Friday, December 1

Aliyepandikizwa figo Muhimbili aenda nyumbani


Dar es Salaam. Mgonjwa wa kwanza kupandikizwa figo Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Prisca Mwingira  ameruhusiwa kurudi nyumbani leo Ijumaa baada ya kuwa chini ya uangalizi wa jopo la madaktari bingwa wa figo kwa siku 10.
Prisca (30) ambaye ni Mwalimu wa Shule ya Sekondari Mikese mjini Morogoro, amechangiwa figo na mdogo wake Batholomeo Mwingira (27).
Akizungumza na vyombo vya habari leo Ijumaa mara baada ya kutoka chumba cha uangalizi maalum (ICU), Prisca ameishukuru Serikali kugharamia matibabu yake na kuiomba kuwekeza zaidi katika matibabu ya kibingwa ili kusaidia Watanzania wengi wasio na uwezo wa kufuata gharama nje ya nchi.
“Kwa kipekee napenda kumshukuru sana ndugu yangu, kaka yangu Batholomeo kwa kupenda niendelee kuishi. Madaktari bingwa wa figo Muhimbili tangu wamenipokea wamekuwa wakinipa matibabu mbalimbali, nimesafishwa damu kwa muda wa mwaka mmoja wamenishauri na mpaka katika matibabu ya kupandikiza figo nyingine,"

No comments:

Post a Comment