Tuesday, August 29

Jengo la 92 Hotel Sinza lavunjwa


Tingatinga likivunja jengo lilikuwa na Hotel ya

Tingatinga likivunja jengo lilikuwa na Hotel ya 92 kando ya Barabara ya Shekilango Sinza jijini Dar es Salaam. Picha na Salim Shao 
Dar es Salaam. Jengo maarufu la 92 Hotel lililopo eneo la Shekilango, Sinza limevunjwa kutokana na amri ya Mahakama kutokana na kesi ya madai.
Watu walioshuhudia jengo hilo likivunjwa wamesema kazi hiyo ilianza majira ya saa 11 alfajiri.
Akizungumza katika eneo la tukio, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya udalali ya Rimina, Abdallah Bakari, amesema wao wanatekeleza kazi hiyo kutokana na amri iliyotolewa na Mahakama Kuu Divisheni ya Ardhi.
Bakari amesema kabla ya kuvunja jengo hilo lenye maduka na ambalo pia linatumika kwa shughuli za ibada, walitoa notisi ya siku 14, ili kuwapa muda watu waliomo ndani wahamishe mali zao.
Hata hivyo, baadhi ya wapangaji wamesema hawakupatiwa taarifa jambo lililosababisha baadhi ya mali zao kuharibika wakati wa kazi hiyo.

No comments:

Post a Comment