Saturday, March 3

Makatibu wakuu 12 watembelea Hifadhi ya Ziwa Manyara

Mwenyekiti wa makatibu wakuu hao, Katibu mkuu
Mwenyekiti wa makatibu wakuu hao, Katibu mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Maimuna Tarishi  
Arusha. Makatibu wakuu wa wizara 15 pamoja na baadhi ya watendaji wa wizara hiyo watembelea Ziwa Manyara kuona hali halisi ya uharibifu wa ambao unatishia kukauka kwa ziwa hilo.
Mwenyekiti wa makatibu wakuu hao, Katibu mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Maimuna Tarishi amesema lengo la ziara hiyo ya kazi ni kujionea uharibifu wa ziwa na kuishauri Serikali.
Amesema hivi karibuni mawaziri ambao wizara zao zinahusiana na ziwa hilo walikutana na kupokea changamoto za ziwa hilo na waliagiza makatibu wakuu kutembelea na kupata hali halisi na baadae kuishauri Serikali.
Mkurugenzi mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa (Tanapa), Allan Kijazi amesema ziwa Manyara lipo hatarini kukauka kutokana na kuongezeka shughuli za kibinaadamu pembezoni mwa ziwa.
Amesema shughuli hizo pia zimeathiri mapito na mtawanyiko wa wanyama katika eneo la ikolojia ya hifadhi za Manyara na Tarangire.
Ziara ya makatibu wakuu inaendelea muda huu na inashirikisha watendaji wa Serikali, ofisi ya mkuu za wakuu wa mikoa Arusha na Manyara, ofisi ya mwanasheria mkuu wa Serikali na maofisa wa  wizara hizo.

No comments:

Post a Comment