Wednesday, October 18

Roselyn Akombe: IEBC haiwezi kufanya uchaguzi wa haki

Kamishna wa IEBC aliyejiuzulu Roselyn Akombe
Image captionKamishna wa IEBC aliyejiuzulu Roselyn Akombe
Katika taarifa bi Akombe amesema kuwa alifanya uamuzi mgumu kuondoka katika tume hiyo ya uchaguzi Kenya.
Uamuzi wangu wa kuondoka IEBC utawakatisha tamaa baadhi yenu.
Nimejaribu nimewezavyo kulingana na hali ilivyo.
Mara nyengine unaondoka, hususan wakati ambapo maisha ya watu muhimu yamo hatarini.
Tume hii imehusika pakubwa katika mgogoro uliopo.Tume hii imezungukwa.
Tume hii kama ilivyo haiwezi kufanya uchaguzi wa haki mnamo tarehe 26 Oktoba 2017.
Akifanya mahojiano na kipindi cha BBC Newsday Programme, alisema.
''Je utakuwa uchaguzi ulio huru na haki , Kwa kweli haiwezekani''.
Kuna uwezekano mkubwa kwamba makosa yaliofanywa na baadhi ya maafisa waliosimamia uchaguzi katika vituo vya kupigia kura yatarejelewa.
Akizungumza kutoka mjini New York nchini Marekani, alisema kuwa wanachama wa IEBC wamekuwa wakipiga kura kwa upendeleo bila kuzungunmzia maswala tofauti yalio na umuhimu mkubwa.
''Makamishna na maafisa wengine wa IEBC walikuwa wakikabiliwa na vitisho kutoka kwa wanasiasa na waandamanaji '', alisema bi Akombe.
Pia alifichua kwamba yeye mwenyewe amepokea vitisho kadhaa na alishinikizwa kujiuzulu
.''Sijawahi kuwa na hofu kama ile niliyohisi nikiwa katika taifa langu''.
Alisema kuwa hawezi kurudi Kenya katika siku za hivi karibuni kutokana na hofu ya usalama wake.
Kufikia sasa tume ya IEBC haijatoa tamko lolote kuhusu swala hilo.
Kiongozi wa upinzani Raila Odinga alisema wiki iliopita kwamba IEBC haina lengo la kufanyia mabadiliko yoyote operesheni zake wala maafisa wake.
Bwana Odinga amepanga msururu wa maandamano dhidi ya IEBC katika wiki za hivi karibuni.
Wakati huohuo, bwana Kenyatta anasema kuwa yuko tayari kuendelea na uchaguzi mpya kama ulivyopangwa.
''Hatuna tatizo kushiriki katika uchaguzi mpya kama ulivyopangwa.Tuna hakika kwamba tutapata kura nyingi zaidi ya uchaguzi uliopita''.

No comments:

Post a Comment