Friday, August 18

MTOTO ALIYEUNGUA MIKONO SASA KUREJEA DARASANI


Mtoto aliyeungua na kushindwa kuendelea na masomo mkoani Mtwara ametibiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) na sasa anaweza kuendelea na masomo pamoja na kufanya shughuli zake za kawaida.

Mtoto huyo aliungua moto baada ya kusukumwa na mwenzake shuleni na hivyo kuungua mikono yote miwili na kusababisha vidole kujikunja na kushikamana.Baada ya kufikishwa Muhimbili madaktari bingwa walifanyia upasuaji na sasa amepona.

Daktari Bingwa wa Upasuaji, Ibrahimu Mkoma amesema mtoto Mwanahidi Hamisi aliungua miaka saba iliyopita na mikono yake kuadhirika na kushindwa kufanya kazi yoyote.

Amesema mwaka 2015 mtoto huyo alifanyiwa upasuaji mkono wake wa kulia katika Hospitali ya CCBRT na kwamba sasa anaendelea vizuri.Dk Mkoma amesema Juni 7, 2017 Muhimbili ilimpokea mtoto huyo na baada ya kufanyia uchunguzi walimfanyia upasuaji mkono wa kushoto na kunyoosha viungo katika vidole vyake ambavyo vilikuwa vimejikunja.

“Baada ya kuungua moto vidole vyake vilishikana na viungo kujikunja, lakini tumefanikiwa kuvinyoosha viungo hivyo na sasa Mwanahidi anaendelea vizuri na matibabu,” amesema Dk Mkoma.Amesema mtoto huyo sasa anaweza kufanya kazi mbalimbali kama kufua na kwamba anaweza kundelea na shule tofauti na awali baada ya kuungua.

Mama wa mtoto huyo, Amina Mohamed Mkadengile ameambiwa kwamba anapaswa kumfanyia mazoezi mtoto wake ili aimarike zaidi.“Daktari amenielekeza jinsi ya kumfanyia mtoto mazoezi, nitakuwa nafanyia mazoezi katika Hospitali ya Mkoa ya Ligula mkoani Mtwara. Nawashukuru sana

No comments:

Post a Comment