Wednesday, November 15

Madai yafanya mhadhiri azuie matokeo ya wanachuo

Chuo kikuu cha Mount Meru kilichopo Ngaramtoni mkoani Arusha kimeingia katika mgogoro na mhadhiri wa wake, Naiman Solomon baada ya kushindwa kumlipa stahiki zake na hivyo kuzuia matokeo ya wahitimu wa Stashahada  Ualimu na Uongozi.
Akizungumza na waandishi leo Jumatano, Solomon amesema licha ya kuzuia mitihani hiyo uongozi wa chuo hicho umegushi matokeo ya mitihani ya wahitimu jambo ambalo ni makosa kisheria.
"Kutokana na mgogoro huu nimemwandikia Waziri wa Elimu, Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, TCU na Necta, kuelezea mgogoro huo  wa kugushi  matokeo ya wanafunzi wa Stashahada ya Ualimu  na Uongozi ya Chuo Kikuu cha Mount Meru kutokana na ukiukwaji wa taratibu za kutolewa kwa matokeo chuoni hapo," amesema.
Akizungumzia hilo kaimu makamu mkuu wa chuo hicho, Utawala na Fedha, Twazihirwa Mzava amesema kuwa  uongozi wa chuo hicho ulilazimika kuwapatia matokeo wanachuo hao nje ya taratibu baada ya mhadhiri kutokuwasilisha matokeo ya mitihani hiyo kwa uongozi wa chuo kutokana na  kudai stahiki zake ambazo alikuwa hajalipwa.
Mzava amesema  mhadhiri  Solomon hakuwasilisha matokeo kwa sababu anadai stahiki zake kwa kipindi kirefu na hiyo inatokana na ukata unaokikabili chuo hicho.

No comments:

Post a Comment