Saturday, March 3

Mwanamke aliyepambana na mamba afanyiwa upasuaji mkubwa wa mguu leo


Mwanamke aliyeshambuliwa na mamba, Martha Malambi (25) amefanyiwa upasuaji mkubwa wa mfupa mrefu wa paja baada ya majeraha aliyopata kutengemaa.
Martha aliyelazwa katika Taasisi ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu (MOI) baada ya kushambuliwa na mamba huyo wakati akiteka maji kwenye Mto Mgeta katika Kijiji cha Ukutu Kata ya Bwakilachini, Morogoro anaendelea vizuri kiafya baada za kufanziwa upasuaji huo leo Machi 2.
Mtaalamu mwandamizi wa upasuaji wa mifupa MOI, Dk Paul Marealle amesema Martha anaendelea vizuri na upasuaji huo umefanikiwa kwa kiasi kikubwa.
"Huu ni upasuaji mkubwa wa mfupa mrefu wa paja, umekamilika vizuri, amewekewa chuma maalumu ndani ya mfupa (sign nail)." amesema.

No comments:

Post a Comment