Wednesday, September 13

Waliofukuzwa kazi na madiwani warejeshwa


Watumishi watatu wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya, ambao walifukuzwa kazi Mei mwaka jana wamerejeshwa kazini.
Hatua hiyo inatokana na watumishi hao kushinda rufaa waliyokata kwenye vyombo vya juu vya utumishi.
Watumishi hao ni Mhandisi  Edwin Magiri, Ofisa Elimu Shule za Msingi, Beth Mlaki na Kaimu Ofisa Ununuzi Eliada Msana ambao walifukuzwa kazi na baraza la madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya kwa makosa tofauti.
Baraza la madiwani chini ya mwenyekiti wake, Mwalingo Kisemba lilifikia uamuzi wa kuwafukuza kazi baada ya kujiridhisha na ripoti ya kamati ilizounda kuchunguza tuhuma dhidi yao.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla  ametangaza leo Jumanne uamuzi wa kuwarejesha kazini watumishi hao kwenye kikao cha baraza la madiwani ili kutoa mrejesho wa hatua iliyochukuliwa na  vyombo vya juu vilivyosikiliza rufaa zao chini ya Tume ya Utumishi.
Amesema vyombo hivyo vimebaini utaratibu uliotumiwa na madiwani ulikuwa na kasoro, hivyo wamerejeshwa kazini na watalipwa stahiki zao zote tangu walipofukuzwa.

No comments:

Post a Comment