Tuesday, October 10

Polisi watumwa kabla ya hotuba kuu Catalonia

Catalan leader Carles Puigdemont at a cabinet meeting in Barcelona, 10 OctoberHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionCarles Puigdemont, rais wa eneo la Catalonia
Kiongozi wa Catalonia Carles Puigdemont anakabiliwa na shinikizo kali za kumtaka achane na mipango ya kulitenganisha eneo hilo kutoka Hispania, kabla ya hotuba muhimu kwa bunge la eneo hilo.
Kuna uvumi kuwa huenda akatangaza uhuru kufuatia kura ya maoni iliyokumbwa na utata.
Polisi waliojihami wametumwa nje ya majengo ya bunge la Catalonia mjini Barcelona kabla ya hotuba hiyo.
Meya ya Barcelona amemshuri Bw. Puigdemont na waziri mkuu wa Hispnia Mariano Rahoy kutuliza hali.
Catalonia's regional police force, the Mossos d'Esquadra, guard the regional assembly parliament building in Barcelona, 10 October 2017Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionPolisi waliojihami wametumwa nje ya majengo ya bunge la Catalonia mjini Barcelona kabla ya hotuba hiyo
Hotuba ya Bw. Puigdemont inakuja baada ya kura ya maoni iliyoandaliwa Oktoba mosi ambapo maafisa wa Catalonia wanasema kuwa karibu asilimia 90 ya wapiga kuwa waliunga mkono uhuru.
Asilimia 43 ya wapiga kura walijitokeza kupiga kura.
Kura hiyo ilitajwa kuw iliyo kinyume na sheria na mahaka ya katiba ya Hispania.
Wapiga kura wa "HAPANA" waliisusia pakubwa kura hiyo na kulikuwa na ripoti kadha za udanganyifu.
Carles Puigdemont and Mariano RajoyHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionCarles Puigdemont, kushoto, na Mariano Rajoy

No comments:

Post a Comment