyo aliyempiga Wakala wa CCM, Hussein Osama ambaye ni mlemavu, kisha akatimua mbio baada ya vijana kutaka kumkamata, nashangaa kumwona yupo hospitali akidai kupigwa, siyo kweli,” alisema Kitaleki.

Mwananchi

Wednesday, June 19

SABABU ZA JESHI LA POLISI KUTUMIA NGUVU YA MABOMU JIJINI ARUSHA MUDA HUU


Jeshi la polisi limekipiga marufuku chama cha demokrasia na maendelo(CHADEMA)kufanya shughuli zozote za kuaga miili ya marehemu kwenye viwanja vya Soweto kwani zoezi la uchunguzi bado linaendelea kwenye viwanja hivyo .

Akizungumza ofisini kwake kamanda wa polisi mkoani Arusha, Liberatus Sabas amesema kutokana na uchunguzi unaoendelea wa tukio la bomu kwenye viwanja hivyo imeonelea kuwa si busara kuweka mkusanyiko wa watu kwani kutaharibu upelelezi.


Kamanda Sabas amedai  kuwa  jeshi la polisi  liliwataka viongozi wa chama hicho kuwaeleza wafuasi wao mahali sahihi watakapoweza kufanyia shughuli hiyo lakini si kwenye viwanja hivyo.

Hali kwenye viwanja hivyo imekuwa ya pilika pilika tangu juzi kwa wafuasi wa chama hicho kujikusanya tokea asubuhi hadi jioni kwa madai ya kuomboleza ..

Hata hivyo viongozi wa chama cha demokrasia na maendeleo walikaidi agizo hilo na  kuanza  kujikusanya uwanjani hapo pamoja na wafuasi wa CHADEMA , hali iliyoleta  mvutano kati ya viongozi  wa jeshi la polisi na  wafuasi hao.

Wakati mabishano hayo yakiendelea, Askari Polisi mmoja  alijichanganya na kuingia katikati ya wafuasi wa Chadema pembeni mwa uwanja huo ambao walikua wanasubiri kujua utaratibu wa kuaga miili ya Marehemu waliolipuliwa na bomu June 15 2013.

Baada ya hapo,Wafuasi hao hawakupenda kitendo cha Polisi kujichanganya nao hivyo ikazuka ugomvi huku wakitaka atoke, baada ya dakika kadhaa  mabumu yalianza kusikika.

Baadhi ya viongozi wa juu wa chama hicho waliokuwepo uwanjani haponi mbunge wa jimbo la ubungo John Mnyika,Ezekia Wenje,Tundu lissu, Halima Mdee...

Wednesday, June 12

"NIKIFA ASHA BARAKA ASIJE KWENYE MSIBA WANGU, NA KAMA ATAKUFA YEYE BASI SITAENDA".....ALLY CHOKI

MKURUGENZI wa Extra Bongo Ally Chocky ametoa kauli nzito kuhusu waajiri wake wa zamani, Asha Baraka na Baraka Msilwa.

Katika maongezi yake Chocky alisema katika watu asiowapenda duniani ni Asha Baraka (Mkurugenzi wa ASET) na Baraka Msilwa (Mwenyekiti wa ASET). Asha Baraka na Baraka Msilwa ni mtu na kaka yake.

Kiongozi huyo wa Extra Bongo akaenda mbali zaidi kwa kusema: “Nikifa leo hii Asha Baraka na Baraka Msilwa wasije kwenye mazishi yangu, na kama watanitangulia wao na mimi sitakwenda kwenye mazishi yao.

“Nina uhakika leo hii nikipata matatizo au nikifa Asha na Msilwa watafurahi, sasa kuna haja gani ya watu kama hao kuja kwenye mazishi yangu.

“ASET ni kama simba wako tayari kukutafuna hadi macho, nimetafakari kwa muda mrefu sana nimevumilia mengi sana lakini nimeshindwa na sasa natamka rasmi, Nikifa wasinizike.”

Chocky ameorodhesha sababu nyingi sana za kufikia hatua hiyo lakini miongoni mwa sababu zake ni hizi tatu:

Kwanza kitendo cha Aset kumpeleka mahakamani kumdai gari, pili Aset kukataa kurudisha pesa za Miraji Shakashia na tatu ni ASET kutothamini michango ya wasanii walioizalishia pesa nyingi.

Chocky ansema kitendo cha Aset kumpeleka mahakamani kumdai gari ambalo walimpa mwenyewe kilimkera sana.

“Mtu anapokupeleka mahakamani maana yake ni kwamba yupo tayari hata ufungwe, ukifungwa maana yake ni kila kitu kwenye maisha yako kinaharibika.

“Gari walinipa wenyewe na maandishi yapo kwamba nikimaliza mkataba wangu gari litakuwa la kwangu.

Lakini badala yake wakanigeuzia kibao na kwenda kunidai mahakamani kwamba nimeiba gari.

Kuhusu Shakashia, Chocky amesema mwanamuziki huyo alichukua shilingi milioni tano za Extra Bongo ili ajiunge nayo na akasaini mkataba wake.

“Lakini badala yake Shakashia akaingia mitini na pesa zetu, Aset wakasema watazirudisha wao na sasa wanakuja na hadithi mpya.

“Wanasema hawawezi kurudisha hizo pesa eti kwa vile wananidai, wanasahau kuwa mkataba wa Shakashia ni kati yeke na Extra Bongo na sio Ally Chocky.

“Hata kama kipo wanachonidai hiyo ni kati ya Chocky na Aset na haiingii akilini kuliingiza suala la Shakashia ndani yake.

“Huu ni utapeli na inatoa picha kuwa Aset walimtumia Shakashia kufanya utapeli huu, lakini wajue kuwa mwisho wa siku atakayeathirika ni Shakashia mwenyewe,” alisema Chocky.

Kuhusu kutothamini wasanii waliozalishia pesa nyingi kampuni, Chocky anasema wasanii walipota ASET na kuizalishia pesa hawana chochote walichopewa kulingana na thamani ya kile walichokizalisha. “Sio pesa tu bali hata heshima pia hakuna,” alifafanua Chocky.

Chocky akazama zaidi na kuwataja wakongwe kama Shem Karenga na Kasongo Mpinda ambao waliwahi kufanya kazi katika familia ya kina Asha Baraka kupitia bendi za MK Group na MK Beats.

“Wako wapi Kasongo Mpinda na Shem Karenga, Kasongo aliwatengenezea pesa nyingi kupitia MK Group “Ngoma za Magorofani” huku Shem Karenga akiwatengenezea utajiri katika MK Beats “Tukunyema”.

“Lakini hebu tujiulize wako wapi hawa wazee na wana kipi cha kujivunia?” alihoji Chocky.

Haikuishia hapo, tuliamua kumpigia Asha Baraka ambaye naye alikuwa na yake ya kujibu kuhusu mapigo ya Chocky.

Asha Baraka amesema hayo ni mambo ya kike na kwamba kuzikana si tija.

Asha Baraka akasema: “Hata mimi sina mpango wa kwenda kwenye mazishi yake na yeye pia asije kwenye mazishi yangu.

“Hivi kuzikana ni nini? Wazazi wangu walifariki na Chocky hakuja kuzika, kilipungua nini? Halafu mi nikifa sitaona na yeye akifa sitaona kwahiyo hiyo siyo ishu, wamanyema wenzangu watatosha kunizika hata wasanii wote wasipokuja achilia mbali huyo Chocky.

“Nilimzikia wazazi wake na hakuliona hilo kwahiyo hata tusipozikana hakipungui kitu.

“Chokcy tunamdai gari na pesa shilingi milioni 13, kwenda mahakamani ni sehemu ya kudai haki na yeye kama anaona amedhulumiwa kuhusu pesa za Shakashia basi aende mahakamani.”

Asha Baraka alimtaka Chocky aelewe kuwa baadhi ya wasanii wa Twanga ni virusi na watammalizia pesa zake bure.

“Wako wasanii wamelelewa vizuri, wamefanyiwa mengi na Twanga na wanaelewa utu kwahiyo akijipendekeza kwao atapoteza pesa zake bure.

“Hao ni virusi wetu, wanatuletea taarifa zote za kila mtu anapotaka kuwachukua.
Asha Baraka amesema kama ni roho mbaya Chocky ndio anaoongoza kwa roho mbaya.

“Alikaa yeye na kamati yake yenye wakiwemo mpaka wafanyakazi wa umma na kuzoa wanamuziki wa Twanga”

Anawataja wasanii wa Twanga waliowahi kuchukuliwa na Extra Bongo ni pamoja na Ferguson, Rogart Hegga, Hosea, Otilya, Nyamwela, Danger Boy, Aisha Madinda, Maria Soloma, Subrina pamoja na Kanuti ambaye baadae alirudisha pesa zao na kubakia Twanga.

Asha Baraka anawataja wasanii wengine wenye damu ya Aset ambao wako Extra Bongo ni Ephraim Joshua, Martin Kibosho, Athanas, Banza Stone na yeye mwenyewe Chocky.

“Kwa mfumo huo utaona wazi kuwa Extra Bongo inapumua kwa nguvu ya Aset lakini sisi hatujasema kitu, kama ni kutoa kauli ya kutozikana basi sisi ndio tulipaswa kuwa wa kwanza,” alifafanua Asha.

“Tunajua pia kuwa Chocky alihusika kushawishi usajili wa Chaz Baba Mashujaa Band akiamini kuwa kwa kuondoka Chaz Twanga itakufa,” aliongeza

Asha Baraka amemtaka Chocky aonyeshe mfano wa namna ya kulea wasanii kwa kuwapa maisha mazuri wanamuziki waandamizi kama Banza na Rogart.

“Asiangalie mambo ya Aset, ajitazame yeye anaishi vipi na Banza anaishi vipi, badala ya kutoa milioni tano kumnunua Shakashia, angemnunulia japo Corola Banza au Rogart.

“Chocky aitishe mkutano wa waandishi wa habari halafu mimi na yeye twende na mikataba ya wasanii inayoonyesha mishahara na marupurupu tuone nani analea vizuri wasanii.

“Mimi nilifanya kazi Bima na sijajengewa nyumba wala kununuliwa gari, silalamiki kwa kuwa haikuwa sehemu ya makubaliano yetu.

“Kama Chocky anadhani muziki unalipa kiasi cha kumnunulia kila mtu gari na nyumba basi atuonyeshe mfano kupitia Extra Bongo.

“Kila baya linalomfika basi mchawi ni Aset, mbona mimi naumwa mguu na sijawahi kusema ni Chocky?

“Chocky akapime afya yake apate ukweli, tunajua rekodi ya sehemu alizopita, sasa asije akadondoka akasema ni Aset …akapime kwanza” alimaliza Asha Baraka.

ALIANZISHA JAYDEE SASA IMEKUWA FASION AMA? HEBU TUELEZANE.

CCM YAPINGA UWEPO WA SERIKALI TATU....

Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimepinga muundo wa Muungano wa Serikali tatu unaopendekezwa katika rasimu ya Katiba Mpya iliyotolewa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba mwanzoni mwa wiki iliyopita. Chama hicho tawala kimesema bado kinaamini katika muundo wa Serikali mbili.


Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye aliwaambia waandishi wa habari mjini Dodoma jana kwamba mapendekezo yaliyowasilishwa mbele ya Tume hiyo yanabaki kama yalivyo, hivyo msimamo wao ni kuwapo kwa muungano wenye muundo wa Serikali mbili.

“Mapendekezo ambayo ndiyo msimamo wa chama tulishayawasilisha kwenye Tume kuwa sisi tunapendekeza mfumo wa Serikali mbili na siyo tatu wala moja,” alisema Nape alipokuwa akitoa taarifa ya uamuzi wa Kamati Kuu (CC) ya CCM iliyokutana usiku wa kuamkia jana kujadili suala hilo.

Kauli ya Nape inafanana na matamshi ambayo yamewahi kutolewa na baadhi ya wanasiasa wakongwe ambao ni makada wa CCM wakiwamo, mawaziri wakuu wastaafu, Frederick Sumaye na John Malecela, Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta na baadhi ya wabunge ambao mara kadhaa wamekaririwa wakipinga pendekezo la Serikali tatu.


Hata hivyo, Nape alisema matamshi ya viongozi hao yalikuwa ni maoni yao binafsi na kauli yake ndiyo rasmi ya chama hicho... “Mimi ndiye msemaji wa chama hiki. Ndiye ninayeeleza msimamo wa chama chetu, yanayozungumzwa na watu wengine hata kama ni viongozi siyo msimamo wa chama ni maoni yao binafsi.”


Habari ambazo gazeti hili ilizipata zinasema katika kikao hicho cha CC kulijitokeza hofu ya suala la wananchi kuwa na mamlaka ya kuwang’oa wabunge ikiwa hawatatekeleza masilahi yao na kwamba pendekezo hilo lina upungufu kwani halitafsiri masilahi hayo ni yapi.

Waunda kamati
Nape alisema rasimu iliyotolewa na Tume siyo waraka wa mwisho kwani bado unatoa fursa kwa Watanzania kuijadili na kutoa maoni yao na kwamba CCM kitatumia nafasi hiyo kuwasilisha maoni yake kuhusu jambo hilo.


Alisema chama hicho kitawasiliana na wanachama wake zaidi ya 6,000 nchini ili waendelee kutoa maoni yao kuhusu suala hilo. “Wengi wanadhani rasimu hii ndiyo ya mwisho… hii ni ya mwanzo tu, itajadiliwa italetwa ya pili na ya tatu, kwa hiyo hatuwezi kusema kilichoelezwa kwenye tume ndiyo msimamo.


Ndiyo maana tumeamua kurejesha suala hili kwa wanachama wetu liendelee kujadiliwa,” alisema na kuongeza:
“Kama wanachama wetu wakiamua kuwepo kwa Serikali tatu, hatutachakachua, tutayachukua na kuyapeleka kama msimamo wetu, lakini tutakubaliana ikiwa uamuzi utakuwa umewahusisha wanachama wetu katika ngazi zote.

“Hatuangalii kipengele kimoja tu. Tutapitia vipengele vyote hadi kuzimaliza kurasa zote zaidi ya 70 zinazoainisha mapendekezo ya Tume ya Jaji (Joseph) Warioba.”

Alisema wanachama wake wanapaswa kuipitia na kuijadili rasimu hiyo kwa kuzingatia mapendekezo kilichoyatoa awali wakati wa mchakato wa kukusanya maoni ya Katiba Mpya. “Tulitoa maoni yetu na sasa tunaijadili Rasimu ya Katiba Mpya kwa kuzingatia maoni yetu yale, CCM tunakwenda kwa mujibu wa sheria,” alisema.


Habari kutoka ndani ya CC ya CCM zinasema chama hicho kimeipa kazi kamati ambayo ilitumika kuandaa mapendekezo yake awali, kupitia rasimu hiyo na kufanya ulinganisho wa yale ambayo chama hicho kilipendekeza dhidi ya yale yaliyozingatiwa katika Rasimu ya Katiba hiyo.


“Kamati itafanya ulinganisho na baada ya hapo tutakwenda kwa wanachama kuwaeleza ni yapi tulipendekeza kama chama na ni yapi ambayo Tume imeyazingatia na hapo tutapata mawazo yao ambayo tutayatumia katika ngazi ya mabaraza ya Katiba,” kilisema chanzo chetu

PICHA ZA WAKENYA WALIVYOANDAMANA JUNE 11 NA KINYAGO CHA NGURUWE NA DAMU WAKIPINGA MISHAHARA YA WABUNGE

Miungano ya kijamii ikiongozwa na Bunge la mwananchi,Muhuri na pawa 254 miongoni mwa mengine yameandaa maandamano ya pili kupinga juhudi za wabunge kuhujumu tume ya kuratibu mishahara nchini kenya SRC ili kujiongezea mishahara ya hadi laki nane kinyume na ilivyopendekezwa na SRC.


Tofauti na wiki kadhaa zilizo pita ambapo waandamanaji waliwaelekeza nguruwe walioandikwa majina ya wabunge walio unga mkono mswada huo, hii leo waandamanaji walibeba kinyago wa nguruwe na damu walio ashiria mwisho wawabunge kukandamiza wakenya. huku wakijimwagilia damu kama ishara ya kuumizwa na kodi ya kuwalipa wabunge.
Waandamanaji pia walibeba mfano wa noti za shillingi alfu moja pesa za kenya zilizo chorwa Nguruwe mkubwa kwa upande mmoja na wanawe kwa upande wa pili, huku wakiwarushia wabunge noti hizo kuashiria kujitakia makuu kwa wabunge hao.


Viongozi wa waandamanaji wameahidi kuendeleza maandamano hadi pale wabunge watakapo sitisha hujuma dhidi ya tume ya bi sara serem ama SRC.
Tume ya SRC imependekeza wabunge kulipwa mshahara wa kati ya shillingi laki Nne hadi laki saba.Ilihali wabunge walipendekeza mshahara wa hadi shillingi millioni moja.

kwamujibu wa freebongo.blogspot.com

Tuesday, May 28

Waunda timu ya urais Uchaguzi Mkuu wa 2015


Mwanza. Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta amesema wakati ukifika, yeye na rafiki zake Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli na Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe, watachagua mmoja wao watakayeona anafaa kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu wa 2015.

Waziri Sitta aliyasema hayo jana katika Kongamamo la Mawasiliano katika Nyanja za Digitali la wanafunzi wa Idara ya Uhusiano na Masoko, Chuo Kikuu cha St. Augustine (SAUT), Mwanza.

Mara ya kwanza, Sitta aliwataja rafiki zake hao juzi wakati wa harambee ya kuchangia Kanisa Katoliki, Josephine Bakita, Parokia ya Igoma, Mwanza.

Pia alisema hatagombea tena Ubunge Urambo ya Mashariki baada ya kuwa katika ulingo wa siasa kwa miaka 35 na badala yake ataangalia namna nyingine ya kuwatumikia wananchi huku akigusia mchakato wa kuwania urais ambao, alisema anamwachia Mungu.

“Kwa ubunge nimekwisha waeleza inatosha sitagombea tena kwani miaka 35 inatosha, … lakini hatima yangu ni nini siwezi kujua lakini nina afya nzuri na mmoja wa wanasiasa wakongwe, wenye afya nzuri, mnaona ninavyopendeza... kwa urais namwachia Mungu tutaona,” alisema Sitta.

Alisema yeye rafiki zake hao wana mawazo yanayolingana katika mustakabali wa nchi hii na kwamba wataendelea kutembea sehemu mbalimbali za nchi kuwajengea wananchi uelewa ili wajue kuwa uongozi ni lazima ukae katika mikono salama.

“Tutaendelea kupita katika nchi hii kuwaeleza wananchi kujua uongozi wa nchi hii lazima ukae katika mikono safi na ikitokea mmoja wetu akatamani urais, basi tutaona inavyofaa, lakini tutasubiri watu wanavyosema pia kuhusiana na nasi,” alisema.

Akijibu swali la mwanafunzi wa SAUT kuhusiana na kumuunga mkono Rais Jakaya Kikwete wakati wa Uchaguzi Mkuu uliopita ilhali akijua kwamba hawezi kuwaletea maisha bora wananchi, alisema kwake ilikuwa ni sawa na kuchumbia na kwamba wakati wa uchumba, mchumba huonekana kuwa bora lakini anaweza kubadilika wakati wa ndoa.

“Sikufanya kosa kuwa katika mtandao wa Rais Kikwete, hii ni sawa na kuoa. Unachumbia. Mchumba hawezi kuwa sawa wakati wa ndoa au wa kuwa mke, inawezekana katika kugombea mtu akawa sawa lakini baadaye akajifunua zaidi mambo yake, huwezi kumjua zaidi mtu labda uwe na Umungu,” alisema Sitta na kusema: “Hata wapiga kura huwakuta hilo kwa kuchagua mtu ambaye huenda kinyume na matarajio yao.”

Hata hivyo, alisema kauli hiyo haina maana kwamba Rais Kikwete hakufanya kitu, bali amefanya mambo mengi na kusema uzuri wa uongozi unapimika wakati anapotoka madarakani hasa pale historia inapoandikwa na kulinganishwa na marais wengine wajao na waliopita.

Katika kongamano hilo la SAUT, Waziri Sitta alifuatana na kada wa CCM, Paul Makonda.

Sunday, May 26

Jeshi lafanikiwa kudhibiti vurugu Mtwara

Shughuli za mauzo na manunuzi zilirejea rasmi jana mjini Mtwara,
baada ya huduma hizo kusimama kwa siku tatu kutokana na
vurugu zilizotokea kuanzia Alhamisi baada ya kusomwa
hotuba ya Wizara ya Nishati na Madini na wana-
Mtwara kubaini kuwa suala lao la gesi halijapewa umuhimu unaostahili.
Picha na Abdallah Bakari  

Mtwara. Mkuu wa vikosi vya aridhini wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Meja Jenerali SM Kijuu amewahakikishia ulinzi wafanyabiashara hao, baada ya kukutana na uongozi wa Chama cha Wafanyabiashara Sokoni (Wabisoco) jana asubuhi, kufuatia wafanyabishara hao kudai kuendelea kusitisha biashara zao kwa kuhofia usalama.

Katibu wa Wabisoco, Saidi Namata ameliambia Mwananchi Jumapili kuwa wafanyabiashara hao wamekubaliana kufungua biashara zao, baada ya makubaliano ya kulinda eneo hilo na askari wa JWTZ.

“Sisi wafanyabiashara tulikuwa tayari kuendelea kusitisha huduma kutokana na hali ya usalama kuwa mbaya, alipokuja kiongozi wa jeshi na kutuhakikishia kuwa dhamana ya ulinzi itakuwa chini yao tulikubaliana,” alisema Namata

Alisisitiza: “Kama ulinzi ungekuwa mikononi mwa polisi, katu tusingefungua. Polisi wenyewe ndiyo hawa wanaovunja maduka na kuiba, kwa kuwa dhamana hii imebebwa na wanajeshi hatuna shaka, tunaomba wafanyabiashara wengine wafungue biashara zao.”

Tangu juzi magari ya matangazo yamekuwa yakipita mjini Mtwara na kuwatangazia wananchi kuendelea na kazi zao kama kawaida kwa kuwa ulinzi umeimarika, huku askari wa JKT na JWTZ waliosheheni silaha wakizunguka mitaani.

Pinda awasili Mtwara

Wakati tukiewnda mitamboni Waziri Mkuu Mizengo Pinda amewasili Mtwara jana jioni na kukutana na viongozi wa mkoa.

Bungeni Dodoma

Suala la mgawanyo wa rasilimali za taifa jana liliendelea kutikisa Bunge, baada ya baadhi yao kueleza kuwa ni haki kwa maeneo yanakotoka rasilimali hizo kunufaika kwanza kabla ya maeneo mengine.

Wakati wabunge hao wakieleza hayo, wengine wamesisitiza kuwa kwa kuwa nchi ni moja Tanzania, rasilimali zote ni mali ya Watanzania wote.

Wabunge wanaotaka rasilimali zinufaishe kwanza maeneo zinakotoka. Wanasema pamoja na ukweli kwamba Tanzania ni moja, watu hao wana haki ya msingi kupata huduma hizo kwanza kuliko wengine.

Mbunge wa Msalala (CCM), Ezekiel Maige alisema anashangaa kwa nini fomula ya rasilimali kuyaendeleza maeneo iliyopatikana, inatumika kwenye Idara ya Wanyamapori na haitumiki katika sekta ya nishati na madini.

“Wananchi walichosema rasilimali tugawane mrabaha. Zinufaishe wao kwanza. Kwenye wanyamapori, tunafanya hivyo kwa nini kwenye madini tunasema taifa litagawanyika? Alihoji.

Maige alisema Tume ya Bomani ilishauri kuwa asilimia 40 ya mapato itumike kuendeleza maeneo ilikopatikana rasilimali hizo na asilimia 60 zikaendeleze maeneo mengine, lakini ushauri huo haufanyiwi kazi.

Mbunge wa Mpanda (Chadema) Said Arfi alitaka hekima kutamalaki katika suala la mgororo wa gesi Mtwara ili taifa iendelee kuwa na hali ya amani na utulivu

“Naishauri Serikali wawashirikishe wananchi katika mambo yanayohusu mustakabali wa maendeleo yao. Elimu ya kutosha ingalikuwapo na ushirikishwa ulio mpana, tusingalifika hapa. Kadiri tunavyochelewa kulitatua tatizo hili, ndivyo tunavyorudi nyuma katika maendeleo,” alisema.

Kwa upande wake Mbunge Mlalo (CCM), Hassan Ngwilizi, alisema anaunga mkono msimamo wa Rais Jakaya Kikwete kuwa rasilimali za taifa ni mali ya Watanzania wote, hivyo ni mwafaka kwa watu kudhani kuwa wanastahili kunufaika na rasimali kwa sababu zimetoka kwao.

“Wale wote wanaofikiri kuleta chokochoko, wajue nchi hii inavyo vyombo vya dola. Kinachowatokea au kuweza kuwatokea, wajilaumu wenyewe,” alisema Ngwilizi na kusisitiza;

Hamad Ali Hamad (CUF) alisema gesi iliyopatikana Mtwara isiwe laana bali ionekane kama baraka. “Serikali ikazungumze na watu wa Mtwara na hili naomba serikali msione tunafanya jambo baya. hakuna lisilozungumzika,” alisema.

Christopher Ole Sendeka wa Simanjiro (CCM) alisema: “Amani ya Tanzania ni tunu isiyoweza kuchezewa na mtu yeyote yule na kwa sababu yeyote ile .

“Natambua kuna haja ya baadhi ya mambo wanayodai kuangaliwa kwa makini, lakini nawashauri Wanamtwara waendelee kuleta madai yao na Serikali iwasikilize kwa sababu wao ni watu wazima, hawawezi kupiga kelele hivi hivi tu,” alisema.

Ole Sendeka alitaka Waziri asikubali kuendelea kudanganywa na watalaamu wake kwa kuwa watamharibia.

“Usikubali kuuziwa mbuzi kwenye gunia,” alisema Sendeka na kuendelea, “ mwaka jana ulidanganywa na watalaamu wako ukalidanganya Bunge kuhusu nguzo za Tanesco na misumari.”

“Mwaka 2010 Rais Kikwete aliahidi kuwapa mgodi wa Tanzanite One wachimbaji wadogo lakini leo tunaambiwa wakifunga, mgodi huo utakabidhiwa kwa Stamico. Sasa Rais Ni Muhongo au Dk Jakaya Kikwete?”

Kamati yaundwa

Bunge limeunda kamati maalumu kwa ajili ya kuchunguza vurugu zilizotokana na mradi wa kusafirisha gesi, kutoka mkoani Mtwara kwenda jijini Dar es Salaam.

Spika wa Bunge Anne Makinda, alisema kamati hiyo itakayoongozwa na Mbunge wa Muleba Kaskazini, Charles Mwijage, itakuwa na hadidu nne za rejea.

Wajumbe wake ni Mbunge wa Mpanda Mjini, (Chadema) Said Arfi , Mbunge wa Sikonge (CCM), Said Nkumba, Mbunge wa Wawi (CUF) Hamad Rashid Mohamed na Mbunge wa Tunduru Kaskazini (CCM) Ramo Makani na Rukia Kassim Ahmed (CCM).

Pia wamo Dk Dalaly Kafumu (CCM-Igunga), Cynthia Hilda Ngoye (Viti Maalumu-CCM), Muhamed Chombo (CCM), Agripina Buyogera NCCR- Mageuzi, Cecilia Paresso (Viti Maalumu-Chadema), Mariam Kisangi (Viti Maalumu- CCM), Seleman Jafo (Kisarawe CCM),

Hadidu za Rejea

Spika Makinda alisema kamati hiyo ambayo hata hivyo hakuipa muda maalumu, itakuwa na jukumu la kufuatilia mambo manne muhimu yanayochangia vurugu hizo.

“Kamati itakuwa na jukumu la kujua nini chanzo cha vurugu, kujua hatua zilizochukuliwa na Serikali, kukutana na wadau mbalimbali ili kupata maoni yao na kuangalia mambo yote yenye uhusiano na vurugu hizo,” alisema.

Imeandikwa na Abdallah Bakari, Elias Msuya , Mtwara na Kizitto Noya, Dodoma. - gazeti la mwananchi

Saturday, May 25

Uhasama kati ya polisi, raia Mtwara


Hali ya uhasama imeibuka kati ya polisi na raia mkoani Mtwara, kila upande ukilalamika kuhujumiwa huku hali ikiendelea kuwa tete, ambapo Jeshi la Polisi nchini limetangaza kukamatwa kwa mtu anayetuhumiwa kueneza ujumbe wa uchochezi kwa kutumia simu ya mkononi.

Barabara nyingi za mjini Mtwara ziko tupu, huku magari ya Jeshi la Wananchi na polisi yakiranda randa kuhakikisha usalama, huku maduka na biashara nyingine zikiendelea kufungwa.

Wakati uhasama huo ukiendendelea, taarifa zinaeleza kuwa vifo vimeongezeka na kufikia watu watatu, huku Mkuu wa Mkoa Kanali Mstaafu Joseph Simbakalia, akisisitiza kuwa na taarifa rasmi ya kifo kimoja tu.

“Mpaka sasa tuna taarifa ya kifo kimoja tu kupitia utaratibu rasmi, kama kuna wengine wamekufa basi mtuletee taarifa kwa kufuata utaratibu,” alisema Simbakalia.

Hata hivyo, taarifa za wananchi zilisema kuwa watu wengine watatu walikufa kwa kupigwa risasi katika maeneo ya Mikindani, huku baadhi ya wanawake wakidai kubakwa na polisi.

Wakati hayo yakiendelea, Jeshi la Polisi nchini limetangaza kumshikilia mtu mmoja (jina limehifadhiwa) kwa tuhuma za kueneza ujumbe wa uchochezi na chuki kwa wananchi na viongozi wa Serikali kwa kutumia simu ya mkononi.

Taarifa ya jeshi hilo iliyotolewa jana kwa vyombo vya habari imeeleza kuwa meseji hizo zinaenezwa kwa lengo la kuchochea fujo, vurugu na kutoa matusi kwa wananchi na viongozi wa Serikali.

Msemaji wa jeshi hilo, Advera Senso alisema jana kuwa mtu huyo amekuwa akifanikisha kazi hiyo kwa kutumia kadi 13 tofauti za simu za mkononi.

“Alikamatwa akiwa na kadi 13 tofauti za simu za mkononi, polisi bado inaendelea kumhoji mtu huyo na ushahidi utakapokamilika atafikishwa mahakamani,” alisema Senso na kuongeza:

“Kwa muda mrefu sasa watu wa kada mbalimbali nchini wamekuwa wakitumiwa ujumbe mfupi wa maneno katika simu zao, unaohamasisha vurugu na uchochezi wa kidini, huku baadhi ya wananchi wakizitupia lawama mamlaka husika kwa kushindwa kudhibiti hali hiyo.”

Jeshi hilo limewataka wananchi wenye taarifa mbalimbali za wahalifu kama hao kujitokeza na kutoa taarifa hizo, ili wanaotuhumiwa wasakwe na kukamatwa ikiwa ni pamoja na kuchukuliwa hatua stahiki.

Wakizungumza wakati wa ziara ya Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk Emmanuel Nchimbi, wananchi wengi wamelilalamikia Jeshi la Polisi kwa kutumia nguvu kubwa katika utulizaji wa ghasia na kusababisha vifo, majeruhi na uharibifu wa mali.

Wakati Waziri Nchimbi akifanya ziara hiyo Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Shamsi Vuai Nahodha naye alitua mkoani humo na kusisitiza ulinzi wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Akizungumza mbele ya Waziri Nchimbi, Diwani wa Kata ya Magengeni Tarafa ya Mikindani, Omar Nawatuwangu alisema, licha ya wananchi kufanya vurugu, Jeshi la Polisi lilijibu kwa kujeruhi watu na kuchoma nyumba.

“Hali hapa siyo shwari, ni kweli wananchi wamefanya vurugu lakini askari hawa tunaotegemea watatulinda, ndiyo wamechoma nyumba za watu na kujeruhi watu kwa risasi,” alidai Nawatuwangu.

Naye Issa Nambanga wa Mikindani alidai kuwa aliwaona askari waliokuwa na bunduki wakichoma nyumba ya jirani yake. “Mimi niliwaona askari wakichukua mali za jirani yangu na baadaye kuichoma moto nyumba yake. Nilishindwa la kusema kwa kuwa niliwaogopa askari hao,” alisema Nambanga.

Kwa upande wake Mariam Abdallah ambaye ni mjane mwenye watoto watatu, alilalamika kuchomewa nyumba na vyombo vyote alivyokuwa navyo.

“Juzi usiku (Mei 22), polisi walikuja na gari lao na kulisimamisha mbele ya nyumba yangu. Nilimwona polisi wa kike akinitaka nitoke nje na watoto wangu, kisha akawasha kiberiti na kuichoma nyumba yangu. Sina chochote nilichookoa na hapa sijui nitaanzia wapi, sina kazi, hata jembe ninalolimia wamelichoma,” alisema.

Waziri Nchimbi alitembelea pia askari waliochomewa nyumba zao huku akimtaka Kamanda wa Polisi mkoani humo, Linus Sinzumwa awasake wote waliohusika na uhalifu huo. Wakizungumzia tukio hilo, baadhi ya askari waliochomewa nyumba, walisema kuwa hali hiyo inaonyesha uhasama uliopo kati yao na raia.

“Siku zote nimeishi hapa na wananchi hata wengine nilikuwa nikiwapa kazi ya ujenzi, lakini katika vurugu za juzi, nilishangaa tu watu wanavamia nyumba yangu na kuichoma moto. Mke na watoto wangu walikimbia kujificha kwa jirani,” alisema Sajini Fakih Sajih anayeishi Kata ya Chikongola.

Wengine waliokumbwa na zahama ya kuchomewa nyumba ni pamoja na mtangazaji wa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC), Kassim Likongolo na mkewe Koplo Fatuma na Koplo Philemon Yatitu.

Mbali na askari hao, waandamanaji pia walichoma ofisi ya CCM, Kata ya Chikongola na ofisi ndogo ya Mbunge iliyopo Mikindani.

Kauli ya Mkuu wa Mkoa

Akizungumzia malalamiko ya wananchi Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali mstaafu Joseph Simbakalia, alikiri kupokea malalamiko ya wananchi na kusema kuwa askari waliohusika na vitendo hivyo wakibainika watawajibishwa kijeshi.

“Malalamiko ya wananchi tumeanza kuyapokea, yatachunguzwa na kama yatabainika kuwa ya kweli askari watachukuliwa hatua za kijeshi,” alisema Simbakalia.

Akizungumzia mfululizo wa vurugu hizo tangu zilipoanza Desemba mwaka 2012, Simbakalia alisema hazina uhusiano na suala la gesi bali ni hujuma dhidi ya maendeleo.

“Ni kweli tulianza kuona viashiria mapema kwa kuwepo vipeperushi na ujumbe wa simu, ndiyo maana tuliweka ulinzi mkali wa polisi. Hali ilipozidi kuwa mbaya, kwa kutumia utaratibu wa kisheria, kama mkuu wa mkoa nikaomba kuongezewa nguvu za kijeshi,” alisema Simbakalia.

Hata hivyo, Simbakalia alishindwa kueleza hatua zilizochukuliwa kwa watu hao tangu vurugu hizo zilipoanza mwishoni mwa mwaka jana, licha ya kukamata zaidi ya watu 90 katika vurugu za sasa.

Vurugu Msimbati

Ghasia zimezuka katika Kijiji cha Msimbati inapochimbwa gesi asilia, ambapo watu wasiojulikana wamechoma moto Ofisi ya Hifadhi ya Bahari jana usiku.

Habari zinasema tukio hilo limetokea kati ya saa 4 na 5 usiku na kwamba polisi waliingia kijijini hapo usiku huo kutuliza ghasia. Mkuu wa Mkoa, Simbakalia amethibitisha kutokea kwa vurugu hizo.

Kauli ya Waziri Nahodha

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Mtwara, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Shamsi Vuai Nahodha alitetea uamuzi wa kuleta Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) Mtwara kwa lengo la kulinda amani.

“Kwa mujibu wa Katiba, tumepewa dhamana ya kulinda wananchi dhidi ya maadui wa ndani na nje hivyo ni wajibu wetu wa msingi inapotokea haja ya kufanya hivyo,” alisema Nahodha.

Alizungumzia pia ajali ya gari la jeshi wilayani Nachingwea mkoani Lindi na kusababisha vifo vya wanajeshi wanne, alisema kuwa vimewasikitisha na majeruhi watapelekwa Dar es Salaam kutibiwa.

“Kwa hiyo wale wenzetu waliopoteza maisha damu yao haikumwagika bure, walikuwa katika kutimiza wajibu wao kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Wamepotea wakiwa katika harakati za kuleta amani.”

Kiama hiki cha gesi Mtwara kisiigawe Tanzania - GAZETI MWANANCHI



Licha ya utajiri huo mkubwa unaweza kujiuliza, je, ni kwanini bara hili limeendelea kuwa maskini kwa miaka mingi huku likikabiliwa na mizozo mingi na migogoro kuhusu mgawanyiko wa rasilimali hizi.

Jiulize, leo ikiwa ni miaka 50 tangu kuanzishwa kwa Umoja wa Nchi Huru za Afrika (OAU), sasa Umoja wa Afrika (AU), kwanini bara hili tajiri kiasi hiki bado linatajwa kuwa maskini pengine kuliko mabara mengine duniani?

Tunaambiwa, Afrika ina asilimia kubwa ya madini, lakini, jiulize, kwa nini asilimia kubwa ya madini hayo haitumiwi vizuri au kikamilifu katika kuliinua bara hili. Kwanini hayalisaidii bara hili?

Kwa kutaja machache, Afrika ni tajiri kwa madini kama vile, almasi, dhahabu, shaba urani na mengine mengi.

Bara hilo linajivunia asilimia 40 ya umeme wa nguvu za maji unaopatikana duniani, linazalisha madini mengine kama chromium, asilimia 30 ya uranium na asilimia 50 ya dhahabu inayopatikana kote duniani.

Pia, asilimia 90 ya cobalt, asilimia 50 ya phosphates, asilimia 40 platinum, asilimia 7.5 au zaidi ya makaa ya mawe, asilimia 8 ya petroli na bidhaa zake, asilimia 12 ya gesi asilia, asilimia 3 ya madini ya chuma na mamilioni ya ekari za ardhi nzuri na inayofaa kwa kilimo cha mazao mbalimbali yakiwamo ya chakula, biashara ambayo ni mengi mno kuyataja.

Pia, bara hili linayo mito, maziwa, bahari ambako kwa kiasi kikubwa wanapatikana samaki wengi na wa aina mbalimbali wakiwamo hata wale wenye bei kubwa katika soko la dunia.

Pia, Afrika inavyo vitu vingine vingi kama mbuga za wanyama ambazo zimejaa tele, zinavutia watalii wengi, ambao huongeza fedha za kigeni, lakini mbona havijaweza kulisaidia bara hili kuondokana na lindi hili la umaskini?

Huenda ni bahati mbaya kwamba mgawanyo usiyo sahihi au sawa kwa rasilimali hizi, ulafi wa baadhi ya viongozi, hasa wale waliokabidhiwa jukumu la kusimamia idara au taasisi zinazoshughulikia uchimbaji, usambazaji wake na usiri mkubwa katika mikataba.

Kutokana na usimamizi duni wa rasilimali hizi zinaweza kuwa baadhi ya sababu za kuzuka kwa mizozo hii mikubwa ambayo inalikumba bara hili, kama ambavyo inaanza kuzuka Tanzania.

Rais Yoweri Museveni wa Uganda katika moja ya hotuba zake mwaka jana wakati akizindua mradi wa kuchimba mafuta katika Ziwa Natron nchini mwake alieleza mengi kuhusu rasilimali hizi na jinsi zinavyoweza kuigawa nchi na Afrika kwa jumla.
Dar es Salaam. Bara la Afrika kwa hakika limebarikiwa kuwa na rasilimali lukuki ambazo ni lulu katika kukuza uchumi.

“Tunafurahi kuwa tunayo mafuta hapa, hii ni rasilimali ambayo haina budi kutuunganisha zaidi sisi (Waganda) badala ya kutugawa,” alieleza Museveni mbele ya wageni, wenyeji na wawekezaji kutoka China ambao wanashiriki katika mradi huo.

Rasilimali hizi nyingi zinapatikana katika Afrika ikiwamo Tanzania ambako imegunduliwa gesi asilia kiasi cha trilioni 41 futi za ujazo kule Mtwara na Lindi.

Kwa bahati mbaya, rasilimali hii imeanza kuimega tunu ya amani, utulivu ambayo nchi yetu ilijaliwa kuwa nayo kwa muda mrefu na sasa ni dhahiri inaweza kuigawa nchi.

Upo ushahidi wa jinsi ambavyo Muungano wa Tanzania, uliotokana na kuungana kwa Tanganyika na Zanzibar kwa siku za karibuni umekuwa ukitiwa majaribuni, kisa ni hisia za kugundulika au kupatikana kwa mafuta kule Pemba au kwingineko katika bahari kuu.

Huu ni mtihani mkubwa ambao matukio haya ya Mtwara yanasababisha wananchi kuamini kuwa gesi inaweza kuwakomboa kutoka katika lindi la umaskini tena kwa haraka bila kuwashirikisha wenzao wa maeneo mengine ya nchi. Huu ni mtihani ambao nchi inatakiwa kuushinda, lakini kwanza inatakiwa kuwa makini.

Kauli za ubabe au vitisho dhidi ya wananchi hao, ziwe kutoka kwa viongozi wetu kama wa Wizara ya Nishati na Madini, chini ya Profesa Sospeter Muhongo na wasaidizi wake, George Simbachawene na Stephen Masele, hazifai.

Pia, kwa kuwa Rais Jakaya Kikwete ndiye amepewa mamlaka na katiba yetu kusimamia mgawanyo huu wa rasilimali, hana budi naye kuchukua hatua sasa, wala si kusubiri wananchi waanze kukumbatia kile kinachozalishwa kwao, kwa maslahi yao.

Ni wazi kwamba kama kuna wanasiasa, kundi la wanaharakati wanaodhani kuwa watafanikiwa kuwatumia wananchi wa Mtwara kudai gesi ibaki ili wapate maendeleo, wanapaswa kujitazama upya.

Ni wazi kwamba gesi inataka uwekezaji mkubwa, inataka masoko ya uhakika, ambayo yanaweza kuwa mbali ya eneo lao, ilimradi wao wahakikishiwe huduma zote muhimu za jamii kama shule, zahanati, barabara nzuri na kadhalika.

Hakuna shaka kwamba huu ni mradi mkubwa ambao Tanzania kama nchi haikuwahi kuwekeza, lakini pia ni mtihani ambao Serikali ya awamu ya nne, chini ya uongozi wa Rais Kikwete na wenzake wote hawana budi kujifunza kutoka yaliyotokea kwingineko.

Afrika, imeshuhudia nchi iliyokuwa kubwa kieneo, Sudan imegawanyika na mojawapo ya sababu ni mgawanyo wa rasilimali, mafuta na sasa imeparaganyika na kubakia mataifa mawili, Sudan na Sudan Kusini, ambazo zote hazijiwezi kiuchumi.

Kumbukumbu za Nigeria na mizozo kule Niger Delta ni ushahidi mwingine wa jinsi ambavyo bila umakini, nchi inaweza kuingia katika vita.

Miundombinu iliyogharimu kiasi kikubwa cha fedha imekuwa ikichezewa, kuharibiwa karibu kila mwaka kule Nigeria ambako nchi imepata hasara, wananchi wamepoteza maisha, jambo ambalo linapaswa kuepukwa kwa gharama zozote zile, kwani nafasi bado ipo ya kuweza kufanya hivyo.

Kwa mfano, mzozo baina ya Nigeria na Cameroon ambazo awali ziliingia kwenye mzozo mkubwa zikigombea rasi ya Bakassi yenye mafuta, hadi jumuiya ya kimaifa imelazimika kuingilia kati, sote tumeona. Je, tumepata fundisho gani kuhusu rasilimali na jinsi zinavyoweza kuwa sababu na chanzo cha mizozo na migogoro?

Kumbukumbu zetu kule Bungeni mjini Dodoma zinatuonyesha kuwa hivi karibuni kuwa wabunge walijadili rasimu ya sera ya gesi na wengi walionekana kuwa na wasiwasi kuhusu ugawaji wa rasilimali hiyo ndani na kwa wageni.

Wabunge wengi walitaka mikataba iwekwe wazi kwa viongozi na wananchi wote ambao kimantiki gesi hiyo ni mali yao.

Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe(Chadema ) alitaka vitalu vya gesi visiuzwe mapema kwa wawekezaji hadi pale sheria rasmi ya gesi itakapokamilika.

Hata hivyo, Profesa Muhongo alisema serikali iliamua kuanza uuzaji wa vitalu hivyo ili isiwe nyuma katika soko la dunia la nishati.

“Hatuna haja ya kubaki nyuma, tukichelewa katika hili tunaweza kukosa fursa kwani nchi nyingine zinazonunua gesi zipo katika mchakato wa kutafuta mbinu mbadala za nishati hiyo” alisema Profesa Muhongo.

Ni dhahiri kwamba hili la Mtwara linaweza kuichelewesha Tanzania, hasa wakati huu ambao jirani zetu, Msumbiji wamewekeza katika gesi kwa kiasi kikubwa.

Ushauri hapa ni kuwa busara zaidi itumike, pande zote ili zichume na kuvuna kutoka kwenye gesi asilia ya Mtwara hadi bomba litakapojengwa, viwanda kama kile cha saruji, wananchi wanufaike, serikali ikusanye kodi, ambazo hatimaye zitasaidia kukuza uchumi.

Inawezekana kuwa hiki kinachotokea kule Mtwara, bila umakini kinaweza pia kuibuka Ruvuma au hata Manyoni (Singida) ambako pia imegundulika urani, madini mengine ambayo pia yameanza kuzua mijadala na mizozo mingi ikiwamo ile ya kimazingira.

Kuna madini aina ya nickel kule Kabanga, Ngara Mkoani Kagera, ambayo pia yana thamani kubwa na ambayo pia yanaweza kuzua mzozo mwingine. Kama nchi, tujihadhari, tujaribu kuwa makini!

Sakata la gesi Mtwara: Wabunge CCM wacharuka


Dodoma. Wabunge wa CCM wamekuja juu na kumtaka Rais Jakaya Kikwete kuwafukuza kazi vigogo wa Serikali mkoani Mtwara, wakiwamo Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Wilaya kutokana na kile walichoeleza ni uzembe uliochangia vurugu zinazoendelea za wananchi kugomea gesi kutoka nje ya mkoa huo.

Wengine waliopendekezwa kuchukuliwa hatua ni kamati nzima ya ulinzi na usalama ya ngazi ya mkoa na wilaya ya Mtwara mjini, wakiwamo makamanda wa polisi.

Kutokana na hali hiyo, vigogo kadhaa mkoani humo wako hatarini kukumbwa na ghadhabu hiyo akiwamo Mkuu wa vikosi vya Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Mkuu wa mgambo na Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).

Wabunge hao walikuwa wakitoa mapendekezo hayo kwenye kikao cha Kamati ya Wabunge wa CCM iliyofanya kikao cha dharura juzi usiku, mjini hapa.

Kikao hicho kiliongozwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, huku Spika wa Bunge, Anne Makinda ambaye wakati huo alikuwa kwenye kikao cha Kamati ya Uongozi wa Bunge, aliwakilishwa na Mwenyekiti wa Bunge, Jenista Mhagama.

Katika kikao hicho maalumu kilichokusudia kutoa ushauri kwa Rais Kikwete juu ya njia mwafaka ya kutatua hali ya machafuko, wabunge wengi wali kukasirishwa na jinsi hali ilivyo mkoani Mtwara. Chanzo chetu kwenye kikao hicho kilieleza kuwa wabunge hao walichukizwa na jinsi Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Wilaya walivyokuwa wakipingana kimsimamo. Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Kanali Joseph Simbakalila, Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mjini, Wilman Ndile na Kamanda wa Polisi Mkoa Linus Sinzumwa wamehusishwa.

Licha ya baadaye kuonekana kuwa kitu kimoja, wabunge hao walidai kuwa walishindwa kutumia nafasi zao katika kutatua tatizo hilo, ambalo hadi juzi Serikali ilisema walikuwa wamekufa watu watano, wakiwamo wanajeshi wa JWTZ waliofariki katika ajali wakati wakienda kutuliza machafuko.

Chanzo hicho kilieleza kuwa iwapo mapendekezo ya wabunge hao yatapelekwa kwa Rais Kikwete kama michango ya wabunge hao ilivyokuwa, huenda rungu likawaangukia pia viongozi wa kisiasa wa CCM mkoani humo. Miongoni mwa wanasiasa hao, chanzo hicho kimesema ni wale waliotoa kauli za waziwazi kuunga mkono msimamo wa kutoruhusu gesi kusafirishwa nje ya mkoa huo.

“Hapa wapo wabunge, madiwani na viongozi wa ngazi mbalimbali wa CCM,” kilieleza chanzo hicho.

Hata hivyo, baadhi ya wabunge walipendekeza mkakati wa kutatua uzembe uliofanyika Mtwara, unapaswa kuchukuliwa kwa uangalifu usije ukasababisha madhara mengine kwa Chama na Serikali.

Walisema suala hilo halina budi kuchukuliwa kwa uangalifu hasa ikizingatiwa kuwa Chama cha CUF ndicho chenye nguvu mkoani humo ukilinganisha na vyama vingine vya upinzani.

Wabunge hao walikituhumu chama hicho kuwa kimekuwa kikijaribu kutumia vurugu hizo kama kigezo cha ushawishi wa kukubalika mkoani humo.

Taarifa zilizopatikana jana mjini hapa zimeeleza kuwa tayari maazimio ya wabunge hao wa CCM yamewasilishwa kwa Rais Kikwete.

Taarifa ambazo hazijathibitishwa pia zinaeleza kuwa leo Kamati ya Uongozi ya Bunge huenda ikatangaza Bungeni maazimio yao kuhusu vurugu za Mtwara.

Kamati ya Uongozi ilianza kukutana kuanzia Jumatano jioni na hadi jana wajumbe walikuwa wamejifungia wakijadili namna wanavyoweza kushiriki na kuishauri Serikali kuhusu hatua mwafaka za kuchukua.

RAMA MLA WATU AACHIWA HURU



Ramadhani Suleiman 'Rama mla kichwa' (kulia) na mama yake mzazi,
Khadija (katikati) walipofikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza.

Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imemuachiwa huru Ramadhani Suleiman (Rama mla kichwa) aliyekuwa anakabiliwa na kesi ya mauaji, baada ya kubaini hana akili timamu.

Jaji Rose Temba alitoa hukumu hiyo jana kutokana na ripoti ya Dk Mdeme Erasto iliyowasilishwa mahakamani hapo kuonesha kuwa, wakati mshitakiwa huyo anatenda kosa hilo hakuwa na akili timamu.

Ramadhani, ambaye alishitakiwa pamoja na mama yake Khadija Suleiman, alidaiwa kukutwa na kichwa cha mtoto Salome Yohana (3) katika eneo la Hospitali ya Taifa Muhimbili kikiwa katika mfuko wa plastiki maarufu kama rambo.


Jaji Temba alisema mshitakiwa alitenda kosa la mauaji, lakini kwa kuzingatia ripoti ya uchunguzi wa akili, mahakama haiwezi kumtia hatiani hivyo aliamuru mshitakiwa huyo awe chini ya uangalizi wa madaktari wa Hospitali za magonjwa ya akili na watatakiwa kuripoti maendeleo ya afya yake kwa Waziri wa Katiba na Sheria.

Aidha mahakama ilimwachia huru mama mzazi wa mshitakiwa huyo, Khadija, kwa kuwa Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) hakuwa na haja ya kuendelea kumshitaki.

Awali Wakili wa utetezi, Yusuph Shehe alidai kuwa mahakama ilitoa amri ya mshitakiwa kwenda hospitali kuchunguzwa kama ana akili na ripoti ya daktari iliwasilishwa mahakamani hapo na kubainisha kuwa hakuwa na akili timamu, hivyo aliomba mahakama imfutie mashitaka.

Akiwasomea maelezo ya awali washitakiwa hao, Wakili wa Serikali Cecilia Mkonongo alidai kuwa Aprili 25 mwaka 2008 saa 2:25 usiku, Salome (marehemu) alikuwa anacheza na Ramadhan pamoja na mtoto Paschal Lucas lakini baadaye alipotea katika mazingira ya kutatanisha.


Alidai saa 2:30 usiku baba wa Salome, Yohana Mussa alikwenda kwa dada yake aitwaye Furaha ambapo Salome alikuwa akiishi, alipohoji mtoto wake yupo wapi ndipo wakaanza kumtafuta bila mafanikio, wakaamua kutoa taarifa kwa balozi.

Aliendelea kudai kuwa, asubuhi ya Aprili 26 mwaka 2008, wakiwa njiani kwenda kituo cha polisi walipewa taarifa kuwa kuna kiwiliwili cha mtoto kimeonekana katika choo cha nyumba ya washitakiwa, walipokwenda walikuta mwili wa Salome ukiwa chini bila kichwa.

Mkonongo alidai wakiwa katika eneo la tukio, polisi walipata taarifa kuwa kuna mtu amekamatwa na kichwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, walikwenda wakiwa na askari na ndugu wengine na kukitambua kichwa hicho.

Ilidaiwa kuwa, Ramadhani alikamatwa na mlinzi wa Hospitali hiyo akiwa na kichwa hicho na kudai anakipeleka kwa shangazi yake anayefanya kazi ya usafi katika hospitali hiyo.

Aprili 29 mwili wa marehemu ulifanyiwa uchunguzi na ripoti ya daktari ilionesha, chanzo cha kifo chake hakikujulikana lakini, ilidai Salome alikatwa na kitu chenye ncha kali na alikuwa na michubuko mwilini.

Rama alipohojiwa na askari, alikiri kukutwa na kichwa hicho na kudai mama yake ndiye aliyemuua Salome kwa kutumia shoka na alikuwa anapeleka kichwa kwa shangazi yake.

Mama wa mshitakiwa huyo (Khadija) alipohojiwa alikiri mwili wa marehemu kukutwa kwenye choo chake na ukiwa umefungwa na shati la Ramadhani.

Baada ya uamuzi huo kutolewa, ndugu wa marehemu waliangua kilio, na walipotoka Upendo Dunstan (mama wa marehemu) na shangazi yake Furaha Mussa walikuwa wakiangua kilio huku baba wa mtoto akilia huku ameshika kiuno nje ya mahakama hiyo.


Washitakiwa walirudishwa rumande kwa ajili ya kukamilisha taratibu, baada ya kusota rumande kwa zaidi ya miaka mitano.

Friday, May 24

HAKUNA JAMII ITAKAYOACHWA NYUMA KIMAENDELEO: TANZANIA

Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa,
Balozi Ramadhan Mwinyi, akizungumza wakati wa
Mkutano wa 12 wa Masuala ya Wazawa,
kuhusu mada ya utafiti uliofanywa kuhusu Ujasiri,
Maarifa ya Jadi na Kujenga uwezo Jamii ya Wafugaji katika Afrika.
Nyuma ya Balozi ni Bi. Ellen Maduhu Afisa wa Ubalozi .


Tanzania imesisitiza kwamba inajukumu kubwa la kuhakikisha kuwa mipango yake ya maendeleo endelevu inamfikia kila mwananchi na kwamba hakuna jamii itakayo achwa nyuma.

Na kwa sababu hiyo, Tanzania imeitaka Jumuiya ya Kimataifa na wadau wengine kushirikiana na Serikali katika kufanikisha azma yake hiyo, lakini pia kutambua kuwa maamuzi mbalimbali inayoyachukua yanafanyika kwa nia njema.

Hayo yameelezwa na Balozi Ramadhan Mwinyi, Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, alipokuwa akichangia majadiliano ya mada ya utafiti kuhusu Ujasiri, Maarifa ya Jadi na Kujenga Uwezo wa Jamii ya Wafugaji katika Afrika.

Mada hiyo ni sehemu ya mada kadhaa zikiwa zao afya, elimu, haki za binadamu, ujasiliamali, vijana mila na tamadu ambazo zimekuwa zikijadiliwa kwa nyakati tofauti katika Mkutano wa Kudumu wa 12 Kuhusu Masuala ya Wazawa. ( Forum on Indigenous Issues) Mkutano huu ambao ulianza mapema wiki hii unafanyika chini ya usimamizi wa Baraza la Uchumi na Maendeleo ya Jamii la Umoja wa Mataifa ( ECOSOC).

Washiriki wa mkutano huu wapatao 2000 wanatoka katika Asasi zisizo za kiserikali wakiwamo wawakilishi kutoka baadhi ya taasisi za kifedha kama Banki ya Dunia, Banki ya Maendeleo ya Afrika na Banki ya Maendeleo ya Asia.

“Tunaendelea na jitihada za kuwaletea maendeleo wananchi wetu ili kuhakikisha kwamba hakuna jamii inayoachwa nyuma kama ambavyo imeainishwa katika Malengo ya Maendeleo ya Millenia ( MDGs) na kutafsriwa katika Mpango wa Maendeleo ya Taifa na mipango migineyo” akasisitiza Balozi Mwinyi.

Hata hivyo akasema licha ya jitihada hizo za serikali , bado kuna baadhi ya jamii chache ambazo zenyewe zimeamua kudumisha mila, tamaduni na maisha yao ya jadi .

Akasema jamii hizo ni zile ambazo hazifahamiki sana katika Jumuiya ya Kimataifa kama ilivyo kwa jamii ya wamasaai.

Akizungumzia masuala ya upatikanaji na ugawaji wa ardhi kwa wananchi zikiwamo jamii ambazo mfumo wa maisha yao unategemea zaidi ardhi na mali asili nyingine. Balozi Mwinyi amewaeleza washiriki wa mkutano huo wakiwamo washiriki kutoka Tanzania, kwamba serikali imejiwekea sheria na taratibu zinazosimamia ugawaji wa ardhi.

Akafafanua kwa kueleza kwamba kwa sheria na taratibu za Tanzania, Hati ya umiliki wa Ardhi katika ngazi ya kijiji hutolewa kwa wanajamii ambao wanaishi au wamekusanyika katika muundo wa kijiji ambao unatambuliwa rasmi.

“ Kwa mujibu wa sheria zetu, ni kijiji ndicho kinatambuliwa kisheria kama chombo huru kinachosimamia masuala ya ardhi ambapo cheti cha ardhi hutolewa kwaajili ya matumizi ya jamii nzima”. Akasema

Na kuongea “ Hata hivyo kuna baadhi ya maeneo hasa yale ya wawindaji ambapo kama idadi ya jamii ile haikukidhi matakwa ya kisheria ya kuwa na hadhi ya kijiji kutokana na uchache wao, bado kwa mfano, mwaka 2011, serikali ilitoa hati ya kumiliki ardhi kwa ya Wahdzabe ingawa walikosa sifa zinazotakiwa kisheria.

Akizungumza kuhusu Loliondo ambako Serikali imetangaza kutenga eneo la kiasi cha kilomita za mraba 2,500 za ardhi kwaajili ya makazi ya jamii ya wamasaai na ambao wengi wao hawakuwa na ardhi na hivyo kuwa katika mazingira magumu. Balozi amesisitiza kwamba uamuzi huo ulikuwa ni wa manufaa kwa jamii hiyo na taifa kwa ujumla.

Akasema kuwa eneo lililotengwa ni kubwa kuliko nchi ya Luxeburg au mara nne ya eneo la nchi ya Singapore ambayo ina kilomita za mraba 624.

Akasema eneo lililobaki la kilomita za mraba 1,500 Serikali imelitenga kwaajili ya hifadhi ya wanyama pori na mazalia yake ikiwa ni pamoja na uhifadhi wa uoto wa asili, utunzaji wa vyanzo vya maji kwa maendeleo endelevu ya uwepo wa wanyama na kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.

Naibu Mwakilishi wa Kudumu akafafanua Zaidi kwa kueleza kwamba, uamuzi huu wa Serikali wa kutenga ardhi kwaajili ya matumizi ya binadamu na mengine kwa hifadhi ya maliasili ni uamuzi halali na wala haukuanza sasa bali umekuwa ukitekelezwa katika maeneo mengi ya nchi tangu uhuru.

HALI BADO NI MBAYA MTWARA....WANAFUNZI WAWILI WAMETANDIKWA RISASI, MMOJA AMEFARIKI HAPOHAPO

Hivi sasa baadhi ya wananchi wa eneo la magomeni mkoani mtwara wamekimbilia katika Hospitali ya Mkoa wa Mtwara Lugula wakihofia usalama wao kutokana na vurugu za kuchomwa kwa nyumba zao pamoja na vibanda vya biashara zilizotokea leo asubuhi katika eneo hilo..

Maduka maeneo ya Magomeni yamechomwa moto ikiwamo pia mali za Askari magereza . Mwanafunzi wa CHUNO amefikishwa hospitali Ligula na majeraha ya risasi mguuni.
Mwanamke mwingine anayekadiriwa kuwa na miaka 25 mjamzito ameuawa kwa kupigwa risasi maiti ipo Ligula.

Inaelezwa kuwa katika baadhi ya mitaa hali imetulia na ni idadi ndogo ya wananchi ndiyo inayoonekana wakitembea mitaani isipokua eneo la magomeni ambako mbomu yanaendelea kusikika huku huduma za kijamii katika mji huo zikiwa zimesimama zikiwemo usafiri, huduma za kibenki na shule








MTWARA: ASKARI WATUHUMIWA KUBAKA NA KUMUUA MJAMZITO......INASEMEKANA WANAFANYA MAKUSUDI ILI KULIPIZA KISASI

Askari wakiwa lindoni/doriani, Mtwara

Hali ya usalama katika Manispaa ya Mtwara Mikindani mkoani Mtwara imezidi kuwa mbaya baada ya askari polisi kudaiwa kufanya unyama kwa kuwabaka wanawake na kumpiga risasi mjamzito

Mbali na unyama huo polisi pia wanadaiwa kuchoma moto nyumba tatu za wananchi katika mtaa wa Magomeni na vibanda vya maduka kadhaa na kupora vitu vilivyomo ndani.

Hata hivyo Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mtwara, Linus Sinzumwa anasema hali ni shwari na kwamba wananchi watoke nje kuendelea na shughuli zao kama kawaida.

Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Ligula, Mohamedi Kodi amethibitisha kupokea mwili wa mjamzito ukiwa na tundu tumboni, zinazoaminika kuwa za risasi na hivyo kufanya idadi ya maiti zilizopokelewa hospitalini hapo kufikia mbili na majeruhi 18:

“Ni kweli kwa leo( jana) tumepokea maiti moja ya mwanamke ambaye ni mjamzito wa miezi saba, amepigwa risasi tumboni.pia tumepokea mwanafunzi wa shule ya sekondari ya Chuno, amevunjwa miguu yote kwa risasi.”

Habari zinadai kuwa mjamzito huyo ameuawa akiwa nyumbani kwake baada ya polisi kuvamia makazi yake.

Huduma za kijamii zimesimama, hakuna maduka yaliyo wazi, hakuna usafiri wa daladala wala pikipiki, mji upo kimya, sauti za milio ya mabomu na bunduki zimetawala, wanajeshi waliovalia sare wameuzingira mji wakiwa katika magari na pikipiki.

Wakizungumza na Waandishi wa Habari kwa nyakati tofauti wakazi hao wamelalamikia kitendo cha askari wa jeshi la polisi kuingia katika makazi yao, kuwapiga, kuwabaka na kuwapora mali zao:

“Magomeni A hatuna amani askari wanaingia majumbani mwetu wanatupiga na kutunyang’anya simu, yani huku Magomeni hatuna amani kabisa, tumepoteza watoto na hatujui hata waume zetu wako wapi” alisema Paulina Idd na kuongeza:

“Majumba yetu yamechomwa moto , wanaofanya fujo ni polisi wenyewe halafu wanakuja wanatubaka na kuiba mali zetu halafu tunateseka sisi yaani tumechoka kabisa na serikali yenyewe,” alisema Paulina.

Kamanda Sinzumwa alipoulizwa kuhusiana na tuhuma hizo alisema hawezi kuzungumzia suala hilo kwa madai kuwa atapingana na Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk Emmanuel Mchimbi aliyewasili Mtwara leo: “Kuhusiana na suala hilo siwezi kulizungumzia kwa sasa kwani nitapingana na Waziri wangu kwani leo ametoa tamko bungeni na leo atawasili,” alieleza Sinzumwa

Wananchi wazungumzia bajeti

Wakizungumzia uwasilishwaji wa hotuba ya Wizara ya Nishati na Madini wakazi wa hapa wamesema kuwa hawakubaliani na ujenzi wa bomba la kusafirisha gesi kwani mpango huo utawaletea dhuluma:

“Mpango wa kusafirishwa kwa gesi asilia hatuna mpango nao kwa wakazi wote wa Mtwara kwa kifupi akina mama wa mtwara hatutaki itoke,” alisema Fatuma Abdallah.

Thursday, May 23

VURUGU ZA MTWARA ZAUA WANAJESHI WANNE NA KUJERUHI 20


Katika tukio lingine askari wanne wa jeshi la wananchi kikosi cha 41 KJ wamefariki dunia na wengine 20 kujeruhiwa baada ya gari lao kupinduka eneo la Kilimani hewa Nachingwea njiani kuelekea Mtwara kuongezea nguvu jeshi la polisi kufuatia vurugu zilizotokea mkoani humo


Mtu mmoja amefariki dunia na kadhaa kujeruhiwa katika vurugu zilizoibuka mkoani Mtwara baada ya bajeti ya wizara ya nishati na madini kusomwa ambapo pia ofisi za CCM wilaya ya Mtwara vijijini imeteketezwa moto pamoja na nyumba nyingine nne ikiwemo nyumba ya mbunge na mwandishi wa habari wa TBC



Nyumba ya mwandishi wa habari wa tbc yachomwa moto huku mabomu yakirindima huko mtwara


Hali imezidi kuwa mbaya katika Mji wa Mtwara na hivi punde watu wanaendelea kufanya uharibifu katika maeneo mbalimbali ya mji huo.
Jengo moja ambalo linadaiwa kumilikuwa na CCM limechomwa moto katika eneo la Majengo na daraja linalounganisha Lindi na Mtwara limevunjwa.
Mbali na hayo pia nyumba ya mwandishi wa habari wa Shirika la Utangazaji la Tanzania (TBC)imechomwa moto.
Katika Mji wa Mtwara milio ya mabomu na risasi ndio inayosikika kila kona. Jeshi la Polisi linajaribu kuwadhibiti vijana na watu wengine ambao wanafanya vurugu hizo.

Kwa mujibu wa - freebongo.blogspot.com

Umefika wakati wa kubadili muundo wa Tanesco


ahitaji ya umeme kwa wateja wake ni Megawati 906, lakini uwezo wake ni kuzalisha 705 tu. Megawati hizo zinazalishwa kupitia mabwawa ya Kidatu (204), Kihansi (180), Mtera (80), Pangani (68), Hale (21) na Nyumba ya Mungu (8).
Jana bungeni, Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo aliwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya wizara yake kwa mwaka huu wa fedha na ndani ya hotuba yake alielezea hali mbaya ya Tanesco akisema inadaiwa zaidi ya Sh900 bilioni.
Haishangazi kusikia Tanesco ina hali mbaya kifedha, kwa sababu tangu shirika hilo lianzishwe mwaka 1964, limeshindwa kutoa huduma ya umeme kwa walau nusu ya Watanzania, hata hao waliounganishiwa, hawapati umeme wa uhakika.
Wizara inayoisimamia Tanesco imeshaongozwa na mawaziri 21 na makatibu wakuu 18. Hoja za baadhi yao ni shirika hilo kuzidiwa kimajukumu, ikiwamo mzigo wa madeni.
Katibu Mkuu aliyepita, David Jairo hakutafuna maneno aliposema hali ya Tanesco ni mbaya, mapato yake ya mwezi hayazidi Sh30 bilioni, wakati kwa siku inatumia Sh566 milioni kuwalipa Songas na IPTL.
Kwa mfano, mahitaji ya umeme kwa wateja wake ni Megawati 906, lakini uwezo wake ni kuzalisha 705 tu. Megawati hizo zinazalishwa kupitia mabwawa ya Kidatu (204), Kihansi (180), Mtera (80), Pangani (68), Hale (21) na Nyumba ya Mungu (8).
Umeme mwingine ni wa nguvu za mitambo iliyopo katika Vituo vya Tanesco vya Ubungo, Megawati 100 na Tegeta 45. Wakati uzalishaji wa umeme ni megawati 705, mahitaji ya Dar es Salaam pekee, ni Megawati 455. Profesa Muhongo ambaye ni waziri wa 21 katika wizara inayoongoza Tanesco, kwenye hotuba yake ya kwanza kwenye Bunge la Bajeti la mwaka jana, alizungumzia hoja ya kuinusuru Tanesco kwa kuipa ruzuku. Hata hivyo, msaada wa ruzuku ya Serikali kwa Tanesco umeonekana kutofua dafu.
Profesa Muhongo ameshawahi kukaririwa akitaka marekebisho makubwa katika shirika hilo, hoja ambayo inaungwa mkono na wananchi wengi. Kwa mfano, wananchi wa Wilaya ya Bunda, Mara wakizungumza kwenye mkutano wa wadau wa umeme walitamka bayana kuwa shirika hilo limezidiwa. Walisema limebeba mzigo mkubwa wa kuzalisha umeme, kuuza na kusambaza.
Ufanisi wa Tanesco umegubikwa na ‘umwinyi’ unaochangia kulidhoofisha, wateja wanaoomba kuunganishiwa umeme hawapewi huduma hiyo kwa wakati, kumekuwa na ulegevu wa ufuatiliaji madeni kwa wateja na hujuma nyingine zinafanywa na wafanyakazi wenyewe.
Kumekuwa na mianya mingi ya hujuma za mapato ya Tanesco, kumekuwa na tatizo la ‘vishoka’ wa kuunganisha umeme na wanaouza Luku na wote hao wana uhusiano na baadhi ya wafanyakazi wa Tanesco.
Pamoja na kuiona Tanesco kwamba imekuwa mzigo, bado kuna waliolifikisha shirika hilo hapo, Serikali na taasisi zake ni mojawapo na kwa kiasi kikubwa hawawezi kukwepa lawama.
Siyo siri, Serikali imekuwa mdaiwa mkubwa wa Tanesco na kutolipa hayo kumechangia kulidhoofisha shirika hilo kimapato.
Tunadhani kwamba hakuna haja ya kuendelea kuibebesha Tanesco mzigo wa kuzalisha umeme, kuuza na kusambaza. Ni wakati sasa kwa Serikali kulivunja shirika hilo ili kulipunguzia mzigo wa majukumu lakini pia kuongeza ufanisi kwa kuleta ushindani katika sekta ya nishati.
Wakati mjadala wa makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini ukiendelea bungeni, tungependa kuwashauri wabunge kuishauri Serikali kubadili muundo wa shirika hilo ili Watanzania wengi ambao ni zaidi ya milioni 40 waweze kunufaika na huduma ya umeme.