Friday, July 28

Serikali kuwatumbua watumishi watakao hujumu Maliasili


Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Maghembe amesema kuwa hatoweza kumvumilia mtumishi yeyote wa wizara hiyo atakayehujumu Maliasili za Taifa kwa kushirikiana na majangili.
Waziri Maghembe ametoa kauli hiyo wakati wa mkutano wa mwaka wa Wahariri na wanahabari wandamizi kutoka vyombo vya habari mbalimbali hapa nchini uliofanyika mkoani Tanga.
“Na sisi watumishi bado tuna shida na watumishi kama mnavyojua, tuna watumishi wengi 90 percent wazuri, lakini tuna 3,4,5,6 wasio waaminifu lakini bado tunaangalia kwa makini na pale tutakapo mngamua mtu yupo kwenye shughuli hiyo inabidi tuwatumbue ili tuweze kuondokana na watu hawa, kwasababu sekta hii ni muhimu sana kwa uchumi wa Taifa letu
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu TANAPA, Allan Kijazi alielezea mchango wao kwa Taifa kupitia sekta ya utalii
“Mwaka jana tulichangia sh. Bilioni 27 kwenye mfuko mkuu wa serikali na mwaka ujao tunategemea kuchangia kiasi cha sh. Bilioni 34.5 kama mchango wa moja kwa moja kwenda kwenye bajeti kuu ya serikali.”
Na Emmy Mwaipopo

No comments:

Post a Comment