Friday, July 28

Serikali kufufua mfuko wa serikali za mtaa

Serikali yakusudia kufufua Mfuko wa Maendeleo ya Serikali za Mitaa (LGDG) ili kuendeleza miradi mbalimbali ya maendeleo iliyoibuliwa na wananchi katika Mamlaka za Serikali za Mitaa nchini.
Akizungumza na wadau mbalimbali wa maendeleo kutoka nchi mbalimbali zinazochangia bajeti ya Serikali katika mkutano uliofanyika, Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Mwalimu Julius Nyerere (JNICC), Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI),George Simbachawene jana jijini Dar es salaam.
“Mfuko huu ulipoanzishwa wananchi walivutiwa sana na walifanya jitihada za kubuni na kuibua miradi mbalimbali kwani Serikali ilitenga bajeti ya fedha kusaidia miradi hiyo, lakini kuanzia miaka ya 2013 hadi 2015 miradi hiyo ilianza kuzorota na ndiyo maana kuna maboma mengi kama vile Vituo vya Afya, Madarasa na Nyumba za Waalimu ambayo hayakukamilika kutokana na mfuko huo kuzorota,” alisema Mhe. Simbachawene
Aidha Simbachaweni alisema kuwa Mfuko huo una umuhimu katika kuinua uchumi na kuleta maendeleo ya Taifa, ambapo wananchi wamekua wakiibua miradi mbalimbali kama vile kujenga barabara, vituo vya Afya, Zahanati, nyumba za Walimu pamoja na madarasa, miradi ambayo imekuwa ikianzishwa na wananchi na kuendelezwa na Serikali.
Na Emmy Mwaipopo

No comments:

Post a Comment