Wednesday, October 18

Kiongozi wa Iran amshutumu vikali Rais Trump kuhusu mkataba ya nyuklia

Iran's Supreme Leader Ayatollah Ali Khamenei gestures as he speaks to students in Tehran on 18 October 2017Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionAyatollah Ali Khamenei said European powers should "avoid intruding into our defensive affairs"
Kiongozi mkuu wa Iran Ayatollha Ali Khamenei, ametetea makubaliano ya nyuklia ya mwaka 2015 na kutumia lugha kali kumkosoa rais wa Marekani Donald Trump kwa kudanganya.
"Sitaki kutupa muda wangu kujibu kuropokwa na kelele za Trump," Ayatollah Ali Khamenei alisema.
Bw. Trump amekataa kuthibitisha kwa bunge la Marekani kuwa Iran imetekeleza yaliyo kwenye mkataba huo.
Amatishia kufuta makubaliano yote ya rais Obama .
Trump alitaka mkataba huo kufanyiwa marekebisho kuizuia Iran kuunda silaha za nyuklia au makombora ya masafa marefu.
Ayatollah Khamenei alisema anakaribisha uungwaji mkono wa mkataba huo kutoka nchi za Ulaya, lakini akaongeza kuwa ikiwa Marekani itavunja makubaliano hayo Iran itayatupilia mbali.
Rais Trump pia aliilaumu Iran kwa kuzua misikusuko nchini Syria, Yemen na Iraq na kukiwekea vikwazo kikosi chenye nguvu nyingi Iran cha Islamic Revolution Guards Corps.
Sasa bunge la Congress litaamua ikiwa litaiwekea tena vikwazo vya kiuchumi, ambavyo viliondolewa kama sehemu ya makubaliano hayo.
Ikiwa hilo litafanyika Marekani itakuwa imekiuka makubaliano kwenye mkataba huo.

No comments:

Post a Comment