Friday, November 10

UN yachagua majaji wanne kuingia ICC

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa
Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa na Baraza la Usalama limewachagua majaji wanne Alhamisi kuingia katika Mahakama ya Kimataifa, ni taasisi ya kisheria ya juu ya UN.
Katika kura ya peke yake, lakini iliyofanyika kwa pamoja, Mkutano na Baraza limewachagua tena Ronny Abraham wa Ufaransa na Abdulqawi Ahmed Yusuf wa Somalia.
Pia majaji wawili wapya, Antonio Augusto Cancado Trindade wa Brazil na Nawaf Salam wa Lebanon, pia wamechaguliwa.
Wote hao wamechaguliwa kutumikia mahakama hiyo kwa kipindi cha miaka tisa, kuanzia Februari mwakani.
Mahakama hiyo iliundwa mwaka 1945, chini ya mkataba wa UN, ambapo Mahakama ya ICC ndiyo taasisi ya kisheria ya juu ya UN.
Shughuli za mahakama hii kwa mujibu wa sheria za kimataifa, ni kusuluhisha migogoro inayowasilishwa na mataifa mbalimbali na kutoa ushauri wa kisheria juu ya masuala yanayoletwa na mashirika ya Umoja wa Mataifa na taasisi maalum.

No comments:

Post a Comment