Saturday, March 31

Simanzi yatawala kifo cha Mtanzania aliyeuawa Uingereza


Arusha. Simanzi imetawala nyumbani kwa Mtanzania, anayeishi Uingereza, Leila Mtumwa aliyeuawa usiku wa kuamkia leo.
Leila anadaiwa kuchomwa kisu na mumewe nchini Uingereza.
Akizungumza na MCL Digital, leo Machi 31, mama wa mtoto huyo, Hidaya Mtumwa amesema amepokea kwa mshtuko habari za kifo cha mtoto wake.
"Juzi usiku nilikuwa nilizungumza naye tulicheka, nilikuwa namwambia kuna mwandishi wa habari anataka kunihoji mambo ya Pepe Kalle aliyenitungia wimbo, sasa baadaye akaniambia anawahi taksi atanipigia," amesema.
Amesema hata hivyo baada ya kupata taarifa ya msiba sasa anaomba kusaidiwa mwili wa mtoto wake kurejeshwa nchini.
Akiwa nchini Tanzania miaka ya 1990, Pepe Kalle alitunga kibao cha Hidaya kilichopata umaarufu kwa wapenzi wa muziki kote Tanzania. 
Akiwa miongoni mwa wanamuziki kutoka DR Congo, Pepe Kalle amewahi kufanya ziara nchini mara kadhaa na kundi lake la Empire Bakuba lililokuwa na wanamuziki wengine mahiri kina Papy Tax, Bileku Mpasi na wengineo wakiwamo wacheza shoo wawili wafupi, Emoro na Jolie Bebe.  Pepe Kalle, alifarki dunia mwaka 1998. 

No comments:

Post a Comment