Friday, December 1

Museveni: Kujiepusha na pombe kumechangia maisha marefu

Kitabu hicho cha Museveni kilichapishwa mwaka 1997Haki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Rais wa Uganda Yoweri Museveni amefichua kwamba huwa hanywi pombe na kusema hilo limechangia maisha yake marefu.
Museveni, 73, ameandika kwenye Twitter kwamba uamuzi wake huo umemkinga dhidi ya maradhi na kusema kwamba hana "muda wowote wa magonjwa".
Wabunge nchini Uganda kwa sasa wanajadili mswada ambao unaondoa kikomo kwenye umri wa rais, ambacho kwa sasa ni miaka 75.
Sheria isipofanyiwa marekebisho na kikomo hicho kuondolewa, Bw Museveni hawezi kuruhusiwa kuwania kwa muhula wa sita uchaguzi wa mwaka 2021.

No comments:

Post a Comment