Wednesday, March 7

Mshauri wa Trump kujiuzulu

Gary Cohn
Mshauri wa uchumi wa ngazi ya juu Gary Cohn anaondoka ikulu ya White House baada ya kutofautiana na Rais Donald Trump juu ya sera za biashara, ikiwa ni tukio la karibuni katika mtiririko wa wale waliojiondoa kutoka ofisi hiyo ya rais iliyoko magharibi ya jengo la ikulu.
Cohn, ambaye ni mkurugenzi wa baraza la uchumi la taifa, amekuwa akiongoza wale wanaopinga ndani ya nchi mpango mzima wa Trump wa kuweka ushuru katika uagizaji wa chuma na aluminium.
Pia aliendelea kuhamasisha juhudi za dakika ya mwisho katika siku za karibuni ili kumfanya Trump abadilishe msimamo wake.
Lakini Trump amekaidi juhudi hizo, na kusisitiza Jumanne ataanzisha ushuru katika siku chache zijazo.
Kuondoka kwake Cohn kumekuja katikati ya kipindi ambacho kuna mkanganyo ambao haujawahi kushuhudiwa katika uongozi wa Trump, na wasaidizi wake wana wasiwasi kuwa wafanyakazi zaidi wa Ikulu watajiondosha katika ofisi hiyo.
Tangazo hilo limekuja saa kadhaa baada ya Trump kukanusha kuwa kuna mvurugano ndani ya White House. Trump ameendelea kusema kuwa ikulu ya White House “ina nguvu yakutosha,” lakini maafisa kadhaa wa ikulu hiyo wamesema kuwa Trump amekuwa akiwashauri wasaidizi wake waliokuwa na wasiwasi kuendelea kufanya kazi naye.
“Kila mtu anataka kufanya kazi White House,” Trump amesema wakati wa mkutano wake na waandishi wa habari akiwa na mgeni wake Waziri Mkuu wa Sweden Stefan Lofven. “Wote hawa wanataka kuwa sehemu ya wafanyakazi wa ofisi ya Rais.”
Katika tamko lake, Cohn amesema ilikuwa ni heshima kubwa kwake kutumikia katika serikali na kuweza kupitisha sheria ya sera za kuboresha uchumi ili kuwanufaisha watu wa Marekani.”
Kwa upande wake Trump amempongeza Cohn pamoja na kuwepo tofauti kati yao juu ya suala la biashara, na kutoa tamko kuwa Cohn “ametumikia nchi yake kwa ufanisi wa hali ya juu.”
Cohn ni mtendaji wa zamani wa Goldman Sachs ambaye alijiunga na ikulu ya White House baada ya kuondoka kutoka kampuni ya Wall Street ambako alipata marupurupu ya dola milioni 285.
Alikuwa na jukumu muhimu la kumsaidia Trump kupitisha sheria ya mabadiliko makubwa katika kodi, na kuratibu suala hilo na wabunge.
Kuondoka kwa Cohen kulitarajiwa lakini kumekuwa ni sikitiko kubwa kwa wabunge na wafanya biashara.

No comments:

Post a Comment