Saturday, December 2

MBUNGE WA ARUMERU MASHARIKI MHESHIMIWA JOSHUA NASSARI AVAMIWA

Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari akiwa na Mbunge wa Arusha mjini, Godbless Lema wameenda kwenye kituo cha polisi Usa River kutoa taarifa ya tukio la uvamizi uliofanyika nyumbani Nassari usiku wa kuamkia leo Jumamosi.
Tukio hilo limetokea Kijiji cha Nkwanekori wilayani  Arumeru mkoa wa Arusha.
Katika ukurasa wake wa Twitter Nassari ameandika, “Nimevamiwa nyumbani kwangu maeneo ya USA RIVER usiku huu na watu wenye silaha, na kufyatua risasi ambazo zimeua mbwa waliokuwepo nje ya nyumba. Nimefanikiwa kukimbia na mke wangu na kuripoti kituo cha Polisi. Nimekuwa nikitishiwa kuuawa kila siku, sina amani ndani ya nchi yangu.”
Baadhi ya majirani na viongozi wa Chadema wamefika nyumbani kwake kumjulia hali na baadaye kumsindikiza kituo cha polisi Usa River.
Mmoja wa majirani ambaye hakupenda kutajwa jina lake amesema alisikia milio ya risasi zaidi ya 12 na baadaye kimya kutawala.

No comments:

Post a Comment