Friday, September 1

SHEIKH SHARIFF MAJINI KUFANYA DUA NZITO MAGOMENI.


Sheikh Shariff Majini kwa siku mbili mfululizo atafanya Dua maeneo ya Magomeni wilayani Kinondoni Jiji la Dar es salaam.

Dua itafanyika katika viwanja vya Mtambani jirani na ofisi za Serikali ya Mtaa na Dua hiyo itakuwa ni ya hadhara lakini pia ni ya pamoja ili kuifanya kuwa na nguvu.

Huu ni mfululizo wa Dua za Sheikh maeneo mbali mbali Nchini.

Kabla ya Magomeni Sheikh amefanya DUA katika mikoa ya Dodoma, Arusha, Tanga, Temeke, Viwanja vya TP Darajani na Ukumbini STARLIGHT.

No comments:

Post a Comment