Friday, July 28

Mfuko wa Serikali za Mitaa kufufuliwa

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), George Simbachawene 
Dar es Salaam. Serikali imejipanga upya kufufua Mfuko wa Maendeleo wa Serikali za Mitaa (LGDG)  ili kuwezesha utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayowagusa moja kwa moja wananchi.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), George Simbachawene amesema hatua za awali za kuufufua mfuko huo zimeshaanza na wadau wa maendeleo wameonyesha utayari wa kuchangia.
Akizungumza wakati wa majadiliano na wadau wa maendeleo kuhusu ufufuaji wa mfuko huo Simbachawene amesema ni matarajio ya Serikali kuwa miradi mingi itatakelezwa.
Kwa upande wake, Mkuu wa Kitengo cha Uchumi na Biashara kwenye Ubalozi wa China nchini, Lin Zhiyong ameishauri Serikali ya Tanzania kuweka nguvu kwenye uendelezaji wa Serikali za Mitaa.
“Mazingira yakiwekwa vizuri ngazi ya nchini inakuwa rahisi hata mwekezaji kufikiria kwenda kuwekeza kijijini, hilo litawezekana endapo kwa dhati Serikali itaamua kwa dhati kutimiza azma hiyo,” alisema.
Amesema China imeweza kufanikiwa kwa kuwa hali ya uchumi katika serikali za mitaa iko vizuri na hiyo ilitokana na kuwekeza nguvu huko ambako hasa ndipo wapo watu wengi.

No comments:

Post a Comment