Friday, November 10

Mbunge asikitika wafanyabiashara kunyanyaswa bandarini


Mbunge wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar (BWL), Jaku Hashim Ayoub amesema  mtu anayekutwa na bidhaa za Zanzibar katika bandari ya Dar es Salaam ananyanyaswa kupindukia.
“Leo mali za Zanzibar ukiingia nayo utadhani umeingiza unga (dawa za kulevya). Wazanzibar mnatuonea sana”alisema na kuongeza kusema;-
“Leo Mzanzibar anachukua gauni zake tatu anakuja nazo bandarini (Dar es Salaam) anaambiwa kaa chini. TV moja tu. Huu muungano wa upande mmoja tu? Amehoji.

Mwakilishi huyo wa Paje, amesema ukiacha zao la Karafuu biashara  ndio nguzo muhimu ya uchumi wa Zanzibar ila kikwazo ni kuwapo kwa tozo mbalimbali kwa wafanyabiashara ambao wanaingiza na kutoa bidhaa mbalimbali kuptia bandari ya Dar es Salaam.
“Suala hili sio la upande mmoja na nakuomba ufike visiwani ili ujionee hali halisi na kujua changamoto zinazowakabili ndugu zetu, ukifanya hivyo na kukusanya mapato stahiki utastahili pongezi kwani kuwaonea katika kila kitu kinachopita bandari ulipie ni uonevu,”amesema Jaku.
Amesema suala la mizigo kutoka nchi jirani ikiwemo Kenya, Rwanda, Burundi na Uganda kuingia nchini bila ya usumbufu wa kulipia kodi katika bandari ni jambo ambalo halikubaliki kwani kwa watu wa Zanzibar imekua tofautio kwa kulipia hata miche mitatu ya sabuni.
“Waziri kwa hili haliwezi kuwa haki kwani kuku ana uwezo wa kutaga yai moja ukimlazimisha kutaga matatu utamkosa na kuku huyo,”amesema Jaku.
Mbali na hilo mwakilishi huyo alisema hali ya biashara imekuwa mbaya kwa baadhi ya milango ya fremu kufungwa bula ya kuwa na biashara kutokana na kodi kubwa ya Serikali.

No comments:

Post a Comment