Thursday, March 8

Wakimbizi kutoka Burundi waliokuepo DRC wahamishiwa Rwanda

Wakimbizi wa Burundi waliohama ni wanawake na watoto
Image captionWakimbizi wa Burundi waliohama ni wanawake na watoto
Wakimbizi zaidi ya 2000 walioingia nchini DRC tangu mwaka 2015, wamefika katika mpaka wa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Rwanda bila taarifa wakiwa wamesindikizwa na wanajeshi wa umoja wa umoja wa mataifa wa Monusoco .
Kwa mujibu wa taarifa kutoka idara ya sekta ya uhamiaji nchini DRC, wanasema kiongozi mmoja wa shirika la Monusoco ambaye hakukata jina lake litajwe alisema hata wao walishanga kuona kundi kubwa la watu hao wakiwa wamefika kwenye mpaka na hawakuwa na taarifa yeyote kutoka serikali ya Rwanda wala ya Kongo kuwa wakimbizi hao watafika katika eneo hilo.
watotoHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionWakimbizi wa Burundi
Kwa upande wa shirika lisilokuwa la kiserikali la kijiji cha kamanyola ambako wakimbizi hao walikuwa wakiishi wanasema hawakubaliani kabisa na kitendo cha wakimbizi hao kuhamishwa ghafla.
Beatrice Tuptunzie ni kiongozi wa shirika la raia kijiji cha kamyola anathibitisha kuwa umoja wa mataifa uliwasindikiza, lakini namna walivyowahalisha ndio haikutufurahisha hata kidogo. Kwa sababu waliona wanawake wengi na watoto lakini wanaume hawakuonekana na haijulikani walienda wapi ?
Huku wakazi wa eneo hilo kuna walishtushwa na tukio hilo wakati wengine wakifurahia kuhamishwa kwa wakimbizi hao ingawa wapo waliokuwa na wasiwasi kuwa kwamba wanaweza kurudi kulipa kisasi kwa kuwa kuna wakimbizi waliouwawa mwaka jana.
Inaelezwa kuwa wakimbizi hawa hawakukubaliwa kukaa Jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo licha ya kuwa waliomba nafasi kwa muda mrefu na kuweza kufanikiwa kukaa nchini humo kwa takribani miaka mitatu.

No comments:

Post a Comment