Thursday, May 23

VURUGU ZA MTWARA ZAUA WANAJESHI WANNE NA KUJERUHI 20


Katika tukio lingine askari wanne wa jeshi la wananchi kikosi cha 41 KJ wamefariki dunia na wengine 20 kujeruhiwa baada ya gari lao kupinduka eneo la Kilimani hewa Nachingwea njiani kuelekea Mtwara kuongezea nguvu jeshi la polisi kufuatia vurugu zilizotokea mkoani humo


Mtu mmoja amefariki dunia na kadhaa kujeruhiwa katika vurugu zilizoibuka mkoani Mtwara baada ya bajeti ya wizara ya nishati na madini kusomwa ambapo pia ofisi za CCM wilaya ya Mtwara vijijini imeteketezwa moto pamoja na nyumba nyingine nne ikiwemo nyumba ya mbunge na mwandishi wa habari wa TBC



Nyumba ya mwandishi wa habari wa tbc yachomwa moto huku mabomu yakirindima huko mtwara


Hali imezidi kuwa mbaya katika Mji wa Mtwara na hivi punde watu wanaendelea kufanya uharibifu katika maeneo mbalimbali ya mji huo.
Jengo moja ambalo linadaiwa kumilikuwa na CCM limechomwa moto katika eneo la Majengo na daraja linalounganisha Lindi na Mtwara limevunjwa.
Mbali na hayo pia nyumba ya mwandishi wa habari wa Shirika la Utangazaji la Tanzania (TBC)imechomwa moto.
Katika Mji wa Mtwara milio ya mabomu na risasi ndio inayosikika kila kona. Jeshi la Polisi linajaribu kuwadhibiti vijana na watu wengine ambao wanafanya vurugu hizo.

Kwa mujibu wa - freebongo.blogspot.com

No comments:

Post a Comment