Monday, October 16

UPELELEZI WA KESI YA KUSAMBAZA TAARIFA ZA UONGO BADO HAUJAKAMILIKA


Na Karama Kenyunko, blogu ya jamii
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu leo imeelezwa kuwa, upelelezi dhidi ya kesi ya kusambaza taarifa za uongo kupitia mtandao wa kijamii  wa Face book kuhusu mazungumzo kati ya Serikali na wawakilishi wa kampuni ya Acacia, inayomkabili Mkazi wa Chato Geita, Obadia Kiko bado haujakamilika.

Wakili wa Serikali, Adolf Mkini amesema hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri kesi hiyo ilipokuja kwa kutajwa.

Baada ya kutolewa kwa maelezo hayo, kesi hiyo imeahirishwa hadi Novemba 14 mwaka huu.

Katika kesi hiyo, inadaiwa Agosti 3, mwaka huu huko Chato Geita mshtakiwa obadia anadaiwa kusambaza maneno kuwa " Taarifa kutoka kikao cha mazungumzo kati ya Serikali na wawakilishi wa kampuni ya Acacia kuwa wanasheria wa upande wetu wanashindwa kutafsiri baadhi ya vifungu vya sheria hadi kufikia kuomba msaada kwa wanasheria wa Acacia sasa huoni hivi ni vituko mwizi anakusaidia sheria haahaa haha."

Inadaiwa aliendelea kusambaza maneno kuwa "Mazungumzo bado yanaendelea lakini wanasheria wetu wamebanwa sana ukizingatia wale jamaa wana vielelezo vyote vya mikataba kiukweli tumuombe mungu maana Serikali ikitaka kuvunja mkataba na Acacia gharama kubwa zitatuusu."

"Lakini pia kuendeleza uvyama utatugharimu saana,  baada ya mh. Rais Magufuli angewashirikisha Mawakili wasomi waliokwishaiva wakili Lissu, wakili Kibatara na Fatma Karume kwenye mambo ya umuhimu kama haya yeye kaleta uchama sasa itatugharimu .// Dicteta Magufuli mist go" . Maneno hayo yanadaiwa kusambazwa na mshtakiwa huyo kupitia mtandao huo wa kijamii wa Facebook.

Ilidaiwa kuwa maneno hayo yalikuwa na lengo la kupotosha umma

No comments:

Post a Comment