Saturday, March 31

Twaweza: Raia Tanzania wanasema hawako huru kukosoa kauli za utawala

Wananchi wangependa kuwa huru kukosoa watawala iwapo hawataridhika na maamuzi ya SerikaliHaki miliki ya pichaTWAWEZA
Image captionWananchi wangependa kuwa huru kukosoa watawala iwapo hawataridhika na maamuzi ya Serikali
Idadi kubwa ya wananchi (60%), nchini Tanzania wanasema hawako huru kukosoa kauli zinazotolewa na Rais wakati asilimia 54 wanasema hivyo kuhusu kauli zinazotolewa na Makamu wa Rais na asilimia 51 Waziri Mkuu.
Hii ni kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na shirika la utafiti lisilo la serikali, Twaweza.
Wananchi wanajisikia huru zaidi kuwakosoa wabunge wao kuliko wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya.
Kwa mujibu wa shirika la Twaweza, hali hii inaweza kuwa ni kwa sababu wananchi wanawachagua wabunge kuwa wawakilishi wao na hivyo wanaona kuwa mbunge anajukumu la kusikiliza mahitaji na vipaumbele vyao na kuvifanyia kazi ipasavyo.
Wananchi wanaunga mkono kwa kiasi kikubwa uhuru wa kujieleza na uhuru wa vyombo vya habari. Wananchi nane kati ya kumi (81%) wanaona ukosoaji wa viongozi wa taifa kama jambo muhimu kwani itawasaidia kujirekebisha na si kuwashushia hadhi.
Asilimia 62 ya wananchi wanasema ni bora zaidi kwa magazeti yanayochapisha taarifa zisizo sahihi kuomba radhi na kuchapisha marekebisho kuliko kufungiwa ama kutozwa faini na serikali. Na wananchi wengine (54%) wanasema serikali isiruhusiwe kuyaadhibu magazeti kabla ya kupata kibali kutoka mahakamani.
Utafiti wa TwawezaHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionUtafiti wa Twaweza

Uhuru wa kujieleza

Utafiti huu umebaini kuwa wananchi wanaunga mkono kwa kiasi kikubwa uhuru wa kujieleza na uhuru wa vyombo vya habari. Wananchi nane kati ya kumi (81%) wanaona ukosoaji wa viongozi wa taifa kama jambo muhimu kwani itawasaidia kujirekebisha na si kuwashushia hadhi.

Wananchi wengi hawafahamu sheria mpya zinazosimamia masuala ya taarifa

Sheria mbalimbali zinazohusiana na masuala ya taarifa zimetungwa na Bunge katika miaka ya hivi karibuni, ikiwemo Sheria ya Takwimu, Sheria ya Makosa ya Mtandao, Sheria ya Upatikanaji wa Taarifa na Sheria ya Huduma za habari. Hata hivyo, wananchi wachache wanazifahamu sheria hizo.

'Misingi kufuatwa'

Akiwa kwenye uzinduzi wa utafiti huo jijini Dar es salaam, msemaji mkuu wa serikali ya Tanzania, Dk Hassan Abbas alisema kuwa 'kumkosoa Rais maana yake ametenda jambo ambalo hukubaliani nalo.Lakini kuna misingi ya kufuatwa . Uwe na utafiti, hoja zinzaofaa na lugha unayotumia.'
Hivi karibuni kumekuwa na ukosoaji dhidi ya kinachodaiwa kuwa kuminywa kwa uhuru wa kujieleza,
Tukio linalokumbukwa ni la Mkalimani aliyedaiwa kutafsiri maneno yasiyo sahihi kutoka kwa mmoja wa watalii aliyetembelea hifadhi ya Ngorongoro, ambaye baadae na
mkalimani huyo anayeitwa Simon Sirikwa aliwekwa chini ya ulinzi kutokana kile kilichokuwa kinatafsiriwa kudaiwa kuwa kilikuwa kinapotosha uhalisia wa maneno yaliyokuwa yakizungumzwa na mtalii aliyekuwa akisifia kile alichokiona baada ya kutembelea eneo hilo la utalii.

No comments:

Post a Comment