Thursday, September 9

TANZANIA MWENYEJI WA ONESHO LA UTALII LA NCHI WANACHAMA WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI

 KATIKA jitihada za kuvutia na kukuza uwekezaji katika sekta  ya Utalii Mawaziri wa Jumuiya  ya Afrika  Mashariki wanaoshughulikia Masuala ya wanyamapori  na utalii wamepitisha mkakati wa kutangaza utalii wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.


Akiongea leo na wandishi wa habari Jijini Dodoma Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mary Masanja amesema onyesho hilo litakuwa linafanyika kwa mzunguko katika nchi wanachama kila mwaka.

Amesema  kwa kutambua utalii ni sekta mtambuka onesha  hilo ni fursa muhimu ya kuhamasisha uhifadhi wa maliasili na malikale pamoja na kuchochea ukuaji wa utalii hususani utalii wa mikutano na matukio (MICE TOURISM) ambao ni zao jipya la utalii la kimkakati la kufanikisha kuongeza idadi ya watalii  katika ukanda wa Afrika Mashariki.

"Napenda kuwajulisha kuwa Tanzania ndio  itakuwa mwenyeji wa kwanza wa onesho hili  la utalii wa jumuiya ya Afrika Mashariki ambapo kauli mbiu ya onesha  hilo inasema " Utangazaji utalii stahimilivu  kwa maendeleo  jumuishi ya kijamii na uchumi, ".

Onesho la EARTE litafanyika jijini Arusha  Oktoba 2021 ambapo litajumuisha  siku tatu za maonesho  na siku tano za ziara maalum ya kutembelea vivutio vya utalii pamoja na fursa za utalii wa ndani kwa Tanzania bara na Zanzibar," Amesema Naibu Waziri Masanja.

Akizungumzia jinsi ugonjwa wa Corona ulivyoathiri sekta ya utalii ambapo kabla ya ugonjwa idadi ya watalii walifika Milioni 1.5  lakini baada ya kuzuka kwa ugonjwa  huo idadi ya watalii ilipungua na kufikia 620,000 huku makusanyo na mapato yakishuka.

" Kwa  sasa hali inaenda vizuri  baada Rais wa awamu ya sita Samia Suluhu Hassan kuleta chanjo ya ugonjwa wa Corona ambapo namba ya watalii kuingia nchini inapanda," amesema Naibu Waziri Masanja.

 

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mary Masanja akizungumza na wandishi wa habari ofisini kwake jijini Dodoma.

Naibu Waziri Wizara ya Maliasili na Utalii, Mary Masanja akizungumza na wandishi wa habari ofisini kwake jijini Dodoma leo alipokua akitangaza juu ya kuanza kwa onesho la utalii kwa Nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

No comments:

Post a Comment