Thursday, March 8

'Kwa kweli sitaki usikilize muziki huu'' DJ anayetengeneza muziki wa kulala

Tom MiddletonHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionMwanamuziki Tom Middleton
"Kiukweli sitaki usikilize muziki huu''. Inawezakana Tom Middleton akawa mwanamuziki wa kwanza kutumia maneno hayo wakati anatangaza albamu yake mpya.
Akiwa ni Dj wa kimataifa,Tom ameweza kuwaburudisha zaidi ya watu milioni katika mataifa 49 na kuwafanya wanamuziki kama Kanye West, Lady Gaga na Snoop Dogg kuanza kupendwa.
Lakini sasa Tom amekuja kivingine baada ya kufanya uchunguzi wa muda mrefu wa tafiti za kisayansi, na kuamua kutengeneza wimbo ambao hauwashirikishi wasikilizaji wake kuusikiliza bali unawataka walale.
Tom alianza kufanya shughuli za kimuziki mnamo miaka ya 90, akiwa anashirikishwa na Aphex Twin pamoja na Mark Pritchard.
Amekuwa akitengeneza muziki kwa kutumia majina mbalimbali katika majukwaa ikiwa ni pamoja na "Reload,Cosmos na Modwheel.
Tom anasema kitu ambacho kimemshawishi kuja na ubunifu huu wa kuandaa muziki wa kumfanya mtu apate usingizi ni kwa sababu amekuwa anafanya kazi karibu na wanasayansi na watafiti.
kkHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionMuziki wa kukufanya ulale
Hivyo alidhani kwamba anaweza kutumia ujuzi wake wa kielektroniki na kuandaa mradi huo.
"nilifikiria mara mbili kuwa ni kitu gani ambacho kilishawahi kufanywa hivyo nikaamua kutumia utaalamu wa sayansi kutengeneza midundo ambayo itamfanya mtu apumzike".
Nyimbo hizi zimebuniwa ili kumtuliza msikilizaji na kumfanya apumue kwa kasi pamoja na kushusha mapigo ya moyo ambayo yatamsaidia mtu apumzike.
Hata hivyo mwanamuziki huyo amesema kwamba nyimbo hizo ambazo kwa sasa ziko sokoni hazijawahi kufanyiwa jaribio la kisayansi.
Na anadhani kwamba itavutia zaidi kama wataangalia utafiti ambao ulifanywa ,ni sauti zipi ziliweza kufanya kazi vizuri na kelele zipi ambazo ziliwahi kufanyiwa jaribio
sayansiHaki miliki ya pichaCARSTEN WINDHORST
Image captionTom sasa ni mtaalamu wa kisayansi wa kumfanya apate usingizi
Mwanamuziki huyo anataka kuongeza eleo kwa watu kwa kuandaa tamasha kuhusiana na hiki alichokiandaa .
"Mtu hawapaswi kusikiliza muziki huu wakati anaendesha gari,anaongoza mtambo wowote katika maji".
Mpaka sasa anasema ameona mafanikio makubwa wakati alipofanya jaribio la kuwasikilizisha watu na kweli uliwafanya wapate usingizi.
Tom anasema kutengeneza albamu hii ni moja ya kazi ambayo imekuwa na changamoto kubwa katika maisha yake na katika taaluma yake kwa ujumla ingawa kwake hayo ni mafanikio makubwa.

No comments:

Post a Comment