Wednesday, June 12

PICHA ZA WAKENYA WALIVYOANDAMANA JUNE 11 NA KINYAGO CHA NGURUWE NA DAMU WAKIPINGA MISHAHARA YA WABUNGE

Miungano ya kijamii ikiongozwa na Bunge la mwananchi,Muhuri na pawa 254 miongoni mwa mengine yameandaa maandamano ya pili kupinga juhudi za wabunge kuhujumu tume ya kuratibu mishahara nchini kenya SRC ili kujiongezea mishahara ya hadi laki nane kinyume na ilivyopendekezwa na SRC.


Tofauti na wiki kadhaa zilizo pita ambapo waandamanaji waliwaelekeza nguruwe walioandikwa majina ya wabunge walio unga mkono mswada huo, hii leo waandamanaji walibeba kinyago wa nguruwe na damu walio ashiria mwisho wawabunge kukandamiza wakenya. huku wakijimwagilia damu kama ishara ya kuumizwa na kodi ya kuwalipa wabunge.
Waandamanaji pia walibeba mfano wa noti za shillingi alfu moja pesa za kenya zilizo chorwa Nguruwe mkubwa kwa upande mmoja na wanawe kwa upande wa pili, huku wakiwarushia wabunge noti hizo kuashiria kujitakia makuu kwa wabunge hao.


Viongozi wa waandamanaji wameahidi kuendeleza maandamano hadi pale wabunge watakapo sitisha hujuma dhidi ya tume ya bi sara serem ama SRC.
Tume ya SRC imependekeza wabunge kulipwa mshahara wa kati ya shillingi laki Nne hadi laki saba.Ilihali wabunge walipendekeza mshahara wa hadi shillingi millioni moja.

kwamujibu wa freebongo.blogspot.com

No comments:

Post a Comment