Monday, October 16

ACT Wazalendo yaungana na Somalia kuomboleza


Dar es Salaam. Chama cha ACT Wazalendo kimeeleza kupokea kwa masikitiko taarifa ya vifo vya watu zaidi ya 250 vilivyotokea Mogadishu, nchini Somalia.
Vifo hivyo vimetokana na mlipuko wa mabomu yaliyokuwa yamewekwa ndani ya lori mjini Mogadishu.
Mbali ya vifo hivyo, watu zaidi ya 400 wamejeruhiwa katika tukio hilo.
Shambulio hilo linadaiwa kutekelezwa na kikundi cha kigaidi cha Al-Shabab usiku wa Jumamosi Oktoba 14, 2017.
Taarifa kwa umma iliyotolewa leo Jumatatu na Venance Msebo, ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa wa ACT Wazalendo imesema inasikitisha kuona maisha ya mamia ya watu yakikatizwa kikatili, wakati viongozi, wananchi na taasisi mbalimbali duniani zikifanya juhudi kuhakikisha dunia inakuwa sehemu salama ya kuishi.
“Tunatoa pole kwa Serikali na wananchi wa Somalia, tunawaombea kwa Mwenyezi Mungu awajalie uvumilivu na ustahimilivu katika kipindi hiki kigumu cha kuondokewa na mamia ya ndugu zao,” imesema taarifa hiyo.
ACT Wazalendo imetoa wito kwa Serikali za Somalia na Tanzania, Jumuiya ya Afrika Mashariki, Umoja wa Afrika na jumuiya za kimataifa kuendelea na juhudi za kuleta amani nchini Somalia.
“Juhudi za makusudi zinapaswa kuchukuliwa ili kuepusha maafa na madhara zaidi yanayoweza kusababishwa na kutokuwepo usalama nchini Somalia,” amesema Msebo katika taarifa hiyo.
ACT Wazalendo imesema Somalia isipokuwa salama Afrika haiwezi kuwa salama

No comments:

Post a Comment