Wednesday, November 29

Wabunge Uingereza wakerwa na 'tweets' za Trump

Waziri Mkuu Teresa May
Wabunge wa Uingereza wameonyesha kukerwa Jumatano na kitendo cha Rais Donald Trump alivyorudia kutuma ujumbe mfupi wa tweet uliokuwa na video isiyo na ukweli ndani yake dhidi ya Waislam.
Video hiyo ambayo Trump aliirudia katika twitter yake ilipostiwa kwanza na kiongozi wa kundi la Uingereza mwenye mrengo wa kulia ambaye aliwahi kuhukumiwa kwa kosa la kutumia kauli za chuki.
Wabunge kadhaa wamemtaka Waziri Mkuu Theresa May kufutilia mbali ratiba ya ziara ya kikazi ya rais Trump iliyopangwa kufanyika mwaka 2018.
“Huyu siyo mshirika au rafiki yetu,” amesema mbunge David Lammy, akiongeza kuwa rais wa Marekani hafai kutembelea Uingereza.

Msemaji wa Waziri Mkuu May amesema Trump amefanya makosa kutuma tena video hiyo ambaye haikuwa tukio la kweli katika ujumbe wake wa tweet.
“Wananchi wa Uingereza kwa pamoja wanapinga shutuma za kisiasa za kibaguzi za mrengo wa kulia, ambazo zinakiuka maadili ambayo yanawakilishwa na nchi hii—upole, kuvumiliana na heshima. Ni kosa kwa rais kufanya jambo kama hili,” amesema.
Kadhalika hata wale wanasiasa ambao kawaida ni washabiki wa Trump wamemkosoa Trump kwa kutuma tena ujumbe wa aina tatu wa twitter uliotolewa na Jayda Eransen, Naibu kiongozi wa kikundi cha mrengo wa kulia chenye sera ya Uingereza kwanza (Britain First) na msimamo dhidi ya wahamiaji, kinachotaka kurejeshwa “kwa maadili ya utamaduni wa Kiingereza” na kutaka kumaliza “kuenea kwa Uislam.”
Tweet alizozituma tena Trump Jumatano asubuhi kufuatia video ya kwanza iliyokuwa haijathibitishwa inayodai kuwa wahamiaji Waislam wakiwa wanampiga kijana wa kiholanzi aliyekuwa anatembelea magongo.
Muda mchache baadae rais alituma tena video ya pili ambayo ilipostiwa na Fransen, iliyodai kuwa “Muislam alikuwa analiharibu sanamu la Bikra Maria.

Tweet ya tatu ilikuwa na ujumbe : “Kundi la Waislam wakimsukuma kijana kutoka katika paa la nyumba na huku wakimpiga hadi kumuua!”
Fransen amekuwa akihojiwa na polisi mara kadhaa kwa sababu ya kutumia kauli zenye chuki kama ilivyokuwa kwa viongozi wengine wa kikundi kinachojiita Uingereza Kwanza (Britain First) ambao wametuhumiwa kwa vurugu za kidini na uchochezi.
Mapema mwezi wa Novemba, Fransen alipatikana na hatia ya vurugu za kidini wakati alipomtukana mwanamke wa Kiislam kwa sababu amevaa hijabu.

No comments:

Post a Comment