Sunday, March 11

Hatua 10 zitakazokuwezesha kupandishwa cheo kazini


Uaminifu ni kitu kizuri na cha maana kinachowashinda wengi wetu. Wakati wowote unapopata nafasi ya kuongea na bosi wako, kuwa mkweli katika kila neno litokalo kinywani mwako, liwe dogo au kubwa, liwe kuhusu wewe mwenyewe au kuhusu mtu mwingine, kuwa mkweli hata katika yale yanayoonekana kukuathiri wewe, amua kuwa mkweli bila kujali mazingira. Kuwa mkweli katika yale unayoyatamani na katika maswala mazima ya maendeleo ya kazi yako, sio tu unazungumza kile unachofikiri bosi wako angetamani ukiseme. Staili za kuongea zaweza kutofautiana mtu na mtu lakini ujumbe ubaki kuwa wa kweli.
Penda mazingira masafi
Wakati wowote penda kuyaweka mazingira yako ya kazi safi, hatakama ofisi sio ya kuvutia sana lakini bado unaweza kuvipanga vitu katika meza yako au pale unapofanyia kazi vikawa vema na vyenye mpangilio mzuri. Wengine wamekuwa wakijidanganya kuwa kama wakipoteza muda wao kufanyia usafi eneo lao la kazi basi mabosi wao wataona kuwa hawana kazi za kutosha za kufanya, hii ni kinyume kwa maana hali yako ya ndani ya kiutendaji yaweza kuonekana pale tunapotazama mazingira ya wewe unapofanyia kazi.
Fanya kazi saa sahihi
Mara nyingi wengi wetu tumejidanganya kuwa kwa kufanya kazi masaa mengi sana, kutoka usiku makazini na kuwahi kufika mapema sana asubuhi ndio tunaandaa mazingira ya kupanda vyeo, bado kuwaza hivi ni kosa. Ukiendelea hivi kwa muda wanaokuzunguka pamoja na bosi wako wanapata ujumbe kuwa unahangaika sana na majukumu yako yanayoonekana kukushinda na hivyo itakuwia ngumu sana kukabidhi kazi katika wakati muafaka.
Jitahidi kufanya majukumu ya zaidi
Kama unadhani unahitaji kufanya majukumu ya zaidi ili upate changamoto za ziada basi inakubidi ukubali kujitolea kutoa msaada katika baadhi ya majukumu ya wengine pale inapobidi. Waweza kuzungumza na bosi wako kuhusu hili pia, jitahidi kuwa halisi zaidi katika matazamio yako na usiweke malengo yaliyo juu ya uwezo wako ka unajua hutoweza kuyatimiza.
Mara uchukuapo jukumu fulani ili kulifanya basi jitahidi kuonyesha kuwa unalifurahia na wala haulijutii, fanya kila ulilosema kuwa utalifanya, na kwa hivyo utaonyesha heshima kubwa na kujionyesha mtu unayeweza kutegemewa. Ni muhimu sana kuwa na tabia hizi kwa maendeleo binafsi.
Uliza maswali
Kukaa kimya tu huku umeinamisha kichwa chini pasipo kusema kitu hakutakusaidia chochote katika kupanda cheo, Usihofu kuuliza swali lolote na kama una kitu au wazo juu ya jinsi gani hali fulani inaweza kuboreshwa basi iseme kwa wahusika. Yawezekana ukajiona kama unayepitiliza mipaka yako ya kazi, na yamkini wengine wasikuelewe, lakini usihofu maana taratibu itawaonyesha kuwa unaipenda kazi na uko tayari katika kuboresha biashara au mafanikio ya ofisi kwa ujumla.
Fanya utafiti
Kama unakiu ya kupanda ngazi katika masuala ya kikazi na ajira basi lazima ufanye tafiti, kama kuna kazi maalumu unataka kuiomba hakikisha unajua kilakitu kuhusu kazi hiyo na uweze kuelezea jinsi gani ujuzi wako unaendana na ule unaohitajika katika kazi husika.
Onyesha mafanikio yako kwa undani iwezekanavyo lakini pasipo kujikweza au kujisifia, mfano; kama umefanikiwa kuvuka malengo ya mauzo yako kwa kipindi fulani, basi acha mabosi wako walijue hilo.
Jifunze kutengeneza nafasi mpya
Kama unafikiri kuna njia rahisi zaidi au za mafanikio zaidi katika utendaji wako wa kazi au kama unaona umuhimu wa kuwepo kwa nafasi nyingine ya kazi ni bora uzungumze na bosi wako. Kwa sababu wewe ndiyo uliyeona umuhimu wa nafasi hiyo na kulitolea wazo, kuna uwezekano mkubwa kwamba wewe ndiyo utakayeonekana kufaa kuchukua nafasi hiyo, hii inamaanisha kwamba utakuwa tayari kubeba majukumu mapya.
Ongeza ujuzi wako
Kama unaona kuna umuhimu wa kuongezea kidogo ujuzi ulionao basi tafuta kozi zinazoendana na kile unachotaka kukifanya, jitahidi kuhudhuria semina, warsha na makongamano mbalimbali ya mlengo wa kazi yako, penda kujua zaidi ya vile wenzako wanavyovijua. Waweza kuwauliza waajiri wako kama kuna fungu kwa ajili ya kujiendeleza ili ulifaidi, onyesha kuwa una kiu ya kujiongezea ujuzi kwa manufaa ya kampuni au ofisi, hii itawafurahisha wakuu wako na kupanua wigo wa kukufikiria kwa majukumu makubwa zaidi

No comments:

Post a Comment