Tuesday, August 29

Kituo cha Sheria chatoa tamko mlipuko ofisi za mawakili

Rais wa Chama cha wanasheria wa

Rais wa Chama cha wanasheria wa Tanganyika(TLS),Tundu Lissu  akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam katika kupinga shambulizi la ofisi za IMMMA Advocate lililotokea hivi karibuni. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi mtendaji wa Shirika la wanawake katika Sheria na aendelao Afrika,Dk Judith Odunga na Mkurugenzi wa kituo cha sheria na Haki za binadamu (LHRC),Dk Kijo Bisimba.Picha na Ericky Boniphace 
Dar es Salaam. Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), kimemtaka Kaimu Jaji Mkuu, Ibrahim Juma kukemea hadharani shambulizi lililofanyika katika ofisi za wanasheria za Immma Advocates.
Mkurugenzi wa LHRC, Dk Hellen Kijo-Bisimba amesema tangu kutokea mlipuko usiku wa kuamkia Agosti 26, hakuna kiongozi wa Serikali ambaye amekemea.
Amesema hata kaimu jaji mkuu anayesimamia mhimili wa Mahakama naye amekaa kimya kama vile hakuna tukio lililotokea.
Dk Kijo-Bisimba amesema leo Agosti 29 kuwa, kitendo cha mawakili kuvamiwa kimewatia hofu wanataaluma hao.

No comments:

Post a Comment