Sunday, March 11

Mita ya maji yaibua kizaazaa 21st Century

Mkurugenzi na meneja uzalishaji wa kiwanda cha nguo cha 21st Century wanashikiliwa polisi baada ya Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Jumaa Aweso kufanya ziara kiwandani hapo na kubaini mita ya maji hung'olewa usiku na kurejeshwa asubuhi.
Naibu waziri amefanya ziara kiwandani hapo leo Jumapili Machi 11,2018 akisema aligundua hilo baada ya kupata taarifa kutoka kwa raia wema.
Aweso akiwa kiwandani hapo alikuta mita ikiwa imeng'olewa huku maji yakiendelea kutumika kiwandani.
Meneja uzalishaji, Clement Munisi amesema hakuwa na taarifa za kuchomolewa mita akimtaja mfanyakazi kiwandani hapo Samwel kuwa ndiye msimamizi wa kitengo cha huduma ya maji.
Alipopigiwa simu mfanyakazi huyo alisema yuko kanisani na hawezi kutoka.
Naibu waziri, Aweso amemwagiza mwanasheria wa mamlaka ya maji Morogoro (Moruwasa), Tumaini Kimaro kufanya utaratibu wa kisheria ili viongozi wa kiwanda hicho wafikishwe mahakamani.
Mkuu wa kitengo cha udhibiti upotevu wa maji cha Moruwasa, Bertam Minde alisema kiasi kilichoibwa kingesaidia maeneo mengine kupata huduma.

No comments:

Post a Comment